1. Mwalimu alichemsha big time kumchagua Mkapa kuwa rais wetu, period! Kwa sababu records zipo very clear kuwa Mkapa alipokuwa Elimu ya Juu, alihusika sana na rushwa na maovu, against wananchi Mwalimu alijua haya kwa sababu aliwezaje kujua ya Lowassa, aliyekuwa waziri kama Mkapa na katika serikali moja ya Mwinyi? Waliokuwa wanampa habari za Lowassa, pia walimpa na habari za Mkapa, lakini kwa makusudi akaamua kuangalia upande mwingine, kwa sababu alimtaka Mkapa kwa manufaa yake binafsi kwanza, ambayo Mwinyi na kundi lake walikuwa wameanza kuyakata.
Na tukimpa akiboronga tutamlaumu Nyerere.... ?Salim Ahmed Salim.
Comment..........
Nami pia naamini mkapa alikuja kubadilika (sidhani kama alikuwa kaficha makucha yake). Mkapa alikuwa na 'both power and authority'. Angeweza kutuletea maendeleo makubwa Watanzania, kama Nyerere alivyotarajia, angetumia vipawa vyake hivyo alivyokuwa navyo.
in 20/20 vitu vingi kweli tusingevifanya
- Tusingepata Uhuru 1961 tungekubali kutawaliwa kwa muda kidogo angalau hadi 1980
- Tusingeungana na Zanzibar
- Tusingeanzisha siasa za kutofungamana na upande wowote
- Tusingetangaza Azimio la Arusha
- Tusingepigana vita na Amini
- Tusingerudisha mfumo wa vyama vingi
- Nyerere angejiuzulu mapema zaidi kama 1971 hivi
- Tusingepinga utawala dhalimu wa makaburu
- Mwingi asingekuwa Rais
- Warioba asingekuwa Waziri Mkuu
- Salimu asingekuwa Waziri Mkuu
- Msuya asingekuwa Waziri Mkuu
- Malecela asingekuwa Waziri Mkuu
- Sumaye asingekuwa Waziri Mkuu
- Tusingefanya hivi na vile... n.k
Hivyo in hindsight naamini kuna mambo mengi yasingefanyika na kuna watu ambao wasingepata nafasi ya kushika madaraka kabisa... yote hayo ni rahisi kuyahukumu in 20/20.... bahati mbaya even God can not change the past!
Swali: Ni nani kiongozi ambaye tunaweza kumpata leo hii ambaye kwa asilimia 50% tunajua kuwa hatobadilika? Na kiongozi huyo ni yupi ambaye atamfurahisha kila mtu kwa asilimia 100? Nyerere alifariki 1999 na mwaka 2000 Mkapa alichaguliwa tena tuendelee kumlaumu Nyerere? Kuna watu ambao pia wamejaribu kumbebesha Nyerere mzigo wa Kikwete na sitoshangaa akija Rais Mpya Slaa au Seif na wenyewe wakaboronga huko mbeleni watetezi wa 20/20 watatuambia "Ni Nyerere ndiye aliyetufanya tuwachague".
Naomba yeyote mwenye uhakika kuwa kuna kiongozi ambaye tunaweza kumuaminisha Taifa letu na ya kwamba hatoharibu au hatofanya jambo lolote kwa maslahi yake au ya watu wa karibu yake na tukamuamini hivyo kwa asilimia 100. Nionesheni na miye nitaanza kumpigia debe!!! Mmoja tu.
I wish Lyatonga angeshinda 1995 maana mzee wa kiraracha naamini angesafisha hizi tabia za kifisadi na leo tungekuwa na true democracy na ningekuwa labda upande wa CCM mana CCM wangekuwa ni watu wenye akili
Kilichokuja kumbadili Mkapa nadhani ni baada ya Mwalimu kufariki na mchango binafsi wa FAMILIA yake kama anavyoteseka Mugabe sasa hivi. Mengine yatabaki kuwa ni historia.
See, this is what I'm talking about!! Tell them man...tell them....Lol
Kwanza, mpaka hapo alipokuwa anampendekeza Mkapa alikuwa poa kabisa. Mkapa alibadilika second term ndiyo ushetani wa hela ukamuingia
Pili, Kubadilika kwa Mkapa ilikuwa nje ya control ya Nyerere.
Tatu, katika wagombea wa 1995 ndani ya CCM, Mkapa was the best choice and was the least devil
Nne, hata leo, kwa CCM Mkapa is far better than the current ruling cligue members. In fact, mimi ukiniambia nichague kati ya Mkapa na JK, nitamchagua Mkapa kwa kuweka tick nyingi sana.
My conclusion: Kwa kuzingatia kwamba ilikuwa lazima achague/apendekeza mgombea kutoka CCM na raia wa Tanzania aliyepo Tanzania, Nyerere hakuchemka hata kidogo- he was more tha right kumsukumiza Mkapa kwenye urais!
Stop just cheering man, you got a brain, use it.
Taifa Stars ilipoifunga Burkina Faso kwao,kila mtu alisema kuwa kocha tunae.Ilipotoa draw na Senegal Mwanza,ndio kabisa tukaona kuwa kombe la dunia tunaenda,wacha hio AFCON! Hapa juzi ilipochemsha mechi mbili za mwanzo wengi walisema kocha hafai,wengine kama mimi tulisema tatizo sio kocha ni wachezaji.Na hilo likaja kudhihirika kwenye mechi mbili vs Cameroon.Kocha haingii katika akili ya mchezaji,anamsoma kutokana na bidii yake ya mazoezi mentality yake na character pia.Lakini mchezaji anapovuka ule mstari na kuingia uwanjani,ni yeye na Mungu wake.Mwalimu ndivyo alivyoona kwa Mkapa
Nothing indeed...!!??
Just thinking aloud;
- Kwa wale wanaokubali kuwa Mkapa alifanya kubadilika baadaye, je kuna alama zozote hivi sasa tukiangalia nyuma tunaziona ambazo tunaweza kuzitumia kumdadisi muungwana aliye kitini?
- Are the pouses key to ufisadi wa Ikulu, Sitti and Anna for example, or the husbands are just hidding behind wake zao?
- If the prez is constitutionally somewhat immune from prosecution, kwa nini tusiende after wake zao na ndugu wao wengine ambao hawana veto ya katiba?
So what the hell is your problem and who the hell do you think you are to tell me (how) to use my brain?
katika uongozi wake wote Mwalimu alikuwa halali usingizi mzuri kwa kuwaza matatizo ya wananchi....Alijitahidi kwa kadri ya uwezo wake kama binadamu kuingoza nchi si kwa manufaa yake wala ya familia yake na hili nadhani hata wasiokubali juhudi zake, hakuna anayeweza kulipinga. Kwa hiyo tunapomuhukumu, tuzingatie kwamba ni vigumu mno katika nchi zetu hizi masikini, kupata kiongozi ambaye kwa dhati kabisa anaweza akaweka maslahi yake pembeni na kujali yale ya wananchi anaowaongoza, kwa asilimia mia kwa mia.