Live: Kizota Dodoma

Live: Kizota Dodoma

  • Thread starter Thread starter MegaPyne
  • Start date Start date
Rita Mlaki, millioni 300 nje?

Good news kutoka huko ni uamuzi wa rais kuteua kamati maalum itakayo jumuisha mawakili, wabunge wa upinzani, wakuu wa dini zote mbili, na wabunge wa CCM, kulifuatilia suala zima la madini,

Magazeti yote leo yamekubali kuwa kwenye hili Muungwana, makes a sense, the bad news ni mkuu Luwassa, kutoka huko akiwa mnyonge sana!

Mkuu heshima yako. Hii itamake sense kama kamati itakayoundwa itapewa meno ya kuiwezesha kufanya kazi bila kuingiliwa na yeyote pale ambapo wanaona kuna haja ya kufanya mabadiliko katika mikataba mbali mbali ya uchimbaji wa madini. Kama kamati hiyo haitakuwa na nguvu zozote basi itakuwa ni kutwanga maji kwenye kinu na hata watakaochagulia kwenye kamati hiyo wanaweza kukataa kuitumikia kamati isiyokuwa na meno.
 
Yaani Sumaye anapitwa na Makongoro Mahanga? ama kweli ukifia mwituni vidudu vyote vitakutambaa....

..masatu!

..mbona hiyi ni obvious!

..kwani kwasasa sumaye ana deal gani?si kazi hata fweza hakumwaga!sasa nani ajiangaishe kumpa kura mtu asiye na deal?

..maisha huwa hivyo mkuu!watu hufanywa kama mavi ya kale!hayanuki!

..kumbuka,ngwe yako ikipita....wale wote waliokuwa wakikuchekea mpaka mapengo kuonekana watakukwepa barabarani!it's human nature!
 
Mkuu Dua,

Heshima mbele,

Uchaguzi bado, kesho mwenyekiti atawasilisha majina ya wajumbe anowataka wa skretariati, jina la katibu mkuu, na wajumbe wa kamati kuu pia watapigiwa kura kesho, kwa hiyo bado mkuu mchezo haujaisha!
 
Mkuu Bubu na Mwafrika wa Kike,

Kamati itakuwa na wajumbe toka upinzani na wakuu wa dini na mawakili, sasa hviv unaamini hawa watakubali kuvutwa kama wajinga? Watakapoona tu kuna unazi watachomoa na kusema wazi WHy?

I mean mnyonge mnyongeni, lakini na haki kidogo tumpe!
 
Miongoni mwa hotuba ambazo ziliwakuna wengi, ni ile iliyotolewa na Makamu Mwenyekiti Mstaafu, John Malecela, ambapo wakati akimshukuru Marais Wastaafu, Benjamin Mkapa na Ali Hassan Mwinyi ukumbi mzima ulitulia.


Wakati Malecela akihutubia, Mkapa alionekana mwenye huzuni na kuna wakati alikuwa anatafuta kimbaa kwa ajili ya kufuta machozi.


Kwa upande wa Makamba tokea kuanza kwa mkutano hakuwa mchangamfu kama ilivyo kawaida yake na hata juzi usiku aliomba CCM isimuacha kwa kuwa wapinzani watamcheka.


?Naomba CCM isinigaragaze ndugu Mwenyekiti, kwani wapinzani watanicheka,? alisema kwa utani


Kiongozi mmoja ambaye anafanya kazi kwa karibu na Makamba, aliiambia Mwananchi kwamba wana wasiwasi kwamba bosi wao ataondolewa katika kiti hicho.


?Mpaka sasa tunahisi katibu anaondolewa katika nafasi, hivyo hata sisi hatujui hatma yetu,? alisema kada huyo.


Wachambuzi wa masuala ya siasa walioko hapa Dodoma, wanasema kuna uwezekano mkubwa wa Makamba kuondolewa katika wadhifa huo hasa ikizingatiwa Makamu Mwenyekiti Mpya, Pius Msekwa ni mtu anayefanya kazi kwa taratibu, kanuni na sheria, wakati Makamba staili yake ya kufanya kazi ni tofauti naye.

Source Mwananchi
 
Mkuu Bubu na Mwafrika wa Kike,

Kamati itakuwa na wajumbe toka upinzani na wakuu wa dini na mawakili, sasa hviv unaamini hawa watakubali kuvutwa kama wajinga? Watakapoona tu kuna unazi watachomoa na kusema wazi WHy?

I mean mnyonge mnyongeni, lakini na haki kidogo tumpe!

Utakuta wapinzani wenyewe walio katika kamati ni kama Bw John Cheyo, Peter Mziray wa PPT na akina Makaidi na wanaofanana nao, hawa hawapo katika lile kundi la vyama vinne vilivyopinga ufisadi Mwembeyanga. Huenda vile vyama vinne vikarukwa. Sitashangaa nikisikia tiktak hii, maana tumezoea usanii.
 
Mzee ES, Karamagi alitamka Bungeni kuwa madai ya Zitto kuwa mikataba bado inaendelea kudusuriliwa hayakuwa ya kweli na kuwa mazungumzo yamekamilika. Sasa huku kwingine kwa nini? Tayari kuna Kamati ya Mabadiliko ya Sheria ambayo imekuwa ikifanya kazi zake je ni kamati hiyo hiyo inaongezwa wajumbe tu, au ni kamati mpya specifically kwa ajili ya madini?

Kama kweli kuna tatizo kubwa katika sekta ya madini na sheria iliyopo haimnufaishi Mtanzania kama inavyostahili, kwanini asisitishe utoaji wa leseni za uchunguzi na uchimbaji hadi sheria mpya itakapopatikana kama walivyofanya Uganda?

Napenda nimpatie haki yake lakini siyo kwa mazingaombwe namna hii? kwanini asiache Bunge ndiyo liunde kamati hiyo?
 
Kwa kweli CCM Kiboko, Kamala kushindwa kwake ni dalili nzuri...the guy was dreaming one day to become the president of this country na waziri mkuu wake awe Matayo David wote hawa licha ya kuwa wanamtandao maslahi ni close allies wa JK .what a crap....nafikiri wana CCM wamefanya nilokuwa nalitamani.......(majina kwenye mabano) washindwe pia U- NEC
 
Mkuu Mwenzangu MMJ,

Ninakusikia, maji yalishamwagika leo rais hawezi kusema bunge likae upya kuunda kamati ya madini na kuchunguza malalamiko ya wananchi, itakuwa ni kumdhalilisha waziri mkuu ambaye ndiye mkuu wa serikali bungeni,

Halafu at the same token, bado tuko kwenye system ya unazi, kumbuka mambo mengi ambayo rais ameyafanya Dodoma this time sio kabisa nia yake binafsi na wenzake wa Mtandao, isipokuwa ni kuelemewa na asilia ndio maana wameanza kukubali, sasa itachukua muda, lakini mimi ninaheshumu the fact kwamba hata eyey mwenyewe amekubali kuwa malalamiko ya wananchi kuhusus madini yanamkera na yeye pia,

Unajua ndio maana nimetabiri mahali nyuma kuwa kuna uwezekano mkubwa Muungwana, asimalze term ya pili, few weeks ago nilikutana naye uso uso na kuongea naye, yaani mkuu wangu ni clear kabisa kuwa mkuu amesha-resigne to his fate kwamba mambo ni mazito na hayawezi!
 
Mkuu Bubu na Mwafrika wa Kike,

Kamati itakuwa na wajumbe toka upinzani na wakuu wa dini na mawakili, sasa hviv unaamini hawa watakubali kuvutwa kama wajinga? Watakapoona tu kuna unazi watachomoa na kusema wazi WHy?

I mean mnyonge mnyongeni, lakini na haki kidogo tumpe!

Mkuu FMES,

Heshima mbele mkuu.

Ni kweli Mnyonge tumempa haki yake vya kutosha mkuu. Ukiona mtu kama mimi ambaye nimeweka wazi hapa JF siwapendi mafisadi wa ccm na mambo yao, lakini weekend hii nilikaa kimya na kuwapa wazee mufanye vitu vyenu bila vipepsi na vifanta toka kwangu.

Kwa kuwa mkutano umeisha na waliopata wamepata. Nadhani sasa ni vyema ukweli ukawekwa wazi hapa forum kuhusu usanii wa JK kwenye hotuba yake.

Hii kamati itafanya nini kama Karamagi alidai bungeni kuwa zitto ni muongo kwa vile zoezi la kupitia mikataba limekamilika?

Hii kamati itafanya nini kama mikataba tayari imesainiwa na mingine inazidi kusainiwa kila siku? au ndio mambo ya IPTL?

Hii kamati itafanya nini kama msimamo wa serikali ni kuwa mikataba ya madini imepitiwa na huu wa Buzwagi ni bora kuliko yote?

Usanii mwingine hata watoto wa kinderg.. wanaweza kuutambua tu na haiitaji Phd au degree ya sheria kujua hili!

Asante
 
waziri mkuu wake awe Matayo David wote hawa licha ya kuwa wanamtandao maslahi ni close allies wa JK wa JK..what a crap....nafikiri wana CCM wamefanya nilokuwa nalitamani.......(majina kwenye mabano) washindwe pia U- NEC

Huyu mkuu alikosea kitu kimoja according to the dataz, ni kwamba kuna soko lilikuwa lijengwe Same East na wafadhili, yeye akaamua kujifanya mjanja na kulihamishia Same West, wananchi wa East wakalalamika kwa rais, alipoulizwa yeye akawakimbilia wake wafadhili na kuwarubuni kuwa wasikubali kulijenga East,

Baadaye Muungwana, akagundua kuwa huyu mkuu, alikwenda kwa wafadhili na kum-betray, kwanza akatolewa wizara ya mlo aliyokuwemo mwanzoni, na hapa amepigwa chini, na bado next cabinet,

Wakati wa kampeni za uchaguzi wa rais, ninao ujumbe mmoja huyu mkuu alimtumia Muungwana, ambamo anamfananisha Muuungwana kuwa ni sawa na Mungu!
 
Kamati kuuangali namna gani madini yawanufaishe watanzania ipo chini ya kina Laurence Masha, alichosema raisi nikwamba yuk tayari kupanua mundo wa hiyo kamata iwe na whandisi, wnasheria, vyama vya upinzani ili kuangalia kama kuna haja ya kuboresha sheria ya madini zaidi,. nia ya kufanya hivyo ni kelele za wananchi na majibu ambayo serikali imeyatoa ambayo kwa sheria iliyopo nothing mre can be done.
 
Kilitime, unakumbuka zaidi ya mara mbili Rais Kikwete alisema "kelele za wapinzani hazinikoseshi usingizi" (labda kwa maneno tofauti tofauti). lakini kimsingi alidai kuwa serikali haiwezi kufanya kazi kwa shinikizo (mawazo yaliyorudiwa na Mohammed Seif Khatib). Sasa kwena kupanua wigo wa tume, na kuiongezea mandate.. siyo kukiri kuwa anasumbuliwa na "kelele" za wapinzani?
 
Mkuu Dua,

Heshima mbele,

Uchaguzi bado, kesho mwenyekiti atawasilisha majina ya wajumbe anowataka wa skretariati, jina la katibu mkuu, na wajumbe wa kamati kuu pia watapigiwa kura kesho, kwa hiyo bado mkuu mchezo haujaisha!

pia kuna majina 10 atapendekeza ambayo sidhani kama yatahitaji kupigiwa kura !
 
Mzee ES, Karamagi alitamka Bungeni kuwa madai ya Zitto kuwa mikataba bado inaendelea kudusuriliwa hayakuwa ya kweli na kuwa mazungumzo yamekamilika. Sasa huku kwingine kwa nini? Tayari kuna Kamati ya Mabadiliko ya Sheria ambayo imekuwa ikifanya kazi zake je ni kamati hiyo hiyo inaongezwa wajumbe tu, au ni kamati mpya specifically kwa ajili ya madini?

Kama kweli kuna tatizo kubwa katika sekta ya madini na sheria iliyopo haimnufaishi Mtanzania kama inavyostahili, kwanini asisitishe utoaji wa leseni za uchunguzi na uchimbaji hadi sheria mpya itakapopatikana kama walivyofanya Uganda?

Napenda nimpatie haki yake lakini siyo kwa mazingaombwe namna hii? kwanini asiache Bunge ndiyo liunde kamati hiyo?

hehehee, hayo maneno mekundu yametamkwa sana mwaka huu !
 
siyo kukiri kuwa anasumbuliwa na "kelele" za wapinzani?

Hakuna mwanasiasa anyeweza kukubali hadharani kuwa anasumbuliwa na wapinzani, lakini kama nilivyosema nimemuona mwenye uso kwa uso, na unajua uso huwa hausemi uongo!
 
Sura zile zile,hakuna kitu walichofanya kama ni ufisadi uko pale pale.Mimi binafsi naona wanazidi kuwatendea wananchi ndivyo sivyo.
 
Back
Top Bottom