Mengi vs Manji: Ukweli ni upi?

Mengi vs Manji: Ukweli ni upi?

Nimesoma kwa makini maelezo ya watu mbalimbali akiwamo Mswahili. Watanzania tumekua na kawaida ya kuchukulia juu kila kitu hata mambo mazito ya kijamii. Hapa suala la msingi RUSHWA. Upo uwezekano wa kutokuwapo ushahidi wa kimahakama, lakini katika mlolongo mzima wa habari husika, utaona wazi RUSHWA ipo kweli. Kwanza kesi yenyewe haina uzito wa kuchukua vikao zaidi ya 60. Kila Mbunge katika wabunge 15 wanalipwa Sh 125,000 kwa siku za kikao. Siku ambazo hakuna kikao wanalipwa Sh 55,000. Kwa hiyo unaongeza hapo na usafiri. Utakuta karibu Sh milioni 100 zimetumika.

Mbali ya kikao kurefushwa, baadhi ya wajumbe walikataa hata kwenda Ulaya katika safari za Kibunge waking'ang'ania kuhudhuria kikao hicho, KUNANINI? Tangazo la MANJI linazungumzia kuhusu tape kughushiwa. Manji si mjumbe na wala hahusiki na kesi hiyo kwa vyovyote, amejuaje ya ndani ya kikao? Jambo la msingi ni kwamba MANJI ni mtu asiyetaka kuguswa na WAKUBWA wanamuogopa sana. Jambo la mwisho MSWAHILI amezungumzia kuhusu tape kughushiwa kutoka dakika kumi na kuwa mbili. Kwa taarifa dakika taarrifa ya habari nzima inaweza kuchukua dakika kumi, kwa hiyo hakuna mtu anayeweza kupewa dakika kumi. Ni uongo mtupu. Huhitaji mtaalamu, kaa katika TV yako na uangalia dakika kumi zitakuwapo habari ngapi. Lakini KUBWA KULIKO YOTE NI KWANINI WAZIRI MKUU AHUSIKE? KWANINI AHALALISHE RUSHWA? KWANINI AONE RUSHWA KUWA KIGEZO CHA UTOAJI HAKI?ATATUSAIDIAJE KATIKA MAPAMBANO DHIDI YA RUSHWA? TUWE WAKWELI NA WAZALENDO, NCHI INAANGAMIA
 
jamani el amekuwa mtu ambaye kweli siku zake zikifika ana majibu mengi ya kujibu watanzania.kwanza ni mla rushwa anapenda sana posho jamaa na hela yake huwa hailali nje ameshikilia vilivyo,pili hajui maadili ya kazi na urafiki ni vitu viwili tofauti.hivi mambo ya bungeni utamuhadithiaje mtu wa nje na wao wameapa kuwa na siri?kwa nini awe mmbea mpaka kwenda kwa mengi kumueleza??hivi el anajua cheo chake kweli??je kama yeye anafanya hivyo hao walio chini yake si wameoza wote??

i dont like this man,he is arrogant,selfish,proud na busara hamna,sasa hivi anapiga tu kelele kuhusu elimu kumbe anawazima watu wasiongelee mambo ya akina ndesamburo.

tunakoelekea mbele ya hukumu el atajibu maswali mengi na watu hawatamuachia.kwa nini kila wakati yeye ndio chanzo cha maovu???
richmondulian yeye,ufuska yeye,ubabe yeye mh kweli.watu huwa wanasema binadamu akilalamika sana lazima kuna yatakayotokea.
 
tusiwe wajinga kuingia katika mchezo wa Mh.Mengi tunapozungumzia kuhusu rushwa Rushwa zipo rushwa za aina nyingi hii ya Mengi ni kubwa na hatari zaidi.Bwana mengi ameprivitaze serikali na CCM,vyombo vyote vya habari,hata hii site hii inampa uwezo wa kutawala mawazo yetu bila kujua mmenasa yabidi kujikomboa Mengi hana tofauti na manji wote wanainterest zao wapiganapo fahari wawili ziumiazo ni nyasi!!!!
 
Mzee MKJJ ninakupongeza kwa uchambuzi wako hapo juu. Huyu ndiye sisi tunayemjua tangia zamani .Hongeara sana kijana wangu . Advocate na wengine wote well said . Tulifanya makosa kuamini kwamba JK angalikuwa na watu serious lakini haya ni matokeo ya Kampeni chafu za JK na rushwa ya kuingia na ile LAANA sasa Mungu anaileta wazi kwamba tulijua na Mwalimu alionya lakini tukaleta ushabiki now what ?
Mengi na Manji wote ni wale wale na serikali haitasema lolote maana wako mfukoni kwa wote kwa interest tofauti .
 
Waheshimiwa Advocate Jasha,na MKJJ na wengineo michango yenu imekuwa mahiri ktk kuweka mambo sawa.Kila ninapofikiri naona kuwa wananchi wamefumbwa macho na kuona suala zima la uongozi haliwagusi bali ni la baadhi ya watu.Hii si kweli!na ni dhambi kubwa kuamini hivyo!.Hawa Viongozi wetu wanakuwa wanyenyekevu mno wakati wa kuomba kura,wakishapita Uchaguzi wanakuwa "Miungu watu" na kudharau hata wala waliowapa ulaji!Eti Mh.Sita anasema Ripoti inayohusu kesi ya Malima Vs Mengi ni ya kwake na haitokuwa wazi kwa wananchi.Hivi huyu Sita ni nani?.Hakuna mtu anayepaswa kuwa juu ya wengine hata kama ana madaraka ya URAIS!
Sielewi kwanini tumepumbazwa kwa kiwango hichi,tuna matatizo mengi ambayo yapo kwenye uwezo wetu,lakini tunashindwa kuyatatua kwa sababu ya Uongozi Mbaya na Ubinafsi.Jamani nani kasema Tanzania tulivu?Tutataanza kuwindana kwa majina sasa,kwa sababu tabaka la wenye nacho(walio madarakani) na maskini (raia wa kawaida) linakuwa kubwa mno.Nyerere alikataa haya,lakini sasa yanarudi kwa Kasi na Nguvu Mpya.
Ndg wanabodi Tufanye nini? maana tumezungumza mengi mno ya maana,lakini kila kunapokucha kunakuja jipya linaloumiza mwananchi wa kawaida kule Magu au Njombe!Kusema na kuandika tu,sio msaada tosha kwa wenzetu walio nyumbani (kwenye hali ngumu).Ipo siku nao watatuona tu wababaishaji kama viongozi wetu!TUAMKE NA SAUTI ZETU ZISIKIKE!
 
Mwawado, iko siku sauti yako itasika, na mlio wake utapasua ukiziwi wetu na kutufanya hatimaye tuone kilichopo mbele yetu, na hapo tutakikataa!!
 
CHADEMA yamgeukia Lowassa







na Tamali Vulu


CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kimemwandikia barua Waziri Mkuu, Edward Lowassa, kikimtaka atoe tamko kuhusu kuhusishwa kwenye tuhuma za rushwa kwa wajumbe wa Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge zilizotolewa na Mbunge wa Moshi Mjini, Philemon Ndesamburo.


Barua ya Katibu Mkuu wa chama hicho, Wilbroad Slaa ya Januari 15, 2006, kwenda kwa Lowassa, inaeleza kushangazwa na ukimya wake pamoja na tuhuma hizo nzito zilizotolewa na Ndesamburo.


Taarifa za uhakika ambazo gazeti hili limezipata kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu zinaeleza kwamba, barua hiyo imeshafika katika meza ya kiongozi huyo wa tatu kimamlaka serikalini, baada ya Rais na Makamu wa Rais.


Hata hivyo jitihada za gazeti hili kuwasiliana ama na Lowassa mwenyewe au mwandishi wake wa habari, Said Nguba, ili kupata maoni yake kuhusu suala hili, zimekuwa zikigonga ukuta kwa takriban wiki moja sasa tangu Ndesamburo alipotoa tuhuma nzito wiki iliyopita, sambamba na kutangaza kujiuzulu ujumbe wa Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge.


Ofisa mmoja wa juu serikalini aliyezungumza na Tanzania Daima kwa sharti la kutotajwa jina, alisema Waziri Mkuu amekaririwa akiyaelezea maneno hayo ya Ndesamburo kuwa yasiyo na ukweli wowote.


Alipotakiwa na Tanzania Daima aeleze hatua ambazo Lowassa amepanga kuzichukua dhidi ya suala hilo ambalo kauli yake inahusishwa, ofisa huyo alisema, vyombo vinavyohusika vitalishughulikia.


“Sisi tunajua ni kwa nini Ndesamburo kasema maneno hayo. Tunajua kila kitu kinachoendelea kuhusu jambo hili. Ni vyema tukanyamaza. Waziri Mkuu anajua anachofanya, hawezi akasema maneno ya namna hiyo. Ipo siku ukweli utabainika,” alisema ofisa huyo wa serikali.


Badala yake, ofisa huyo wa serikali alieleza pia kushangazwa kwake na ukimya wa Mengi ambaye ndiye aliyetajwa na Ndesamburo kumwambia maneno hayo kuendelea kukaa kimya pasipo kutamka hadharani, iwapo ni kweli alifikisha maneno hayo au la.


“Ninyi mnamtafuta Waziri Mkuu atoe tamko, mbona hatujasikia Mengi akisema hadharani ni kweli kuwa alimwambia Ndesamburo maneno haya? Si yuko na anapatikana, mbona amekaa kimya?” alihoji ofisa huyo.


Slaa katika barua aliyomwandikia Lowassa anasema: “Pamoja na uzito wa tuhuma hizi na hasa ukizingatia uzito wa nafasi yako ya Uwaziri Mkuu mpaka sasa hujajitokeza wewe mwenyewe kukanusha au kukubali taarifa hii.


“Kwa vyovyote ukimya wako katika suala hili kadiri unayoendelea, unaweza kuwafanya wananchi kupoteza imani kuhusu msimamo wako katika vita dhidi ya rushwa na jihihada za kuleta utawala bora nchini.


“Kama kweli wewe ulifahamu kuwa kuna mtu ametoa rushwa kwa wabunge na hukuchua hatua zinazostahili, kwa vyovyote ni kinyume cha sheria, maadili ya uongozi, na dhamira ya Mheshimu Rais Jakaya Kikwete ya kupambana na rushwa bila kumfumbia macho mtu.


“Kwa upande mwingine, tuhuma kwamba mhimili wa serikali unaingilia mhimili wa Bunge zinakuelekea wewe (Waziri Mkuu) moja kwa moja kama kiongozi wa shughuli za serikali bungeni. Suala hili ni kinyume na utawala bora na mgawanyiko wa madaraka uliomo katika sheria na katiba ya nchi ambayo umeapa kuilinda,” ilieleza sehemu ya barua hiyo ambayo nakala yake imepelekwa kwa Rais Jakaya Kikwete na Spika wa Bunge, Samuel Sitta.


Tayari Spika amemwandikia barua Ndesamburo akimtaka kumwandikia kwa maandishi tuhuma za rushwa alizozitoa dhidi ya kamati hiyo.


Wiki iliyopita, Ndesamburo alitangaza kujiuzulu ujumbe katika kamati hiyo kwa madai kuwa alielezwa na Mwenyekiti wa Kampuni za IPP, Reginald Mengi, kuwa aliambiwa na kiongozi mwandamizi serikalini kwamba, wajumbe wa kamati hiyo wamepewa rushwa kutoka kwa mfanyabiashara, Yusuf Manji, ili asitendewe haki kwenye kesi yake na Mbunge wa Mkuranga, Adam Malima.


Ndesamburo alieleza kuwa anahofia usalama wa maisha yake na hataki kuhusika na maamuzi ambayo yanagubikwa na tuhuma za rushwa, huku akitaka kuitwa na Mengi na kiongozi huyo ili kuthibitisha madai hayo.


Akichangia bajeti ya Wizara ya Habari, Utamaduni na Michezo, Malima alimtuhumu Mengi kwa kujipa muda mwingi kujitangaza kwenye matukio yanayomhusu huku akitoa muda mfupi katika matukio yanayomhusu Rais na Waziri Mkuu.


Kutokana na tuhuma hizo, Mengi alilalamika kwa Spika kuwa Malima hakumtendea haki kumtuhumu sehemu ambako hawezi kujitetea.


Baada ya malalamiko hayo, Spika alipeleka mashauri hayo kujadiliwa kwenye kamati hiyo, hatua iliyozusha malalamiko kutoka kwa baadhi ya wabunge kuwa haikuwa haki.


Tayari Manji ameshatoa tamko kukanusha kuhusika kwa namna yoyote kuwapa rushwa wabunge na amemtaka Ndesamburo aeleze kile ambacho alidai kinafichwa katika suala hilo zima.
 
Inasemekana Mengi ana ushahidi wa kutisha kuhusiana na tuhuma za Ndesamburo.
Ndesamburo aliombwa na Sitta asijiuzulu,(maana inasemekana kwenye hili Sitta alikuwa upande wa Mengi) kwa sababu Sitta alitaka kuunda tume nyingine tena kuchunguza hizo tuhuma za Ndesamburo.Ndesamburo hakusikiliza ushauri wa Sitta,na kinachosemekana ni kuwa baada ya yeye kujiuzulu,hii issue imekuwa between CCM na upinzani(CHADEMA).Kihivyo,imemuweka Sitta katika wakati mgumu sana,maana hawezi kukipa bega chama.EL na Sitta inaonekana kama hawaivi.

Na leo hii asubuhi NDesamburo alihojiwa na Clouds FM na akaulizwa kuhusu yeye kumtuhumu Yusuf Manji....Ndesamburo akasema yeye anamshangaa Yusuf Manji kumshambulia,maana yeye Ndesamburo hakumtaja YUSUF Manji,yeye alitaja jina la Manji tu,unless yeye Manji aseme ni yeye tu mwenye hilo jina.

Kwa kifupi ni kwamba this has become quite damning to EL,maana inasemekana ushahidi alionao Mengi unamhusu EL.Mengi na Ndesamburo ni marafiki wa siku nyingi sana,na yeye Ndesamburo obviously anajua what Mengi has ndio maana akakimbilia kujiuzulu kutoka kwenye hio kamati,lakini hio sasa inaonekana kama ilikuwa ni wrong move.

Lets wait and see,but theres definately more to come on this
 
Zanaki if you say it was a wrong move what would have been the right one which could accommodate the truth ? Tuweke sawa . Mengi na Ndesa si wajinga na Sitta anajua kakali moto EL yuko kimya anatafuta namna ya kuupinga ushahidi wa Mengi lakini kazi ni kubwa . We cannot buy the arguement kwamba sasa ni CCM na Chadema huo ni utoto issue ni rushwa kubwa ambayo imekuwa engulfed na EL mengine ni mchezo wa kitoto mbona hakuna kati ya Lowasa ama Manji anayetaja kwenda Mahakamani kama kawaida yao ? Ukweli hapo upo na tutaona nini mwisho wake .
 
Zanaki,
Mwaga vitu. Naona points zako. Sasa naelewa kwa nini EL alimwambia Mengi kuwa wabunge wameshanunuliwa. Inaonekana alimtaka Mengi asiendelee na kesi ili ukweli wa kuhusika kwa El na Manji usijulikane. Uchafu huu ni lazima utoke kama Tanzania tutafika promised land.
 
Wrong or right move kwa Tanzania hakuna tofauti. Hawa akina EL wataendelea kula nji bila shida yeyote na huku wafuasi wao wakiwasifia kuwa viongozi hodari. Iweje kiongozi mzima akumbwe na kashfa ya namna hiyo lakini hadi leo anaendelea kupeta bila hata kushtuka kidogo. Ama kweli yasiyowezekana duniani kote yanawezekana Tanzania.
KIlichowazi ni kuwa Ndesamburo alikuwa anajua anachokifanya na naamini ni sahihi kuchukulia kuwa alikuwa na baraka zote za Mengi alipoamua kulihusisha jina lake, sasa kama watu hawa waliamua kupambana na Goliati Richmonduli waziwazi maana yake kuna ukweli wa kutisha kwenye hizi tuhuma. Viongozi (watawala) wetu hawaguswi kama huna ushahidi makini. Na bila shaka hayo Ndesamburo na Mengi wanayafahamu fika.

All said, ulikuwa ni upuuzi mkubwa kwa huyo Malima kwenda bungeni na kutoa hoja ya ovyo ovyo kama hiyo, who cares ITV wanampa nani much air time? Kama hufurahii kwa nini usiangalie, TVT, Chanel ten, Star etc. Lakini pili ilikuwa ni utoto kwa Mengi kulialia kama mtoto mdogo kwa sababu tu one irresponsible MP kaongea utumbo bungeni.
Tatu upuuzi mkubwa ni kutumia kodi zetu kujadili jambo hilo kwa vikao sitini wakati lingeweza kutumia saa moja (kama kulikuwa na ulazima). Cha mno kilikuwa nini kwenye hilo?
 
Tabasamu usemayo sahihi,ila ndo tumeshafika hapa.Zaidi 100M zimeliwa.Hivyo hatuna budi kupata ukweli.
Mie kwa ujumla bunge la Tanzania naliona ni upuuzi mtupu,pamoja na kuwa na watu waliosoma sawasawa lakini wanaleweshwa na rushwa wanapewa na serikali(posho za vikao,mishahara na marupurupu makubwa,Mashangigi pamoja na 25M wanazopewa kila baada ya miaka5).Zinawafanya wasi critisize na kusimamisha Shilingi ktk issue yoyote hata iwe bomu namna gani!!Wanaogopa kupoteza hivyo nilivyotaja hapo juu.Wasomi na wataalm wanagombania kuingia huku si kwa ajili ya uwakili ila ni hiyo rushwa ndo inawavuta.Hebu ipunguzwe(ingawa sitarajii) na kuwa posho halali uone moto utakavyowaka huko bungeni.Kwani wote watakaoamua kugombea hawatafuata pesa bali kuwawakilisha wananchi.
 
Kuna interesting point inaibuka hapa kuhusu uhusiano hafifu kati ya EL na Sitta.Anything to do with mpasuko ndani ya wanamtandao?Nilikuwa naongea na mtu mmoja Bongo ameniambia kuwa mbio zakuelekea Ikulu 2010 ni kama zimeshaanza na pia kuna tetesi za mpasuko ndani ya wanamtandao.Inasemekana pia kuwa JK anamwandaa Dr Mwinyi kumrithi Karume suala mabalo baadhi ya watu hawaafikiani nalo.Watabiri wasio rasmi wa siasa za bongo wanadai kuwa kuna mengi yatajitokeza zaidi wakati CCM inatengeneza timu yake kwenye next election ya chama hicho.
 
Mlalahoi
Habari za Mwinyi ni kweli . Mpasuko wa mtandao sina hakika ila EL anautaka Urais mwaka 2010 kazi kubwa iko .Spika na EL kutoiva inawezekana maana wote ni wala rushwa sasa kazi kubwa .
 
hata mimi nasikia habari za mwinyi ni kweli na ndio mana akaacha jimbo lake la mkuranga kuhamia zbar ni hatua za kujitayarisha kumrithi karume.
 
Ukweli sisi wananchi wa kawaida tulie tu. Spika alishasema hata wabunge wenyewe watapewa 'summary' ya ripoti na sio ripoti kamili, sasa kama hali ndio hiyo I doubt kuhusu utawala bora, na tafsiri ya hilo suala ni kuwa atakayeujua ukweli wote wa kwenye ripoti ni spika na wajumbe wa kamati!
 
Lunyungu,the right move would have been to stay in the kamati,kwa sababu Sitta alitaka ku-explore tuhuma za Ndesamburo kwa kuunda kamati nyingine.Sasa kama ulivyoona Chadema wameshamwandikia EL barua,kwa kufanya hivyo inaonekana kama wao wameivalia njuga hio issue,hence sasa kuonekana kuwa its now between CCM na CHADEMA.Lakini kama Ndesamburo angebaki,Sitta ilikuwa afanye kama nilivyosema hapo juu.

Ni kweli wabunge wamechukua pesa kutoka kwa Manji,na hili tulili-discuss humu siku nyingi wakati kamati hiyo ndio kwanza imeundwa.Inasemekana Mengi aliombwa a-withdraw malalamiko yake dhidi ya Malima,lakini aligoma(tena inasemekana kwa jeuri) kwa sababu ya huo ushahidi.

Vitu zaidi vinakuja...
 
Jeikei,
Hii report ya Ndesa ni muhimu sana mbona imekwatwa katwa?
Vipi haiwezekani kupatikana yote.... maanake hicho kidogo tu kimeniacha domo wazi... ama kweli Rule of Law nchini hakuna kabisa!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom