Mazishi ya Mh. Regia Mtema huko Ifakara (updates)

Mazishi ya Mh. Regia Mtema huko Ifakara (updates)

Nakulilia mdogo wangu na rafiki yangu Regia. Niko kitandani hapa nakabiliana na maradhi (kama ulivyokuwa unajua). Nimefuatilia yaliyokuwa yanajiri tangu kifo chako kwa majonzi sana. Nimesikitika sana lakini nimefarijika kwa kuwa moyo wangu umeniambia umelala mahali pema. Nauamini moyo wangu ndio maana naamini iko siku moja tutaonana tena. Kwaheri mjukuu wangu, kwaheri rafiki yangu kwaheri Regia wangu. Upumzike kwa amani mama.
Pole sana Asprin.Kumbe bado unagonjwa?upone haraka tumekumisi jamvini.
 
Tunashukuru sana mama yetu Josephine kwa updates zote,umetufanya tujisikie kama nasi tumehudhuria msiba.tunamuombea dada regia apumzike kwa amani!
 
Inauma sana,ina maana siku unatuhutubia pale UDOM,siku ya uzinduzi wa tawi,ilikuwa siku yangu ya mwisho? Regia regia reggggiiií tjmgajptmjgjtjg
 
Asante kea updates! Jioni hii natumaini shughuli zimekwisha, kama siamini Rm amekwenda moja kwa moja!!
 
Vimvua vya furaha kuonyesha kua hata mbingu imefurahia kurejea kwa dada yetu Regia Mtema huko mbinguni,baada ya wajibu wake na mazuri yete aliyoifanyia Tanzania!Morogoro ilikupenda sana dada,Tanzania ilikupenda pia,kapumzike kwa amani Reggy
hakika mkuu hali ya hewa ni ya utulivu hapa ifakara manyunyu kwa mbali mji wote zimebaki story za dada yetu regia.tuzidi kuiombea familia yake ibaki na amani na MUNGU awape faraja yake.TUNAOMBA TANESCO warudishe power maeneo ya ifakara.
 
pumzika mama!...

...you must be in a better place now!...we all pray for that..!
 
Taratibu, mmoja mmoja tuna kwenda mbinguni kwa baba na kila mmoja wetu atakwenda kwa njia yake....

Kwa heri Kamanda Regia......
 
Jamani, kuna kitu au vitu mimi kiasi nashindwa kuvielewa hasa juu ya mambo yanayosemwa na watu mbalimbali juu ya Marehemu wetu Regia.

Nikisikiliza hayo maneno na sifa zinazotolewa juu yake na nikiangalia umri alofariki nao, kiasi fulani nashawishika kusema MANENO KAMA PENGO LAKE HALIZIBIKI AU HATATOKEA MTU KAMA HUYU, naona kama zinasemwa kwa UNAFIKI TU, given the young age of her, ni lipi/yapi hasa aloyafanya kiasi cha kupata hii attention yote.

Ni wangapi wema zaidi ya Regia wamefariki na hawakupata attention yoyote??? Nafikiri kuna haja ya jamii yetu kujiangalia kwa undani je tunayoyafanya kweli yana maananisha hicho kilichopo moyoni mwetu au ni ile tu watu waseme na yeye alisema???
...sekunde,masaa,siku,miezi au miaka hizi ni namba tu,kitu tunachoangali hapa ni matendo yako ktk muda ulioishi hapa duniani,je umefanya nini?.Unaweza ukabahatika kuiishi ata miaka zaidi ya mia lakini usifanye kitu cha maana kitakacho kufanya ukumbukwe,lakini unaweza kuishi miaka michache sana kama Regia lakin ukafanya mambo ambayo yatakumbukwa kwa muda mrefu.Kwahiyo ndugu yangu "babayah67" elewa-kwamba matendo mema ya mtu huwa hayafi na ndo maana Watanganyika hadi leo tunaishi na Nyerere kwa kukumbuka mazuri iliyotendea nchi hii...R.I.P Regia
 
asante sana Dr, kwa kujali na kuwa msikivu. Mambo haya wala hayahitaji kutembea na warehouse, ni laptop tu yenye uwezo mzuri na kamera, bila kusahau mtu makini na mwenye mapenzi na kazi ya habari. Hu umekuwa wimbo kama si kilio cha muda mrefu kuhusu idara ya hbr ya CDM. Mbona ni kitu kdg tu, hata mimi niliyesoma shahada ya wanyamapori nafanya.

Unachokisema inawezekana kilikuwa na ukweli lakini unapaswa kufahamu matatizo ya coverage ya network kwa nchi kama tanzania na baadhi ya nchi zilizoko katika mstari wa Ikweta. Dr. Slaa alifafanua vema kuwa ni matatizo ya network na siyo labda kama unavyojaribu kusema kuwa ni shida ya hardware ( capability ya computer)

Kuna sehemu mkifika katika nchi hii ni lazima wataalamu wafanye kazi ya kujenga temporaly network waweze kufanikisha zoez zima
 
Kuna mkenya mmoja ameniuliza swali gumu, nikashindwa kujibu na akanipa jibu lililo nisisimua sana, naomba kama kuna mtu mwenye jibu zuri zaidi anisaidie. Nimeulizwa, Regia alikuwa nani? Mbona ameziteka sana nyoyo za watanzania? Nilimjibu alikuwa mbunge wa watu. Akaniambia wapo wengi na pia tangia amekaa Tz hajawahi kuona mazishi makubwa hivi ukiachilia nyerere. Akasema hata kawawa hakupata mazishi makubwa hivi. Hapo nilikosa jibu. Akaniambia Mandela alishawahi kusema "Mtu shujaa atazikwa kwa heshima na historia yake inaanza kuandikwa siku ya kifo chake na siku zote watu watasema, hapa amelala mtu shujaa, lakini mtu mwoga mwisho wa historia yake ni pale udongo wa mwisho utakapowekwa kwenye kaburi lake. Kwa hiyo akasema Regia amewavuta sana Watanzania na ameweza kupasua pazia la vyama, ukabila , udini nk kwa kuwa alikuwa shujaa na daima watu watalitembelea kaburi lake na kusema hapa amelala shujaa.

Maneno haya yamenigusa sana. Ni kweli Regia hakuwa na pesa, wala hakuwa na uzoefu wa kisiasa,wala hakuwa na elimu kubwa, tena alikuwa na ulemavu ila alikuwa jasiri shujaa. kuna mabilionea na maprofesa wamezikwa, leo wala hakuna anayewakumbuka. Hawakuwa mashujaa, walikuwa waoga na kujali maslahi binafsi ambayo mwisho wake ulikuwa ziku za kuzikwa kwao.

Tujifunze kwa Regia, Nyerere at el, fanya kazi ya umma, kuwa mtu wa watu, kuwa mkweli, shujaa na usiwe mwoga, wala usiweke maslahi ya familia yako mbele, utazikwa kama shujaa. Una nafasi ya kuchagua kuwa shujaa ufe masikini ila uzikwe kwa heshima na ukumbukwe milele au uwe mwoga, uwe tajiri wa rushwa ila uzikwe kama mbwa! Mwana JF ni wakati wa kuchagua!
 
Unachokisema inawezekana kilikuwa na ukweli lakini unapaswa kufahamu matatizo ya coverage ya network kwa nchi kama tanzania na baadhi ya nchi zilizoko katika mstari wa Ikweta. Dr. Slaa alifafanua vema kuwa ni matatizo ya network na siyo labda kama unavyojaribu kusema kuwa ni shida ya hardware ( capability ya computer)

Kuna sehemu mkifika katika nchi hii ni lazima wataalamu wafanye kazi ya kujenga temporaly network waweze kufanikisha zoez zima

Nadhani wewe ndio unapaswa kuelewa kwenye hili, Chadema ina tatizo Sugu katika kitengo cha Public relation na hili si tatizo la leo tu, hapa huwa tunasimamia ukweli no matter Kwamba Dr Slaa ndio ametoa hii excuse lakini mimi hainiingii akilini hata kidogo, ziko Blog wameshapost picha za leo msibani why not hao maofisa wa Chadema? tabia za kizembe za kiccm hazikubaliki kamwe.
 
Matola,

..katika ile thread ya kwanza ya taarifa ya msiba huu Kiranga alitoa rambirambi zake.

..kwa mtizamo wangu Kiranga always expected the best frm Regia[r.i.p] na ndiyo maana mkaona mara kwa mara alikuwa akimbebea bango.


Mkuu kwa jinsi ulivyomuwakilisha na kumsemea Kiranga ni kama vile umeongea nae kabla hujapost.

Nways all is well.
 
ni CHADEMA....na ndio maana kila pande ya nchi na hata ambao tupo nje ya nchi tunasikitika kwa pamoja
 
Kuna mkenya mmoja ameniuliza swali gumu, nikashindwa kujibu na akanipa jibu lililo nisisimua sana, naomba kama kuna mtu mwenye jibu zuri zaidi anisaidie. Nimeulizwa, Regia alikuwa nani? Mbona ameziteka sana nyoyo za watanzania? Nilimjibu alikuwa mbunge wa watu. Akaniambia wapo wengi na pia tangia amekaa Tz hajawahi kuona mazishi makubwa hivi ukiachilia nyerere. Akasema hata kawawa hakupata mazishi makubwa hivi. Hapo nilikosa jibu. Akaniambia Mandela alishawahi kusema "Mtu shujaa atazikwa kwa heshima na historia yake inaanza kuandikwa siku ya kifo chake na siku zote watu watasema, hapa amelala mtu shujaa, lakini mtu mwoga mwisho wa historia yake ni pale udongo wa mwisho utakapowekwa kwenye kaburi lake. Kwa hiyo akasema Regia amewavuta sana Watanzania na ameweza kupasua pazia la vyama, ukabila , udini nk kwa kuwa alikuwa shujaa na daima watu watalitembelea kaburi lake na kusema hapa amelala shujaa.

Maneno haya yamenigusa sana. Ni kweli Regia hakuwa na pesa, wala hakuwa na uzoefu wa kisiasa,wala hakuwa na elimu kubwa, tena alikuwa na ulemavu ila alikuwa jasiri shujaa. kuna mabilionea na maprofesa wamezikwa, leo wala hakuna anayewakumbuka. Hawakuwa mashujaa, walikuwa waoga na kujali maslahi binafsi ambayo mwisho wake ulikuwa ziku za kuzikwa kwao.

Tujifunze kwa Regia, Nyerere at el, fanya kazi ya umma, kuwa mtu wa watu, kuwa mkweli, shujaa na usiwe mwoga, wala usiweke maslahi ya familia yako mbele, utazikwa kama shujaa. Una nafasi ya kuchagua kuwa shujaa ufe masikini ila uzikwe kwa heshima na ukumbukwe milele au uwe mwoga, uwe tajiri wa rushwa ila uzikwe kama mbwa! Mwana JF ni wakati wa kuchagua!

Ni ukweli mtupu.
 
Pole sana Asprin.Kumbe bado unagonjwa?upone haraka tumekumisi jamvini.


Mama ulikwenda Ifakara kumsindikiza kamanda Regia? Sijakuona hapa muda mrefu.

Btw, huyo babu yako keshapona, nenda kule uwanja wa nyumbani Mount Meru University (MMU) utamkuta anafanya mazoezi ya kulenga shabaha.
 
Inauma sana,ina maana siku unatuhutubia pale UDOM,siku ya uzinduzi wa tawi,ilikuwa siku yangu ya mwisho? Regia regia reggggiiií tjmgajptmjgjtjg

nakumbuka aisee, ki2 cha ng'ox, alikuja na lema alitaja familia 9 zinazotawala tz. 4rm hapo nilimkubali hadi ana2toka. R.i.p mama
 
Back
Top Bottom