Jokakuu,
Shukran kubwa mkuu umerudia hoja ambayo kwa miaka karibu mitano nimekuwa nikijibu na wala sintapotosha maelezo yangu ya awali..na pengine nitajaribu kutumia mtindo wa Mzee mwanakijiji ambaye kakupa maelezo yake kulingana na ufahamu wake..
sasabasi ngoja nianze na kipengele cha kwanza, kumbuka tu mimi sifanyi theories ambazo zinabuniwa hapa kutafuta sababu ya kunyoosha kidole bali ni reality na hali halisi iliyotokea..
Mkuu unachoshindwa kuelewa ni kwamba Nyerere alitawala kwa miaka 23, hivyo huwezi pima maisha ya viwanda nchini kwa kutazama miaka minne 4 ya mwisho..
Sikubaliani na usemi wa wengi kwamba viwanda hivi vilijengwa tukiwa hatuna wasomi, mkuu hili sio kweli kwa sababu Nyerere alihakikisha vijana wanakwenda soma ndani na nje kupata ujuzi ktk kila kiwanda alichojenga. Hawa wazee wetu, kaka zetu, wajomba zetu wengi leo hii watakwambia alisoma Israel, Urusi, Cuba, Uturuki, Uk, Marekani, France na hata Canada tena vyuo vya hali ya juu sana na wote hawa waulize vizuri upate kujua walisomea kitu gani... utakuta specific kwa kile Mwalimu alichotaka kujenga nchini.
Kifupi hata wapishi wa TRC ama Hotel zetu wote walisoma nje..hata watandika vitanda walisoma nje..Madaktari wakubwa wote leo hii Bongo wamesomeshwa na Mwalimu, hata Ma lawyer wazuri ni wale wa mwalimu kwa sababu leo hii hakuna mtu binafsi kama sio fisadi anaweza kulipia ada ya shule alizotupeleka mwalimu.. hii ni fact sifanyi kuzusha!...
The downside ya hoja yako kwa hawa wasomi wetu ni kwamba hawahawa aliyewaamini ndio leo wamekuwa mafisadi!..sasa kama kosa ni kuwapa elimu hapo nipo nawe hata hivyo yeye hakuwa mtume kuyajua yote haya..
Mimi naamini kabisa kwamba kwa asilimia ya wasomi wetu Nyerere alipeleka wanafunzi nje zaidi ya kiongozi yeyote ktk Utawala uliomfuatia, leo hii vijana wengi wanakwenda nje kusomea lugha Kiingereza wengine hizo Open Univesiuty na College mabzo hata UK ama USA kwenyewe hazifahamiki.. zaidi ya kuitwa community college utafikiri za misaada ya IMF, Tofauti kabisa na wakati wa mwalimu na pengine naweza kusema ndio viongozi wetu wa leo hii ktk nafasi zote kubwa.
Viwanda vyote toka Urafiki, UFI, Bandari, Tenesco - tulicheza Mbowe hadi asubuhi hakuna kukatiwa umeme, hizo Posta, Bima, ATC zote zilikuwepo na zikifanya kazi vizuri sana na vijana wote wa mjini ndiko tulifanya kazi.
- Tatizo kubwa la mfumo wa Ujamaa ilikuwa miradi yote hii ni kwa sababu ya matumizi ya ndani zaidi ya kusafirisha nje kwa sababu SIASA za wakati wa Mwalimu ziliambatana na uchumi wa nchi..
Nitarudia kusema kwamba wakati wa Nyerere hapakuwepo na hii kitu UTANDAWAZI!.. inaopnyesha watu wengi mnasahau hili kwamba Tanzania kwa kujikita Na nchi za mashariki Kisiasa moja kwa moja tulitangaza kufungwa kwa milango mikubwa ya kibiashara...
Pamoja na makosa yote ya Mugabe, nitasema hakuna kiongozi yeyote anayeweza kucheza Kiuchumi Zimbabwe bila kuwepo suluhu ya Kisiasa kuhusiana na ardhi za wazungu. Huko Gaza, Palestina hakuwezi kuwepo suluhu yoyote kiuchumi kama wataendelea kutoitambua Israel...
Kwa hiyo, makosa ya Nyerere makubwa yanaweza kuwa yamesababishwa na kwanza Kutaifisha mali za watu na kisha kujitangaza kuwa sisi ni Wajamaa jambo ambalo alikatazwa na kina Mtei..Hii ikiwa na maana kujitangaza tu kuwa sisi ni Wajamaa tayari alikwisha weka doa. Hivi vitu viwili ndio vimekuwa sumu ya Ubepoari na hasa nchi za magharibi kwani ukitazama nchi zote za Kijamaa ziliyafanya haya na ndio ugonvi mkubwa ulipotokea kati ya wanamapinduzi dhidi ya nchi hizi za magharibi..Tuliyaona Cuba na sasa hivi tunayaona Venezuela..
Mku unaponiuliza mimi kuhusu mazingira hayo sijui nikwambie kitu gani maanake hapa leo hii mada kibao zinambana Kikwete hali yeye kuyakuta mazingira hayo...
Nitasema hivi wizi wa vipuli umetokana na RUKSA! miaka mitano ya kwanza ya utawala wa Mwinyi hapakuwepo na wizi huo.. meaning Nyerere kisha ondoka miaka mitano ndio tuklaanza kuona vifo vya viwanda vyetu, sasa nambie huyo Mwinyi kwa zaidi ya miaka mitano alikuwa bado hawezi kurekebisha kitu?... na inakuiwaje leo tunamlaumu Kikwete ambaye yupo madarakani miaka miwili tu.
Mkuu changes zinaweza fanya na kiongozi ktk siku 100 tu kama tunavyoona huko Cuba leo hii..Na sio huyu Mwinyi aliyewapeleka waziri wa mabo ya ndani na mkuu wa majeshi kumuuliza mwalimu kwa nini anazungumza na wapinzani kina Mrema na Seif Hamad?..hadi akataka kurudisha kadi ya chama.. who else can do that!..
Mkuu hapa ndipo unapokosea, haya mashirika yangeshindana na nai katika Uzalishaji ikiwa mwenye mali ni huyo huyo?..Pili soko lipo ndani ya nchi na sio nje kutokana na masharti hayo ya standard na kadhalika ambayo yalitawaliwa sana na kutazama msimamo wa nchi kisiasa...
Miaka ya kati hadi mwisho wa 70's unajua bia yetu safari iliwahi kuibuka na gold medal kama bia bora ktk maonyesho ya bia Ujarumani?.. Mvinyo wetu wa Dodoma uliwahi kushinda vile vile lakini kutokana na siasa zetu milango ilikuwa imefungwa, zaidi tuliachiwa kidirisha cha kutuwezesha kukopa tusije kufa kwa njaa....
Mkuu hata Ulaya Union pamoja na Taasisi za wafanyakazi huingilia kati maamuzi ya kitaalam pale kwenye haki..Kwa maoni yako basi sionmi hata haja ya kuwepo Polisi maanake nao huingilia sana maamuzi ya wataalam ktk Ufisadi na Ujambazi..maanake wakati wa Nyerere hawa wataalam walitaka kutumia sana nafasi zao hata kutoa ajira. Leo hii, mwanamke kama hatoi vitu kesho kazi hana na hana pa kwenda! huu utaalam ni utaalam gani unaohusiana na watu badala ya kazi...
Nitasema hivi, mkosa ya mwalimu ktk kazi yalihusiana na MISHAHARA..lakini sio iliyosababisha kuanguka kiuchumi ama kuanguka kwa viwanda hivi isipokuwa ulikuwa mtaratibu mbaya sana kiasi kwamba watu walikuwa wakifanya kazi masaa labda manne 4 kwa siku. Watu walikuwa wakilala kazi kila siku kusingizia magonjwa na hapakuwepo na utaratibu wa kuhakikisha Uzembe na Upuuzaji kazi utapigwa vita hadi tukajenga Utamaduni huo wa Uzembe na Upuuzi.
za mafisadi..Najua kabisa aliyelitengezeza deal hilo... labda nikupe hint (ex balozi wetu huko South).. Kwa hiyo bado unarudia pale pale kuwa hatungeweza kufanya kitu tofauti ikiwa kiwanda cha bia ni mali ya serikali...na huna Mtanzania hata mmoja aliyewekesha ktk bia kabla ya Uhuru..Jambo jingine ni kwamba leo hii kuna wanywaji bia mara tatu ya miaka ya mwalimu soko limeongezeka..hivyo demand ya bia imekuwa kubwa sana kiasi kwamba miaka ile ya mwalimu bia ilikuwa sii hivyo.. Mchagga alkitamani Mbege yake zaidi ya bia labda tu iwe baada ya chakula. Leo hii hata Gongo lina wateja kuliko wakati wowote ule hata Konyagi ambayo ilikuwa haina soko ndani wala nje pmaoja na kwamba ilikuwa ikisafirishwa nje toka enzi za mwalimu,sasa ni hadithi nyingine kabisa...hivyo basi tunarudi palepale ktk Demand na Supply. Ukiwambia Mwalimu leo Gold ni dollar 1000 kwa ounce anaweza omba arudi kutawala Tanzania...na pengine furaha na kicheko kikubwa kiasi kwamba malaika wanamshangaa kufikiria katuachia mtaji safi.
Haya ni mawazo yako kwa sababu tayari jibu ni kwamba - Tuli fail kiuchumi...
sababu ni nyingi sana tena zinaambatana na sisi wenyewe kuwa Wazembe na Wapuuzi kama tunavyopuuza leo maswala ya Mafisadi, kesho tutakuja mnyooshea tena mkono mwalimu... Kwa mtaji huu tuta fail tena na hapo wengine tutaanza kumtafuta sijui Mkapa na FIKRA zake za UWAZI na Globolization kuwa ndio sababu ya sisi kushindwa tena...
Shukran kubwa mkuu umerudia hoja ambayo kwa miaka karibu mitano nimekuwa nikijibu na wala sintapotosha maelezo yangu ya awali..na pengine nitajaribu kutumia mtindo wa Mzee mwanakijiji ambaye kakupa maelezo yake kulingana na ufahamu wake..
sasabasi ngoja nianze na kipengele cha kwanza, kumbuka tu mimi sifanyi theories ambazo zinabuniwa hapa kutafuta sababu ya kunyoosha kidole bali ni reality na hali halisi iliyotokea..
..kiwanda kikijengwa halafu hata kisizalishe kinaweza kuwa ni hasara kuliko kisingejengwa kabisa.
Mkuu unachoshindwa kuelewa ni kwamba Nyerere alitawala kwa miaka 23, hivyo huwezi pima maisha ya viwanda nchini kwa kutazama miaka minne 4 ya mwisho..
Sikubaliani na usemi wa wengi kwamba viwanda hivi vilijengwa tukiwa hatuna wasomi, mkuu hili sio kweli kwa sababu Nyerere alihakikisha vijana wanakwenda soma ndani na nje kupata ujuzi ktk kila kiwanda alichojenga. Hawa wazee wetu, kaka zetu, wajomba zetu wengi leo hii watakwambia alisoma Israel, Urusi, Cuba, Uturuki, Uk, Marekani, France na hata Canada tena vyuo vya hali ya juu sana na wote hawa waulize vizuri upate kujua walisomea kitu gani... utakuta specific kwa kile Mwalimu alichotaka kujenga nchini.
Kifupi hata wapishi wa TRC ama Hotel zetu wote walisoma nje..hata watandika vitanda walisoma nje..Madaktari wakubwa wote leo hii Bongo wamesomeshwa na Mwalimu, hata Ma lawyer wazuri ni wale wa mwalimu kwa sababu leo hii hakuna mtu binafsi kama sio fisadi anaweza kulipia ada ya shule alizotupeleka mwalimu.. hii ni fact sifanyi kuzusha!...
The downside ya hoja yako kwa hawa wasomi wetu ni kwamba hawahawa aliyewaamini ndio leo wamekuwa mafisadi!..sasa kama kosa ni kuwapa elimu hapo nipo nawe hata hivyo yeye hakuwa mtume kuyajua yote haya..
Mimi naamini kabisa kwamba kwa asilimia ya wasomi wetu Nyerere alipeleka wanafunzi nje zaidi ya kiongozi yeyote ktk Utawala uliomfuatia, leo hii vijana wengi wanakwenda nje kusomea lugha Kiingereza wengine hizo Open Univesiuty na College mabzo hata UK ama USA kwenyewe hazifahamiki.. zaidi ya kuitwa community college utafikiri za misaada ya IMF, Tofauti kabisa na wakati wa mwalimu na pengine naweza kusema ndio viongozi wetu wa leo hii ktk nafasi zote kubwa.
Nitarudia kusema kwamba viwanda vyetu na mashirika havikufa hili nalipinga mpaka kesho kwa sababu Mwinyi anaingia madarakani mimi niko Bongo..viwanda vya nguo vyote toka Urafiki hadi Mutex..vilikuwa vikifanya kazi tena jamaa yangu marehemu sasa (Ismail) alipatia Utajiri wake pale Mwanza kwa kuuza kanga za Mwatex na Mutex...hebu tueleze sababu zilizopelekea viwanda hivi kujengwa na kufa mara moja. je, maamuzi gani ya serikali ya Baba wa Taifa yalisababisha hilo?
Viwanda vyote toka Urafiki, UFI, Bandari, Tenesco - tulicheza Mbowe hadi asubuhi hakuna kukatiwa umeme, hizo Posta, Bima, ATC zote zilikuwepo na zikifanya kazi vizuri sana na vijana wote wa mjini ndiko tulifanya kazi.
- Tatizo kubwa la mfumo wa Ujamaa ilikuwa miradi yote hii ni kwa sababu ya matumizi ya ndani zaidi ya kusafirisha nje kwa sababu SIASA za wakati wa Mwalimu ziliambatana na uchumi wa nchi..
Nitarudia kusema kwamba wakati wa Nyerere hapakuwepo na hii kitu UTANDAWAZI!.. inaopnyesha watu wengi mnasahau hili kwamba Tanzania kwa kujikita Na nchi za mashariki Kisiasa moja kwa moja tulitangaza kufungwa kwa milango mikubwa ya kibiashara...
Pamoja na makosa yote ya Mugabe, nitasema hakuna kiongozi yeyote anayeweza kucheza Kiuchumi Zimbabwe bila kuwepo suluhu ya Kisiasa kuhusiana na ardhi za wazungu. Huko Gaza, Palestina hakuwezi kuwepo suluhu yoyote kiuchumi kama wataendelea kutoitambua Israel...
Kwa hiyo, makosa ya Nyerere makubwa yanaweza kuwa yamesababishwa na kwanza Kutaifisha mali za watu na kisha kujitangaza kuwa sisi ni Wajamaa jambo ambalo alikatazwa na kina Mtei..Hii ikiwa na maana kujitangaza tu kuwa sisi ni Wajamaa tayari alikwisha weka doa. Hivi vitu viwili ndio vimekuwa sumu ya Ubepoari na hasa nchi za magharibi kwani ukitazama nchi zote za Kijamaa ziliyafanya haya na ndio ugonvi mkubwa ulipotokea kati ya wanamapinduzi dhidi ya nchi hizi za magharibi..Tuliyaona Cuba na sasa hivi tunayaona Venezuela..
Pia kama kiwanda kinazalisha na wafanyakazi wanakitegemea kwa maisha yao hawawezi kuanza kuiba vipuri. kwa msingi huo yapo mazingira yaliyosababisha wafanyakazi wakose nidhamu kiasi hicho. sasa mazingira hayo yalisababishwa na siasa za Baba wa Taifa, au Mzee Mwinyi?
Mku unaponiuliza mimi kuhusu mazingira hayo sijui nikwambie kitu gani maanake hapa leo hii mada kibao zinambana Kikwete hali yeye kuyakuta mazingira hayo...
Nitasema hivi wizi wa vipuli umetokana na RUKSA! miaka mitano ya kwanza ya utawala wa Mwinyi hapakuwepo na wizi huo.. meaning Nyerere kisha ondoka miaka mitano ndio tuklaanza kuona vifo vya viwanda vyetu, sasa nambie huyo Mwinyi kwa zaidi ya miaka mitano alikuwa bado hawezi kurekebisha kitu?... na inakuiwaje leo tunamlaumu Kikwete ambaye yupo madarakani miaka miwili tu.
Mkuu changes zinaweza fanya na kiongozi ktk siku 100 tu kama tunavyoona huko Cuba leo hii..Na sio huyu Mwinyi aliyewapeleka waziri wa mabo ya ndani na mkuu wa majeshi kumuuliza mwalimu kwa nini anazungumza na wapinzani kina Mrema na Seif Hamad?..hadi akataka kurudisha kadi ya chama.. who else can do that!..
NB:
..kwa maoni yangu kulikuwa na siasa nyingi ktk uendeshaji wa viwanda, mashirika,na uchumi kwa ujumla.
..badala ya kushindana ktk uzalishaji mashirika yalikuwa yakishindana kwa vikundi vya ngoma, timu za mpira na netiboli, kwaya, matawi ya chama na juwata.
..pia kulikuwa na mashindano ya kudhamini shughuli za chama na serikali.
..viongozi wa chama na serikali walikuwa hawaishi kutafuta fadhila na zawadi toka kwa wakuu wa mashirika ya umma.
Mkuu hapa ndipo unapokosea, haya mashirika yangeshindana na nai katika Uzalishaji ikiwa mwenye mali ni huyo huyo?..Pili soko lipo ndani ya nchi na sio nje kutokana na masharti hayo ya standard na kadhalika ambayo yalitawaliwa sana na kutazama msimamo wa nchi kisiasa...
Miaka ya kati hadi mwisho wa 70's unajua bia yetu safari iliwahi kuibuka na gold medal kama bia bora ktk maonyesho ya bia Ujarumani?.. Mvinyo wetu wa Dodoma uliwahi kushinda vile vile lakini kutokana na siasa zetu milango ilikuwa imefungwa, zaidi tuliachiwa kidirisha cha kutuwezesha kukopa tusije kufa kwa njaa....
.Matawi ya chama na Juwata yaliwaingilia Mameneja ktk kufanya maamuzi ya kitaalamu
Mkuu hata Ulaya Union pamoja na Taasisi za wafanyakazi huingilia kati maamuzi ya kitaalam pale kwenye haki..Kwa maoni yako basi sionmi hata haja ya kuwepo Polisi maanake nao huingilia sana maamuzi ya wataalam ktk Ufisadi na Ujambazi..maanake wakati wa Nyerere hawa wataalam walitaka kutumia sana nafasi zao hata kutoa ajira. Leo hii, mwanamke kama hatoi vitu kesho kazi hana na hana pa kwenda! huu utaalam ni utaalam gani unaohusiana na watu badala ya kazi...
Nitasema hivi, mkosa ya mwalimu ktk kazi yalihusiana na MISHAHARA..lakini sio iliyosababisha kuanguka kiuchumi ama kuanguka kwa viwanda hivi isipokuwa ulikuwa mtaratibu mbaya sana kiasi kwamba watu walikuwa wakifanya kazi masaa labda manne 4 kwa siku. Watu walikuwa wakilala kazi kila siku kusingizia magonjwa na hapakuwepo na utaratibu wa kuhakikisha Uzembe na Upuuzaji kazi utapigwa vita hadi tukajenga Utamaduni huo wa Uzembe na Upuuzi.
Unaendelea kusahau kwamba mazingira ya biashara duniani wakati wa mwalimu na leo hii ni tofauti sana. Kisha wakati kaburu anaingia kampuni yetu ya Bia haikuwa imekufa wala imeingiza hasara isipokuwa ni kati ya asilimia 10Wengi tunashangaa kwanini kaburu ameweza kuendesha TBL. tunasahau kwamba ameondokana na vikundi vya sanaa, timu za mpira,juwata etc etc.
za mafisadi..Najua kabisa aliyelitengezeza deal hilo... labda nikupe hint (ex balozi wetu huko South).. Kwa hiyo bado unarudia pale pale kuwa hatungeweza kufanya kitu tofauti ikiwa kiwanda cha bia ni mali ya serikali...na huna Mtanzania hata mmoja aliyewekesha ktk bia kabla ya Uhuru..Jambo jingine ni kwamba leo hii kuna wanywaji bia mara tatu ya miaka ya mwalimu soko limeongezeka..hivyo demand ya bia imekuwa kubwa sana kiasi kwamba miaka ile ya mwalimu bia ilikuwa sii hivyo.. Mchagga alkitamani Mbege yake zaidi ya bia labda tu iwe baada ya chakula. Leo hii hata Gongo lina wateja kuliko wakati wowote ule hata Konyagi ambayo ilikuwa haina soko ndani wala nje pmaoja na kwamba ilikuwa ikisafirishwa nje toka enzi za mwalimu,sasa ni hadithi nyingine kabisa...hivyo basi tunarudi palepale ktk Demand na Supply. Ukiwambia Mwalimu leo Gold ni dollar 1000 kwa ounce anaweza omba arudi kutawala Tanzania...na pengine furaha na kicheko kikubwa kiasi kwamba malaika wanamshangaa kufikiria katuachia mtaji safi.
Nitarudia kusema kwamba mwalimu alitengeneza viwanda ktk stage ya kwanza ambayo ilikuwa kwanza kutosheleza matumizi yetu sisi wenyewe kabla hatujafikiria kuingia ktk soko la mashindano, hivyo ilikuwa ni kutujenga sisi zaidi kuelewa ufundi wa vitu hivi kama walivyokuwa wakifanya China. Biashara wasn't a main objective isipokuwa kuunda jeshi la kiuchumi ambapo viwanda hivyo vilikuwa kama ndio silaha. Mwanajeshi kubeba silaha sii lazima awe vitani laa anajifunza namna ya kuitumia kwanza (kama unakumbuka tulisema Muingereza alituacha sisi watupu bila elimu wala viwanda hivyo hatungeweza kuingia sokoni ghfla bin vuuu tukitegemea kuuza mali iliyotengenezwa na wanafunzi...Mameneja walikuwa hawaruhusiwi kupunguza wafanyakazi hata kama kiwanda/shirika limelemewa.
..Sasa ukichanganya chama kushika hatamu[sera za Baba wa Taifa], under-capitalization ya mashirika yetu, utaona kwamba we were bound to fail.
Haya ni mawazo yako kwa sababu tayari jibu ni kwamba - Tuli fail kiuchumi...
sababu ni nyingi sana tena zinaambatana na sisi wenyewe kuwa Wazembe na Wapuuzi kama tunavyopuuza leo maswala ya Mafisadi, kesho tutakuja mnyooshea tena mkono mwalimu... Kwa mtaji huu tuta fail tena na hapo wengine tutaanza kumtafuta sijui Mkapa na FIKRA zake za UWAZI na Globolization kuwa ndio sababu ya sisi kushindwa tena...
Kwa hiyo leo hii tunavyo fail pamoja na kwamba tunafuata mashauri ya hao wajuzi waliomshauri mwalimu enzi hizo bado utasema nini?...ama ktk kamusi yenu mtu akisha fail hawezi tena kuamka ndio tumeshakuwa doomed!Ukweli utabaki kwamba Baba wa Taifa alielezwa mazingira yaliyolikabili taifa, na maamuzi aliyopaswa kuchukua. alikataa ushauri ambao unaashria ungetusaidia. matokeo yake ni kuanguka kwa mashirika na uchumi wetu kwa jumla.
..kwa msingi nasema Mwalimu alifanya makosa na anastahili lawama.