Kuajiriwa ni utumwa

Kuajiriwa ni utumwa

Sema kweli hiki kitu hata me kinaniwazisha sana, kwa mshahara wangu huu hata nikisema nijibane siwezi pata nauli ya kwenda Dubai na kula maisha kwa wiki. Wakati nina wana kibao walioko kwenye business zao mjini sehemu kama Dubai na China wanaingia karibu kila mwezi . Kuna siku nitafanya maamuzi magumu inshallah
Usiige KUNYA kwa tembo utapasuka msamba! Unajua wanafanya biashara gani?
 
Waliojiajiri ndo wametoka kupiga asubuhi hii kwa watumishi wa umma wakopeshwe, nao wa umma ndiyo tumetoka ku clear madeni kwa mangi chenji ni liquor store baadae

Kabla hujaqcha kazi jitathimini vya kutosha de guna, jipange haswa

Binafsi ntaanza kuwekeza bado nipo kwenye ajira hasa ufugaji, na kilimo biashara naangalia ipi nzuri zama hz sio za kujikita kwenye mangi shop au niuze nguo ndani ya vioo!! Hapana ntajikita kutafuta biznez idea nzuri na ambayo ntaifanya ili kupata circulation hata ndogo per day

Nikiwa sawa na retire early 50's uhuru ninao saa kumi kamili nipo nje saa moja kamili tusha sign in......
 
Nchi zilizoendelea raia wake hawana shida ya kuajiriwa. Ukionekana umeajiriwa basi wewe huna akili za kujiajiri. Inabidi serikali au kampuni binafsi iweke dau kubwa la mshahara ili ipate wafanyakazi. Utampata wapi mfanyakazi kindezi wakati kila mtu ana shughuli yake inayomuingizia hela nyingi na kumpa maisha mazuri? Huku madongokuinama raia hawana elimu ya kutosha kuendesha maisha yao, wana njaa kali hawana hela, wanategemea kuajiriwa na kufanya vibarua, umasikini mtupu umewajaa. Wanaona ukombozi wao uko kwenye kuajiriwa tu ndio watapata hela huko
 
Mkuu, wazo lako la kuacha kazi na kujiajiri ni bonge la wazo, usirudi nyuma.

Me nlichukua maamuzi mwaka jana December nikapiga kazi chini, nikajiajiri. Kwa sasa nipo kwenye biashara ya vifaa vya ujenzi, na tayari nina miezi saba tangu niingie rasmi kwenye kujiajiri.

Sina uzoefu mkubwa wa kuweza kuelezea biashara, ila nitakuambia kitu kimoja tu: kila kitu kinawezekana. Imagine, sehemu ninapoishi sasa hivi nalipa kodi kwa kutegemea hii hii biashara yangu, na pia nafanya saving kwa maandalizi ya kodi ya mwakani January. Hii ni ishara ya mwanzo mzuri na inatia moyo kwa kuonyesha kuwa kila kitu kinawezekana.

Kitu pekee ambacho nimekipata, na kwa kiasi fulani kilinitesa mwanzoni ila sasa nimekizoea, ni kuamka mapema kila siku ili saa mbili kamili niwe dukani, halafu nafunga saa moja usiku. Mwanzoni nilikuwa nachoka sana, ila sasa nimezoea.

Kwa kuongezea tu, me nafungua duka hadi Jumapili. Yaani nikitoka church moja kwa moja naenda dukani. Kwa hiyo naweza kusema nimepata uhuru ambao kwenye ajira niliukosa, ila nashindwa kuufurahia huo uhuru kwa sababu biashara yangu inahitaji muda wangu zaidi.

Kazi kwako, mkuu.
 
Nchi zilizoendelea raia wake hawana shida ya kuajiriwa. Ukionekana umeajiriwa basi wewe huna akili za kujiajiri. Inabidi serikali au kampuni binafsi iweke dau kubwa la mshahara ili ipate wafanyakazi. Utampata wapi mfanyakazi kindezi wakati kila mtu ana shughuli yake inayomuingizia hela nyingi na kumpa maisha mazuri? Huku madongokuinama raia hawana elimu ya kutosha kuendesha maisha yao, wana njaa kali hawana hela, wanategemea kuajiriwa na kufanya vibarua, umasikini mtupu umewajaa. Wanaona ukombozi wao uko kwenye kuajiriwa tu ndio watapata hela huko
Huu ni uongo kama ule wa wanaaiasa.
 
Mkuu, wazo lako la kuacha kazi na kujiajiri ni bonge la wazo, usirudi nyuma.

Me nlichukua maamuzi mwaka jana December nikapiga kazi chini, nikajiajiri. Kwa sasa nipo kwenye biashara ya vifaa vya ujenzi, na tayari nina miezi saba tangu niingie rasmi kwenye kujiajiri.

Sina uzoefu mkubwa wa kuweza kuelezea biashara, ila nitakuambia kitu kimoja tu: kila kitu kinawezekana. Imagine, sehemu ninapoishi sasa hivi nalipa kodi kwa kutegemea hii hii biashara yangu, na pia nafanya saving kwa maandalizi ya kodi ya mwakani January. Hii ni ishara ya mwanzo mzuri na inatia moyo kwa kuonyesha kuwa kila kitu kinawezekana.

Kitu pekee ambacho nimekipata, na kwa kiasi fulani kilinitesa mwanzoni ila sasa nimekizoea, ni kuamka mapema kila siku ili saa mbili kamili niwe dukani, halafu nafunga saa moja usiku. Mwanzoni nilikuwa nachoka sana, ila sasa nimezoea.

Kwa kuongezea tu, me nafungua duka hadi Jumapili. Yaani nikitoka church moja kwa moja naenda dukani. Kwa hiyo naweza kusema nimepata uhuru ambao kwenye ajira niliukosa, ila nashindwa kuufurahia huo uhuru kwa sababu biashara yangu inahitaji muda wangu zaidi.

Kazi kwako, mkuu.
Kama bado matumizi yako ya kila siku unategemea hiyo hiyo biashara ,kwa nini usingeendelea kupiga kazi na ukafungua hilo duka la vifaa vya ujenzi ukaweka utaratibu na kanuni , halafu ukaajiri mtu hapo?
 
Kama bado matumizi yako ya kila siku unategemea hiyo hiyo biashara ,kwa nini usingeendelea kupiga kazi na ukafungua hilo duka la vifaa vya ujenzi ukaweka utaratibu na kanuni , halafu ukaajiri mtu hapo?
Hii ni non sense idea, utaajiri vp mtu kwenye biashara ambayo huna experience nayo, au unatak kuibiwa mkuu 🤔
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom