Live: Kizota Dodoma

Live: Kizota Dodoma

  • Thread starter Thread starter MegaPyne
  • Start date Start date
POLENI WAJUMBE BAADA YA KUANGALIA NA KUSIKILIZA ONYESHO LA KWANZA LA MSANII KINGWENGU NGWENDULILE....kwa sasa burudikeni na muziki na misosi laini wakati msanii wa pili MANYWELE anapojiandaa kupanda....tupo pamoja hapo...dom.

Hapa ndipo credibility ya JF inapohojiwa, it's very sad!
 
1.


So far the dataz ni kilio cha Lowassa na Mtandao, Muungwana amewaacha njia panda, historia ndogo ya kupigwa mweleka kwa mtandao kufikia huu mkutano,

1. Kesi ya Malima Vs Mengi, Mtandao walikuwa wamepanga kumuondoa Six, kwa kumtumia Mzindakaya, waliyem-plant ili aanzishe hoja ya kutkouwa na imani na Spika, iwapo angetoa hukumu against Malima, kabla ya siku ya hukumu Spika, akagundua na kwenda usiku kwa jm akiwa analia kama mtoto mdogo, "....Makamu nisaidie what to do... on this..", maana kuhusu kesi ni clear kuwa Malima, amekosea na anahitaji kuadhibiwa, akaambiwa haya kesho nenda utoe busara badala ya hukumu, na kuwapiga Mtandao, at their own game, tukaishiwa kuuziwa busara kwa shillingi millioni 100,

2. Muungwana aakawanyima vyeo vote ndani a CCM alipowapa kina Makamba, Mwanri, na Mwambi!

3. Ngasongwa, Mkali, na Londa another mtandao wakapigwa kiboko kwenye NEC!

4. Tom akapigwa kiboko cha moto huko Mbeya na Mwandosya, akisaidiwa na wabunge wa CCM, hela alizotumia Tom na Mtandao huko, inasemekana kuwa haijawahi kutokea, lakini wabunge kwa kushirikaina na wazee wa Mbeya, wakaweka mkakati mzito kuwa Tom na baba yake ni wa-Zambia, sio wabongo, Mwandosya aliyekuwa ameshakata tamaaa akaambiwa atulie ngoma inachezwa na wabunge!

5. Sasa Lowassa na Mtandao, kiboko cha moto tena kwenye umakamu, it is over, na Muungwana personally ameamua kuwafungia kazi kwenye hizo nafasi 20 za NEC, wasipate kabisaa maana inaaminika kuwa kuna mkono wa Sofia Simba, kwenye kifo cha Mbatia, maana kuna kabarua kadogo aliko mtumia akiwa Mwanza, kabla ya kwenda huko Kusini ambako ni clear kuwa kuna kitu alikuwa anakijua, na akakimbilia South Africa kama cover, Muungwana alionywa kabla ya huu mkutano na amesikia, kwa hiyo kwa mtandao, the party is over!


Sasa in the wake ya all this, what to expect? Kwa maoni yangu Msekwa sio makamu functional, ila ni symbol ya kukataa ujinga wa mtandao, makamu ni cheo ambacho ukweli ni kwamba hauna chochote na ni absolutely powerless position, kazi ni kutembelea matawi ya CCM, na kumfikishia ujumbe mwenyekiti wa yanayojiri kwenye matawi ya CCM, ambako sio rahisi kwa viongozi wa chini kumpa info, mpaka wamuamini, it won't happen in one day, halafu most of the time info nyingi huwa ni majungu tu against each other ambayo unless makamu ni makini anaweza kumpelkea habari rais ambazo sio za ukweli,

Makamu aliyeondoka alikuwa na good relations na wakuu wa chini, ndio maana siku zote aliweza kushinda uchaguzi wa wabunge, pamoja na ujanja janja, lakini siku zote alikuwa na viongozi wengi wa upinzani kwenye level ya chini kwenye payroll, kwa sababu kwa kawaida viongzi wa juu wa upinzani huwatelekeza kabisa viongozi hao wa chini mpaka unapotokea uchaguzi tu, ndio maana kule Tunduru, makamu alishituliwa mapema na wapinzani kuwa mbunge wa zamani wa CCM Nyimbo, alikuwa akiwasaidia, sasa this inahitaji humbleness ambayo kama unamjua Msekwa, ni tatizo sana kwake, isipookuwa kuna kujifunza kwenye job, huenda kaamudu,


but, sasa hivi ndio vita kali imeshaanza kati ya Mtandao Vs Asilia, so far Asilia wanaonekana kuwa some few steps ahead, Asilia stregth zina-rest na makamu aliyetoka, bila ya yeye they are dead, Msekwa asipokuwa makini kuna uwezekano wa kutomaliza term yake ya 7 years, ingawa sasa hivi kutokana na huu uchaguzi hata Shein anakuwa safe sasa, maana another Mtandao aliyekuwa akimlalia macho alipigwa mweleka yaani Shamuhuna, na pia kuna uwezekano wa Muungwana kutomaliza term ya pili, huenda anawaandaaa asilia kuja kushika hatamu, mengi yapo online, lakini ninaahidi kuwa between now and kesho, nitaleta more ugly dataz ya yaliyojiri na yanayojiri, sasa hivi beyond hotuba na uchaguzi,

Ninazo nyingi, lakini ninahitaji kuzi-clarify kwanza!

Mkuu ES,
kuna kitu kimoja tu nilipokisoma haikuhitaji nimalizie kusoma ili kukupa thanks, hii habari imejaa ukweli kwa asilimia kubwa sana kwa kusema ukweli !
Nakupa hongera kwa hilo, naona sasa hivi UMEKUJA KAMILI !
Lakini kuna viongozi pia watatajwa nadhani watu watashangaa !
 
Hapana,

Nipo kizota, ni mapumziko. JK amesisitiza kuhusu uungwana, kuhusu kejeli zenu na jinsi anavyoyachukulia. Jk amelaani Mtandao kuwapa wapiga kura orodha nzima ya NEC (wakupigiwa kura) kutoka kila kundi, amewaita wazi wazi Watoa Rushwa, na kasisitiza wapiga kura wawachague hata wale wasio na uwezo wa kwenda mikoani kutoa rushwa.

JK ameelezea maendeleo mbali mbali, ameongelea tatizo na Mbolea na namna serikali inavyolikabili, kwa kujenga kiwanda kwa ajili ya Minjingu Phosphate(sic)

JK ameongelea kuunganisha nchi kwa barabara, ya lami, ametaja ya Lindi na Singida zimeanza.

JK ameongelea kuundwa/kujengwa kwa reli ya kuunganisha TZ mpka BUrundi na Rwanda. Na kusema ya sasa (reli) njia ni ya mwaka 1910, hata mabehewa na Injini ukitaka kuagiza inabidi utengenezewe special kwa ajili yako, only TZ UG and Kenya are using this old tech.

JK ameongelea madini, ameelezea kuhusu mikataba, akasema wanaojadili hawana uwezo wa kuhujumu kwa kuwa sheria zote zimo. Amesisitiza loss carry forward ya 15% ndio tatizo na analishughulikia. Pia amesema madini inaingiza 1.9% ya pato la taifa. Ameelezea vizuri, kasoro ni moja why mikataba ni siri ndio hakusema

JK amesema kuhusu umeme Kilwa (soon kukamilika, Lindi na Mtwara kutumia umeme wa Gesi ya Mnazi mmoja.

Jk ameongelea namna falsafa yake ya maisha bora kwa kila mtz inavyofanya kazi.

JK ameongelea mafunzo kwa askari wetu na kuwajengea nyumba maafisa wake. Amesisitizia mafunzo kwa askari wakati wa amani.

JK ameongelea tatizo la Umeme kwa ujumla na kusema ni 10% tu ya watanzania wote wanapata umeme, wanaifanyia kazi hilo.

JK amesema mazungumzo ya muafaka yata resume soon, yalisimama kwa ajili ya kampeni ya CCM.

JK ameongelea mambo ya michezo na kusema wanaifanyia kazi.

JK ameongelea umasikini na jinsi alivyoifanyia kazi, jinsi alivyozungumza na CEOs katika CEO's roundtable, akaongela kuwa kama uchumi ukipanda kwa asilimia 10 kila mwaka basi pato la mtanzania inaweza kufikia kiasi fulani (nimesahahu) ikifika mwaka 2025, kiwango ambacho ni kidogo pia, amesema analifanyia kazi.

JK ameongelea UFISADI, amesema kuwa kuna tume ya maadili ipo na kuna PCCB, ameeleza wazi kwa wao hata ukituma SMS ni mali kwao Mwenyewe amesema anapokea SMS za tuhuma mbalimbali na zote zinashughulikiwa. Amesema, hata ukisemea mwembe Yanga au ulaya au hata kama ni minog'ono wao wanayafanyia kazi.

Jamani nasikia njaa ngoja nikapate msosi, foleni imepungua. Kaongea mengi sana ya maana jamani.

It was one of the best HOTUBA.

Unedited

Mzee wa Dom kwa leo

Kwa sisi ambao tuko mbali na nyumbani tunapenda kupata habari kamili na wala si mzaha-mzaha, ninakushukuru sana Mkuu.
 
Lunyungu, either haupo Kizota au hauna access na TV, naona hapo juu mmeandika kuwa TV zote zinaonyesha.

Hotuba ya JK ilikuwa nzuri sana, na ameongela mambo karibu yote!
Ambacho hakuongelea ni kwanini mikataba ni siri.

Uliza swali lolote nikujibu kama alivyoelezea kwenye hotuba yake. Kaelezea mpaka BOT. Jamani hivi nyinyi ni wapinzani mnaotaka damu imwagike au mnataka nini?!

Jaribuni kujadili vitu kwa kufikiria kwanza! Sio kupinga tuuu.

Niko pamaoja na wewe FD, nadhani wale wasioripoti yanayoendelea Chimwaga kama yanavyojitokeza wanawanyima haki ya kimsingi kabisa watumiaji wengi wa JF. Kama Lunyungu anamchukia mtu au CCM hilo ni tatizo lake binafsi, asipotoshe umma wa JF. Akumbuke kuwa watu waliopo katika JF ni kutoka pamde zote za dunia ambao kwao habari kamili ndiyo siha yao.
Ahsante sana FD.
 
Kazi,
Mjadala mzuri. Katika ilani kumi za Chama alizotaja. Ameongela moja baada ya nyingine na kuelezea zilivyotekelezwa so far.

Ukiangalia kwa makini ameongelea kuanzia walivyodhibiti Ujambazi mpaka tatizo la Umeme.

Kwa ufupi ni kuwa katoa mifano hai katika kila kipengele.
Yaani ilikuwa hotuba safi sana kaka, itafute uisome.

Mimi nimeleta to hints, ila kaka mimi huwa natazama pande zote za shillingi ndio maana utaona kuwa nimesema, HAKUONGELEA KWANINI MIKATABA NI SIRI. Ila kaongela kuundwa kwa tume huru, nyinyi wapinzani na viongozi wa dini mtakuwemo!

FD bado nasisitiza tupo pamoja, katika Mkutano Mkuu kama ule Mwenyekiti atategemewa zaidi kuongelea maendeleo / yatokanayo na ilani ya CCM, na hapo ndipo wakati wake wa kuelezea nini kimefanyika na wala sio jukwaa hasa la kupiga blah blah. Na kama asingefanya hivyo wa-CCM na wengine wetu tungemshangaa zaidi. JK knows exactly nini anachotakiwa kufanya.
 
1.


So far the dataz ni kilio cha Lowassa na Mtandao, Muungwana amewaacha njia panda, historia ndogo ya kupigwa mweleka kwa mtandao kufikia huu mkutano,

1. Kesi ya Malima Vs Mengi, Mtandao walikuwa wamepanga kumuondoa Six, kwa kumtumia Mzindakaya, waliyem-plant ili aanzishe hoja ya kutkouwa na imani na Spika, iwapo angetoa hukumu against Malima, kabla ya siku ya hukumu Spika, akagundua na kwenda usiku kwa jm akiwa analia kama mtoto mdogo, "....Makamu nisaidie what to do... on this..", maana kuhusu kesi ni clear kuwa Malima, amekosea na anahitaji kuadhibiwa, akaambiwa haya kesho nenda utoe busara badala ya hukumu, na kuwapiga Mtandao, at their own game, tukaishiwa kuuziwa busara kwa shillingi millioni 100,

2. Muungwana aakawanyima vyeo vote ndani a CCM alipowapa kina Makamba, Mwanri, na Mwambi!

3. Ngasongwa, Mkali, na Londa another mtandao wakapigwa kiboko kwenye NEC!

4. Tom akapigwa kiboko cha moto huko Mbeya na Mwandosya, akisaidiwa na wabunge wa CCM, hela alizotumia Tom na Mtandao huko, inasemekana kuwa haijawahi kutokea, lakini wabunge kwa kushirikaina na wazee wa Mbeya, wakaweka mkakati mzito kuwa Tom na baba yake ni wa-Zambia, sio wabongo, Mwandosya aliyekuwa ameshakata tamaaa akaambiwa atulie ngoma inachezwa na wabunge!

5. Sasa Lowassa na Mtandao, kiboko cha moto tena kwenye umakamu, it is over, na Muungwana personally ameamua kuwafungia kazi kwenye hizo nafasi 20 za NEC, wasipate kabisaa maana inaaminika kuwa kuna mkono wa Sofia Simba, kwenye kifo cha Mbatia, maana kuna kabarua kadogo aliko mtumia akiwa Mwanza, kabla ya kwenda huko Kusini ambako ni clear kuwa kuna kitu alikuwa anakijua, na akakimbilia South Africa kama cover, Muungwana alionywa kabla ya huu mkutano na amesikia, kwa hiyo kwa mtandao, the party is over!


Sasa in the wake ya all this, what to expect? Kwa maoni yangu Msekwa sio makamu functional, ila ni symbol ya kukataa ujinga wa mtandao, makamu ni cheo ambacho ukweli ni kwamba hauna chochote na ni absolutely powerless position, kazi ni kutembelea matawi ya CCM, na kumfikishia ujumbe mwenyekiti wa yanayojiri kwenye matawi ya CCM, ambako sio rahisi kwa viongozi wa chini kumpa info, mpaka wamuamini, it won't happen in one day, halafu most of the time info nyingi huwa ni majungu tu against each other ambayo unless makamu ni makini anaweza kumpelkea habari rais ambazo sio za ukweli,

Makamu aliyeondoka alikuwa na good relations na wakuu wa chini, ndio maana siku zote aliweza kushinda uchaguzi wa wabunge, pamoja na ujanja janja, lakini siku zote alikuwa na viongozi wengi wa upinzani kwenye level ya chini kwenye payroll, kwa sababu kwa kawaida viongzi wa juu wa upinzani huwatelekeza kabisa viongozi hao wa chini mpaka unapotokea uchaguzi tu, ndio maana kule Tunduru, makamu alishituliwa mapema na wapinzani kuwa mbunge wa zamani wa CCM Nyimbo, alikuwa akiwasaidia, sasa this inahitaji humbleness ambayo kama unamjua Msekwa, ni tatizo sana kwake, isipookuwa kuna kujifunza kwenye job, huenda kaamudu,


but, sasa hivi ndio vita kali imeshaanza kati ya Mtandao Vs Asilia, so far Asilia wanaonekana kuwa some few steps ahead, Asilia stregth zina-rest na makamu aliyetoka, bila ya yeye they are dead, Msekwa asipokuwa makini kuna uwezekano wa kutomaliza term yake ya 7 years, ingawa sasa hivi kutokana na huu uchaguzi hata Shein anakuwa safe sasa, maana another Mtandao aliyekuwa akimlalia macho alipigwa mweleka yaani Shamuhuna, na pia kuna uwezekano wa Muungwana kutomaliza term ya pili, huenda anawaandaaa asilia kuja kushika hatamu, mengi yapo online, lakini ninaahidi kuwa between now and kesho, nitaleta more ugly dataz ya yaliyojiri na yanayojiri, sasa hivi beyond hotuba na uchaguzi,

Ninazo nyingi, lakini ninahitaji kuzi-clarify kwanza!

Hii 'historical background' imetulia kiaina, ila tunasubiri zaidi uchunguzi wa ajali ya huyu waziri kwa hamu, kwa sababu hio conspiracy hapo juu inatutia shaka kidogo!
 
Nilitaka kuja na hoja yangu binafsi humu Jf. Lakini naiahirisha kwa muda nikisubiri matokeo/actions za hotuba ya leo. ninatoa hadi december mwishoni. nisipoona dalili yoyote nitatoa tamko rasmi kwamba JK is not the President tuliomchagua bali ni kanyaboya aidha CCM au wazungu/wawekezaji wametubadilishia.

Naomba niwe mvumilivu kwa mara nyingine.
 
Nilitaka kuja na hoja yangu binafsi humu Jf. Lakini naiahirisha kwa muda nikisubiri matokeo/actions za hotuba ya leo. ninatoa hadi december mwishoni. nisipoona dalili yoyote nitatoa tamko rasmi kwamba JK is not the President tuliomchagua bali ni kanyaboya aidha CCM au wazungu/wawekezaji wametubadilishia.
Naomba niwe mvumilivu kwa mara nyingine.

babu dont worry speaking your opinion, unaweza ukasema time yoyote hiyo opinion yako !

nadhani watu walishasema pia before kwamba jk is the worst prezzo, so utakuwa unaendeleza libeneke !

great !
 
FD,
Kwa hiyo alichozungumza ni nadharia tu na hakuna kitu cha maana,unajua sisi watu wa hesabu tunajua 2+2=4.haya mambo ya tunafanya kwa siri ndio tusio yataka ktk ulimwengu wa sasa.basi yote ni utumbo tu hakuna jipya punda na masikio.manu 2,arsenal 1

Katibu Tarafa,
Siri lazima ziwepo, huwezi kuzifuta katika ulimwengu huu. Si kila jambo linalofanywa ki-maamuzi na kiutendaji lianikwe haitakuwa ni practical.
Si unajua hatavyumba vyenye pesa huwekewa kijina-siri, kuingia pia kwenye mtandao wa JF lazima uwe na kijina-siri.
 
1.


.....inaaminika kuwa kuna mkono wa Sofia Simba, kwenye kifo cha Mbatia, maana kuna kabarua kadogo aliko mtumia akiwa Mwanza, kabla ya kwenda huko Kusini ambako ni clear kuwa kuna kitu alikuwa anakijua, na akakimbilia South Africa kama cover....

Heshima kwako,Mkuu.

Nadhani sikuwa peke yangu niliyekuwa nasubiri "za jikoni" kutoka kwako,na hujatuangusha tuliokuwa tukisubiri.

Hili la Sophia Simba limenishtua na kunisononesha kweli.Hivi hawa watu walio tayari kupoteza maisha ya wenzao kwa ajili tu ya madaraka,wanadhani wakifanikiwa katika azma hizo za kishetani hata hayo madaraka yatakuwa matamu?Muuaji yeyote anaendeshwa na tamaa na ubinafsi,na kwa maana hiyo muuaji akipata madaraka baada ya kutoa roho ya mtu mmoja hatoshindwa kuondoa roho nyingine,aidha kwa kurejea kuua mtu wingine physically au kuendekeza ufisadi utakaopelekea kupoteza maisha ya watanzania kadhaa kwa kukosa huduma muhimu kwa maisha yao.

Hivi Sophia akiambulia patupu ktk uchaguzi huu atabaki na amani kweli?
 
babu dont worry speaking your opinion, unaweza ukasema time yoyote hiyo opinion yako !

nadhani watu walishasema pia before kwamba jk is the worst prezzo, so utakuwa unaendeleza libeneke !

great !


Kada,

Hii itakuwa ya kwangu binafsi na wala sitamshawishi mtu kuunga mkono. ndiyo maana nikasema, naomba kuwa mvumilivu kwa muda na wala sikukandia hotuba yake. nimetoa maoni kwamba hotuba ni nzuri kama Fd alivyotuabarisha na kwamba ita value only and only if atafanya kama alivyo yazungumza.
 
Kada,

Hii itakuwa ya kwangu binafsi na wala sitamshawishi mtu kuunga mkono. ndiyo maana nikasema, naomba kuwa mvumilivu kwa muda na wala sikukandia hotuba yake. nimetoa maoni kwamba hotuba ni nzuri kama Fd alivyotuabarisha na kwamba ita value only and only if atafanya kama alivyo yazungumza.

sawa babu !
 
Mimi nilidhani kwa kuwa waliwaalika Wapinzania basi ustaarabu ungalikuwa lukuki kumbe baadaye akina Cheyo waliona jengo dogo baada ya kuanza kustwa . Hata kama ujumbe ulikuwa unaenda kwenye vyama 4 pekee ambao walikuwa branded kama waroho wa madaraka kwa kuitwa paka mbele ya panya lakini Cheyo was heavily embarrased huku JK akitumia neno la mtaani na kuonyesha kutokuwa serious kwa kuwaita wapinzani watani wao wa jadi .Pale nilianza kuingiwa na maswali na again they laid their standing that they will never put their hands on rushwa nje ya Chama yaani serikalini.

Kweli mkutano huu una maajabu yaani wameamua kutojibu tuhuma na wamekimbilia kusema wao wana wajibika so mambo ya akina Karamagi ndiyo mwisho wake kwa CCM.JK he went far to suggest kwamba watoa tuhuma waende Mahakamani badala ya kutumia majukwaa ya kisiasa that was an indication kwamba kuna collective responsibilty na kuhitimisha maneno ambayo nimeyasikia hapa Dodoma kwamba Karamagi anasema JK hawezi kuthubutu kumuengua kwenye uwaziri kwa kuwa anamjua viilivyo na anaweza kumwanika.Baada ya jana sasa asubuhi nimekuwa natafakari na kuona kuna ka ukweli ndani ya haya madai .

Serikalo zote 2 za bara na visiwani walielezea jinsi wanavyo sifiwa na mataifa ya nje lakini ndani wanadharaulika . Hili lilikuwa ni jambo la kushangaza maana hao akina Bush hawajafika kijijini waone Mgambo, watendaji wa vijiji na kata anavyo wanyanyasa watu . Hawajafika waone watu wanavyo lala njaa , wanavyo kufa bila ya huduma za hospitali,hawana nguo wanavaa viraka, hawajui milo 3 wala shule za misingi haziko karibu na zikiwepo hakuna walimu wala nyumba za walimu.

Poleni sana kama mlitegemea kitu serious bali mliweza kupata presha hadi JK akayumba na kutumia maneno yale kubeza wapinzani. Nikabaki na maswali kibao nikijiuliza kwamba wale ni wana muziki wanaouza muziki wao na wakaanza kuwaponda wapinzani je wanunuzi wa muziki wao ni CCM pekee ?

Je na wale wasio kuwa na vyama wana nafasi gani katika muziki wa wana ccm wale ?

Mungu isaidie Tanzania tuko mbali .
 
Serikalo zote 2 za bara na visiwani walielezea jinsi wanavyo sifiwa na mataifa ya nje lakini ndani wanadharaulika . Hili lilikuwa ni jambo la kushangaza maana hao akina Bush hawajafika kijijini waone Mgambo, watendaji wa vijiji na kata anavyo wanyanyasa watu . Hawajafika waone watu wanavyo lala njaa , wanavyo kufa bila ya huduma za hospitali,hawana nguo wanavaa viraka, hawajui milo 3 wala shule za misingi haziko karibu na zikiwepo hakuna walimu wala nyumba za walimu.

Poleni sana kama mlitegemea kitu serious bali mliweza kupata presha hadi JK akayumba na kutumia maneno yale kubeza wapinzani. Nikabaki na maswali kibao nikijiuliza kwamba wale ni wana muziki wanaouza muziki wao na wakaanza kuwaponda wapinzani je wanunuzi wa muziki wao ni CCM pekee ?

Je na wale wasio kuwa na vyama wana nafasi gani katika muziki wa wana ccm wale ?

Mungu isaidie Tanzania tuko mbali .

Aise Lunyungu

Kura tano

Nyerere alisema kuwa ukiona watu wa nje wanakusifia ujue una kasoro.

Je JK alichaguliwa na Bushi au ndiyo kutapeli watanzania? Mbona ni huyo huyo aliomba majina ya wala rushwa? Nafikiri kafirisika kimawazo. Anahitaji msaada wa mawazo na wataalamu zaidi.
 
Lunyungu vipi mbona leo kimya? tupe update yanajiri huko Dom au mpaka aanze CMB na wewe ndio unaunganisha "ukiwa Dodoma"
 
Now I can see the original Mzee ES aka FMES. Mzee hongera sana, hayo maneno yako ni mazito giving an insightful picture of what is going on. Hivi ndivyo nilivyokujua mimi kule bcs na ndivyo heshima yako ilivyojengeka. Keep up the good work!
 
Bado nitaendelea kuhoji credibility ya JF?

Ukitaka kuona credibility ya JF ungeanza kwako kwanza. Hapa tupo watu wa mitazamo mbali mbali, mawazo yetu hayafanani kamwe! Hoji kwanza credibility ya hao waliomwalika huyo unayemtetea.
 
Back
Top Bottom