Mengi vs Manji: Ukweli ni upi?

Hata mtoto wa kindergarten anajua kuwa hawa NSSF wanaendekeza udini.Kama kuna watafiti ama researchers anzeni kuangalia kuanzia ngazi ya juu chini ndani ya shirika letu tukufu linaloheshimika kwa kufuja mishahara ya wazee wetu wastaafu wasio na hatia kwa mambo ya anasa.
I short huyo muheshimiwa mdau ameweka mitandao ambayo inahalalisha dini yake inapewa kipaumbele katika kila kitu ndani ya hilo shirika kuanzia ajira,kusoma,kupandishwa cheo,mikopo,mikataba minono lakini mibovu na mambo mengi ambayo hayafai kuelezwa kwani yanahitaji pia uchunguzi wa kina.
 
Kilbark

Mbona unajibu kwa emotions? Nimeuliza maswali mepesi ili niweze kuchangia katika mjadala.

Kwa kuwa wewe si mtoto wa kindergarden, naomba unijibu:

Je Dr Dau ni dini gani?

Je Dr Dau ni kabila gani?

Au wewe dini yako ni tofauti na ile ya Dr Dau?

Jibu Hoja please!
 
Kwani Kuna Haja Gani Ya Kulipa Hiyo Kodi, Kama Kodi Yenyewe Inaishia Mifukonio Mwa Wajanja Wachache, Maana Tangu Watanzania Tulipoanza Kuambiwa Kuwa Pato La Taifa Limeongezeka Mara Nyingi Tu,ni Muda Gani Umepita Watanzania Hawana Makuu Wewe Ukiwa Kiongozi Na Ukitaka Kutafuna Pesa Yao Ni Kuwatangazia Tu Figa Uliyopata Halafu Unawaacha Wanapiga Makofi Na Vigelegele Baada Ya Hapo Ni Kuanza Kuzitafuna Tu Maana Najua Huwa Hawaulizi Matumizi.kwani Kenyata Alipomwambia Nyerere Anatawala Marehemu Alikosea?kwani Kutawala Tanzania Kuna Ugumu Gani Hata Chizi Anaweza Kutawala Cha Msingi Awe Muongo Tu, Na Mambo Yatakuwa Bam Bam
 
Hata Kama Wewe Ni Kiongozi Halafu Ukaboronga Mahala Usiwe Na Wasiwasi Cha Msingi Wewe Wapoteze Maboya Tu Yaani Unatafuta Waandishi Wa Magazeti Wawili Unawakatia Halafu Unawatungia Hadithi Yoyote Ya Uongo Kama Vile "nitawaleta Wataalamu Kutoka Thailand Na Watakuja Kutengeneza Mvua Mara Moja Kwa Hiyo Hatutakuwa Na Ukame Daima Na Milele"baada Ya Hapo Wanasahau Mabaya Yako Tena Kwa Miaka Mitano Na Usijali Maana Hakuna Atakayekuuliza. Si Marehemu Hao
 
Kama magazeti ya ippmedia yaliandika habari za kweli kuhusu Quality Group na kama Quality Group wanaona kuwa habari zilizoandikwa na magazeti hayo ni za uongo na za kashfa kwanini Mengi anataka wakae chini wazungumze? Ni mgongano gani kati ya Watanzania wa rangi mbalimbali anaohofia Bw. Mengi? Hivi mgawanyiko kati ya Wahindi wa Weusi umeanza leo kwenye kisa cha mashirika hayo makubwa na kati ya watu hawa matajiri zaidi nchini?

Ni kitu gani ambacho hawakisemi???

Acheni mahakama iamue!!!!
Tujikumbushe walikotoka hawa wafanyabiashara bwana Manji na Mengi na sasa wengine wanne wakiwa na Rostam.
 
Zanaki kwanza karibu
Halafu nakuomba useme kwa sauti kubwa kwamba unan Uhakika JK si mla rushwa ? Una uhakika huo kwamba anaangushwa na wenzake lakini yeye ni safi ? Baaada ya hapo ujiandae kujibu maswali zaidi . Hapa tunakata issue na si kampeni .Nijibu kwanza
Zanaki aje ajibu hii
 
Zamani,nilikuwa nadhani ubaguzi ni kitu kibaya sana.Baadye nikaelimishwa kuwa kuna ubaguzi wenye manufaa.Na huo ndio naomba utumike hapa.Let's be realistic,forum hii ni babkubwa zaidi ya zote.Pengine haijulikani sana lakini la uhimu sio kujulikana kwa sababu,kwanza,kizuri chajiuza chenyewe,na pili,ijulikane sana ili iweje.Uzuri wa forum hii ni mkusanyiko wa vichwa vyenye kujua uchambuzi na vyenye uchungu wa dhati wa nchi yao.Kwa matinki hiyo,ni dhahiri kuwa tukiwaacha bila kuwadhibiti hao wanaotufanya tukutanike hapa (wala rushwa,matapeli,wanasiasa uchwara,majambazi,wababaishaji pamoja na wapambe wao) basi tutakuwa tunajaribu kushindana na kanuni za asili kwamba maji na mafuta kamwe hayachanganyiki.Nikishauri kuwabagua simaanishi kuwa watu wasiojulikana mttizamo wao wasiruhusiwe kuposti mada.Hapana,wanaopaswa kudhibitiwa kwa nguvu zote ni hao wanaotumwa kuharibu forum hii.Nasema wanatumwa kwa vile tunawajua wanaokula nchi yetu ni wavivu wa kutembelea sehemu kama hizi,wanaacha kazi hiyo kwa vibaraka na wapambe wao.

Kwa hiyo Bwana Administrator,mimi naomba kutoa hoja:ubaguzi wenye manufaa unahitajika kwenye forum hii,na kwa namna flani hilo limewezekana.Uhuru ni mzuri lakini uhuru bila sheria ni vurugu.Na sheria ni neno lenye tafsiri tofauti.Kwangu,sheria ni muhimu katika kudhibiti vurugu.Kwa mpambe wa mla rushwa anayetaka kuharibu forum hii,sheria zitazomdhibiti zitaonekana kwake kama unyanyasaji au uonevu.But who cares?Acha walalamike lakini waungwana tunakutana hapa kujaldili hatma ya nchi yetu.Trust me,jamboforums ni for the time being THE best among TZ forums,na naamini kuwa ina nafasi nzuri ya kupanuka hadi kwenye forms nyingine kama majarida au hata redio (sifa za forums zitazagaa,wafadhili watajitokeza,hasa wale wenye uchungu na nchi yao na wale wanaopigania haki duniani,na mwishowe tunaweza kujikuta na Jambo as a magazine au Jambo Radio...Let's keep it up!!!
Unabii
 

Similar Discussions

3 Reactions
Reply
Back
Top Bottom