Mazishi ya Mh. Regia Mtema huko Ifakara (updates)

Mazishi ya Mh. Regia Mtema huko Ifakara (updates)

HATIMAYE HATUNA REGIA TENA! Mungu utupe nguvu maana watu wako tumekata tamaa. RIP my beloved sister!

Tumuombe Mwenyezi Mungu atuinulie Regia mwingine ili aweze kuendeleza ndoto alizokuwa hajatimiza kwa watanzania wenzake.
 
Hakika tumemaliza.

Salamu za shukrani kutoka kwa familia.

Nawashukuru nyote mlionipa ushirikiano nilipokuwa na post kwa uchache sana.Asanteni kwa kunisahihisha pale nilipokosea.

Tutaendelea kuwa pamoja.

Regia alisema,JF ni shule na pia ni numbani,ni kweli haijawahi kupita siku bila kungulia JF.

ASANTENI SANA.

Bravo Mama kwa kazi nzuri .Pale ulipokosea umefanya hivyo kama binandamu na hukuwa na hira ndani mwako. Mungu wa Bwana Yesu akutangulie katika safari yako na wengine wote na uendelee kuwa visionary na proactive.You are role model
 
Dada Josephine asante sana na Mungu akubariri, japo tuko mbali hakika kupitia wewe tumeshiriki kumzika mpendwa wetu Regia. Ubarikiwe sana dada, Acha Regia apumzike sasa
 
Kwa wale wote mliohudhuria maziko.

Ni vizuri sana kushika wasia wangu.

Kwa wale wanaotumia vyombo vya moto ni vizuri sana kufuata sheria za barabarani ikiwa pamoja na kufunga mikanda wakti chombo kinakwenda na wale wa vyombo vya matairi mawili au matatu ni vizuri kuvaa kofia ngumu.

Vile vile kumbukeni mwendo kasi ni khatari kubwa.
Msisahau kuwa Pombe ni khatari kubwa kwenu jiepusheni na pombe mnapoendesha vyombo vya moto.

Lakini pia tunajuwa wengi mumechoka sana hususan katika harakati mzima za maziko. Kuweni makini na dereva kusinzia akiwa njiani.

Kumbukeni tunawapenda sana wote na tunawatakia safari njema na Mola awatangulie.
Mkuu Barubaru umenena ukweli, kufunga mikanda ni muhimu saana!!!!!!!!! Naomba niongezee kidogo tuu, dereva pumzika kwanza kama umechoka ili usije kulala kwenye usukani!!!!!!!!!!!

FUNGENI MIKANDA KUANZIA DEREVA HADI ABIRIA!!!!!!!!!!! WAENDESHA PIKIPIKI VAENI HELMET WOTE DEREVA NA ABIRIA!!!!!!!!!! CHUNGA MAGARI MENGINE PIA, USIOVERTAKE KAMA HUONI MBELE KUNA NINI!!!!!!!!!!

MBARIKIWE WOTE, TUNAWATAKIA SAFARI NJEMA KURUDI KWENYE VITUO VYENU!!!!!!!!!
 
mkuu mm mkristo, ila naona bandiko la pasco lina logic aisee, bora kuweka picha nzuri watu waione kuliko uso ulioharibika.

Nakubaliana na wewe Mkuu. Regia amefariki kwa ajali iliyopasua kichwa chake, so lazima kutakuwa na uharibifu mkubwa wa sura, ndio maana hata picha 2zionazo magazetini na kwenye TV hazioneshi sura kwa karibu. Jambo la muhimu ni kwamba Mwili wa Regia umepumzika sasa, tuendelee kumuombea.
 
Nakulilia mdogo wangu na rafiki yangu Regia. Niko kitandani hapa nakabiliana na maradhi (kama ulivyokuwa unajua). Nimefuatilia yaliyokuwa yanajiri tangu kifo chako kwa majonzi sana. Nimesikitika sana lakini nimefarijika kwa kuwa moyo wangu umeniambia umelala mahali pema. Nauamini moyo wangu ndio maana naamini iko siku moja tutaonana tena. Kwaheri mjukuu wangu, kwaheri rafiki yangu kwaheri Regia wangu. Upumzike kwa amani mama.

Pole mkuu kwa kuugua, twamuomba Mungu akujaalie afya njema ili tuendelee na mapambano ya kuikomboa nchi yetu. Maneno yako yamenitoa machozi.
 
Nakulilia mdogo wangu na rafiki yangu Regia. Niko kitandani hapa nakabiliana na maradhi (kama ulivyokuwa unajua). Nimefuatilia yaliyokuwa yanajiri tangu kifo chako kwa majonzi sana. Nimesikitika sana lakini nimefarijika kwa kuwa moyo wangu umeniambia umelala mahali pema. Nauamini moyo wangu ndio maana naamini iko siku moja tutaonana tena. Kwaheri mjukuu wangu, kwaheri rafiki yangu kwaheri Regia wangu. Upumzike kwa amani mama.
Pole sana rafiki............ kwa kweli inahuzunisha sana
 
Nakulilia mdogo wangu na rafiki yangu Regia. Niko kitandani hapa nakabiliana na maradhi (kama ulivyokuwa unajua). Nimefuatilia yaliyokuwa yanajiri tangu kifo chako kwa majonzi sana. Nimesikitika sana lakini nimefarijika kwa kuwa moyo wangu umeniambia umelala mahali pema. Nauamini moyo wangu ndio maana naamini iko siku moja tutaonana tena. Kwaheri mjukuu wangu, kwaheri rafiki yangu kwaheri Regia wangu. Upumzike kwa amani mama.

Mkuu tunakuombea upate uponyaji na kurejea katika uzima wako kama ilivyokuwa awali ili uendelee kuitumikia familia yako, JF na Tanzania kwa ujumla.
 
Mbona Nyerere alikaa siku 3 kama sikose pale uwanjani? kwa kuwa ni utaratibu uko hivyo, wacha uendeleeeeeeee, maana huwezi sema kwa kuwa aliagwa dar basi, ifarakara nao wanahaki

Mkuu kumbuka dada Regia alikuwa na majeraha makubwa kichwani, nadhani hapo ndipo point ya Pasco ilipo. Na inaonekana dawa zilizotumika kuhifadhi mwili wake hazikuwa nzuri.
 
Dada Josephine mbona unatuliza upya jamani? Asante kwa taarifa dada japo zinaumiza sana. Pumzika Regia, pumzika kwa amani.
 
Mama yetu Josephine twakushukuru sana kwa moyo wako wa kujitolea. Tambua kuwa Mungu akitujaalia uzima mwaka 2015 wewe ndiye utakuwa mama mjengo officially ingawa kwa sasa sote tunatambua kuwa u mama wa kwanza mioyoni mwa watanzania wengi, nakushauri sana endeleza hii tabia uloionyesha leo ya kujishusha na kuwa karibu sana na watu, take my words heshima yako itakuwa juu kwa vizazi vyote Tanzania.

Leo nimekukubali sana mama yetu.
 
Naomba kutoa shukrani zangu Kwa Josephine, Pasco na wengine waliofanya juhudi za dhati kabisa kutu habarisha kilichokuwa kina endelea.....Asanteni sana


R.I.P REGIA hakika tutakukumbuka......
 
Mkuu Josephine,

Hakika nikiwa ofisini nilisitisha shughuli zangu zote na kufatilia maziko ya mpendwa wetu Regia Mtema. Umeonyesha ni kwa kiasi gani unavyojitolea katika jamii na kujishusha kwa kutupatia updates ambazo mnacho kitengo ndani ya Chadema cha kufanya uliyoyafanya.

Btw, nakushukuru, nakupongeza na udumu katika kuwa karibu na wananchi kama hivi. Pole sana kwa machungu ya kufiwa kwa ukaribu uliokuwa nao na marehemu. Sisi waislamu hunena 'INNALILLAHI WAINAILAIH RAJIUN'.
You deserve to be WHO you are !!!
Hatimaye yametimia! Huzuni zetu zisitufanye kusahau kumshukuru na kumsifu Mungu kwa kutuletea Regia duniani! Kupitia dada Regia Mungu ameonyesha upendo wake na jinsi tunavyopaswa kuishi kwa kujitoa kwaajili ya wengine! Mungu ni mwema sana na daima anatuletea mifano hai ili tujifunze kuwa inawezekana! Turudishe sifa kwa Mungu kwa upendo wake kupitia dada yetu Regia Mtema! Hakika Acha Mungu aitwe Mungu! Asante dada Regia kwa kuitii dhamira njema ya Mungu kujitoa kwaajili ya wengine na hakika safari yako ya Wokovu imetimia!!
 
Dah!......

Hakika wema hawaishi maisha marefu....

Yaani kila nikitaka kuandika nazidi kuumia tu.....

Upumzike kwa amani mpendwa wetu Regia Dotto Mtema...

Watanzania tunakulilia,wana Morogoro wanakulilia,wana Kilombero wanakulilia,CHADEMA wanakulilia, CCM wanakulilia, CUF wanakulilia, NCCR-Mageuzi wanakulilia, UDP wanakulilia, Vijana watakulilia,wazee watakulilia, JF inakulilia............Nami daima nitakulilia Regia.......Upumzike kwa amani Regia.....

Daraja liliounganisha watanzania,wana Morogoro, wana Kilombero.....Daraja liliounganisha CHADEMA na vyama vingine,daraja liliounganisha vijana,daraja liliounganisha JF na Bunge,JF na siasa nk limevunjika wakati bado likiendelea kuhitajika kuwa kiunganishi katika safari ya Tanzania.......Upumzike kwa amani Regia....

Daima nitakulilia Regia........Upumzike kwa amani Regia....

Raha ya milele umpe mpendwa wetu Regia ee bwana na Mwanga wa milele umuangazie apumzike kwa amani......Amina...

Inauma sana yaani......

 
Last edited by a moderator:
Nakulilia mdogo wangu na rafiki yangu Regia. Niko kitandani hapa nakabiliana na maradhi (kama ulivyokuwa unajua). Nimefuatilia yaliyokuwa yanajiri tangu kifo chako kwa majonzi sana. Nimesikitika sana lakini nimefarijika kwa kuwa moyo wangu umeniambia umelala mahali pema. Nauamini moyo wangu ndio maana naamini iko siku moja tutaonana tena. Kwaheri mjukuu wangu, kwaheri rafiki yangu kwaheri Regia wangu. Upumzike kwa amani mama.
Pole sana Mkuu Aspirin. Mungu akujalie upone haraka.
 
Nakulilia mdogo wangu na rafiki yangu Regia. Niko kitandani hapa nakabiliana na maradhi (kama ulivyokuwa unajua). Nimefuatilia yaliyokuwa yanajiri tangu kifo chako kwa majonzi sana. Nimesikitika sana lakini nimefarijika kwa kuwa moyo wangu umeniambia umelala mahali pema. Nauamini moyo wangu ndio maana naamini iko siku moja tutaonana tena. Kwaheri mjukuu wangu, kwaheri rafiki yangu kwaheri Regia wangu. Upumzike kwa amani mama.

jamani babu pole,hujapöna tu?I wish u a quick recovery
 
Back
Top Bottom