Mbowe awaponda wenzake
*Asema wapo kwa maslahi ya tumbo
*Kuungana sawa na kufika mbinguni
Na Eliya Mbonea, Iramba
MGOMBEA urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Bw. Freeman Mbowe (CHADEMA), amesema uwezekano wa viongozi wa kambi ya Upinzani nchini kuungana ni mgumu sawa na tajiri kuona ufalme wa Mbingu.
Alitoa kauli hiyo jana, alipokuwa akihutubia wakazi na wanafunzi wa chuo na sekondari ya Kinampanda mjini hapa, baada ya kuulizwa swali lililotaka kujua sababu ya wagombea urais wa kambi hiyo kutoungana na kuwa kitu kimoja.
Bw. Mbowe alisema chama chake kimekuwa cha kwanza katika historia ya upinzani nchini kuweka mbele dhana ya ushirikiano baina ya wapinzani.
"Vyama vichache vimepandikizwa na CCM kwa maslahi ya tumbo, CHADEMA mwaka 1995 haikusimamisha mgombea, badala yake iliungana na NCCR-Mageuzi, mwaka 2000 tukawaunga mkono CUF, jitihada zetu zote za kushirikiana zimekuwa hazizai matunda, hivyo mwaka huu tumesimamisha mgombea," alisema.
Aliongeza kuwa viongozi wengi wa Upinzani hawawezi kuungana kwa dhamira ya kuwatetea Watanzania, kwani wapo kwa ajili ya maslahi binafsi.
"Msifikirie kuwa kila mgombea urais au Mwenyekiti wa chama yupo kwa ajili ya kupigania mustakabali wa nchi, wamegeuza siasa kama biashara na wanaitumia kama vyanzo vya mapato," alisema mgombea huyo.
Alisema lazima CCM ikubali lawama za kulifikisha Taifa katika hali mbaya na ya kutisha, na kuwafanya wananchi wajione kuwa matatizo yao ni tofauti ya rangi za bendera badala ya kuwaeleza kuwa tatizo kubwa ni umasikini.
Akizungumzia nafsi yake, Bw. Mbowe aliwaeleza wananchi kuwa hakuingia kwenye siasa kwa ajili ya kutafuta ajira, kwani anachopigania si maslahi ya CHADEMA bali ya wananchi wote. "CHADEMA si mama yangu naweza kuiacha wakati wowote," alisisitiza msimamo wake.
Alisema kamwe hataacha kutumia busara na hekima za Mwalimu Nyerere katika kujenga utaifa, kwani kipindi chote cha miaka 44 bado misingi ya utaifa aliyoicha Mwalimu haijatekelezwa.
SASA MASWALI YA KUJIULIZA :
Kama vyama vingine vya upinzani (isipokuwa chadema)vipo kwa ajili ya matumbo, WHY DID HE JOIN THEM ? Doesnt this LOGICALLY make him one of them ??
Kuungana ni sawa na kufika mbinguni ? Anaijua mbingu huyu au anasema tu ? Je ashafika huko since waungane ?
Anaendelea kusema kwamba vyama vimepandikizwa na CCM, then DOES IT MAKE ANY SENSE KWA YEYE KAMA MWENYEKITI WA CHADEMA KUUNGANA NA VYAMA VILIVYOPANDIKIZWA NA CCM ? AU NA YEYE AMEPANDIKIZWA ?? WHO SHOULD WE TRUST HERE ??
(Kuna bonge la nyuzi litashuka kuhusu uchaguzi mkuu, hiyo itaangushwa anytime)!!
Tujumuike katika kuchangia !