Mkandara said:
Ukisema hivyo basi kuna kila haki ya kusema aliye fail ni kati ya Mwarabu, Mjarumani, Muingereza maana hata mwalimu alikuta uchumi mbaya..
..I am open to that debate.
..kukusaidia, mkoloni Mngereza ali-invest kidogo sana ktk masuala ya elimu. Baba wa Taifa alikuja kubeba mzigo wa kuwa na taifa lisilo na Wataalamu kutokana na utawala mbaya wa kikoloni..
Mkandara said:
Hivi viwanda mkuu vilikuwa ndio kwanza vimejengwa... hata uwanja wa ndege kabambe la Uingereza limeshindwa kufanya kazi siku za mwanzo na technologia yote hiyo..
Ni uongo na uzushi mkubwa kuwa viwanda hivi vilikufa tazama list ya mali zote tulizouza kisha unambie kilichofa ni kipi, Vilikufa wakati wa Mwinyi, tulipoanza kuiba vipuri na kuviuza nje kama wanavyofanya RITTES, hata magari ya Polisi na mabasi ya UDA, transifoma za umeme na kadhalika.. mkuu tulikuwa Bongo katikati ya maswala haya yakitokea.
..kiwanda kikijengwa halafu hata kisizalishe kinaweza kuwa ni hasara kuliko kisingejengwa kabisa.
..hebu tueleze sababu zilizopelekea viwanda hivi kujengwa na kufa mara moja. je, maamuzi gani ya serikali ya Baba wa Taifa yalisababisha hilo?
..pia kama kiwanda kinazalisha na wafanyakazi wanakitegemea kwa maisha yao hawawezi kuanza kuiba vipuri. kwa msingi huo yapo mazingira yaliyosababisha wafanyakazi wakose nidhamu kiasi hicho. sasa mazingira hayo yalisababishwa na siasa za Baba wa Taifa, au Mzee Mwinyi?
NB:
..kwa maoni yangu kulikuwa na siasa nyingi ktk uendeshaji wa viwanda, mashirika,na uchumi kwa ujumla.
..badala ya kushindana ktk uzalishaji mashirika yalikuwa yakishindana kwa vikundi vya ngoma, timu za mpira na netiboli, kwaya, matawi ya chama na juwata.
..pia kulikuwa na mashindano ya kudhamini shughuli za chama na serikali.
..viongozi wa chama na serikali walikuwa hawaishi kutafuta fadhila na zawadi toka kwa wakuu wa mashirika ya umma.
..Matawi ya chama na Juwata yaliwaingilia Mameneja ktk kufanya maamuzi ya kitaalamu.
..wengi tunashangaa kwanini kaburu ameweza kuendesha TBL. tunasahau kwamba ameondokana na vikundi vya sanaa, timu za mpira,juwata etc etc.
..Mameneja walikuwa hawaruhusiwi kupunguza wafanyakazi hata kama kiwanda/shirika limelemewa.
..sasa ukichanganya chama kushika hatamu[sera za Baba wa Taifa], under-capitalization ya mashirika yetu, utaona kwamba we were bound to fail.
..ukweli utabaki kwamba Baba wa Taifa alielezwa mazingira yaliyolikabili taifa, na maamuzi aliyopaswa kuchukua. alikataa ushauri ambao unaashria ungetusaidia. matokeo yake ni kuanguka kwa mashirika na uchumi wetu kwa jumla.
..kwa msingi nasema Mwalimu alifanya makosa na anastahili lawama.