Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Kumbuka tulitoa £80M kwa mchezaji kama Maguire.

Ukienda Serbia na hiyo hela unarudi na defenders wa maana wanne.

Maguire avuliwe kitambaa abaki kuwa mchezaji wa kawaida.

Bora tungebaki na Smalling kuliko kutoa hela nyingi hivi kwa mchezaji ambaye baada ya msimu mmoja tunatafuta replacement yake.

Maguire should deliver. Hatuna muda wa kubembeleza na hela ya kuchezea.

Tungekuwa na kocha kichaa, Maguire angekuwa anakula mbata akileta ujinga.
Nasikia waligombana na Bruno kwenye dress room

Sent from my SM-A105F using JamiiForums mobile app
 
Consider pia umri wake, demands za EPL (intensiveness) ukilinganisha na League 1, the Fact kwamba hajacheza muda mrefu na anaikuta ligi iko katikati (fitness).

Nadhani wameangalia sana vitu hivyo ndiyo maana amepewa mkataba wa mwaka 1 mara 2.
Katika kigezo cha umri,,Ibrahimovic alipokuja man u alikuwa na umri kama wa cavani,, nadhani uliona shughuli yake..
Sio kama hajacheza muda mrefu ,,sio kwl..
Na hata kama cavani hajacheza muda mrefu,,, sababu sio majeruhi,,ni aina ya uchezaji ndy iliyomuweka bench ,
Cavani bado ni world class top goal scorer ..
He is a goal machine
He is a finisher..
A sniper..
A bad man..
Only one bullet can kill an elephant.
Sio hawa wengine wanatumuia bullets 100 kuua tembo mmoja..
 
Huyu Mimi hata YouTube tu sijaona kama ana kitu cha ziada cha kufanya nistuke!
huyu dogo anajua ni kama tu Djames kipind anafika man utd,bt shida ni kwamba Djames alikua kama huyu kocha akamdidimiza kipaji chake je vip kuhusu huyu pia? ukiangalia kwa umakini utagundua huyu ni daniel james wa pili hivo bado tunarud palepale ila kocha afukuzwe tu hana jipya kiufund. Yani eti pogba, Djames, bissaka, maguire wote hawa hawajui na hakuna kocha alichowaongezea sasa hata bruno ameanza kupoteza makali
 
huyu dogo anajua ni kama tu Djames kipind anafika man utd,bt shida ni kwamba Djames alikua kama huyu kocha akamdidimiza kipaji chake je vip kuhusu huyu pia? ukiangalia kwa umakini utagundua huyu ni daniel james wa pili hivo bado tunarud palepale ila kocha afukuzwe tu hana jipya kiufund. Yani eti pogba, Djames, bissaka, maguire wote hawa hawajui na hakuna kocha alichowaongezea sasa hata bruno ameanza kupoteza makali
Kuna tofauti kubwa ya D james na huyu dogo.
D james ana speed.. lakin hana dribbling skills.

Huyu ana ball control.. dribbling skill. Plus anacheza nafasi zote. Kulia na kushoto na kati yani kama 10.
Hawa ni watu wawili tofauti.

Ila kitu kimoja tu ni kuwa vipaji hivi vitakufa under management mbaya. Na hapa ndipo uwezo wa kocha unatakiwa kuonekana.
 
Siku Suarez anaenda AM, niliuliza humu, mbona ameuzwa kwa €7M? Very cheap actually.

Nikajibiwa kwasababu ni mzee.

Nadhani Suarez alikuwa best option kwa central striker.
Tatizo si pesa.. yeye mwenyewe angekubali kuja united?
 
Yaani Solkjaer kazunguka duniani kote second option yake kwa Sancho awe Adam Traore ??

Haiwezekani hapa ni kwamba Woodward kashindwa kufanya usajili kaamua kununua mtu yoyote aliyeko sokoni bila hata consultation na Mwalimu.

Kimsingi Ole mpaka sasa Van Gaal alionewa, Mouringo alionewa pia na sasa ni zamu ya Ole kuonewa na Woodward.

Muda utasema.

Sent from my SM-A105F using JamiiForums mobile app
Woodward ana matatizo yake lakini tusimtwishe mzigo wa kusema amenunua mchezaji yoyote aliye sokoni without consultation ya Mwalimu. Kwa hili sitaki kuamini.

Ole mwenyewe aliwahi kutamka kuwa 'He has the say of who to go and who to stay.' Pia juzi tuu hapa kasema kuwa timu inaongozwa na watu makini na wanaojielewa. Unless He is Hypocrite, basi naye ana lawama zake katika hizi transfer.

Nakumbuka muda kidogo wakati ule Mchakato wa kuwa na DoF umepamba moto mtandaoni, Ed alitoka na kusema kuwa Si sahihi kusema kuwa Football Decisions zinafanywa na watu wasiojua Football. Hii inamaanisha kuwa kunakua na consultation na bench la ufundi.
 
lakini gharama za sancho ni kubwa sana na pengine ed hakutegemea kuwaona dortmund wakiwa na msimamo usioyumba ndio maana uongozi wa klabu wamekuwa wakisita kufanya uamuzi.

ukiachana na sancho bado naamini united hatukuwa na target mbadala
Sancho kwa hiyo bei naungana na bodi kutomnunua. The only thing nailaumu ni kutokua na alternative kwa miezi yote mitatu. Hoi inaonesha ni kwa jinsi gani bench la ufundi na bodi kwa ujumla walivyo clueless na naweza kusema hawajui what they actually need as a team.

Hakuna mipango ya ku improve team na wala hatuna goals za wapi tunataka timu iende. Ninachokiona what the team fights for ni kupata CL Football and Inshaallah huku tukijificha kwenye kivuli cha Rebuilding.
 
Niliwahi andika hapa juu ya alichosema Van Gaal.

Alisema "Pale Bayern CEO ni mtu wa mpira anajua nini kinatakiwa kifanywe na nini hakitakiwi. Wakati hapa CEO ni mtu aliyekua akijihusisha na uwekezaji benki. Nafikiri unaweza kuona tofauti"

Mwekezaji wa benk alifuta nafasi ya Director of Football na kujikaimisha yeye. Mlitarajia nini?
Sikumbuki Utd kuwa na hiyo nafasi. Hawakufuta, ila wanakataa isiwepo kwa kisingizio bench la ufundi work hand in hand na bodi hivyo football decisions zinafanywa na watu wa mpira (bench la ufundi)

Clueless Utd.
 
Man u ina matatizo makubwa:-

Kuna matatizo ya Tajiri

Kuna matatizo ya management

Kuna matatizo ya kocha

Kuna matatizo ya wachezaji

Kuna matatizo ya mashibiki.

Mtafukuza makocha mpaka lini? Tatueni tatizo la msingi (Uongozi wa club).
Shabiki wa Chelsea anashauri kuhusu kufukuza makocha, yaani Chelsea.!
 
Kwa position wanayaotakiwa kucheza tulihitaji mchezaji ambaye tayari ameshaprove

Sent from my SM-A105F using JamiiForums mobile app
Hapo Sawa. Hizi sajili zinaonesha ni jinsi gani hatuna mipango ya nini tunataka and when. Hatuwezi kusubiri hadi deadline day kusajili watoto wa academy.

Ila siwezi kutoa hukumu ya uwezo wa hao madogo, let us wait and see.
 
Back
Top Bottom