Mbona Hassy Kitine hakualikwa/hakuhudhuria?

Mbona Hassy Kitine hakualikwa/hakuhudhuria?

Nimeufuatilia huu uzi mwanzo mwisho ila sijaona lolote la maana zaidi ya historia na sifa kedekede za wana usalama wa taifa wa kipindi hicho...jambo la kushangaza ni kwamba mpaka leo uchumi hovyo demokrasia mahututi bin taaban usalama wenyewe nao uko mashakani...

hata hawa millenials wetu wakituangalia wanashindwa kuelewa hizi sifa ni za nini hasa na kwa manufaa gani yasiyoonekana.

Itoshe kusema basi tukae kama taifa na kujadili aidha tuwe nao au tuwafutilie mbali hii idara isiyojulikana kama inalitumikia taifa au chama tawala. Huu ni usalama wa taifa kwa maslahi ya taifa au maslahi ya watawala...hapa tunahitaji mjadala mpana kwa manufaa ya taifa...

malengo ya kuundwa kitengo hicho yalikuwa nini hasa na je bado yanafaa kwa dunia ya sasa tuliyonayo?

kwa mujibu wa vipimo vya mkemia mkuu
Mkuu Usalama wa nchi hii sio kwenye Uchumi na Ufisadi
Bali ni kuilinda CCM
Kuangalia Ufisadi ukifanyika bila kuuzuia
Kuvuruga vyama vya upinzani
BUT kwa sifa wanazopewa basi nchi hii kwa Uchumi ingetakiwa tuwe namba 1 Africa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
..nilimuona Mzee Mwanguku mstaafu wa Magereza naye amealikwa.

..Mwanguku ni wa zamani labda aliondoka Magereza kabla hata Mzee Mwinyi hajaingia madarakani. Sina uhakika lakini.

..Pia sina uhakika kama alistaafu mwenyewe au kuna mtikisiko ulitokea akalazimika kujiuzulu. Naomba unikumbushe kuhusu suala hili.

NB.

..IGP Philemon Mgaya, Gen.David Musuguri, Gen.Marwa Waitara, na Col.Hassy Kitine,.ndiyo wastaafu ambao hawakuhudhuria.

..Inawezekana wanasumbuliwa na matatizo ya utu uzima.

Cc Pascal Mayalla
Mwanguku alikuwa kamishna wa Magereza miaka ya 1990 na umri wa kustaafu ulifika mrithi wake alikuwa Jumanne Mangara

Sent using Jamii Forums mobile app
 
kwaninavyomjua Kitine huwa hapendi mambo ya kipuuzi.

Kwa taarifa yako amebaki jina tu, hana impact, halafu isitoshe yeye miiko ilimshinda, unakumbuka alidanganya akaenda kumtibia make wake gono Ulaya?
 
Mi kesho jpili baada ya kutoka ibada nitakwenda nielekeze kambi gani nikachungulie nione hekaheka zao
JKT Kanembwa operation Kimbunga kulikuwa na dogo form six katk risasi kumi alikosa target moja tuu. Ktk mita 100. Alipewa offer ya kuendelea na jeshi alikataa kisa anataka kuingia chuo. Hao masniper wapo na wanazidi kuzaliwa hata hivyo kutofautiana kwa ujuzi kupo.
 
Emilio Mzena ambaye nae aliwahi kuwa Mkurugenzi Mkuu wa TISS bado yupo hai? Sijamsikia siku nyingi? Huyu ndio aliyeratibu kumtorosha Mwalimu Nyerere na Kawawa Ikulu na kwenda kuwaficha Kigamboni mwaka 1964 wakati Jeshi lilipoasi.

Kwa mchango wake mkubwa ndani ya Idara, Hospitali ya wanakitengo pale Makumbusho imepewa jina lake.
 
Kama nakumbuka sawasawa Mzee Kitine aliwahi kuwa mkuu wa kitengo chetu pale Eagle house. Sikumwona kwenye picha. Najua wana Eagle mmo humu. Tujuze yuko wapi na kwa nini hakuhudhuria?
Kwani ilikua lazima kuhudhuria?
Ulimuona waitara?je kama alikua mgonjwa au yupo nje ya nchi?
 
Ni Kweli kabisa na Hata Afande Kimario Mwenyewe alitumia Hati ya kusafiria ya Ghana sio Tanzania

Wale Jamaa haitokuja tokea Sytem strong Kama ile, iliyotibua Mapinduzi na Uhaini Mara 8 ikiwemo kumsaidia Raila Odinga kumtikisa Daniel Arapa Moi 1983 na jaribio liliposhindwa wakamtorosha Raila mpaka Canada Ikiwa ni revenge kwa Kenya kusaidia Uhain wa kina Kapten Maganga na Akina Maghee Upande wa Tz

Kipindi hicho Tanzania ilikuwa Israel ya Maziwa Makuu na Africa Mashariki kwa jumla sio hii ya Leo Kibiti inatutoa jasho
.......
......Tumepotea?
 
Emilio Mzena ambaye nae aliwahi kuwa Mkurugenzi Mkuu wa TISS bado yupo hai? Sijamsikia siku nyingi? Huyu ndio aliyeratibu kumtorosha Mwalimu Nyerere na Kawawa Ikulu na kwenda kuwaficha Kigamboni mwaka 1964 wakati Jeshi lilipoasi.

Kwa mchango wake mkubwa ndani ya Idara, Hospitali ya wanakitengo pale Makumbusho imepewa jina lake.
Sasa kama unajuwa hospitali ya Usalama wa Taifa pale Kijitonyama inaitwa Mzena Memorial, je ulijipa hata nafasi ya kujiuliza nini maana ya Memorial?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu analysis na historian kuchanganywa hivi kunaonyesha jinsi ujamaa umejiharibu hadi ndani. Hizi habari na usemaji wake una mixed ideas. Huwa uswahilini hii style huwafaa sana akina Mohammed said.
Wala Sijaelewa ulichokisema ama ulichokimaanisha.

Karibu tena kwa ufafanuzi.
 
Malisa yupo Wa Afya Njema.
Labda kama unamsema Malisa Godlisten, lakini kama ni Onel Malisa kamishna mkuu mstaafu wa Magereza alishafariki msiba ulifanyika nyumbani kwake Kinyerezi kwa Malisa na nilihudhuria, hii ni family friend na familia yangu, mtoto wa Onel Malisa nimesoma naye same class Oystebay Primary school, baadaye akaagwa kwa heshima za jeshi kwenye gereza la Ukonga na baadaye kusafirishwa na kuzikwa nyumbani kwao Old Moshi.

Natowa onyo msipende kuinajisi JF watu wengi wanaitegemea kwa information kama hujui kitu shut up tuliza wowowo lako.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Labda kama unamsema Malisa Godlisten, lakini kama ni Onel Malisa kamishna mkuu mstaafu wa Magereza alishafariki msiba ulifanyika nyumbani kwake Kinyerezi kwa Malisa na nilihudhuria, hii ni family friend na familia yangu, mtoto wa Onel Malisa nimesoma naye same class Oystebay Primary school, baadaye akaagwa kwa heshima za jeshi kwenye gereza la Ukonga na baadaye kusafirishwa na kuzikwa nyumbani kwao Old Moshi.

Natowa onyo msipende kuinajisi JF watu wengi wanaitegemea kwa information kama hujui kitu shut up tuliza wowowo lako.

Sent using Jamii Forums mobile app
Asante kwa Taarifa na Pole Sana kwa familia yake, binafsi sikuwa nafahamu hilo. Nikiri pia kuwa na ukaribu wa "kiasi" na hiyo familia lakini sikupata taarifa za huo msiba wa ghafla.

Again shukrani ingawa onyo sijalipokea.
 
Salute kwenu wote mnaopita kimya na mnaocomment humu mchango wenu eagles ni mkubwa mbali na kelele nyingi za miluzi ambazo naamini hazimpotezi mbwa. wapo watu wenye imani moja na nyinyi "state over everthing"
Once again hongereni sana.
 
Back
Top Bottom