mwalimu nyerere hakuwa Mungu, na hata mtikila aliwahi kutamka hilo, kwa hiyo kufanya makosa alifanya kama binadamu wengine, pia kuna mambo aliwahi kufanya yakawa chukizo mbele ya mwenyezi Mungu, mnakumbuka kuwa aliwahakikishia waliohudhuria ile birth day yake pale diamond jublee, 1997 kuwa alikuwa anakula vizuri, na kuwa alikuwa ana uhakika wa kuishi hata miaka 100. tena akasema kuwa alikuwa na uhakika wa kuona rais ambaye angekuja kumrithi mkapa, yaani angekwenda mpaka nyakati hizi za kikwete. watu wakamwambia mwalimu hapo umeteleza, lakini wapambe wake waaanza kula ugali wa mtama(chakula cha mwalimu), eti ili waishi maisha marefu, ulikuwa ni april 1997, mwishoni mwa 1997 tayari leukemia ikawa imethibitishwa na ahadi yake ya kuishi kwingi ikawa imekwenda na maji.
lakini mwalimu, alikuwa ni mtu anayekubali makosa, kwa kipindi cha kwanza tu alishagundua makosa ya mkapa
mfano alipinga wazi wazi kuuzwa kwa benki ya NBC, hatujui kama angekuwawepo mpaka sasa angepinga mangapi.
mkapa alikuwa ni mwanafunzi mnafiki wa mwalimu. ni wale wanafunzi wanaokuwa wanafiki wa ajabu. wawapo darasani na mbele ya mwalimu hushtaki wengine na kujipendekeza kwa mwalimu, lakini wawapo nje ya darasa ni wale wavuta bangi wakuu.
ni unafiki wa mkapa uliomfunika mwalimu asijue kuwa huyu alikuwa chui ndani ya ngozi ya mwanakondoo. ni yeye aliyemfuata mwalimu usiku kumtonya kuwa akina njelu kasaka na wenzake walikuwa wanapeleka hoja ya serikali tatu bungeni. na nyie aliyehariri kwa siri kitabu cha mwalimu UONGOZI WETU NA HATIMA YA TAIFA LETU.
mrema ni tofauti kidogo, ni mwanasiasa asiye mnafiki. asiye weza kuficha hasira yake(mfano : nikichaguliwa kuwa rais ccm watakunywa maji na karai), asiyeweza kufucha furaha yake hata kama kwa kufanya hivyo kutamfanya awe kituko, mfano, alifurahia wazi wazi na kutamka wazi wazi kuwa, yule mbunge wa mchinga mudhiri m. mudhihir ambaye alikatika mkono kwa ajali muda mfupi, baada ya kumshambulia zito kabwe bungeni , alipata adhabu ya mwenyezi mungu.
mrema pia hawezi kuficha hudhuni yake, akiugua kisukari anasikitika wazi wazi. sifa hizi zilitosha kumpa signal mwalimu na kumwelewa kirahisi kuliko mkapa