Kwaherini JF

Kwaherini JF

Hey people,

Uzi huu ni wa kuwaaga wanaJF wenzangu

Nimekutwa na cancer ambayo kimsingi nimepewa taarifa kwamba ndani ya miezi miwili sitakuwepo

Naumia lakini sina jinsi
Pole Joanah ,unaendeleaje? Nikutoe hofu naamini utakuwa sawa ,nakumbuka niliwahi kumuuguza mzee wangu kuna doctor aliniambia huyu mzee akiishi sana ni miezi sita tuu chaajabu mzee aliishi miaka nane zaidi.
 
Pole Joanah ,unaendeleaje? Nikutoe hofu naamini utakuwa sawa ,nakumbuka niliwahi kumuuguza mzee wangu kuna doctor aliniambia huyu mzee akiishi sana ni miezi sita tuu chaajabu mzee aliishi miaka nane zaidi.

Asante orturoo
Naendelea vizuri

Mimi Mungu kama ananisikia namuomba nizidi kuishi zaidi ya miaka nane aliyeongezewa mzee wako 🙏
 
Nina imani stori yangu itaishia huku kwenye vipimo vilivyokosewa ili niendelee kuwepo

How comes nina cancer na sijisikii kuumwa chochote hapa
Mdogo wangu aliwahi kufanya checkup ya moyo kwenye hospitali fulani kubwa ya rufaa (hakuwa na dalili za kuugua, alikuwa na utamaduni wa kufanya checkups tu anapojisikia) akaambiwa ana ugonjwa wa moyo na kupewa rufaa kwenda JKCI haraka asizidishe wiki mbili, kwamba tatizo lipo serious sana! Kutokana na msongo wa mawazo ndani ya siku chache wakati tukiandaa safari hiyo alikuwa tayari ana dalili kibao za ugonjwa huo!

Cha ajabu baada ya kufika JKCI alifanya vipimo 11 tofauti huku madaktari wakishangaa huko hospitali ya rufaa walipimaje hadi kubaini tatizo kubwa lisilokuwepo. Katika process za vipimo dogo alikuwa anaimarika kadri vipimo vinavyoendelea. Hadi vinakamilika zile dalili alizokuwa ame develop zilishatoweka kabisa anadunda zake. Hakupewa hata panadol za kumeza.

Nawe pia nenda hospitali kubwa zaidi upime, namini huumwi. Mungu akutangulie.
 
Kwa kweli wale wa karibu yangu waliokufa kwa cancer nikawashuhudia sio kitu cha mchezo, miezi ya mwisho ni ya mateso makali sanaaaa!
Kabisa, juzi kati kuna uncle wangu tulienda naye ocean road weeh..!! Niliogopa ile siku, watu wanaumwa jamani..!!

Nilirudi home usingizi ulikata nilikosa raha..!!
 
Uko kama mimi, naogopa kufa kabla sijamkula Lamomy bila kusahau mchepuko alionigea To yeye
Wewe una shida gani? Wenzako tuna huzuni hapa wewe unawaza papa langu..!! 😳

Haya uko wapi nikufungashie nikutumie ulitafune ukimaliza unirudishie mtsiewww..!! 😏
 
Mdogo wangu aliwahi kufanya checkup ya moyo kwenye hospitali fulani kubwa ya rufaa akaambiwa ana ugonjwa wa moyo na kupewa rufaa kwenda JKCI haraka asizidishe wiki mbili, kwamba tatizo lipo serious sana! Kutokana na msongo wa mawazo ndani ya siku chache wakati tukiandaa safari hiyo alikuwa tayari ana dalili kibao za ugonjwa huo!

Cha ajabu baada ya kufika JKCI alifanya vipimo 11 tofauti huku madaktari wakishangaa huko hospitali ya rufaa walipimaje hadi kubaini tatizo kubwa lisilokuwepo. Katika process za vipimo dogo alikuwa anaimarika kadri vipimo vinavyoendelea. Hadi vinakamilika zile dalili alizokuwa ame develop zilishatoweka kabisa anadunda zake. Hakupewa hata panadol za kumeza.

Nawe pia nenda hospitali kubwa zaidi upime, namini huumwi. Mungu akutangulie.
Kuna hichi kizazi kilichoingia kinataka kazi alafu hakitaki kufanya kazi unaenda unakutana na doctor ana Google kila kitu siku hizi kesi ni nyingi sana kwenye mahospitali in short sikuhizi hamna madaktari kuna mzee mmoja aliwahi kupewa dozi yakifafa bahati tuu alikuwa na taaluma ya udaktari wa mifugo,aliporudi kwa doctor anashangaa kumbe kwenye dirisha la dawa mfamasia hajui hata aina ya dawa.
 
Nina imani stori yangu itaishia huku kwenye vipimo vilivyokosewa ili niendelee kuwepo

How comes nina cancer na sijisikii kuumwa chochote hapa
Ndio maana nimekwambia vipimo vyetu bado, utajiua bure tu wakati una muda mrefu Mungu kakupangia.

Babu yangu pia alikua na kansa na akaamua kukaa kimya bila kuwaambia wanae, hakua akitumia dawa ipasavyo, hakua anaenda hospital ili asistukiwe ila alikaa almost 3 yrs mpaka hali yake kuja kua mbaya kabisa.
Na mpaka anakua na hali mbaya bado matumaini ya kupona yalikuwepo ni vile nae umri ulikua umemtupa mkono mno, alikua late 70's yrs.
 
Umenitisha rasmi

Nilikuwa na hopes kwamba vipimo vitakuwa vimekosewa kwasababu sijisikii kuumwa, kumbe naweza kupitia maumivu wiki za mwisho 🥺
Nyie watoa comments, kuweni makini na majibu yenu, mnazidi kumtisha huyu dada...mkumbuke hayuko sawa huyu msione majibu yake ya kishujaa hapa!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom