Kaka! nashinda nikijiuliza, kwa nini pamoja na utajiri wetu mkubwa wa maliasili(nikijumuisha na nguvukazi ya takribani watu milioni 20) hatujapiga hatua tunayostahili kuwa...kwa nini? nilikuwa rwanda wiki ya juzi, nilichokiona kilithibitisha taarifa za kusifia (hususan za kitakwimu) maendeleo ya kiuchumi na kijamii, ambayo rwanda imeyapata ktk kipindi kisichozidi miongo miwili...rwanda kirasilimali kuilinganisha na jamhuri ya muungano, ni kuionea!...lkn kimaendeleo, ukitazama walivyokuwa miaka 18 iliyopita, na tulivyokuwa sisi ktk miaka hiyo 18....aaah! ni nini siri ya wenzetu wa rwanda...NIDHAMU....!sisi hatuna nidhamu inayotakiwa, ambayo ikichanganywa na rasilimali tulizonazo itatuwezesha kupata maendeleo yanayolingana na utajiri wa raslimali tulizonazo...hatuna nidhamu ya kuendeleza demokrasia ya kweli na ya dhati ktk taifa letu na ndani ya vyama vyetu vya siasa...! hatuna nidhamu ya kutii sheria..mambo yetu ya kukosa nidhamu kiujumla unaweza kuyalinganisha na vitimbi vya madereva wa dalala...!tujirekebishe, sisi sote...wapiga kura, na wapigiwa kura, tuwe na nidhamu inayostahili..kisha tupate maendeleo tunayolingana nayo...HATUNA MAENDELEO TUNAYOSTAHILI SABABU HATUNA NIDHAMU INAYOTAKIWA KITAIFA , KUPATA MAENDELEO YANAYOLINGANA NA UTAJIRI NA RASLIMALI TULIZONAZO...HATA AJE NANI KIUONGOZI, BILA KUWA NA NIDHAMU....BURE!!!!....lord almight....guide and guards all the inhabitants of this part of "mama africa" towards nothing short than deserved displine needed for our political, economical, and social progress and development...
 
Kaka! nashinda nikijiuliza, kwa nini pamoja na utajiri wetu mkubwa wa maliasili(nikijumuisha na nguvukazi ya takribani watu milioni 20) hatujapiga hatua tunayostahili kuwa...kwa nini? nilikuwa rwanda wiki ya juzi, nilichokiona kilithibitisha taarifa za kusifia (hususan za kitakwimu) maendeleo ya kiuchumi na kijamii, ambayo rwanda imeyapata ktk kipindi kisichozidi miongo miwili...rwanda kirasilimali kuilinganisha na jamhuri ya muungano, ni kuionea!...lkn kimaendeleo, ukitazama walivyokuwa miaka 18 iliyopita, na tulivyokuwa sisi ktk miaka hiyo 18....aaah! ni nini siri ya wenzetu wa rwanda...NIDHAMU....!sisi hatuna nidhamu inayotakiwa, ambayo ikichanganywa na rasilimali tulizonazo itatuwezesha kupata maendeleo yanayolingana na utajiri wa raslimali tulizonazo...hatuna nidhamu ya kuendeleza demokrasia ya kweli na ya dhati ktk taifa letu na ndani ya vyama vyetu vya siasa...! hatuna nidhamu ya kutii sheria..mambo yetu ya kukosa nidhamu kiujumla unaweza kuyalinganisha na vitimbi vya madereva wa dalala...!tujirekebishe, sisi sote...wapiga kura, na wapigiwa kura, tuwe na nidhamu inayostahili..kisha tupate maendeleo tunayolingana nayo...HATUNA MAENDELEO TUNAYOSTAHILI SABABU HATUNA NIDHAMU INAYOTAKIWA KITAIFA , KUPATA MAENDELEO YANAYOLINGANA NA UTAJIRI NA RASLIMALI TULIZONAZO...HATA AJE NANI KIUONGOZI, BILA KUWA NA NIDHAMU....BURE!!!!....lord almight....guide and guards all the inhabitants of this part of "mama africa" towards nothing short than deserved displine needed for our political, economical, and social progress and development...

Matatizo yote yameshatajwa na wachangiaji hapa JF na jinsi ya kutatua matatizo tunajua. Sasa wananchi wana weza kuacha kuchagua mafisadi na wakachagua watu watakao leta maendeleo. Mahakama aiheshimiki, Ubinafsi wa hali ya juu.Rwanda wana udikteta kama tunautaka Tanzania tuseme
 
Matatizo yote yameshatajwa na wachangiaji hapa JF na jinsi ya kutatua matatizo tunajua. Sasa wananchi wana weza kuacha kuchagua mafisadi na wakachagua watu watakao leta maendeleo. Mahakama aiheshimiki, Ubinafsi wa hali ya juu.Rwanda wana udikteta kama tunautaka Tanzania tuseme
...Mama wa matatizo yote ambaye yamedumaza harakati zetu za kujiletea maendeleo ni ukosefu wetu wa nidhamu....sisi kama wapiga kura, kwa kiasi kikubwa hatuna nidhamu na tunanunulika kwa bei poa ya au, pesa ngapi, dini gani, kabila gani, mkoa gani, ukanda gani, na hata jinsia gani...hiyo ndio "bei" ya wapiga kura wasio na nidhamu, kutoka kwa "wapigiwa" kura wasio na nidhamu....nukta inayowakutanisha jamii ya wapiga kura wa aina hiyo, na wapigiwa kura wa aina hiyo ina sifa moja kuu! RUSHWA!...wapiga kura wanakuwa "rushwa rushwa, na waliopigiwa halikadhalika pia...ni sodoma na gomora ya rushwa, yenye kina lutfa wachache...!wengi wetu tuko kwenye "mduara" wa sodoma na gomora ya rushwa...! fursa ya "sisi wa mitaani" ktk nchi hii iko ktk utekelezaji wa dhati wa misingi ya demokrasia...na suluhisho la umasikini wetu liko ktk ukuaji uchumii wenye uwiano sawa , ambao ktk utandawazi unategemea zaidi na zaidi makundi ya ushirika wa uzalishaji mali, biashara na utoaji huduma... yenye kuundwa na "wa mitaani" kwa msaada wa serikal,i na asasi zisizo za kiserikali, yenye kuwezeshwa ki vitendea kazi, kielimu,kiujuzi, kifedha...na kupatiwa kipaumbele kwenye zabuni za umma na za serikali..ikibidi hata kwa upendeleo, ili pato litakalolipwa kwa zabuni hizo liende moja kwa moja kunufaisha wengi mitaani...lkn ktk hali ya rushwa rushwa, hilo halifanyiki...sijawahi sikia mgombea yeyote (si wa chama tawala, wala vya upinzani) kwenye kampeni zake akitoa wito na mikakati ya kupunguza umasikini wa "wa mitaani" kupitia ushirika, zaidi ya (wanasiasa hao) kuhamasisha "wa mitaani" kumpa "kula" na kulinda masanduku ya uchaguzi yasiibiwe...kupitia kagame rwanda ilipata/imepata dawa ya harakati za maendeleo yake ambao msingi wake ni zaidi ya demokrasia....udikteta wa kagame ni mawazo ya wapinzani wa kagame...ANGALIZO...
"..DEMOKRASIA NDIYO ILIMUWEKA "FUHRER" MADARAKATI NA CHAMA CHAKE CHA NAZI....."
 
Imeelezwa kuwa kasi ndogo ya kupungua kwa umasikini nchini inatokana na sekta zinazoendesha uchumi kutoajiri watu wengi.

Hayo yamesemwa na Mshauri Mwelekezi wa Taasisi ya Utafiti wa Masuala ya Kiuchumi na Kijamii (ESRF), Deo Mtalemwa, wakati akizungumza katika warsha ya siku moja ya kutoa maoni ya wadau wa serikali za mitaa na asasi za kiraia juu ya malengo ya milenia (MDG), mjini hapa jana.

Mtalemwa ambaye amefanyakazi na Benki ya Afrika (ADB) kama Afisa Mikopo na Afisa Uhusiano kwa miaka 20, alisema sekta za msingi zinazoendesha uchumi wa nchi kama vile, madini, viwanda, ujenzi na utalii zimeajiri idadi ndogo ya Watanzania ikilinganishwa na sekta ya kilimo ambayo licha ya kuajiri idadi kubwa ya watu lakini imekosa msukumo wa kutosha kuchangia ukuaji wa uchumi.

Sababu nyingine alizotaja kukwamisha jitihada za Tanzania kupunguza umasikini ni, kuwepo kwa migawanyo mibovu ya rasilimali za nchi, baadhi ya mikoa kuwa na rasilimali nyingi na mingine ikiwa haina rasilimali za kutosha na kuwepo kwa mifumo mibovu ya ukusanyaji kodi na usimamizi wake.

Alisema ili kukabiliana na changamoto hizo, ni lazima Tanzania ikapanua wigo wa ukusanyaji kodi ili Watanzania wote walipe kodi na kutolea mfano wa posho za vikao mbalimbali kuwa zimekuwa zikitolewa pasipo kukatwa kodi jambo ambalo alidai ni eneo jingine linaloweza kupanua wigo wa kodi.

Aidha, Mutalemwa aliwataka Watanzania kutotumia njia za ujanja ujanja kukwepa kodi badala yake walipe kodi kwa hiari ili kujenga ujasiri wa serikali wa kuhoji pale ambapo wanaona matumizi ya fedha zao hayafanywi kwa usahihi.

Hata hivyo, alisema Tanzania imefanya vizuri katika kukuza uchumi wake kutoka asilimia 6.8 mwaka jana hadi kufikia asilimia 7.1 mwaka huu.

Alisema utafiti uliofanywa na Umoja wa Mataifa umebaini kuwa, umasikini nchini umepungua kwa asilimia 5 katika kipindi cha miaka 18 toka mpango wa milenia wa kupunguza umasikini duniani ulipopitishwa na mataifa 189 Tanzania ikiwemo na kuanza kufanyiwa kazi mwaka 1994 mpaka sasa.

Takwimu za umoja huo zinaonyesha uchumi wa Tanzania umekuwa kwa asilimia 7.1 mwaka huu toka asilimia 6.8 mwaka 2011, huku Uganda ikionyesha uchumi wake kukua kwa kasi zaidi kwa toka asilimia 4.1 mpaka kufikia asilimia 6.0.

Nchi nyingine katika ukanda wa Afrika Mashariki ni Rwanda ambayo uchumi wake umekua kwa asilimia 9.9 kutoka asilimia mwaka 2011 hadi asilimia 8.8 mwaka huu, huku Burundi ukikua kwa 4.8 mwaka huu toka asilimia 4.2 mwaka jana.

Kwa upande wa Kenya, uchumi wake unaonyesha kushuka kwa asilimia 1.6 kutoka asilimia 5.1 mwaka jana hadi asilimia 3.5 mwaka huu.


CHANZO: NIPASHE
 
pamoja na sababu za mutalemwa sababu nyingine ni uongozi mbaya na usio na ubunifu, ufisadi uliotukuka, uvivu na uzembe wa waTanzania walio wengi na kuhusudu sana anasa
 
Ateuliwe kuwa mshauri wa Jakaya Mrisho Kikwete since ye hajui kwa nini invisible ni masikini..
 
Huyu mtaalamu naye anababaisha kweli!!! Du!! Tatizo la ajira na kukwepa kulipa kodi is not the primary cause of poverty in Tanzania! What about Corruption and lack of transparency in public finances? What about poor economic policies? What about unfair contracts performed by business companies in Tanzania? What about unfair international Trade imbalance? Kwa hiyo ndio kusema kwamba huyo mtalaamu wetu haya yote hakuyajua au aliyasahau kidogo?
 
huyu naye anaimba wimbo ule ule wa kila siku wote tunajua ili tuendelee tunahitaji vitu 4 bila kujali tunafata mfumo gani wa siasa1.watu 2. ardhi 3.siasa safi na 4.Uongozi bora badala ya kusubiri Un watufanyie utafiti inabidi tujiangalie wenyewe wapi tumekwama aache kutuletea hadithi tunahitaji vitendo
 
TANZANIA INA MADINI, GESI, MALIASILI NA ARDHI KUBWA, KWA NINI NI MASKINI?





Makaa ya mawe ya Kiwira, Mbeya.
KWANZA kabisa tuanze makala haya kwa kumshukuru Mungu kwa kuweza kutupa uhai na afya, hivyo wote tunalazimika kumtukuza na kumuabudu milele.
Niwakumbushe tu Watanzania wenzangu kwamba nchi ambazo leo zinatajwa kuwa ni tajiri kama vile Singapore, Korea Kusini, Malaysia na Taiwan zilikuwa pamoja nasi katika fungu la nchi maskini sana duniani wakati tunapata uhuru mwaka 1961.
attachment.php





Mitambo ya gesi Ubungo jijini Dar.
Ajabu ni kwamba wenzetu wametuacha tukiendelea kuogelea katika lindi la umaskini wa kutisha hadi hii leo licha ya kuwa na madini, gesi na rasilimali za mali asili na ardhi kubwa.
Sasa nini kifanyike? Kwanza lazima tukubali kwamba tumechelewa sana kuandaa nguvu kazi ya kusimamia na kuendesha sekta za madini na nishati na mbaya zaidi ni kwamba baadhi ya wanaoteuliwa kusimamia siyo waaminifu.
Mnakumbuka aliyewahi kuwa waziri wa mambo ya ndani ya nchi, Augustine Lyatonga Mrema aliwahi kukamata dhahabu ya mabilioni ya shilingi uwanja wa ndege? Hujasikia kuwa kuna michanga ya madini inapelekwa nje ya nchi huku Watanzania wakiwa hawana la kufanya?
Umewahi kusikia kwamba kuna makontena yanakamatwa nje ya nchi yakiwa na nyara za serikali? Hujasikia kuwa kuna mikataba mibovu ya madini ambayo huwanufaisha wawekezaji badala ya wananchi?
Hujawahi kusikia kuwa kuna wanyama pori hai ambao wamekuwa wakisombwa hapa nchini na kupelekwa nje ya nchi kwa manufaa ya watu wachache?
Hakika sekta ya nishati na madini ni hovyo na tulipaswa kuwa tumetoa mafunzo kwa vijana wengi katika ngazi na viwango mbalimbali kadiri inavyowezekana ili sekta hizo zisimamiwe na kuendeshwa na wananchi wazalendo badala ya wageni.
Gesi Tanzania tunayo na Watanzania wengi wanakumbuka kuwa, ugunduzi wa mwanzo wa gesi asilia ulifanyika katika maeneo ya Songosongo, mkoani Mtwara na baadaye katika eneo la Mnazi Bay, mkoani Lindi kati ya mwaka 1974 na 2004, hiyo ni miaka mingi sana, tujiulize Watanzania wamenufaikaje hadi sasa?
Kama vile hiyo haitoshi, ugunduzi mwingine wa gesi asilia ulikuwa katika eneo la Mkuranga, mkoani Pwani mwaka 2007 na eneo la Kiliwani mwaka 2008 ambalo lipo kusini mwa Songosongo na kwamba ugunduzi mkubwa zaidi ulikuwa mwaka 2010 kwenye kina kirefu cha maji katika Bahari ya Hindi.
Wataalamu katika sekta ya nishati sasa wamethibitisha kwamba Tanzania ina kiwango kikubwa cha mafuta ya petroli katika maeneo mbalimbali.
Ugunduzi huo ni mbali na ule wa kuzalisha umeme kwa kutumia upepo mkoani Singida; ugunduzi wa makaa ya mawe ya Kiwira, Mchuchuma na Ngaka; ugunduzi wa Urani katika Mkoa wa Ruvuma; na ule wa kuzalisha umeme kwa kutumia mbolea ya Ammonia maeneo ya Kilwa na Minjingu katika Mikoa ya Lindi na Arusha.
Ninaposema Tanzania siyo maskini sitanii, ni kweli angalia mifano hiyo michache. Tukichanganya miradi hiyo na mingine mingi ambayo ilianza uzalishaji miaka kadhaa iliyopita, ikiwamo ya dhahabu, almasi, Tanzanite na chuma, tunaona kwamba Tanzania ina utajiri wa kupindukia.
Ni wazi kwamba iwapo rasilimali hizo zitatumiwa kwa umakini na kwa manufaa ya wananchi wote na kwa kusimamiwa na viongozi wenye uzalendo wa kweli, wasio wabinafsi, nchi yetu itatoka katika fungu la nchi maskini na kuwa katika fungu la nchi tajiri duniani.
Tumeambiwa kuwa serikali ina mpango wa kuzindua mradi wa mafunzo na elimu ya ufundi stadi kwa ajili ya sekta ya gesi na mafuta katika Chuo cha Veta Mtwara na inapaswa kupeleka wataalamu wengi zaidi katika vyuo na nchi zinazotoa mafuta kwa wingi kama Norway, ili wakirudi waendeshe na kusimamia sekta hizo katika idara zote.
Lakini pia tumeambiwa kuwa kuna mpango wa kufundisha katika vyuo husika na kusimamia taasisi za nishati na madini kama Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) na Shirika la Madini la Taifa (Stamico).
Nasema huo ni utaratibu mzuri na nasisitiza kuwa tusikubali tena kufanya kosa la kukabidhi utajiri na rasilimali zetu kwa wageni wanaoingia nchini kwa jina la wawekezaji.
Baadhi yao ndiyo hao wanaotuingiza mkenge kwa kuingia mikataba yenye hasara kwa taifa na wanawatumia maofisa wetu wasio waaminifu ambao hawajali utu au thamani ya maendeleo ya nchi na badala yake kujinufaisha wenyewe.
Hakika kwa kuwa tuna vitu hivyo, ardhi kubwa tunayo, tunachohitaji sasa ni wasomi waaminifu watakaohakikisha nchi inafika kwenye neema kwa manufaa ya raia wote.
Jipu limepasuka, siwezi kuwa adui kwa kusema ukweli.


 

Attachments

  • SongoSongogasplant.JPG
    SongoSongogasplant.JPG
    42.6 KB · Views: 518
ujamaa na kujitegemea ni siasa mbaya sana . Siasa hii ndiyo iliyotuleta hapa katika umasikini uliopo. Siasa hiii ilipiga marufuku kuwepo kwa matajili na hata wale wenye kumiliki maduka . Haya niliyaona pale vywawa mbozi kwa wahindi kunyang'anywa maduka yao yote na kufungua duka moja tuu la walaji.

Siasa hii ya ujamaa na kujitegemea haikujenga shule wala vyuo vya ualaimu ili kutoshereza mahitaji ya watanznaia. Iliweka ualimu wa UPE na kila kukicha darsa la saba waliofeli walishindiliwa mashambani kufanya kilimo badala ya kusomesha vijana wengi kujenga nchi.

Siasa hii iliweka vikwazo kwa vijana kwenda jiunga na chuo kikuu na wakaweka azimio la musoma ili kila kijana kae nyumbani akifanya kazi kwa miaka miwili na baadae apply chuo kikuu.

Siasa hii chini ya azimio la arusha ilifuta hati miliki kwa wanamuziki na hivyo hata kukaktaa kujenga kiwanda cha santuli ili watu wenye fani ya muziki watajilike nayo. matokeao yake mziki ulikuwa haulipi kama ilivyi siku hizi. hakuna hata mwanamuziki mmoja wa kitanznaia aliyefikia pato la kununua gari. awe balisidya, mbaraka, malijani au ahmedi kipande wote waliishia kufa masikini wa kutupwa.

Halafu siasa hii ya ujamaa na kujitegemea haikupenda ma investors wala nchi tajiri. ma investors iliwaita wanyinyaji na investment iliita milija ya kunyonya.

halafu kitu kingine kibaya zaidi ni pale raisi mtawala wa nchi hii alipojiwekewa kinga kikatiba kuwa aharuhusiwi kishitakiwa hata akifanya kosa gani. Pili raisi kujiwekewa madaraka makubwa kupita mahakama kuuu na bunge.

Nchi yeyote inayolea wananchi katika mazingira kama hayo na raisi kijipendelea kikatiba namna hiyo inaishia kuwa masikini wa kutupwa ingawa ina rasilimali kali kupita ubelgiji. hii ndiyo sababu nchi yetu ni maisikini mpaka leo na kesho asubuhi. mimi naamini kuwa mungu yupo na aliukomalie ukomunisti ufe kwa sababu moja tuu, nayo kuiokoa nchi yetu ilikuwa inakwenda mbele bila dira. hata hayati horace kolimba aliisha wahi kusema.

Ndugu yangu ukibahataka kutoka nje ya nchi, halafu uone mataifa hapa duniani yanavyojitahidi kufanyia kazi kitu kiitwacho unemployment kwa kuweka urafiki na mataifa kama UK, USA na Israel. Halafu uone kwa jinsi nchi yetu ilivyo jifanya haijui kufanyia kazi kitu kiitwacho unemployment na kuzidi kuichukia USA, UK na Israel kwa mtazamo wa kisiasa tuu. utabakia unalia kila siku!! ndio maana umasikini wetu hauwezi kuisha kirahisi!
 
TANZANIA INA MADINI, GESI, MALIASILI NA ARDHI KUBWA, KWA NINI NI MASKINI?





Makaa ya mawe ya Kiwira, Mbeya.
KWANZA kabisa tuanze makala haya kwa kumshukuru Mungu kwa kuweza kutupa uhai na afya, hivyo wote tunalazimika kumtukuza na kumuabudu milele.
Niwakumbushe tu Watanzania wenzangu kwamba nchi ambazo leo zinatajwa kuwa ni tajiri kama vile Singapore, Korea Kusini, Malaysia na Taiwan zilikuwa pamoja nasi katika fungu la nchi maskini sana duniani wakati tunapata uhuru mwaka 1961.
attachment.php





Mitambo ya gesi Ubungo jijini Dar.
Ajabu ni kwamba wenzetu wametuacha tukiendelea kuogelea katika lindi la umaskini wa kutisha hadi hii leo licha ya kuwa na madini, gesi na rasilimali za mali asili na ardhi kubwa.
Sasa nini kifanyike? Kwanza lazima tukubali kwamba tumechelewa sana kuandaa nguvu kazi ya kusimamia na kuendesha sekta za madini na nishati na mbaya zaidi ni kwamba baadhi ya wanaoteuliwa kusimamia siyo waaminifu.
Mnakumbuka aliyewahi kuwa waziri wa mambo ya ndani ya nchi, Augustine Lyatonga Mrema aliwahi kukamata dhahabu ya mabilioni ya shilingi uwanja wa ndege? Hujasikia kuwa kuna michanga ya madini inapelekwa nje ya nchi huku Watanzania wakiwa hawana la kufanya?
Umewahi kusikia kwamba kuna makontena yanakamatwa nje ya nchi yakiwa na nyara za serikali? Hujasikia kuwa kuna mikataba mibovu ya madini ambayo huwanufaisha wawekezaji badala ya wananchi?
Hujawahi kusikia kuwa kuna wanyama pori hai ambao wamekuwa wakisombwa hapa nchini na kupelekwa nje ya nchi kwa manufaa ya watu wachache?
Hakika sekta ya nishati na madini ni hovyo na tulipaswa kuwa tumetoa mafunzo kwa vijana wengi katika ngazi na viwango mbalimbali kadiri inavyowezekana ili sekta hizo zisimamiwe na kuendeshwa na wananchi wazalendo badala ya wageni.
Gesi Tanzania tunayo na Watanzania wengi wanakumbuka kuwa, ugunduzi wa mwanzo wa gesi asilia ulifanyika katika maeneo ya Songosongo, mkoani Mtwara na baadaye katika eneo la Mnazi Bay, mkoani Lindi kati ya mwaka 1974 na 2004, hiyo ni miaka mingi sana, tujiulize Watanzania wamenufaikaje hadi sasa?
Kama vile hiyo haitoshi, ugunduzi mwingine wa gesi asilia ulikuwa katika eneo la Mkuranga, mkoani Pwani mwaka 2007 na eneo la Kiliwani mwaka 2008 ambalo lipo kusini mwa Songosongo na kwamba ugunduzi mkubwa zaidi ulikuwa mwaka 2010 kwenye kina kirefu cha maji katika Bahari ya Hindi.
Wataalamu katika sekta ya nishati sasa wamethibitisha kwamba Tanzania ina kiwango kikubwa cha mafuta ya petroli katika maeneo mbalimbali.
Ugunduzi huo ni mbali na ule wa kuzalisha umeme kwa kutumia upepo mkoani Singida; ugunduzi wa makaa ya mawe ya Kiwira, Mchuchuma na Ngaka; ugunduzi wa Urani katika Mkoa wa Ruvuma; na ule wa kuzalisha umeme kwa kutumia mbolea ya Ammonia maeneo ya Kilwa na Minjingu katika Mikoa ya Lindi na Arusha.
Ninaposema Tanzania siyo maskini sitanii, ni kweli angalia mifano hiyo michache. Tukichanganya miradi hiyo na mingine mingi ambayo ilianza uzalishaji miaka kadhaa iliyopita, ikiwamo ya dhahabu, almasi, Tanzanite na chuma, tunaona kwamba Tanzania ina utajiri wa kupindukia.
Ni wazi kwamba iwapo rasilimali hizo zitatumiwa kwa umakini na kwa manufaa ya wananchi wote na kwa kusimamiwa na viongozi wenye uzalendo wa kweli, wasio wabinafsi, nchi yetu itatoka katika fungu la nchi maskini na kuwa katika fungu la nchi tajiri duniani.
Tumeambiwa kuwa serikali ina mpango wa kuzindua mradi wa mafunzo na elimu ya ufundi stadi kwa ajili ya sekta ya gesi na mafuta katika Chuo cha Veta Mtwara na inapaswa kupeleka wataalamu wengi zaidi katika vyuo na nchi zinazotoa mafuta kwa wingi kama Norway, ili wakirudi waendeshe na kusimamia sekta hizo katika idara zote.
Lakini pia tumeambiwa kuwa kuna mpango wa kufundisha katika vyuo husika na kusimamia taasisi za nishati na madini kama Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) na Shirika la Madini la Taifa (Stamico).
Nasema huo ni utaratibu mzuri na nasisitiza kuwa tusikubali tena kufanya kosa la kukabidhi utajiri na rasilimali zetu kwa wageni wanaoingia nchini kwa jina la wawekezaji.
Baadhi yao ndiyo hao wanaotuingiza mkenge kwa kuingia mikataba yenye hasara kwa taifa na wanawatumia maofisa wetu wasio waaminifu ambao hawajali utu au thamani ya maendeleo ya nchi na badala yake kujinufaisha wenyewe.
Hakika kwa kuwa tuna vitu hivyo, ardhi kubwa tunayo, tunachohitaji sasa ni wasomi waaminifu watakaohakikisha nchi inafika kwenye neema kwa manufaa ya raia wote.
Jipu limepasuka, siwezi kuwa adui kwa kusema ukweli.


ndugu yangu umezungumza points nzuri mno ambazo mawaziri waliopo madarakani hawazitaki kusikia wala kuzizingatia. Ili uliyoyasema yatimie ni lazima kwanza raisi wa nchi anyang'anywe uwezo wa kimadaraka wa kutawala nchi na halafu madaraka yake yagawanywe kwa bunge na mahakama kuu. halafu raisi lazima asiwe na haki ya kikatiba kukingwa kama akifanya makosa.

Yaani tukifanyikiwa kumbana mzee wa hekima Giussepe au joao warioba ayaweke katika katiba yetu mpya. nakuhakikishia kuwa tutajenga nchi huku kila mtu akiogopa kuiba wala kula rushwa. Hivi ndivyo walivyofanya wamarekani na waisrael walipoanza kujenga nchi zao.

hongera sana amigo kwa walaka wako ambao ni mtamu saaanah saaanah!
 
ndugu yangu umezungumza points nzuri mno ambazo mawaziri waliopo madarakani hawazitaki kusikia wala kuzizingatia. Ili uliyoyasema yatimie ni lazima kwanza raisi wa nchi anyang'anywe uwezo wa kimadaraka wa kutawala nchi na halafu madaraka yake yagawanywe kwa bunge na mahakama kuu. halafu raisi lazima asiwe na haki ya kikatiba kukingwa kama akifanya makosa.

Yaani tukifanyikiwa kumbana mzee wa hekima Giussepe au joao warioba ayaweke katika katiba yetu mpya. nakuhakikishia kuwa tutajenga nchi huku kila mtu akiogopa kuiba wala kula rushwa. Hivi ndivyo walivyofanya wamarekani na waisrael walipoanza kujenga nchi zao.

hongera sana amigo kwa walaka wako ambao ni mtamu saaanah saaanah!

Tango73 siyo mahakama na bunge tu bali vyombo vyote vya dola vishirikishe raia kabla ya kufanya maamuzi yake yawe ya kisera au ya teuzi za viongozi....................kwa kupitia uhakiki........sisi ndiyo tunawajua jinsi wanavyotudhulumu tukipewa nafasi tutakuwa tukiwaumbua wabaya wetu na mambo yatakwenda vyema...........
 
Nasema huo ni utaratibu mzuri na nasisitiza kuwa tusikubali tena kufanya kosa la kukabidhi utajiri na rasilimali zetu kwa wageni wanaoingia nchini kwa jina la wawekezaji.
Baadhi yao ndiyo hao wanaotuingiza mkenge kwa kuingia mikataba yenye hasara kwa taifa na wanawatumia maofisa wetu wasio waaminifu ambao hawajali utu au thamani ya maendeleo ya nchi na badala yake kujinufaisha wenyewe.
Hakika kwa kuwa tuna vitu hivyo, ardhi kubwa tunayo, tunachohitaji sasa ni wasomi waaminifu watakaohakikisha nchi inafika kwenye neema kwa manufaa ya raia wote.
Jipu limepasuka, siwezi kuwa adui kwa kusema ukweli.

MziziMkavu tuna raisi ambaye hajui kwanini sisi ni masikini lakini angependa kututoa kwenye umasikini ambao chanzo chake hakifahamu...........................utajiri wa nchi siyo maliasili zake ila utashi wa kukataa dhuluma kwa kujenga misingi ya kuimarisha taasisi ili ziweze kutenda haki...........la ajabu viongozi wa zamani hawataki kusikia hilo kama Malecela anayedai kuwa tusipunguze madaraka ya raisi nchi bado changa sasa itakuwa lini na hii dhuluma ya kuwatimua wazawa na kumilikisha nchi wageni? Kisingizio ni kuwa tupishe wawekezaji kama vile mzawa siyo mwekezaji................hii sasa ni aibu yetu.
 
MziziMkavu tuna raisi ambaye hajui kwanini sisi ni masikini lakini angependa kututoa kwenye umasikini ambao chanzo chake hakifahamu...........................utajiri wa nchi siyo maliasili zake ila utashi wa kukataa dhuluma kwa kujenga misingi ya kuimarisha taasisi ili ziweze kutenda haki...........la ajabu viongozi wa zamani hawataki kusikia hilo kama Malecela anayedai kuwa tusipunguze madaraka ya raisi nchi bado changa sasa itakuwa lini na hii dhuluma ya kuwatimua wazawa na kumilikisha nchi wageni? Kisingizio ni kuwa tupishe wawekezaji kama vile mzawa siyo mwekezaji................hii sasa ni aibu yetu.
Mkuu Rutashubanyuma Uchumi mnao lakini mnaukalia!!!
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Rutashubanyuma Uchumi mnao lakini mnaukalia!!!

MziziMkavu uchumi hatuna tungelikuwa nao tungelikuwa mbali. Uchumi siyo madini, ardhi au chochote kile bali ni maadili ya kumwogopa Mungu na yeye ndiye huifanya nchi iwe tajiri.........maadili ya khofu kwa Mungu ndiyo huondoa dhuluma na kujenga misingi ya utu ambayo ndiyo chimbuko la maendeleo ya nchi yoyote duniani. Hakuna nchi iliyoweza kuendelea bila ya kuwa na misingi ya kuuhehsimu utu wa mwanaadamu bila ya kujali khali yake ya kipato au jinsia au maumbile yake au imani yake uya dini.............Hiyo misingi ya utu ndiyo uchumi sisi hatuna kwa hiyo hatujakalia chochote kile ila upumbavu wetu wa kujenga misingi ya dhuluma chini ya kibwagizo cha "mpishe mwekezaji............"
 
Tanzania sio nchi Masikini,tuna mlima Kilimanjaro unoingiza fedha nyingi za kigeni,madini pekee ya tanzanite,nk.Tatizo letu ni usimamizi mbovu,siasa chafu,uongozi usio bora,tamaa ya kujilimbikizia mali,kukosa uzalendo mfano mchanga wenye madini kusafirishwa nje,kwani wenye mamlaka hamuoni?zaidi wenye dhamana na nchi hii wana laana ya kilio cha wananchi wake,kwenye sekta ya kilimo,"wakulima mnajua''.kwa upande wa Watumishi ,kilichopo ni kudanganywa kama watoto mfano wanapandishwa madaraja kwa barua tu,mshahara haubadilishwi.MWISHO!"KAMA WENYE DHAMANA NA NCHI HII MMESHINDWA KUINUA UCHUMI WETU NA KUFANYA MAISHA YAWE BORA KWA KILA MTANZANIA BASI ACHIENI NGAZI NA KARIBISHENI WACHINA WAJE KUTUINULIA UCHUMI"
 
Kuna watu wa ajabu sana hii nchi . Wewe baada ya kufanyakazi ujikwamue na umasikini na usaidie ndugu zako waondokane na umasikini lakini umekaa kwenye key board unajiuliza eti kwanini tz masikini. Je wewe tajiri?
 
Back
Top Bottom