Kesi ya Mbowe na wenzake inaanika hadi 'mambo ya siri za nchi'. DPP hujachelewa kuifuta

Nimekuwa nikifuatilia kwa ukaribu mkubwa mwenendo wa kesi ya ugaidi inayomkabili Mwenyekiti wa CHADEMA Freeman Mbowe na wenzake watatu. Nafuatilia kwa kwenda mwenyewe Mahakamani. Hata sasa nipo Viunga vya Law School of Tanzania ilipo Mahakama Kuu Divisheni ya Uhujumu Uchumi kwa ajili ya kuhudhuria kesi ya akina Mbowe. Sitaki kupitwa wala kusimuliwa. Najionea na kusikia mwenyewe moja kwa moja.

Yanayozungumzwa Mahakamani hapa yanashtua, yanaogofya na kuanika hata visivyofaa kuanikwa. Wengi wanaofuatilia wanajua kuwa kesi hiyo sasa imezaa kesi ndogo. Kesi ndogo ni imezaliwa baada ya Maelezo ya Mshtakiwa wa pili (Adamoo) kupingwa na upande wa Utetezi Mahakamani hapa. Ndipo Jaji Siyani anayeisikiliza kesi kuu alipotoa amri ya kuendeshwa kesi ndogo ndani ya kesi kuu kuhusu pingamizi hilo.

Mwisho wa kesi ndogo inayoendelea kutolewa ushahidi sasa ni kukubaliwa au kukataliwa kupokelewa kwa maelezo ya Adamoo yanayodaiwa aliyatoa huko Polisi alipokamatwa na kuhojiwa/kuchukuliwa maelezo. Yeye mwenyewe Adamoo kwenye ushahidi wake ameyakana Maelezo hayo akisema aliletewa yakiwa yameshaandikwa na kusainishwa chini ya vitisho vikubwa vya polisi (ACP Kingai). Jana shahidi wa pili (Bwana Ling'wenya) alianza kutoa ushahidi wake na anaendelea leo hii.

Kuna mambo yameshasemwa hapa Mahakamani na mashahidi wa Utetezi yanaogofya sana. Kwanza, kuna idadi kubwa ya wanajeshi wamekamatwa na wanateswa kwenye vituo vya polisi. Kuna nini na kumetokea nini jeshini huko hadi kufikia hapo? Pili, aliyetajwa na ACP Kingai kama mtoa taarifa za uhalifu wa Mbowe na wenzake (Luteni Urio) naye alishakamatwa na kuteswa na polisi. Je, aliteswa ili 'amchome' Mbowe na wenzake?

Kuna jambo linaogofya zaidi. Ushahidi wa kwamba wanajeshi wanakamatwa na kuteswa na polisi waweza kupika chuki na hasira kwenye mioyo ya wawili hao na kuzua suitafahamu ambayo itashindikana hata kusemeka huko mbeleni. Yaani, kunaweza kukachemka 'bifu' kati ya wapambanaji hao. Ikifika hapo, hali itakuwa tete. DPP, hujachelewa kuzuia kuvuja zaidi mambo ya ndani kuliko maini ya nchi na kuzuia taharuki isiyo na hata mkuki.

Buriani Ole Nasha!

Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam


Je Askari waliotumikia nchi tena vitani kwa level ya komandooo wakiondolewa kazini kuna kosa kujitafutia kipato halali ? Mbona Lugumi naye alichukua wa aina hiyo walioko mitaani wakawa walinzi wake ? au wanataka wakawe walinzi wajummbani au walinde ATM ? au wanataka wakaajiriwe na waasi huko DRC na nchi zingine maana ajira ziko nje nje ….
Kama Rais Samia alivyosema ; Tutende haki ili Mungu asituadhibu….
Kama hii kesi haingeenda mahakamani tungejua vipi kuwa Komando huyu haonekani kama ilivyo kwa Komando Ramadhani Kadego ( na pengine wameuliwa
Serikali ya JPM imetuachia makovu sana na kimsingi tunahitaji mambo mengi zaidi kama haya yawe wazi ili tuweze kufanya marekebisho makubwa
Mfano leo hiii wanajeshi wanawafikiria vipi Polisi ?
 
wenye akili zao hawewezi kuamini maneno ya uongo ya Ligwenya/ Adamoo, huyo ni mtuhumiwa wa Ugaidi anaye daiwa kumtumikia mtuhumiwa Mbowe.
kama walidhani wanaweza kupoteza amani yetu ya Tz basi wajue amani ya Tz lazima ilindwe kwa gharama yoyote ile.
HAKIKA wewe ni mkuundugu yangu
 
Nyerere ndie alieweka misingi mibovu ya taifa ili!! Nyerere alishindwa kuweka misingi imara ya nchi,yeye na wenzake waliongoza nchi hii kwa misingi binafsi na ukatili wa hali ya juu sana.

Ndio maana kila mtawala anaefata anaongoza kwa utashi wake na sio kwa misingi ya katiba,maana system inayotumika ni ile ile ya Nyerere aliyorithi kutoka kwa wakoloni,mbinu wanazotumia ni zile zile walizo tumia wakoloni na Nyerere, kutesa,kuua, kubambika kesi, kuhujumu wapinzani wake mbinu ni zile zile tu.

Mwinyi kidogo alikuwa mcha Mungu ndio maana akutesa watu ila system ilimlazimu kupitisha wananchi jehanamu,waliofuata wote kuanzia kwa Mkapa,Kikwete,Magufuli wamedhulumu sana uhai wa watu wengi sana mpaka sasa, kwa utawala wa uyu mama dhuluma ya uhai na mateso inaendelea ni kawaida approach inayotumika ni ile ile ya Nyerere, kutesa na kuua hakuna utu.

Nyerere alivyoona hana nguvu tena ndio akajigeuza malaika na kuanza kuhubiri demokrasia ambayo yeye hakuitenda hata robo na wala hakuwahi kuiamini katika utawala wake,Mungu ampumzishe uko aliko kushindwa kwake kujenga misingi mizuri ya taifa ili ndio kunatughalimu mpaka leo.
 
Acheni uoga mmezidi kutishia uhai viongozi wa nchi. Huyu au yule akifanya hivi mnamtishia kifo. Saiv mmetulizwa kimyaaaaa sijaona tena vitisho kwa ndungai wala mama Samia. MLIZIDI MKOME
Utakuwa una mpasuko kwenye ubongo,au ubongo wako umejaa maji,yaani watu wasiokuwa na madaraka yeyote wamtishie Rais wa nchi hii kifo?! Are you serious? Rais ambae ni amiri jeshi mkuu wa majeshi ya ulinzi na usalama,atishiwe uhai wake na mkulima mmoja? Utakuwa umeandika kufurahisha genge tu nafikili
 
Povu lote pumba tupu.
Utakuwa una mpasuko kwenye ubongo,au ubongo wako umejaa maji,yaani watu wasiokuwa na madaraka yeyote wamtishie Rais wa nchi hii kifo?! Are you serious? Rais ambae ni amiri jeshi mkuu wa majeshi ya ulinzi na usalama,atishiwe uhai wake na mkulima mmoja? Utakuwa umeandika kufurahisha genge tu nafikili
 
Tunaomba kuonyeshwa japo mabaki ya MOSES LIJENJE sisi kama ndugu zake tukazike!!
 
Yaan unataka kesi ifutwe?Inaonekana ,unataka tusiyajue mengi.
Kesi ya Mbowe ni mpango wa Mungu ili kufunua yote yaliyofunikwa. Kwa mfano mpaka kesi iishe tutakuwa tumejua idadi kubwa ya vikundi vya wale wanaoitwa "WASIOJULIKANA!" ambao hata Polisi wanasema hawawajui. Tumeanza kujua nani wanakamata watu, kuwaficha, na kuwaua!
 
Nawaza kimya kimya makomando wa jeshi waliofukuzwa kazi wanapoajiliwa na kiongozi mkuu wa upinzani siri za serikali zinakuwa salama? hatuna haja ya kujiuliza akina kigogo wanapata wapi taarifa
 
nawaza kimya kimya makomando wa jeshi waliofukuzwa kazi wanapoajiliwa na kiongozi mkuu wa upinzani siri za serikali zinakuwa salama? hatuna haja ya kujiuliza akina kigogo wanapata wapi taarifa
Kwani kiongozi wa upinzani ni Raia wa nje ya nchi?? au mwanajeshi anatumikia v
ccm??

Utopolo fc
 
nakumbuka miaka ile watu wananyonywa damu na kuchunwa ngozi.
miili iliokotwa na wahanga hawakulipwa chochote hakuna aliefuatilia.

kuna wakati wakajichanga wakamnyonya damu mtoto wa kuu mmoja wa kikosi fulani cha jwtz.

alichokifanya mkuu yule kwenye eneo lile.nafikili ndio ikawa mwisho wa watu kunyonywa damu.

wakabadili mbinu na kutaka watu wajitolee.

na hawa hivyohivyo.kunasiku atafanyiwa ubaya mtoto wa levo zoa, ndio patachimbika.
Kule uganda mtoto wa waziri wa ulinzi aliuliwa kwa risasi baada ya uchafuzi mwaka huu
 
nawaza kimya kimya makomando wa jeshi waliofukuzwa kazi wanapoajiliwa na kiongozi mkuu wa upinzani siri za serikali zinakuwa salama? hatuna haja ya kujiuliza akina kigogo wanapata wapi taarifa
Kwa taarifa yako DW iliwahi kutangaza kuna waliokuwa wanajeshi wa Tanzania wameajiriwa Congo na waasi na wezi wa madini,wewe unaongelea kiongozi wa upinzani ambaye anaweza kuwa rais ajaye.
Tatizo hawaandaliwi vizuri wafanye nini utumishi wao jeshini ukikoma,kwani wengi wao wanjua kupigana tuu.
 
Mpaka sasa tunasema Too late!
Nimekuwa nikifuatilia kwa ukaribu mkubwa mwenendo wa kesi ya ugaidi inayomkabili Mwenyekiti wa CHADEMA Freeman Mbowe na wenzake watatu. Nafuatilia kwa kwenda mwenyewe Mahakamani. Hata sasa nipo Viunga vya Law School of Tanzania ilipo Mahakama Kuu Divisheni ya Uhujumu Uchumi kwa ajili ya kuhudhuria kesi ya akina Mbowe. Sitaki kupitwa wala kusimuliwa. Najionea na kusikia mwenyewe moja kwa moja.

Yana

Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam
 
Mungu ni mwema sana damu za watu itakua nyingi zimemwagika tena watumishi waliolitumikia Taifa lazima karma iwaumbue kweli karma inafanya kazi watoa kesi ndio wanaomba kesi ifutwe tena haina maana wanaumbuka...
Ifutwe wakati kuna maelezo ya mto kutoweka?
 
Kwenye hili suala la kuwepo wanajeshi vituo vya polisi hata mimi limenistua,na huyo shahidi anasema hao wenzie nao walikamatwa kwa kesi hizo hizo za ugaidi,kulitokea nini huko jeshini?!

Yule shahidi anasema aliona Luteni Urio akiteswa na wanajeshi wa special forces(aliokuwa nao kambi moja so anawajua) pamoja na polisi kwenye magari mabovu pale Tazara police.
Na mimi nimeamini kabisa ushahidi huu maana sidhani kama wanajeshi wangeweza kukamatwa na kushughulikiwa bila kuhusisha wajeda wenzao.Sasa nini kilitokea huko jeshini?
Kuna nini pia kwa wanaostaafu huko jeshini?

Pili,ni kwanini kesi hii imeachwa wazi hivi huku inaonekana kama inakwenda kureveal vitu vizito dhidi ya serikali ambavyo si busara kuviweka hadharani?
Naamini kabisa tiss wangetaka iwe kimya kimya wasingeshindwa kwa mvua kwa jua na hii kesi isingekuwepo kabisa in the first place,lazima ingefutwa kama ni Mbowe na Chadema wangetafuta namna nyingine ya kudeal nao.

Hii kesi naishangaa sana.
Kuna smokescreen gani hapa?!
🤔
 
Kwenye hili suala la kuwepo wanajeshi vituo vya polisi hata mimi limenistua,na huyo shahidi anasema hao wenzie nao walikamatwa kwa kesi hizo hizo za ugaidi,kulitokea nini huko jeshini?!

Yule shahidi anasema aliona Luteni Urio akiteswa na wanajeshi wa special forces(aliokuwa nao kambi moja so anawajua) pamoja na polisi kwenye magari mabovu pale Tazara police.
Na mimi nimeamini kabisa ushahidi huu maana sidhani kama wanajeshi wangeweza kukamatwa na kushughulikiwa bila kuhusisha wajeda wenzao.Sasa nini kilitokea huko jeshini?
Kuna nini pia kwa wanaostaafu huko jeshini?

Pili,ni kwanini kesi hii imeachwa wazi hivi huku inaonekana kama inakwenda kureveal vitu vizito dhidi ya serikali ambavyo si busara kuviweka hadharani?
Naamini kabisa tiss wangetaka iwe kimya kimya wasingeshindwa kwa mvua kwa jua na hii kesi isingekuwepo kabisa in the first place,lazima ingefutwa kama ni Mbowe na Chadema wangetafuta namna nyingine ya kudeal nao.

Hii kesi naishangaa sana.
Kuna smokescreen gani hapa?!
Watengeneza kesi hawakutafakari kabla walikurupuka kutengeneza kesi tu huko moses lijenje akifa kwa mateso baada ya kuamua kuwa kimya kwa kuwambia kuwa hajui ugaidi wowote kwani yeye na Lt Urio walimpa mbowe Asikari wasitaafu kwa nia ya kuwapa ajila mpya tu wapate ridhiki, hawakujua chochote zaidi ya hayo, kitendo cha kutuma MP na Asikari kwenda kuwatesa kuwalazimisha waseme ugaidi hewa, ugaidi ambao hawana haupo kilikuwa kitendo cha kinyama ni kinyume cha haki za binadamu, ikumbukwe kuwa kesi ya mbowe ilisukwa na magufuli kwa lengo la kuidhoofisha chadema lakini washauri wa magufuli kipindi kile akina Sabaya ndiyo wakabuni mbinu za hovyo za kuwabambikia kesi za ugaidi huku mahita kingai wakipiga sana kuwafunga pingu mikono miguu saa 24 ni unyama ulioje, hawakutarajia siri kuvuja mahakamani ampapo sasa vichwa vinawauma kwa uonevu waliotenda dhidi ya mbowe na walinzi wake
 
Back
Top Bottom