Mengi vs Manji: Ukweli ni upi?

Mengi vs Manji: Ukweli ni upi?

Wanabodi,

Nadhani kuna kitu ambacho ninapungukiwa kitu hapa , kwani siku hizi ITV ni TV ya taifa ? Na kama jibu ni hapana sasa kwa nini huyo malima mdogo anataka kuingilia ni habari gani zipewe kipaumbele ?
 
Manji amjibu Ndesamburo



na Mwandishi Wetu



MOTO aliowasha Mbunge wa Moshi Mjini, Philemon Ndesamburo (CHADEMA), umeanza kusambaa, na tayari mfanyabiashara, Yussuf Manji, ameibuka na kukanusha tuhuma zilizoelekezwa kwake.


Katika taarifa yake kwa vyombo vya habari, aliyoitoa jana, Manji alikanusha madai ya Ndesamburo, yaliyokuwa yakimhusisha yeye (Manji) kuwahonga wajumbe wa Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge, wanaosikiliza kesi ya mmiliki wa vyombo vya habari vya kampuni za IPP, Reginald Mengi, dhidi ya Mbunge wa Mkuranga (CCM), Adam Malima.


“Kitendo cha Philemon Ndesamburo cha kunituhumu mimi kuwahonga wajumbe wa kamati hiyo, hakina ukweli wowote. Ni cha kukurupuka, na kinaonyesha jinsi asivyo makini katika mambo yake,” alisema Manji katika taarifa yake hiyo, ambayo imechapishwa kwa urefu ndani ya gazeti hili.


Manji katika taarifa yake hiyo, aliyoipa kichwa cha habari kisemacho; “Ndesamburo unachotafuta kwangu ni nini?” alieleza kushangazwa na madai aliyotoa mbunge huyo kuwa, maneno kwamba yeye aliwahonga wabunge, aliyapata kutoka kwa Mengi.


Huku akitumia mfano wa mzee mmoja wa Baraza aliyewatuhumu wazee wenzake kuhongwa na mshitakiwa; Manji alisema kitendo cha Ndesamburo, ambaye alikuwa Mjumbe wa Kamati ya Bunge ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge, kukutana na Mengi na kuzungumza naye masuala yanayohusu shauri lake lililokuwa likijadiliwa na chombo hicho, ni rushwa.


Bila ya kutaja mahali wala siku, Manji alirejea kile alichokielezea kuwa, ni maneno ya Ndesamburo, ambaye aliwahi kunukuliwa akimtuhumu Mengi kwa kupeleka kwenye kamati hiyo ya Bunge, mikanda (ya redio na televisheni) iliyoghushiwa.


“Inawezekana Ndesamburo ni mwepesi wa kusahau, kwa hiyo napenda kumkumbusha jambo litakalomrudisha katika kumbukumbu zake… Ndesamburo umesahau kwamba ulisikika ukisema kuwa, Mengi kapeleka kwenye kamati mikanda iliyoghushiwa?” alihoji Manji.


Mfanyabiashara huyo, ambaye kwa muda mrefu mwaka jana habari zake ziliandikwa sana katika magazeti ya ‘This Day’ na ‘Kulikoni’, yanayomilikiwa na moja ya kampuni za Mengi, alihoji pia iwapo ni yeye aliyekuwa nyuma ya mikanda hiyo iliyoghushiwa.


Manji, pasipo kuingia katika undani wa sakata hilo, ambalo bayana linaonyesha kuficha mambo mengi nyuma, alimtaka Ndesamburo aeleze kile hasa alichokuwa akikificha.


Akizungumza kwa simu na Tanzania Daima jana kuhusu suala hilo, Ndesamburo alieleza kushangazwa na maneno hayo ya Manji, na akahoji ni wapi alipata kumsikia akitamka kuhusu mikanda ya Mengi?


“Inaelekea pengine anajua mazungumzo ya siri katika vikao vya kamati za Bunge. Pengine angeeleza ni wapi alisikia nikisema maneno hayo. Mimi niko tayari, na katika hili wala sikuwa na sababu ya kumpendelea Mengi wala mtu mwingine yeyote,” alisema Ndesamburo jana.


Mwanzoni mwa wiki hii, Ndesamburo aliitisha mkutano wa waandishi wa habari, ambao pamoja na mambo mengine, alitangaza uamuzi wake wa kujiuzulu ujumbe katika Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge, kwa kile alichokieleza kuwa, ni kutoridhishwa kwake na namna kamati hiyo ilivyoyashughulikia madai yanayoihusisha kupokea rushwa katika kesi inayowahusisha Mengi na Malima.


Mengi alifungua kesi hiyo akilalamikia kauli iliyotolewa na Malima bungeni mwaka jana, akivituhumu vyombo vya habari vinavyomilikiwa na mfanyabiashara huyo (Mengi), kutoa muda mchache kwa masuala yanayohusu taifa, wakati vikitumia muda mwingi kuelezea mambo yanayomhusu yeye mwenyewe.


Katika barua yake ya kujiuzulu, aliyokabidhi kwa Spika, Ndesamburo, alisema kumekuwapo na madai kwamba, wabunge (akimaanisha wajumbe wa kamati hiyo) walikuwa wamepewa rushwa na Manji ili kuacha kulifuatilia suala linalohusu kesi ya Mengi na Malima.


Pili, katika barua hiyo ya Januari 10, mwaka huu, Ndesamburo alibainisha pia kuwa, uamuzi wake wa kujiuzulu, unatokana na kauli zenye utata zinazotolewa na kiongozi mmoja wa juu serikalini, akidai kuwa zina lengo la kumharibia maisha yake.


Alisema kuwa, wakati kesi ikiendelea, Mengi aliwahi kumwita na akamweleza kuwa aliitwa na kiongozi huyo wa juu serikalini, na kutakiwa kuondoa kesi hiyo, kwani atashindwa kwa kuwa Manji alikuwa ameihonga kamati hiyo ili yeye ashindwe.


“Halikuwa jambo dogo, nililifikisha kwenye kamati na wenzangu walishtushwa na hili, tukakubaliana tumwite (Mengi), atuthibitishie hayo… tukahitimisha kikao cha kamati ile tukaenda kwenye Krismasi,’’ alisema Ndesamburo.



Nimesoma habari hii yote nimegundua kwamba the issue is very hot na kuna ukweli mwingi.Mzee Ndesa aweza kuwa kapiga Ikulu.Si kawaida ya Manji kuongea namna hii kwa kuchagua maneno bila kuishia kuombwa radhi na kwenda Mahakamani. Again nasema Mzee Ndesa hajakurupuka kama mtu mmoja anavyo taka tuamini hapa . Mbona hakuna anaye ongea kwenda Mahakamani this time ? Mbona Serikali na Lowasa hadi sasa wako kimya ? Mbona watu wanasema Mzee Ndesa awe ignored ?Kazi kubwa na wacha tuangalie tunako elekea. Ndiyo matokeo ya kuwaacha Wahindi ama matajiri kuwa na mkono katika serikali . Mzee Ndesa anaonyesha kwamba kuna mambo mambo ndanu ya Vikao Manji anayajua .Je kama ni kweli hivyo ndivyo ilivyo bado watu watakataa kugongwa ?CCM na Bunge lenu , PM come out clean tafadhali .
 
Interesting!!!!!,

absolutely vague statement from Manji!!!!,

Kama kuna mtu anaijua background ya Malima itakuwa ni bora zaidi atuwekee hapa ili tumchambue kama tulivyomchambua Mengi na wanbodi tukapigwa STOP!!, This time tumuangalie Hon Malima. Itatusaidia wanabodi kuona kwamba huyu Malima ni credible or not. Au ndio KUJIKOMBA KWENYEWE HUKO??............... pathetic!!!!

Lunyungu,
Maswali yako hapo juu ni ya msingi sana, na kama wapo member wa kamati ambao ni accused ni vema wajiuzulu ili kurudisha imani (integrity) ya kamati husika, mpaka hapo watakapokuwa proven otherwise then wanaweza kurudishwa kamatini.

kuna mtu kauliza, je ITV ni TV ya taifa??? Je kuna sheria inayowa-govern wenye vyombo vya habari kuhusu muda gani apewe "kiongozi wa Taifa" ndani ya TV Binafsi?
 
Ogah,
Mimi nadhani hakuna swala la kujiuzuru.. waondolewe mara moja kama inavyofanyika ktk korti zetu kuhusu wazee wa baraza - Jury.

Hawa watu waondolewe mara moja na baraza jipya liundwe tena wasipewe nafasi ya kuonana na mtu yeyote kujadili kesi hii.
 
Mnhhhhh Hapa a pazito ,kazi ipo!! Pesa yetu wenyewe wafanyakazi tunaotoa michango yetu NSSF na Mashirika ya Umma PPF na PSPF zinaanza kutuharibia hata bunge!!!!! Kweli nchi imeoza tumeshauzia wahindi.
 
Mengi awataka Watanzania kuacha woga
2007-01-13 09:36:42
Na Joseph Mwendapole


Mwenyekiti Mtendaji wa IPP, Bw. Reginald Mengi, amesema woga ni adui mkubwa wa maendeleo na amewataka Watanzania na watu wengine duniani kujiamini wanapotafuta maendeleo.

Aliyasema hayo jana jijini Dar es Salaam wakati akizungumza na ujumbe wa wanafunzi 40 kutoka Chuo Kikuu cha Yale cha nchini Marekani.

Alisema mtu anapotaka kuanzisha biashara ama mradi, anapaswa kujiamini na kuacha woga ili aweze kufanikiwa.

Mkutano huo ulihudhuriwa pia na Ofisa Mtendaji Mkuu wa Shirikisho la Wenye Viwanda Nchini (CTI), Bi. Christine Kilindu na aliyekuwa Mwakilishi wa Tanzania kwenye Umoja wa Mataifa, Balozi David Mwakawago.

Bw. Mengi alisema yeye binafsi alizaliwa kwenye umaskini wa kupindukia, lakini ameweza kufika hapo alipo kutokana na kuamini kuwa anaweza kufanya mambo makubwa.

Alisema mbali na kujiamini, watu wanapaswa kumweka mbele Mwenyezi Mungu katika mambo wanayoyafanya na kwamba wakifanya hivyo Mungu hawezi kuwaangusha.

Alisema mtu anayefanya biashara anapaswa kuwa na wazo na biashara kabla ya kupata mtaji na alionya kuwa kutafuta mtaji kabla ya kupata wazo la biashara kunaweza kusiwe na manufaa.

"Mimi nilipata wazo kwanza kabla ya kutafuta mtaji, niligundua kuwa peni zimeadimika nikaanza kujifunza kutengeneza peni na sehemu ya nyumba yangu nikaigeuza kuwa kiwanda," alisema.

Alisema baada ya kupata wazo la biashara ya kufanya ndipo alipoanza kutafuta mtaji kwa kukopa katika benki mbalimbali.

Alisema kilichomsaidia mpaka kufika hapo alipo ni imani aliyoiweka kwa Mwenyezi Mungu na kujiamini yeye binafsi kuwa anaweza kufanya mambo makubwa.

"Siku zote nilikuwa nikisema kuwa 'I can, I will and I must', na maneno hayo ukiyaangalia ni marahisi lakini yana maana kubwa sana, kujiamini ni kitu kikubwa ili uweze kufanikiwa, " alisema.

Aidha, alisema Watanzania na watu wengine wanapaswa kuona umaskini wanaokabiliwa nao kama changamoto badala ya kuuona kama tatizo endapo wanataka kukabiliana nao.

Alisema katika Bara la Afrika, watu wameshindwa kuondokana na umaskini kutokana na kuuona umaskini kama tatizo, badala ya kuuona kama changamoto.

"Mimi binafsi niliuona umaskini kama changamoto kwa hiyo nikajitahidi kukabiliana nao, kila nilichokabiliana nacho niliona kama changamoto na nikapambana nacho kwa nguvu zote," alisema.

Aliongeza kuwa, watu wengi wanashindwa kupata maendeleo kwa sababu ya umaskini unaowakabili, hali inayowafanya waishi kwenye hali ngumu kwa maisha yao yote.

"Ukiamini kuwa huwezi, mawazo yako yatakuelekeza kuthibitisha kuwa kweli huwezi na ukiamini kuwa unaweza mawazo yako yatakuelekeza kuthibitisha kuwa unaweza," alisema.

Alisema kwa kutojiamini, nchi nyingi barani Afrika zimejikuta zikiita wataalamu kutoka nje ya nchi kufanya kazi ambazo wangeweza kufanya wananchi wa kawaida.

Alisema kuku alishindwa kuruka kama ndege kwa kuwa aliamini kuwa hawezi kuruka angani, hivyo alishauri watu kuiga mfano wa ndege aliyeamini kuwa ana uwezo wa kuruka na akafanikiwa.

Alisema wako watu wanaoshindwa katika masuala mbalimbali kabla ya hata kuanza kutokana na kuweka mbele woga na imani kuwa hawawezi.

Aliwataka wanafunzi hao kuwa wananuia makubwa katika maendeleo na kwamba mtu anayenuia makubwa hupata makubwa, wakati anayenuia madogo hupata madogo.

Bw. Mengi alisema mtu anayetaka kufanya biashara anapaswa pia kuhakikisha anakuwa na washiriki wazuri wa kufanya nao biashara ili aweze kukuza mtaji wake na kupata masoko mengi.

Kuhusu uwekezaji nchini, Bw. Mengi alisema watu wengi wanaokuja kuwekeza hawaijui vyema Tanzania na aliwashauri kushirikiana na wazalendo watakapokuja kuwekeza.

Alisema kuna nafasi nyingi za uwekezaji ambazo wakizitambua zinaweza kuwa za manufaa kwao na alitoa mfano wa sekta ya Teknolojia ya Mawasiliano (IT).

SOURCE: Nipashe
http://www.ippmedia.com/ipp/nipashe/2007/01/13/82220.html
 
Nadhani kauli ya Malima ilikuwa ni ya kujikomba tu.Kama alikuwa seriously critical of coverage ya ITV kwanini hakulaumu namna kituo hicho kinavyoonyesha habari za masuala ya maendeleo na matatizo ya wananchi (in case hakitimizi wajibu wake upasavyo) na badala yake alalamikie coverage za ziara za viongozi?

Kumbukumbu yangu ndogo inaniambia beef la Mengi na Malima ni part of songombingo kati ya Mengi na Manji.Adam Malima ni mtoto wa Kighoma Malima (need I say more about Kighoma's son when it comes to his world view?).Put it roughly,Malima ni miongoni mwa watu like Kapuya,Dau,etc ambao wali-take side na Manji baada ya huyo gabacholi kuingiza kadi ya udini.Nukuu ifuatayo from makala yenye kichwa "Athari za viongozi wa dini kujihusisha na dola – 2" Tanzania Daima la terehe 24/08/2006,inaweza kutoa picha ndogo ya Mh Adam Malima.

"Viongozi wa NRA akiwemo hayati Abubakar Ulotu waliishutumu CCM na serikali kwa kifo cha Profesa Malima wakidai kilipangwa. Hizi zilikuwa ni shutuma mbaya sana dhidi ya serikali, lakini busara za mzee Mwinyi zilitumika kufuta hisia hizo kwa kushiriki kwake kikamilifu katika mazishi ya Profesa Malima.

Hata hivyo, wanasiasa kadhaa walitaka sana kujaribu kumtumia mwana wa Profesa Malima kuendeleza chuki za kidini na kisiasa. Adam Kighoma Malima alipewa nafasi ya kugombea ubunge kwa tiketi ya NRA na hatimaye CUF, lakini akashindwa kwa kura nyingi. Hatimaye alijirudisha CCM na kushinda ubunge wa Mkuranga 2005.
"


Pengine kabla ya kulalamika jinsi gani ITV ilivyokuwa "na mapungufu" angajiuliza iwapo kituo hicho ni taasisi ya serikali kama TVT.
 
Bwana Y. Manji ni kijana ambaye hajavuka miaka thelathini na tanao lakini anamiliki makampuni ambayo rasilimali zake ni za mabillioni ya shillingi!
Katika miaka ya tisini mwanzoni (mpaka sasa nafikiri) alikuwa maarufu wa kununua vibali vya JAPANESE IMPORT SUPPORT FUND kutoka kwa watu waliokuwa wamepewa fund hizo lakini hawakuwa na cash cover ya 30% - so Manji simply bought them out!!! Wengi wa waliokuwa wanapata hizo import support ni wabunge na jamaa zao wa karibu ambao vibali vyao alivinunua kwa pesa. Mchezo huo kaufanya year in year out ikihusisha pia na uagizaji wa mbolea!!

Japanese Import Support Fund is supposed to be refunded so that it could keep on circulating to other aspirants!! Kilichotokea ni kwamba waliomuuzia Manji vibali walikuwa wakipewa milioni kumi au kumi na tano kwa kibali cha milioni mia moja while they unknowingly kept on shouldering liability 100%.

What happened by then was some companies (MPs used their real names) that applied for the funds had neither traceable records with the registrar of companies nor known physical address apart from the P. O. Boxes!! So it became practicable impossible for the Ministry of Finance to exercise an effective recovery of the funds... sasa mambo yamebadilika hizo fund zinakuwa monitored na TIB na hapo Manji ndipo kakwaa kisiki but surely is has made afortune along with our MPs!!

Nasikia kuna wabunge (mawaziri) huwa wanakwenda kuchukua posho in return of favours towards Quality Group (nasikia Quality garage kaifilisi - liquidated!). Mpambe aliyekuwa naye karibu ambaye nasikia sasa hivi wamekosana kwa sababu ya mabo haya haya ya Import Support ni jamaa mmoja ana ofisi IPS city center, alikuwa anamiliki biashara ya petrol station ENGEN Ubungo, Baa Africenter Mchikichini na Monvila Bulawayo Chang'ombe lakini vyote hana sasa hivi! Inasemekana Manji kamhujumu!!

Huo ndo ulikuwa mwamzo wa Manji kuanza kuliweka bunge letu mfukoni, nasikia alimlipia mzee Makamba nyumba aliyouziwa na serikali..... na alimshukuru saana na kuahidi kulipa fadhila.

Tanzania...... ndiyo hii

OFF THE RECORD: Nasikia huyu kijana ni mtoto kati ya wamiliki wa kampuni ya K. J. Motors ambayo nayo ilkifilisika wakati ikiwa imepewa pesa za ku deliver malori na pikipiki wizara ya ujenzi.
 
Naomba kuhabarishwa:

End result ya kazi ya hiyo kamati ya maadili katika hili shauri la Mengi v/s Malima ilitakiwa iwe nini? Yaani, je ilikuwa ni kutafuta ukweli tu kisha mmoja alazimishwe kumuomba radhi mwenzie yaishe au kungekuwa na zaidi ya hapo?

Yaani, kama Mengi angeshindwa mathalan, je kungekuwa na 'adhabu' ambayo angepewa ... which would somehow benefit Manji, kiasi aaamue kuhonga wajumbe wa kamati .. (ikiwa ni kweli)?

I'm trying to find out if there was a bigger motive zaidi ya huu ushindani wao unaoendelea.
 
Jamani, nilikuwa nje ya forum kwa muda. Nimefuatilia hii issue na kugundua ni upumbavu na utoto unaendelea hapa. Hivi aliyesema wajumbe wa kamati wamekula rushwa ni PM au Ndesamburo. Ndesamburo amejitoa kwenye kamati kutokana na kutolidhishwa na mwenendo wa vikao na ushahidi wa maneno toka kwa Mengi. Hivi kwa nini Congress hawaongelei kwa nini Bush haoneshwi kwenye BET Networks. What a primitive society!
 
Wapendwa,

Kama kuna suala linachukua muda wangu mwingi kwa wiki hii basi ni hili. I hope this time around will be a big catch!.

Nawaombeni nisisime chochote kwa sasa ila niseme tu kwamba ikifika hatua mwafaka nitaweka bayana kilichoendelea. Na yale yaliyokuwa yakiendelea nyuma ya pazia maana niko karibu na Mzee Ndesa katika hatua mbalimbali.

Ila kwa wale wanaosema Mzee Ndesa alikurupuka watafute tape ya press conference yake wapate picha ya ujumla ya kwa nini alichukua uamuzi huo kwa kuwa kwa bahati mbaya karibu vyombo vyote vya habari pamoja na kuwepo katika mkutano husika viliandika ndivyo sivyo!

This game is sweet, lakini litakuwa tamu zaidi kama mwisho wa siku Tanzania na watanzania ndio watashinda!

JJ
 
Naomba Tuwe na subira,na tuache kutukanana.Ukweli wote utaonekana hapa,Mzee Nesamburo hakuwa mwendawazimu kuita Waandishi wa Habari na kutoa habari za ndani za Kamati ya Bunge!Mambo yalimfika kooni na hakutaka kuwa ndumilakuwili kama walivyo wengi waliomo kwenye kamati hiyo!.UKWELI wa jambo hili utaonekana wazi kwa sababu unahusu mambo mengi Rushwa,Udini na matumizi mabaya ya madaraka lakini sio Ukabila kama baadhi ya waliotangulia walivyozungumza.Napenda kuwathibitishia kuwa kila kitu kitakuwa wazi sasa.
Na pia ndio mtakavyoona Mzee Spika anavyokuwa muoga kuwa muwazi kwenye mambo yanayowahusu wakuu wa serikali Bungeni,Spika yupo Japan lakini akili yote inafuatilia sakata hili la Mzee Ndesamburo,kwani Mzee anamwaga kila kitu nje!Kama EL aliwatisha watu wasiulize mambo ya Richmond Bungeni,sasa amekwama.Kwa maoni yangu naomba Muungwana asimuonee haya huyu Rafiki vinginevyo atapoze umaarufu kwa wananchi kwa sababu ya huyu PM.Amekuwa si muoga na anafanyakazi kwa miongozo anayoijua yeye mwenyewe,si muoga na ana ujeuri ambao unavuruga sifa za Mkuu wake wa kazi.Naomba kutoa Hoja.
 
Mwawado haya maneno ndiyo niliyasema mwanzoni na kumkataza Mzee MKJJ kuchukua side kwa kuwa ni mwana CCM . Muda utafika ukweli utajulikana .
 
Uzoefu umeonyesha kuwa viongozi wetu huwa wepesi sana wa kutishia kwenda mahakamani kama wasipoombwa radhi pindi zinapotolewa tuhuma nzito dhidi yao.Nakubaliana na wanabodi wanaoomba tuwe na subira kujua hatma ya sakata hii lakini ushahidi wa kimazingira,pamoja na uzoefu wa reactions za wanasiasa wetu,nashawishika kuamini kuwa hoja za Ndesa zina mantiki flani.Hivi kwanini EL asikanushe au kutishia kwenda mahakamani asipoombwa radhi iwapo tuhuma zilizotolewa na Ndesa ni za uzushi?Mengi nae amekaa kimya kuashiria kuwa alichoseam Ndesa sio uzushi,vinginevyo angekanusha.Uzoefu umeonyesha kuwa Manji ni mwepesi sana wa kukimbilia mahakamani,lakini nashangaa kuwa pamoja na kutuhumiwa kuwa kahonga baadhi ya wajumbe wa kamati ya Bunge ameishia kukanusha katika lugha "isiyo yake" kwa tuliomzowea.

Hapa kuna ishu nzito.Wanaomlaumu Ndesa kuwa mzushi wanasahau kuwa simple logic inatueleza kwamba "uzushi au uongo utaendelea kuwa perceived kuwa ni ukweli hadi hapo atakapotokea wa kuuthibitisha otherwise."Na hapo wa kuthibitisha sio Manji kwa vile huyu in a way ni suspect,and it goes without saying hawezi kukubaliana na tuhuma za Ndesa.Wa kutufumbua macho ni LOWASSA and,to a lesser extent,Mengi.
 
Lunyungu

Mzee Lunyungu Wacha kutunyungulisha hapa wewe unawashambulia wanabodi hapa wakati kila siku unabadili kauli kama kinyonga. Toa maoni yako na usiandike kama uko darasani hapa unamsimamia nani? Toa hoja zako na heshimu mawazo ya wengine

Kila kinachoandikwa unataka kuongeza vijineno vyako, nani kakupa hiyo kazi? Kwanza ni muongo na ndumila kuwili kama huna la kusema kaa kimya. Unafikiri Tanzania yote ni ya kwako? Wengine wasiseme ila wewe na vikaragosi vyako. Wacha upuuzi wako.
 
Wacha hoja ndiyo hizo kumbe wewe kwako hoja ni zipi ?Kutia kaneno ni kawaida kama nakubaliana ama nakataa .Hakatazwi mtu kusema hapa ila tuna kataa kupumbazwa na kampeni za kijinga .
 
Hivi jamani tuongee mambo ya msingi kabisa hapa. Mkurugenzi wa PCB anateuliwa na Rais, anawezaje kumhoji Waziri Mkuu kwa tuhuma za rushwa? Mambo yote hayo ni viini macho tu ambavyo watanzania wanafanyiwa!

Hata mfumo wa Bunge lenyewe ni kama ngonjera vile, mbunge anapeleka maswali wizarani halafu anasubiri kuja kujibiwa bungeni. Kwa nini asijibiwe huko huko ofisini kwake!? Sasa hapo mmeona suala la Mengi na Malima na hizo tuhuma za Ndesa spika anashauri iundwe kamati nyingine tena!!!!!!! Hizo kamati zina sitting allowances kubwa sana kama hamjui....Na pesa za walipa kodi ambao watoto wao wanakaa chini kwa kukosa madawati. Siku hizi hata Chuo Kikuu cha Dar pale Mlimani nao pia wanajazana mpaka wengine wanakaa chini! AIBU!

Tanzania kuna maigizo tu, kuanzia uchaguzi wa viogozi, jinsi wanvyotuongoza na hata utendaji wao wa kazi za kila siku. Bora hata kipindi cha Mkapa kulikuwa na afadhali kuliko sasa! Serikali ya awamu hii hata wakiziba mashimo manne ya barabarani wataita waandishi wa habari waje kuwapiga picha waonekane kwenye taarifa ya habari!

Ni viongozi wa kuonekana kwenye vichwa vya habari vya magazeti, taarifa za habari za redio na televisheni!

Na waandishi wa habari wa Tanzania nao wanatia kichefuchefu. Ndio maana magazeti ya Kenya yakachora kikatuni cha kuwaonyesha wanamlamba miguu JK halafu wakalaani kitendo hicho. Wakati ni ukweli. Hata JK mwenyewe wakati mwingine anawashangaa! Wasipoandika habari za JK an EL wanahisi hawatauza gazeti, which is deadly wrong. Eti hata zile bilioni moja za mkopo kwa kila mkoa zinaitwa bilioni moja za JK!!!! Lord have mess....Serikali ya JK imekusanya lini hizo pesa mpaka igawe namna hiyo? Ni pesa za Mkapa hizo! Na mipango minngi ya maendeleo inayotekelezwa kwa sasa ni mipango iliachwa an serikali ya Mkapa! Tena kuna mingine imedorora baada ya serikali mpya kuingia madarakani! Mfano kasi ya ujenzi wa barabara kuu imefifia kabisa!

Serikali imejaa marafiki wa JK ambao wala hawamuogopi kama mnavyofiria. Hakuna kinachoendelea zaidi ya "window dressing" ya kwenye magazeti! Nahisi tunarudi kwenye kipindi kama cha Mwinyi RUKSA....Kama mnabisha mtaona!
 
Walisema za mwizi ni arobaini...mimi naomba nitabiri kuwa CCM haina zaidi miaka 20 kuanzia sasa kabla haijasambaratika. Huu ni mwanzo wa mwisho wake...makundi kama wana Mtandao yataendelea kujitokeza ndani ya chama na mwishowe yatasambaratisha chama...hapo ndio wakati wadanganyika wataanza kuona upinzani wa kweli.
 
Wala rushwa hawawezi wakaonyeshwa hadharani kama hakuna ushahidi wa kutosha,je wewe jina lako likionyeshwa hadharani bila ya ushahidi ili mradi tu wajue wewe ni mla rushwa hiyo halali?Issue hiyo Ndesamburo ni MUONGO,yeye anatumiwa tu na Mengi,lazima ieleweke wazi,Mengi alitoa Million mia tatu(3m)za kukodo Helkopta aliyofanyia kampeni Chairman wa CHADEMA,therefore this is paybeck time for CHADEMA na WACHAGGA.Kwa hiyo Ndesamburo hana jipya.Yeye mwenyewe ni MLA RUSHWA vile vile!!!!

MZEE WA LONDON

Hii ni hasara!!!! hasara!!!!! kwa BW.MENGI kwani nini alisubiri yafike huku yeye anajijua hayuko clearn sasa huu ndiyo mwisho wa muheshimiwa huyu

kwasababu ana skendo nyingi kama EL alimwambia afute kesi alikuwa anasubiri nini hii forum ilimfutia kesi nyingi zaidi ya 350 sasa tukaacha kumuandika sasa bwana tunakurudisha humu kila mtu akujuwe wewe

unaonekana mpole sana lakini ......... mimi kusema huu ndiyo mwisho wako siyo kufa nikatika vyombo vya habari vya tanzania kununuliwa na MAKABURU KWA ASILIMIA ZAIDI YA 50% sasa kaa mkao wakuporomoka hii ni deal ya MANJI ambaye ni Rostam wa EL

Nnakuonea huruma wewe ndiye tajiri mzawa mwenye vyombo vingi vya habari itabaki historia.

pingamizi lako kwa vyombo vya habari sijui kama litafanya kazi omba mungu sana ndugu yangu

tunajua LOWASSA ni rafiki yako sana hata wakati mmoja alikutumia sana kusuluisha matatizo ya wewe na tajiri mmoja wa mererani aliye kuwa patina yako BW.H.NYITI ulikuwa unampigia EL simu 60 kwa siku alikushauri vizuri lakini wewe ukusikia.
Naumeshawai kumfukuza EL na Yona aliye kuwa waziri wa madini ofisini kwako kuhusu mtafaruku uliyokuwa baina yako na Nyiti baada ya mzee wa matanzanite kumchukuwa EL akamuombee msahaa kwako.
hii ni habari kwa ufupi
 
Nafikiri kama walivyosema baadhi ya wajumbe ya mjadala huu ni bora tusubiri ukweli ujulikane.Japo nionavyo Manji na Mengi wote ni Matajiri lkn ukweli wa namna kila mmoja alivyopata utajiri unajulikana na wao wenyewe na watu wa karibu. na wao wote kwa zama tofauti wamekuwa wakiwatumia viongozi wa Serikali ili biashara zao ziende au kama walivyosema baadhi ya wajumbe ktk mada anuai kuwa wanakwepa Kodi. Wasiwasi wangu ni kuwa mmoja anatumia kile kinachoitwa uzawa na mwingine anatumia fursa aliyonayo kwa baadhi ya viongozi. Ikiwa PM ni mtu wa karibu ya Mangi au wote wawili haoni busara mmoja wao kushindwa ktk kesi yoyote. Tumeona kwa nyakati tofauti kila mmoja ktk Press akitoa misaada ya Kundi Fulani kwa Nyakati anuai, wengine wamesaidia nafasi za masomo na wengine viwete n.k. Pia sababu za uzawa zinazotumika nafikiri baadhi ya watu hawajui madhara yake lkn pia Sehem yoyote ile iliyoendelea basi maendeleo yameletwa kwa pamoja wazawa na wageni. Angalia leo hii DSM. Wazaramo peke yao au Wamanyema wasingeweza kuujenga mji peke yao. Pia ukiingalia historia za Nchi zilizoendelea zote utakuta wageni wanamchango mkubwa ktk maendeleo. Kibaya ambacho wengi hatupendi ni wacheche walio ktk MAMLAKA za Nchi kujineemesha peke yao huku Kundi la watu likifa kwa Njaa.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom