Roving Journalist

JF Roving Journalist
Apr 18, 2017
2,813
11,991
Rais Samia akizungumza na Wakazi wa Jiji la Mwanza baada ya kuwasili kwa Ziara ya Kikazi leo Juni 12, 2023.



Akitoa Salamu kwa Wananchi wa Jiji la Mwanza waliojitokeza kwenye uwanja wa Ndege kumpokea, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan amesema Tanzania ni Nchi moja, haiwezi kugawanyika wala kuuzika.

“Baada ya kusema hayo jioni imeingia, na ninaambiwa wapo wengine wengi kule nilitaka tu niwasalimie, lakini salamu moja kubwa ni kwamba Mama huyu ni Mtanzania. Atafanya kila analoweza kufanya Tanzania iendelee. Na Tanzania ni moja, haigawanyiki wala haiuziki. Kwa hiyo ndugu zangu mama ni Mtanzania, maendeleo yetu ndio muhimu. Kila linalofanyika ni kwa maendeleo ya Watanzania” amesema Rais Samia.

IMG_7590.jpeg

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Amos Makalla mara baada ya kuwasili katika uwanja wa Ndege wa Mwanza uliopo Ilemela Mkoani humo

Aidha, Rais Samia amesema pamoja na kukagua miradi ya Maendeleo Mkoani humo, atashiriki pia maadhimisho ya miaka miwili ya Uchifu aliopewa Mkoani humo, Uchifu Hangaya.

“Kama chifu Mkuu sikuwaza kama nisije. Kama chifu Mkuu lazima nije. Mwanza ndiko nilikokabidhiwa Uchifu na Uhanganya, kwahiyo tumekuja kwenye maadhimisho yetu ya Miaka 2 ya Uhangaya lakini sherehe zetu zile za Bulabo. Sherehe za kutunza Mila na utamaduni wetu.” ameongeza Rais Samia.

IMG_7591.jpeg

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwasalimia wananchi wa Ilemela waliofika kumpokea katika uwanja wa Ndege wa Mwanza mara baada ya kuwasili
Naye Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Amos Makalla amesema kuna kundi kubwa la vijana wa Bodaboda zaidi ya 300 wamejiandaa kumpokea Rais Samia mkoani humo huku akiweka bayana pia kuwa hali ya Usalama ni Shwari.
 
Rais Samia akizungumza na Wakazi wa Jiji la Mwanza baada ya kuwasili kwa Ziara y Kikazi leo Juni 12, 2023.



Akitoa Salamu kwa Wananchi wa Jiji la Mwanza waliojitokeza kwenye uwanja wa Ndege kumpokea, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan amesema Tanzania ni Nchi moja, haiwezi kugawanyika wala kuuzika.

“Baada ya kusema hayo jioni imeingia, na ninaambiwa wapo wengine wengi kule nilitaka tu niwasalimie, lakini salamu moja kubwa ni kwamba Mama huyu ni Mtanzania. Atafanya kila analoweza kufanya Tanzania iendelee. Na Tanzania ni moja, haigawanyiki wala haiuziki. Kwa hiyo ndugu zangu mama ni Mtanzania, maendeleo yetu ndio muhimu. Kila linalofanyika ni kwa maendeleo ya Watanzania” amesema Rais Samia

Ila wakuu wa mikoa wamezidi sana, sifa nyingi kuliko uhalisia.
 
“Mama huyu ni Mtanzania, atafanya kila analoweza kufanya Tanzania iendelee na Tanzania ni moja haigawanyiki wala haiuziki, maendeleo yetu ndio muhimu na kila linalofanyika ni kwa maendeleo ya Watanzania.”

Ameeleza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akizungumza na wakazi wa Mwanza baada ya kuwasili mkoani humo kwa ziara ya kikazi inayoanza leo tarehe 12 Juni 2023
 
Yeye ni Mzanzibari na anachofanya ni hujuma Kwa wa Tanganyika
Wanzanzibar wanafki sana hawa watu ukitaka kufahamu hilo nenda Zanzibar au ukiwa nje ya nchi jamaa hawajitambulishi kama wa Tanzania Bali wanzanzibar wana hadi umoja wao wa wanzanzibar UK, USA.
Kwa wqlivyo wanafki kwenye umoja wa watanzania nje utakuta wapo, halafu hapo hapo wana kaumoja Chao cha wazanzibar ambapo watu wa bara hawaruhusiwi kujiunga
Huyu Mama anaongea unafki
 
“Mama huyu ni Mtanzania, atafanya kila analoweza kufanya Tanzania iendelee na Tanzania ni moja haigawanyiki wala haiuziki, maendeleo yetu ndio muhimu na kila linalofanyika ni kwa maendeleo ya Watanzania.”

Ameeleza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akizungumza na wakazi wa Mwanza baada ya kuwasili mkoani humo kwa ziara ya kikazi inayoanza leo tarehe 12 Juni 2023
Wanatangaza Amani huku wameficha Mapanga.

Lakini pia tusisahau alishawahi kusema yeyé ni Sawa na Magufuli, wapi sasa
 
Mimi binafsi rai yangu kwake wao kama viongozi wetu wajipe muda wa kutafakari tena kuhusu swala la mkataba wa bandari.
Kwa sababu wanadai haya makubaliano ya awali wamepeana muda wa miezi 12 kama hawatoafikiana chochote kuhusiana na ile mikataba ya kazi ambayo itasainiwa baina ya TPA na DPW huu mkataba wa sasa utakuwa umekufa automatically basi ni vyema watumie fursa hiyo ili kupata muda zaidi wa kujitafakari na kutoa elimu kwa wananchi au waachane kabisa na huo mpango wao.
 
Back
Top Bottom