Kwaherini JF

Kwaherini JF

Status
Not open for further replies.
Bro acha basi.

Kuna auntie yetu (shoga yake mama) aliambiwa mwaka jana mwenzi wa 11 ata RIP lakini mpaka leo navyoandika yupo. Ana kansa ya titi.

Juzi hapa ameambiwa sijui cell mpya zimezaliwa sijui nini (lugha ya kidaktari kuna muda siielewi)

Kwahivyo bado kuna hope, Pole…

Uongeze maombi sasa
 
Hey people,

Uzi huu ni wa kuwaaga wanaJF wenzangu

Nimekutwa na cancer ambayo kimsingi nimepewa taarifa kwamba ndani ya miezi miwili sitakuwepo

Naumia lakini sina jinsi
Kama ni Muhimbili au Ocean Road au Sekouture (Mwanza) wala hata usijali, nenda India utarudi na majibu ya tofauti. Labda kama umeshaenda huko, Mungu akubariki
 
Kibongobongo hizo kansa huwa hawakadilii vizuri ama lah vipimo vyao vina walakini.

Utaambiwa hutoboi miezi miwili ajabu ikawa miaka na mikaka ukaendelea kuwepo.

Usijikatishe uhai, usijifanyie ukatili na kuwafanyia ukatili wanaokutegemea na wanaopenda uwepo wako, vuta subira.

Nina imani stori yangu itaishia huku kwenye vipimo vilivyokosewa ili niendelee kuwepo

How comes nina cancer na sijisikii kuumwa chochote hapa
 
Nakufa ndoa yangu ikiwa changa ambayo hatujapata uzao wowote 😭😭

Nakufa namuacha baba yangu
Nakufa namuacha mama yangu

Ee Mungu
Joanah mbona unaandika kwa msisitizo kana kwamba hicho kikao chako na huyo Dr Kanjanja Mungu naye alikuwepo!?

Jambo ambalo hulijui ni kwamba, kada ya afya imevamiwa na wasaka tonge ambao hawana wito wala ùelewa wa kina wa kazi yao(sio wote).

Tulia nenda kahakiki sehemu zisizopungua tatu tofauti, kama kote jibu ni hilo, basi tulia na fuata maelekezo ya utakayeona ana uelewa mzuri wa hili tatizo.
Usitangulize hisia za kufa, siku ya mtu kufa ni fumbo.
 
Nina imani stori yangu itaishia huku kwenye vipimo vilivyokosewa ili niendelee kuwepo

How comes nina cancer na sijisikii kuumwa chochote hapa
Kuna bibi mmoja pia niliwahi kumkuta Ocean Road. Mwanae alinisimulia kuwa waliambiwa ana miezi mi nne tu ya kuishi. Lakini mpaka muda ule ananisimulia miezi mi nne ilikuwa imeshapita. Yule bibi alimaliza matibabu, akapata nafuu na akaruhusiwa kurudi nyumbani ila akapangiwa clinic.

Usivunjike moyo, bado kuna tumaini.
Mungu wa Mbinguni akuponye. Pole sana. Usiache kuzingatia matibabu na maelekezo yote ya daktari na wataalam wa afya
 
Mimi sinywi pombe wala kilevi chochote situmii so obvious muda hautabadili kitu
Na ujanja wote huo kumbe hunywi gambe?....unaona sasa unasepa hujaonja bia na kitimoto vitu vitamu ajabu duniani😋😋😋

Jokes aside, Joanah umejua kuniliza, nilipenda mautani yako asee🥹🥹😭😭😭
Mimi sinywi pombe wala kilevi chochote situmii so obvious muda hautabadili kitu
Mi ndo maana nakula Savannah na nguruwe kama sina akili nzuri, embu ona mdada mrembo, charming, very young anasepa woiiii🙌🙌🙌
 
Na ujanja wote huo kumbe hunywi gambe?....unaona sasa unasepa hujaonja bia na kitimoto vitu vitamu ajabu duniani😋😋😋

Jokes aside, Joannah umejua kuniliza, nilipenda mautani yako asee🥹🥹😭😭😭

Mi ndo maana nakula Savannah na nguruwe kama sina akili nzuri, embu ona mdada mrembo, charming, very young anasepa woiiii🙌🙌🙌

Mkuu pombe sio starehe ya kila mtu, binafsi sioni uzuri wa pombe

Kitimoto kwangu mie ni haramu, situmii na sitarajii kutumia
 
Status
Not open for further replies.

Similar Discussions

Back
Top Bottom