ERTUGRUL BEY
JF-Expert Member
- Aug 6, 2020
- 11,532
- 21,533
Masahaba baada ya kujua kuwa swala humkataza mja na mambo machafu na maovu
Wakamwambia Mtume Muhammad swala aallahu alaih wa salam,fulani mchana huswali halafu ikifika asubuhi anaiba
Mtume akawajibu "hivi karibuni swala yake itamkataza na mambo maovu na machafu"
Kwahiyo ndugu yangu muislamu kama unatabia yoyote mbaya basi we swali tu,kwani kwa hakika ipo siku utakuwa mtu tofauti kabisa,swali kwa ikhas na si kwa kujionyesha,swali kwa unyenyekevu mkubwa ipo siku swala yako itakubadilisha
Na tupende kuwabashiria watu mema,kwani ndivyo Mtume alivyotaka iwe hivyo,maana tuna ile tabia ya kuwakatisha watu tamaa kwa kuwaambia " wewe mwenyewe unazini halafu unaswali ya nini?
Tunakosea sana kwani tujue kuwa mtu akishikamana na swala kwa unyenyekevu kabisa na kwa ajili ya Allah ipo siku atabadilika,kwahiyo kuwa mtu wa kutoa bishara njema kwa watu na kuwapa moyo wa kufanya mambo ya kheri
Wakamwambia Mtume Muhammad swala aallahu alaih wa salam,fulani mchana huswali halafu ikifika asubuhi anaiba
Mtume akawajibu "hivi karibuni swala yake itamkataza na mambo maovu na machafu"
Kwahiyo ndugu yangu muislamu kama unatabia yoyote mbaya basi we swali tu,kwani kwa hakika ipo siku utakuwa mtu tofauti kabisa,swali kwa ikhas na si kwa kujionyesha,swali kwa unyenyekevu mkubwa ipo siku swala yako itakubadilisha
Na tupende kuwabashiria watu mema,kwani ndivyo Mtume alivyotaka iwe hivyo,maana tuna ile tabia ya kuwakatisha watu tamaa kwa kuwaambia " wewe mwenyewe unazini halafu unaswali ya nini?
Tunakosea sana kwani tujue kuwa mtu akishikamana na swala kwa unyenyekevu kabisa na kwa ajili ya Allah ipo siku atabadilika,kwahiyo kuwa mtu wa kutoa bishara njema kwa watu na kuwapa moyo wa kufanya mambo ya kheri