Dah pole sana Joanah, inahitaji ujasiri mkubwa mno kuandika ujumbe wa namna hii, so big respect kwako Joanah kwa kuwa muwazi hivi. Ni kweli binadamu wote safari yetu ni moja na hakuna anayeishi milele, lakini hii approach yako ya kukubali ukweli inaonyesha jinsi ulivyo mtu imara sana kiakili.
Hata hivyo, usiruhusu hofu icchukue maisha yako kwa sasa. Kila dakika unayopumua sasa hivi ni ya thamani kubwa sana. Cha msingi ni kupunguza stress na maumivu kadri inavyowezekana ili akili na mwili wako vipate utulivu. Tuko na wewe pamoja sana.