NSSF tunataka majibu ya tuhuma kuhusu 'udini'

NSSF tunataka majibu ya tuhuma kuhusu 'udini'

Status
Not open for further replies.
Nehemiah Mchechu na Dau wote wawili ni watu waliokosa ubunifu.

Nianze na Mcheche: Nyumba zile ambazo zipo katika maeneo ambayo kodi kwa apartment moja ni $3000+ kwa mwezi kuziuza ni kuua future ya NHC na kuwamilikisha mabepari wachache mji.

Pili, hizo nyumba mnazoziita za gharama nafuu kwa akili ya wenye kipato kidogo hazilingani na mshahara wa mwenye kipato kidogo. Mshahara wa kima cha chini haufikii masharti ya mtu kukopeshwa 48m aweze kununua nyumba ya Mcheche ya tuvyumba tuwili. Kwa hiyo Mchechu hana mtumishi wowowte wa mfano kwa jamii, labda kwa wa chache wenye uwezo wa kukopa mamilioni Benki kwa dhamana na vyeo vyao.

Namna pekee ya mnyonge kuwa na kajumba kake ni kutafuta kiwanja, angalau kile cha high density 400sqm na kuwekeza hapo around 10m utapata kibanda cha kujisetiri.

Ramadhan Dau: anaendesha mfuko wa hifadhi ya serikali. Wakati mifuko mingine ikiwa bize na wellbeing ya members wake, NSSF iko bize na miradi ya serikali. Kwa kuwa walalahoi hawakopesheki kwenye taasisi za fedha basi si vibaya bwana Dau akafanya la maana kwa kuwapa wanachama haki ya kutumia amana zao kama dhamana wanapotaka kukopa ktk taasisi za fedha badala ya kuikopesha serikali tajiri.

Kwa hy, hoja ya fulani na fulani kati ya hao unaowataja hapa ni thuufri.




Kusema ukweli NSSF wametusahau sana wanachama. Hakuna hata issue moja ya kujivunia now kama member, benefit zao zipo chini mno
 
hawa wasio waislam(makafiri) wana tabu kweli!!!!sehemu ikiongozwa na waislamu,utasikia udini,rejea udom.mini nipo chuo cha serikali,malecture woote wanaonifundisha makafiri.utasikia waislaam wamekosa vigezo luwa malecture.ila sehemu ikiwa na waislaam wengi,udini.

Makafiri hawana jema ! ....... unategemea nini kwa mtu aliyemfanya mungu wake sanamu au anaye dai mungu wake kateswa ili yeye akombolewe !
 
Mtoka pabaya,Real Estate ni wigo mpana.
Kuuza apartment ni moja tu ya strategy zao na pia ni beneficial.kumbuka price set huwa imeshaangalia lufe span ya mjengo,na factor nyinginezo.hiyo ni sawa na kusema serikali au kampuni isiuze gari zake bado zinaonekana zinadai,huku maintenance cost imeshakuwa kubwa karibu nusu ya thamani ya gari lenyewe.

Sikusema kuwa kuuza nyumba sio beneficial, yes it is. Is it long term benefit?

Achana na maneno ya vitabuni na milinganisho ya ulaya vilikoandikwa vitabu. Twende kwenye haya mazingira yetu. Sijui wewe unaishi wapi na shughuli zako unafanyia wapi. Wakurugenzi wa kampuni nayoifanyia kazi nyumba walizopangiwa wanalipiwa na kampuni kati ya $5000 na $7000 kwa mwezi. Hii ni kodi ya nyumba moja katika jengo lenye nyumba ya kukaa familia 10 - 20. Managers na expatriates wengine kati ya $3000 na $4500 kulingana na nyadhifa zao.

Kama unazo sentensi za kuniaminisha kuwa biashara ya kuiuza nyumba hii ni nzuri kuliko kuipangisha, basi nayaomba hayo maneno. Lakini katika hali ya kawaida, kwa kuwa shirika hili lilipaswa kuwa endelevu, muda si mrefu (kwa kuwa mji wetu si mkubwa) hakutakuwa na nyumba nyingine ya kuuza kwenye maeneo nyeti. Nikukumbushe kuwa, thamani ya ardhi katika maeneo hayo ndio ilipaswa kulindwa na kubakia mali ya umma.
 
Kusema ukweli NSSF wametusahau sana wanachama. Hakuna hata issue moja ya kujivunia now kama member, benefit zao zipo chini mno

Kinachonikera ni kuwa HATURUHUSIWI KUHAMA, sijui kama kuna mtu angebaki huko....labda uwe shabiki wa ligi za kienyeji. Huu mfuko nuksi kabisa
 
Nimefurahi sana habari ya leo kwa kuondolewa yule mvusha makontaina bure, yaani mkuu wa TRA sisi alitung'ang'ania tukalipa milioni kumi wakati ni gari ya shule, kumbe anapitisha makontina ya bilioni 80,bure jamani dhambi gani hii?
 
hawa wasio waislam(makafiri) wana tabu kweli!!!!sehemu ikiongozwa na waislamu,utasikia udini,rejea udom.mini nipo chuo cha serikali,malecture woote wanaonifundisha makafiri.utasikia waislaam wamekosa vigezo luwa malecture.ila sehemu ikiwa na waislaam wengi,udini.

ndo zao hawa jamaa.kuwapiga vita waislam,,,,,,,,mbona tunayoyaona kwao hatuyasemi?
 
mfumo, kichwa chako kinafanya kazi lkn sio kazi nzuri. Mimi siko kwenye hoja yenu ya udini lkn nikukosoe kidogo kuhusu 'uzuri' wa mipango ya huyo mjombaako hadi umnadi kuwa kufanya mambo makubwa kwa jamii.

NSSF isomeke kwako kama National Social Security Fund yaani Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii.Lengo la uanzishwaji wa mifuko ya mfumo huu ni USTAWI wa JAMII.

Mifano yako ya uzuri wa Bwana Dau ni chukizo kwa wanachama maskini wa mfuko, kwa sababu ujenzi wa madaraja na vyuo vikuu ni kazi ya serikali na sio NSSF. Nikukumbushe kuwa, ustawi unaopaswa kusimamiwa na NSSF ni wa individual member na sio daraja la Kigamboni.

Ukihitimisha hoja yako mfu, umethubutu kulinganisha Deadly NSSF na mifuko mingine kiasi cha kuiita ni yenye vikao vya kula kitimoto. Hapo ndio unadhihirisha ukomo wa ubongo wako kuwaza.

Ingia kwenye tovuti ya PSPF, utakutana na tangazo la ONDOA STRESS, ONGEZA ASSETS. Ule ndio ubunifu ambao Mzuri Dau wako na NSSF wamekosa. Mwambie Dau akajifunze toka PSPF namna ya kuwahudumia wanachama wa NSSF badala ya kuihudumia serikali ambayo inakopesheka kwenye taasisi nyingine.

Watanzania wengi (hasa walioko NSSF) ni watu wa kipato cha chini, hawakopesheki kwenye taasisi za fedha sababu hawana dhamana. PSPF imetoa fursa kubwa na ya kupongezwa inayomuwezesha mnyonge kutumia amana yake iliyoko kwenye mfuko kumiliki ardhi, huu hasa ndio utumishi kwa jamii ambao unaleta natumaini. Wakati PSPF inawafaidisha wanachama wake kuona faida ya amana zao, NSSF iko bize na miradi isiyo na direct impact kwa watu wa kipato kidogo.

Kama DAU ni mjombaako, tafadhali mwambie kwamba, ni jambo linalotia uchungu kwenda Benki kukopa 5m ili ununue kiwanja ukakataliwa kwa kuwa huna dhamana at the same time unayo maana yako NSSF mara mbili ya kiasi unachotaka kukopa lkn huwezi kuikopa wala haiwezi kutumika kukudhamini badala yake inakopeshwa serikali ambayo inavyo vyanzo vingi vya mapato na dhamana.

Dau akiendelea kuiongoza NSSF, sisi wanachama wa NSSF tutaendelea kuwa wapangaji kwenye nyumba za wanachama wa PSPF. Najua hapa unaweza ukaleta ngonjera ya mikopo ya NSSF kupitia SACCOSS, ashakhum si matusi....uhuni ule. Saccoss ni kiini macho na huwezi kunigroup na watu wasio na shida inayofanana na ya kwangu.

Tukiliacha hili la kukosa ubunifu, uwajibikaji kwa wafanyakazi wa NSSF ni hiyari. Huu ndio mfuko ambao staff wake Hawana muda wa kuingiza entry za michango ya wanachama kwenye mfumo wa komputa. Ukienda kuangalia salio lwako, utakuta kuna entry mbili tatu za miaka ya nyuma, wanachofanya ni kukupa adjustment form umpelekee muajiri wako. Kwa maana hiyo wanategemea taarifa toka kwa muajiri wao database yao ni maandazi na chai yenye hiliki. Sasa ikiwa taarifa za michango yangu wao wanazitaraji kutoka kwa mwajiri, ikiwa michango yangu haipelekwi, kuna anayejua na kuchukua hatua kweli? Hapa ndio napata mashaka kuwa, upo uwezekano kweli ajira pale ni za namna ya kufahamiana badala ya kulenga uwajibikaji.

Nakuhakikishia kwamba, siku sheria kandamizi za nchi hii zikijaruhusu mwanachama kuhama kutoka mfuko mmoja kwenda mwingine, watu wengi watachagua fedha zao ziwawezeshe wao wenyewe kumiliki asset na sio kujenga madaraja.

Kwa kumalizia, kuhusu kitimoto na bia, nikwambie kwamba, mifuko mingine hii inapotangaza kuwa unapata FAO la kuanzia maisha haitanii, kweli unapata, tena fasta.

Mimi ni mhanga wa Dau kukosa maono na ubunifu. Fedha zangu hazininufaishi, Dau anataka akae nazo hadi wakati atakaponipa uwezo wangu usiwe wa kiuwekezaji bali zitumike kununulia sanda ya kuzika mwili wangu.

Mwambie mjombaako, Mwana Mtoka Pabaya naye anatamani kumiliki kiwanja kilichopimwa kama anavyomiliki Ally Mzee, mwanachama wa PSPF, daraja la Kigamboni kwangu halina maana kwa kuwa hata ningetaka kwenda huko kukodi Shamba la kulima matikiti, serikali sikivu ya CCM ilishapiga marufuku kuiona pikipiki yangu ikikatiza mjini kwa kuwa inaleta foleni


Hii nimeipenda umefanya uchambuzi yakinifu na inaonekana una uelewa mkubwa kuhusu mifuko ya jamii. Nakushauri ufungue Uzi wako watanzania wapate elimu
 
Last edited by a moderator:
Kifupi ataukuzoea kuwaona kina said maofisini tuliozea kuwaona kina Paulo kwahiyo hapa kinachotupa shida ni mazoea na mfumo tu ndio unaowasumbua
 
Hii nimeipenda umefanya uchambuzi yakinifu na inaonekana una uelewa mkubwa kuhusu mifuko ya jamii. Nakushauri ufungue Uzi wako watanzania wapate elimu
Madaraja tunapita pamoja wanachama wa nssf na pspf na vyuo vile wanasoma pia watoto wetu sema wewe una shida binafsi
 
Wadau,
Kama tunavyofahamu Tanzania ni nchi isiyoongozwa kwa misingi ya dini fulani japokuwa wanaoutuongoza wana dini.

Kwangu mimi naona ni jambo jema endapo hatutaangalia dini zetu ili tupate au kutoa huduma mbalimbali za kijamii. Ni hivi majuzi mfuko wa jamii ya watanzania wote NSSF imetangaza nafasi lukuki za kazi lakini zimo tuhuma ambazo zinatolewa na watu wanaodai ni wafanyakazi na wenginesio wafanyakazi kuwa NSSF kuna udini eti kama hauna 'sigda' haupati kazi au kama wewe si Abubakari au Hamisi haupati kazi.

Tuhuma hizi ni mbaya na kubwa kwa mfuko unaoitwa wa jamii. Eti ili wakuajiri si kwamba umefaulu interview bali kwa majina na dini yako. Ni jambo linalohitaji ufafanuzi na ushahidi wa kutosha aidha kukubali au kukataa kuwa kuna udini au hakuna maana litaleta mpasuko kwa taifa.

Moto wa dini ni rahisi kuuanzisha na kuuchochea lakini ni ngumu kuumaliza. Kesho tutaskia na PPF kuna 'UDINI' Keshokutwa tutaskia mahakamani kuna udini na mwisho itakuwa ni jeshi na ikulu kuna udini huku mamlaka zikiwa kimya.
Fitina.chuki.na ubinafsi ndio kinaweza kupeleka mtu kuandika Uzi kama huu
 
Hitimisho

Tuache upendeleo. Fair play

Hapa kazi TU. mwisho

.............................
 
idara nyingi za binafsi na za serikali zina hiki kirusi..."udini &ukabila" kukiondoa zinahitajika juhudi za pamoja
 
kumbe maguguli anafukuza waislamu tu,loh kumbe ni mkakati anaofanya huyu mkatoliki mdini.

Temea mate chini Mkuu,Magufuli angekuwa Mdini asingemchagua Waziri Mkuu ambaye ndiye Mtendaji Mkuu wa Serikali yake Mwislam,Jamaa anatenda haki kabisa na aliyemfukuza huyo Mkuu wa TRA ni Waziri Mkuu kama sikosei na sio Magufuli na yeye alizingatia ubadhirifu uliotokea wa wizi wa makontena na hakuangalia eti huyu ni wa dini yangu hivyo amuache,kwa stahili hatutafika popote pale
 
Mtoa post utakuwa na matatizo makubwa ndani ya ubongo wako maana unaandika vitu hata taahira hawezi kuviandika na hayo ni matokeo ya chuki na udini unaokusumbua ambao umetengeza tatizo linalokaribiana na kansa ya ubongo kwa kushindwa hata kuandika vitu vyenye kueleweka ! Unatia mashaka hata uwezo wako wa kitaaluma na huenda hata hiyo kazi yenyewe ulibebwa!Unafikiri dkt.magufuri ni rais wa wakristo tu au wadhani wakristo ndio wanye haki pekee ya kufaidika na rasilimali za nchi hii na kushika nafasi za uongozi katika serikali na taasisi zake ?Au unadhani rais anafanya kazi kwa kutumia taarifa za kimajungumajungu na wivu wa kike kama zako?Kwanza tuambie wewe ni nani ndani ya shirika na upo kitengo kipi na ofisi ipi?Pili tuambie nani na nani walifukuzwa kwa sababu ya dini zao ndani ya shirika?na hao staff wanatoka idara zipi? mkoa ama wilaya ipi? Halafu zaidi kama unaona una ishu serious si uziandikie mamlaka husika juu ya suala hilo? Nakutahadharisha kuwa makini na posts zako kwani majukwaa haya si kwa ajili ya uchochezi na wala usidhani ukipost upumbavu na mambo ya kibaguzi kama yako na kutaka kuharibu image za watu wengine dola itakunyamazia! Kwa kifupi inaonyesha wewe ndio kati ya wale mnaohujumu shirika kwa dhumuni la kumkomoa dg ili aonekane hafai na kwa bahati mbaya sana hila zenu,matendo yenu machafu yanafahamika si tu na dg bali hata na idara nyeti ndani ya serikali yetu. Kumbuka aliyepewa kapewa tu na huwezi kumpokonya kwa chuki zako za kijinga! Kadhalika fahamu huyo unaemchukia ataondoka hapo kwa mipango ya mungu tu na pale muda wake ukifika na wala si kwa vipost vya kishambenga kwani tumeshawazoea!!!
Boya kweli sasa umeandika nini hapo kwa hiyo hutaki watu wamjadili mkubwa wako hapa nikuanikwa kwa uozo wowote ajalishi kwakuwa ni public figure atasemwa tu!Ficha ujinga tuone busara zako!
 
THE BIG SHOW mbona unakosa ustaarabu, unapenda kuongea matusi kila wakati!!
Huwezi kuwa na heshima, kujiheshimu??
Naona hata huo Wislamu unaotetea hauna, maana maustadhi wanajiheshimu, hawawezi kuwaambia wenzao eti wamejinyea, huoni aibu??
 
Last edited by a moderator:
Angalia huyu punguani anaropoka tu mkikaa kwenye vijiwe vyenu vya mapuya mnadanganyana tu lini Dr.Dau alikuwa NECTA.

dau sio tu kuwa muislam ila mdini na mbaguzi kmanin watu wakandie tu NSSF?kwan ndo taasis pekee inayoongozwa na muislamu?

Tuoneshe majina ya top brss wa NSSF na list ya management staff ya NSSF.

Na hilo neno "udini" unamaanisha nini?

Au kwa neno "udini" unamaanisha Dau ni Muislam?

Kama una maana hiyo basi naam, Dau ni Muislam swafi kabisa na hatetereki.

Vipi wewe, hauna udini?
 
Tuoneshe majina ya top brss wa NSSF na list ya management staff ya NSSF.

Na hilo neno "udini" unamaanisha nini?

Au kwa neno "udini" unamaanisha Dau ni Muislam?

Kama una maana hiyo basi naam, Dau ni Muislam swafi kabisa na hatetereki.

Vipi wewe, hauna udini?


Wacha kumpaisha muhuni tu yule siye ndo twamjua...

Hana lolote mbabaishaji tu....
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom