Kwaherini JF

Kwaherini JF

Status
Not open for further replies.
mi nachoweza kusema wala usiogope. labda TAFUTA ligonjwa lingine kabambe zaidi ya kakansa hako kama LIEBOLA hivi,, eheee dawa ya moto ni moto, ata sphiis zamani ikikuwa inatibiwa kwa maleria..... yaani in short kuwa kauzu mpaka hicho kigonjwa kione kimepotea njia... pia try new thing vuta fegi au bangi get new experience

katika playlist na recomend hii song kwako by Tim Mcgraw " live like your dying" bonge la ngoma hutojutia...
 
Saratani ya nini, waliokutabiria miezi miwili ya kuishi ni hospitali ya nje ya nchi au? Wapo watu wanaishi na saratani na bado wanadunda, inategemea ni saratani ya nini.​
 
Nimezunguka wee nimerudi tena mmmh japo ni anonymous niseme ukweli inauma Joanah sina maneno ya kukwambia,ila usiache kushirikisha ndugu japo wachache watakaokusaidia katika safari za hospital. I wish its just a joke,a prank and april fools but its august now.
 
Hey people,

Uzi huu ni wa kuwaaga wanaJF wenzangu

Nimekutwa na cancer ambayo kimsingi nimepewa taarifa kwamba ndani ya miezi miwili sitakuwepo

Naumia lakini sina jinsi
sad emoji.jpg
Pole sana ndugu yetu, mwanaJamii mwenzetu.
Mama mtoto wangu anapitia hayo, ni habari nzito kuimudu. Nimemwambia tumweke Mungu mbele (ya Mungu ni mengi), asiruhusu masikitiko yatawale (japo si rahisi) kwa sababu mwili huwa unaitikia feelings espesheli unapojaribu kujiponya. Pia nimemshauri atafiti dawa zetu za kienyeji pamoja na milo mizuri ya kiasili yenye sifa za kuponyesha na/ama kurutubisha mwili kichanya.
 
Andiko hili limenitafakarisha sana. Tuache kwanza habari ya Joanah. Tujiulize sisi wenyewe, sisi ambao hatujui siku, saa, wala muda wetu umefika lini, tumejiandaaje?

Huenda unaandika hapa kumpa pole, kumwonea huruma au kumfariji mtoa mada kwa sababu ameambiwa ana prognosis ya miezi miwili au chini ya hapo.

Lakini hebu geuza swali hilo kwako mwenyewe. Kama ingekuwa wewe umeambiwa, “Una miezi miwili tu au chini ya hapo,” ungefanya nini?

Wengi wetu tungeanza kusema, Nitajikaribisha zaidi kwa Mungu. Nitatubu. Nitasali zaidi. Nitawaomba msamaha nilio wakosea. Nitawasamehe walionikosea. Nitakaa karibu na familia yangu na watu ninaowapenda. Nitatengeneza mambo yangu na Mungu.

Vizuri kabisa! Lakini swali ni hili, Kwa nini tusifanye hivyo sasa?
Kwa nini tusimtafute Mungu kwa moyo wote wakati bado hatujaambiwa tuna miezi miwili?

Kwa nini tusitubu leo, badala ya kusubiri siku tutakayoogopa kifo?
Kwa nini tusisamehe leo, badala ya kusubiri dakika za mwisho?
Kwa nini tusimpende Mungu leo kwa nguvu zetu zote, badala ya kusubiri mwili utakapokuwa hauna nguvu tena?

Tunajua kabisa kwamba kifo hakitupi appointment. Hakipigi simu kusema, “Nakuja kesho saa 10.” Hakituandikii ujumbe kusema, “Jiandae, zimebaki siku 30.”

Wengine wanapewa taarifa ya muda wao. Sisi wengine tunaishi bila taarifa hiyo.
Na labda hapo ndipo kuna tofauti kubwa.
Yeye amepewa kile ambacho sisi hatujapewa. Nafasi ya kuhesabu siku zake.

Lakini sisi tunaishi kana kwamba tumepewa miaka mingi.
Tunapanga kesho, mwezi ujao, mwaka ujao… lakini hatujui kama tutafika huko.
Huenda mtu anayejua amebakiza miezi miwili ndiye aliyeanza kuishi kwa umakini kuliko yule anayefikiri ana miaka ishirini mbele yake.

Kwa hiyo, tusimwangalie tu kwa huruma.
Tujitazame sisi wenyewe.
Kama leo ungeambiwa huu ndio mwezi wako wa mwisho, ungeendelea na maisha haya haya?
Ungeendelea kubeba chuki hiyo?
Ungeendelea kuahirisha toba?
Ungeendelea kusema, “Nitabadilika baadaye”?
Ungeendelea kuishi mbali na Mungu?
Kama jibu ni hapana, basi kwa nini unasubiri mpaka uambiwe una muda mfupi wa kuishi?

Neema si kuambiwa siku yako ya mwisho. Neema ni kupewa leo.
Leo bado unaweza kutubu.
Leo bado unaweza kusamehe.
Leo bado unaweza kurekebisha.
Leo bado unaweza kumtafuta Mungu.
Leo bado unaweza kusema, “Bwana, niko hapa.”

Kwa hiyo, huenda hatuna neema ya kujua tumebakiwa na muda gani kama alivyoambiwa yeye. Lakini tunayo neema kubwa zaidi ambayo mara nyingi tunaipuuza.

Tunaishi leo.
Na leo ndiyo siku ya kujiandaa.
Usisubiri prognosis ikufundishe thamani ya maisha. Usisubiri kifo kikufundishe kumtafuta Mungu. Usisubiri dakika za mwisho ndipo uanze kuishi kwa ajili ya Mungu.

Kwa sababu ukweli mchungu ni huu:
Sote tuna prognosis tofauti ni kwamba hakuna aliyetuambia tarehe yake.

Tafakari.
Chukua hatua.
Mungu atusaidie tusije tukatamani tungepewa zile siku tunazopoteza leo. 🙏
Mnajuaje huyu kabakisha muda fulani wa kuishi
 
Hey people,

Uzi huu ni wa kuwaaga wanaJF wenzangu

Nimekutwa na cancer ambayo kimsingi nimepewa taarifa kwamba ndani ya miezi miwili sitakuwepo

Naumia lakini sina jinsi
Umekosea sana kukubali Akili za mwanadamu.
Tuombe msamaha, mwenye hatma ya mwisho ya uhai wako ni Mungu tuu. Usitoe ruhusa kwa shetani kukufanya apendacho.
 
Niko na mixed feelings yaani hata sielewi nikuandikie nini kikupe faraja 😭
Sema kama uwezo upo jaribu hospitals tofauti,ikiwezekana nenda hata nairobi ukapate second opinion.
Hizi hospital zetu za bongo kwakweli sio za kuziamini mara moja kwa issue nzito kama hizi,
Kivyovyote vile usikubali kuondoka kirahisi jaribu kupambania uhai wako as you said bado mdogo mno!
 
Status
Not open for further replies.

Similar Discussions

Back
Top Bottom