Mwalimu Nyerere alikuwa hawezi kukaa meza moja na mtu anayempa changamoto. Hii ilimfanya awafukuze hata wasomi kadhaa ambao tulikuwa nao mara baada ya uhuru kwa kuwa tu walionyesha kumpa changamoto.
Sasa na wewe unakuja na kauli ambayo inatakiwa ichukuliwe kama factual. Ni wasomi gani "kadhaa" ambao tulikuwa nao baada ya uhuru na walifukuzwa kwa kumpa "changamoto". Na kuna ukweli gani kuwa Nyerere hakuweza "kukaa meza moja" maana sisi wengine tunakumbuka sana mijadala ya Chuo Kikuu ambayo hata Kikwete hawezi hata dakika moja kwenda pale Nkrumah (well anaweza baada ya kumuweka Mukandala)...
Mwalimu alivijenga vyama vya siasa alivyoanzisha kwa mtindo ambao vingemheshimu na kumtii bila kuhoji alichofanya wala kutengua anachopanga.
Once again, vyama vya kisiasa alivyovianzisha. Hivi hujui kuwa kuna watu walimpinga na kuna maamuzi yaliyobadilishwa? Inabidi urudi kwenye historia tu usiwe kama mtu mmoja humu anayetoa kauli za kuhukumu bila ushahidi wowote japo wa mantiki.
CCM ya sasa inasemwa sana kuwa imeacha mwenendo wa Nyerere. Mimi nikuhakikishieni kuwa CCM imeacha tu mwelekeo wa kijamaa wa Nyerere. Lakini tabia za kuhodhi madaraka, kujiona miungu watu, siasa za kulindana, kupeana madaraka kwa fadhila, chuki na hujuma dhidi ya upinzani, ukabila wa kichini chini, siasa kuamua namna uchumi wa nchi utakavyoendeshwa na mengi mengi yanayotokea sasa yalizaliwa enzi za uongozi wa Nyerere. Kwa hiyo udhaifu wa CCM wa sasa hauwezi kutengwa kabisa na Mwl. Nyerere.
Kuna uliyoyasema hapa ambayo naamini yana ushawishi wa ukweli. Hata hivyo madai ya rejareja kama tabia kadhaa zinazoendelea sasa ni matokeo ya Nyerere kunathibitisha vitu vichache; moja hakuna kiongozi ndani ya CCM ambaye yuko mbali na mweleko wa "kinyerere". Lakini hilo la kudai kuwa "siasa kuamua namna ya uchumi wa nchi unavyoendeshwa" ni mojawapo ya madai yasiyo na msingi. Dunia nzima ni siasa ndiyo inayoamua namna ya uchumi wa nchi unavyoendeshwa na ni wanasiasa wanaoamua nchi inaendeshwaje.
"Mti hutambuliwa kwa matunda yake"
Mwalimu alipanda mti, akaunyeshea, akaulinda usiharibiwe na yeyote. mti ukakua. Na sasa unazaa matunda. Sasa kama matunda yake ni machungu kwa nini mnajitahidi kuonyesha kuwa huo mti haukupndwa na mtu mzuri msiyetaka achafuliwe?? Mwembe huzaa maembe: Mpapai huzaa mapapai. Mchungwa huzaa machungwa. Ukiona ndimu basi limetokana na Mndimu na si Mwembe. Kama Mwl alitaka Maembe asingepanda mti wa ndimu. HAKWEPI LAWAMA HAPA!!
Mfano mzuri sana hapa, tatizo ni kuwa mti hukua unapopandwa! kama udongo hauna rutuba na hata mtu akitumia mbinu gani wakati mwingine mti haukui! Lakini wakati mwingine mtu anaweza akapanda vizuri mti wake lakini "akaja adui naye akapenda magugu"!
Inawezekana ndugu zangu ninyi hamna hata habari kuwa asili ya kushindikana kwa zoezi la kutengeneza katiba muafaka kwa mazingira ya siasa ya vyama vingi Tanzania ni Mwl. Nyerere.
Wewe unayejua utuambie miaka karibu nane tangu afe na ishirini na ushee tangu aachie madaraka mbona tumeshindwa. Na nikuhakikishie kwa kuendelea kumlaumu Nyerere usitarajie Katiba mpya. Angalia mada moja hapa inayomhusu mama Nagu aliyesema mwaka jana kuwa "hakuna haja ya Katiba mpya". Nyerere alimpanua mdomo kusema? Muulize kiongozi yeyote wa CCM akuambie kama ipo haja ya Katiba mpya...!
Na inawezekana pia kuwa hamjui kuwa katiba yetu inatoa mianya kwa mafisadi kujiporea rasilimali za nchi yetu wanavyoona wenyewe yafaa ili mradi tu wakiimarishe chama cha Mwalimu.
Yote hayo yanajulikana lakini Nyerere hayupo CCM leo; wabebeshe mzigo wahusika. Mwisho mtamlaumu Nyerere kwa Rada, Richmond, Buzwagi, Posta, NBC n.k!
Mngekuwa mnayaona hayo, basi mngegundua pia kuwa umasikini wetu unaanzia kwenye mianya ya katiba na mfumo mbaya wa Siasa na Uchumi wa nchi.
Mbona hayo yote yanajulikana? Tatizo kwanini CCM wanashindwa kubadilisha mambo hayo wakati Nyerere hayupo? Hivi unambebesha Mwinyi, Mkapa, na Kikwete lawama zozote za yale yanayoendelea hivi sasa? Kila mtu hubeba mzigo wake mwenyewe! Hivi mnataka Nyerere atoke kaburini kuja kutueleza kuwa kuua maalbino ni vibaya? Hivi Nyerere atoke kaburini na kutuambia kuna haja ya kujenga mitaro safi ya maji machafu? Unataka Nyerere atoke kaburini na kutuambia kuna haja ya kujenga shule zenye vyoo bora?
Kama binadamu wa kawaida sioni ufahari kumkejeli Mwl. wakati huu ambao hayuko nasi, wala sioni vema kumvunjia heshima mtu ambaye ametangulia mbele ya haki. Kikwetu kila mtu anapotutoka tunamwagia sifa kem kem.
Huo huitwa unafiki; yaani kumpa mtu sifa asizozistahili. Bora uwe kama YNIM kwa sababu yeye hana chema chochote cha Nyerere na hilo tumelikubali. Kama unaona Nyerere alikuwa hivi au vile sema tu usiogope au kumvisha kilemba cha ukoka.
kwa hiyo ndugu yangu uliyeanzisha hoja hii amini kabisa kuwa mimi sina mpango wa kumvunjia heshima Mwalimu bali nataka kukushawishi ujue kuwa matunda tunayokula ya CCM leo yametokana na mti aliopanda Mwl. Na kabla hujaleta hoja jukwaani nakuomba sana uifanyie utafiti. Usilete hoja tukakufikiria kuwa umetumwa na watu wachache. wanaotaka kuharibu ukweli wa historia ya nchi yetu.
Hivi unafikiri Nyerere alianza kuvunjia heshima leo au jana? Ukifanya hivyo utakuwa kwenye msururu wa watu wengine waliotangulia kabla yako na huo ndio uzuri wa uhuru wa maoni.
Nyerere aliupanda mti katika ardhi aliyopewa; aliupanda mti kwa utaalamu aliokuwa nao na kwa kutumia mbinu alizokuwa nao. Mti umekuwa na sasa tunaanza kuvuna matunda yake tunaanza kumlaani mpanzi ati kwa sababu mbona kuna magugu pembeni? Mbona hakung'oa magugu yote, mbona hakutuchumia matunda na kutusindikia; Yaani kwa mawazo yako Nyerere angefanya kila kitu ili wewe na mimi tubweteke na kula jasho la kazi ya Mwalimu!
Hayo ni mawazo ya watu wavivu. Jukumu lako na langu ni kuona wapi mwalimu alishindwa na kutengeneza kuanzia hapo badala ya kulia kuwa "mwalimu alipanda mtu mbovu mbona sasa tunakula matunda mabovu". Kama unaamini mti ulipandwa ni mbaya, ung'oe panda mwingine!
Nyerere asingeweza kupanda, kumwagilia, kutia mbolea, kuhamia ndege n.k halafu baadaye achume mazao na kutuwekea ghalani na tungemwomba atutengenezee chakula na sisi kama makinda yaliyodekezwa tupanue midomo yetu na kula tu! Hivi katika maelezo yako yote hayo Nyerere alikuwa anafanya kazi peke yake? Hivi muda wote huo Nyerere alikuwa anatembea kila kijiji, kila mkoa na kila nyumba kuangalia watu wanatendaje kazi? Ni kwa kiasi gani wasaidizi au watu wenyewe walishindwa kuteleleza majukumu yao? Je hali iliyopo sasa inaweza kuelezewa kuwa ni matokeo ya mchanganyiko wa sababu za mbalimbali na Nyerere ni mojawapo ya sababu hizo? au katika mawazo yako Ni Nyerere tu ndiye mbaya wa Tanzania kama anavyoamini YNIM?
Hata Yesu mwenyewe alishindwa kufikisha ujumbe wake kwa watu wote lakini akawatuma wengine wafanye kazi kwa niaba yake; Vivyo hivyo Mohammed naye ni mpaka alipokufa ndio kiini cha ujumbe aliopewa ndivyo ulivyoenezwa na wafuasi wake. Lakini je ujumbe wa wote wawili umefika leo hii bila kupitia wakati mgumu au hata kugawanyika? Je kwa sababu leo tunaona matatizo katika Ushia au Usunni, Ukatoliki au Uprotestanti maana yake Nyerere na Muhammad ndio waliopanda mbegu mbovu ambazo zimezaa matunda mabovu? Je ni kwa kiasi gani mapadre na watawa wanaolawiti watoto wadogo au maghaidi wanaojilipua na kuua watu bila hatia wanawajibika kwa vitendo vyao wao wenyewe?
Kuna wakati lazima ujifunze kuwajibika kwa matendo yako mwenyewe na vivyo hivyo watu wengine nao wawajibike kwa matendo yao wenyewe.