Juu ya OIC na Mahakama ya Kadhi

Juu ya OIC na Mahakama ya Kadhi

Utangulizi:

KWANZA, natoa shukrani za wazi kwa Sheikh Ido Mohammed Iddi wa Msikiti wa Mnyamani kwa kuwa mstari wa mbele kuzungumzia haki ya Waislamu kuwa na Mahakama yao ya Kadhi kama ilivyo Zanzibar, Kenya na sehemu nyingine Afrika. Yeye na viongozi wengine wa Kiislamu tunaomba wasikate tamaa maana ushindi ni wa Allah -Subuhana wa taalaa na sio viumbe hapa duniani.

FAIDA ZA MAHAKAMA YA KADHI
Baada ya kusema hayo, leo napenda kuanza kwa kuzungumzia faida za kuwa na Mahakama ya Kadhi na hasara zitakazotokana na kutokuwepo kwa Mahakama ya Kadhi-kama ilivyo kuwa huko nyuma, ilivyo sasa na baya zaidi hali itakavyokuwa huko mbele.

Faida za mahakama ya Kadhi pamoja na mengineyo zaweza kugawanya katika makundi matatu makubwa: Faida katika kutafuta ufumbuzi wa matatizo wa kudumu na usiobeba dhambi mbele ya Mungu hususan, kuhusu kifamilia na maisha ya kila siku ya Muislamu; faida zitakazotkana na kutatua matatizo ya maingiliano ya kiuchumi na kijamii kwa Waislamu; na faida zitakazopatikana kutokana na kutatua matatizo ya Uongozi, Usimamizi na Uadilifu miongoni mwa viongozi wa misikiti na taasisi mbalimbali za Kiislamu.


Matatizo ndani ya familia na jamii za Kiislamu:


Kundi hili la kwanza la hoja ni kuhusiana na maisha ya kila siku. Hapa tunaonesha madhambi Waislamu wanayolazimishwa kuyabeba kwa sababu ya kukosekana mahakama ya Kadhi:
  1. . Hukumu za ndoa kufanyika kwa mujibu wa sheria za Kiislamu na Kitabu cha Mwenyezi Mungu-Al-Furqhan.
  2. . Talaka hazitatolewa tena nje ya kile kilichoamrishwa na Mwenyezi Mungu na mahakimu ambao wakati mwingine si Waislamu.
  3. . Ujanja unaofanywa na watu kurithi pale wasipostahili kurithi utafichuliwa na watakaomrithi mtu kwa kiasi kikubwa watakuwa ni wale tu wanaostahili haki hiyo.
  4. . Familia zinazotekelezwa zitatunzwa na mifuko maalum itakayopatikana kutokana na zaka na sadaka za Waislamu ambayo baadhi yake itapewa ofisi hiyo ya Kadhi.
  5. . Mayatima watalindwa hasa pale wanapokuwa wadogo lakini wazazi wao wameacha mali mbalimbali ambazo zitakuja wafaa ukubwani.
  6. . Wazee wengi wa Kiislamu, hasa katika mikoa ya Pwani na kwingineko, ambao kwa sasa wanaishi kwa dhiki na ukata mkubwa wataangaliwa kwa namna moja au nyingine na mahakama hiyo na hivyo kuondoa uwezekano wa watu wa dini nyingine kuwaritadisha watu hao uzeeni kutokana na ufukara wao na kukosa taasisi ya kitaifa inayowajali na kuwatunza wazee
Matatizo ya mahusiano ya kiuchumi na kijamii
  1. . Masuala ya elimu na taasisi za elimu za Kiislamu yatapata ofisi moja au mbili za kuyasimamia na hivyo kupunguza udhaifu na uendeshaji mbaya uliopo hivi sasa.
  2. . Aidha taasisi za tiba za Kiislamu zitakuwa chini ya macho makali ya idara za ofisi ya Kadhi ili kuona haki inatendeka kwa kutolewa huduma muhimu kwa gharama zinazokubalika ndani ya wakati tuliomo.
  3. . Masuala ya kibenki na taasisi za fedha yataangaliwa ili yaendane na kutowaingiza Waislamu katika dhambi wasiyoiona au kuijua.
  4. . Kadhalika shughuli za huduma mbalimbali na biashara zitasimamiwa ili zikidhi haja ya wateja Waislamu na wasio Waislamu na vilevile kuhakikisha kuwa biashara zote zinakuwa za halali kwa upande wa Waislamu na zinazofanyika kwa njia ya halali bila kuwapunja, kudhulumu au kuwanyonya wateja.
  5. . Masuala ya uwekezaji na mitaji ambayo sasa yanafuata utaratibu unaoendana zaidi na dini nyingine yatapata usimamizi wa kuhakikisha kuwa sasa yanaendana na maagizo ya Mwenyezi Mungu.
  6. . Juu ya yote maingiliano na wasio waislamu yataratibiwa ipasavyo na kuhakikisha Waislamu wanawatendea haki watu wengine na wao pia wanatendewa haki na watu wengine ikiwemo watawala na viongozi wa dini nyingine.
  7. . Mahakama ya Kadhi itatoa mchango mkubwa katika kutenganisha masuala ya dini na kisiasa na hasa misikitini jambo ambalo sasa limekosa mtu wa kudhibiti.
  8. . Mahakama ya Kadhi itachambua Taassisi za Kiislamu zilizopo ili kuzifuma upya ziondokane na viongozi wabovu na waovu ili Waislamu warejeshe imani kwa viongozi wao pamoja na umoja na mshikamano ndani ya taasisi hizo zinazoyumba kwa sasa kutokana na kuvamiwa na siasa na wanasiasa.
  9. . Kuchochea imani, uzuzi na ubunifu miongoni mwa Waislamu ili waweze kuwaamini viongozi wao kwani kila kitu sasa kitakuwa wazi chini ya Ofisi ya Kadhi na hivyo kuwezesha Waislamu kutunisha mifuko yao mbalimbali na kuacha kabisa kwa taasisi za Kiislamu kutegemea serikali au wanasiasa na ruzuku katika kuendesha mambo yao.

Matatizo ya taasisi, uongozi, na viongozi wa Kiislamu
  1. . Ofisi yaKadhi pia itakuwa mstari wa mbele katika kulinda mali za Waislamu. Tofauti na ilivyo sasa ambapo baadhi ya Waislamu na wasio waislamu wanaweza wakauza au kununua mali za Wakfu za Waislamu na kulindwa na sheria isiyo ya Kiislamu kutokana na udhaifu wa kutokuwa na Mahakama ya Kadhi ambayo ingelikuwa ina hakiki mali zote za Waislamu na kuwekea mikataba lakiri isiyoweza kubadilishwa ila kwa amri ya Mahakama hiyo tu.
  2. . Baadhi ya taasisi, wilaya, mikoa hadi ngazi ya Taifa zina viongozi wabovu ambao wanalindwa na wanasiasa na mahakama zilizopo. Endapo mahakama ya Kadhi itakuwapo basi itawashughulikia viongozi wabovu na waovu kwa namna inayochunga mambo ya Waislamu yasikwame.
  3. . Inasemekana kwamba mali bila daftari hupotea bila habari. Misikiti na taasisi nyingi za Kiislamu karibu katika ngazi zote zina matumizi mabaya sana ya fedha na hakuna wa kuwawajibisha kutokana na kutokuwepo na Mahakama ya Kdhi ambayo ingelikomisheni wataalamu wa mambo ya fedha wa Kiislamu kubuni na kuanzisha mfumo wa uhasibu kwa ajili ya misikiti na taasisi hizo utakaopaswa kufuatwa na wote na vilevile kuwa na wakakguzi wa shughuli za dini na za kibiashara kwa Waislamu ili kuona hakuna wajanja wanofanya vitu vyao ndani ya taasisi hizo wakati wote. Kiujumla Ofisi ya Kadhi itawezesha Waislamu kuweka taratibu za uhasibuna utunzaji madaftari na utunzaji kumbukumbu za fedha au mali, mapato na matumizi miongoni mwa misikiti na taasisi nyingine za Kiislamu.
  4. . Ofisi hiyo ya Kadhi itakuwa pia na majukumu ya kuwasimamia wakaguzi maalum wa Kiislamu kukagua mali za waislamu kwa mujibu wa sheria za Kiislamu na kuwachukulia hatua wanaokiuka taratibu na miiko iliyowekwa tofauti na ilivyo hivi sasa.
  5. . Ofisi ya Kadhi itakuwa na mchango mkubwa pia katika kusaidia kusimamia makadirio na utozaji wa zaka tofauti na ilivyo sasa ambapo kutokana na kutokuwa na Ofisi ya Kadhi Waislamu ndio walio wengi katika lindi la umasikini kwa sababu umekosekana mfumo unaokubalika wa kukusanya zaka na kuwaondoa Waislamu waliomo katika umasikini kutoka kwenye lindi la ufukara unaowatia katika ukafiri kirahisi mno,
Hasara za Waislamu kunyimwa haki yao ya msingi ya kuwa na Kadhi:
  1. . Kesi za ndoa kuhukumiwa ndivyo isivyo (yaani nje ya Kitabu cha Allah).
  2. . Masuala ya talaka kuamuliwa kinyume cha sheria za Kiislamu.
  3. . Wenye kustahili mirathi kunyimwa au kupunja na wasiostahili mirathi kupewa urithi usio halali.
  4. . Familia, yaani, mke na watoto wanaotekelezwa kucheleweshewa haki yao kutokana na mlolongo wa mashtaka kama haya mahakama za kawaida. Ugumu mkubwa katika kutambua kama waliotekelezwa kweli ni nasaba kwa mme au ni watu wa kupachikiwa.
  5. . Mayatima wa Kiislamu kulelewa na wasio Waislamu na hivyo kuwa katika hatari ya kupoteza au kupotoshewa imani yao.
  6. . Wazee wengi wa Kiislamu kuendelea kuteseka uzeeni kutokana na kukosekana kwa huduma nzuri na ya uhakika kwa watu kama wao katika jamii.
Aidha, haya pia yataendelea kuwasibu Waislamu tofauti na wenzao wa dini nyingine ambao dini zao zina mifumo ndani kwa ndani inayoshughulikia masuala kama haya lakini wao Waislamu hawana:

  1. . Elimu na taasisi nyingine za Kiislamu kuendelewa kuendeshwa ovyo ovyo kwa sababu hakuna mlezi wa taasisi hizo ambaye hawezi kuwa mwingine ila Muislamu muadilifu na mcha-Mungu ambaye ni kadhi na bingwa wa sheria na hukumu za Kiislamu kuhusu masuala husika.
  2. . Huduma za tiba kwa Waislamu zimekuwa zikibadilika lakini nazo zinakabiliwa na matatizo ya menejimenti, kiutawala, kiuendeshaji, kifedha na kimaendeleo kwa kukosa msimamizi mkuu kama Kadhi na Ofisi yake.
  3. . Katika miaka hii ambapo Waislamu wamefunguka macho kuhusu dhambi ya RIBA ni muhimu Waislamu kuwa na Kadhi ambaye kwa mashirikiano na Maulama wa ndani na nje wanaweza kupitishwa fatwa mbalimbali kuhusu masuala ya kibenki na kifedha. Kukosekana kwa mahakama ya Kadhi kunachangia kwa kiasi kikubwa Waislamu wengi kula kuchwao kuingia kwenye dhambi ya KULA AU KULISHA wengine RIBA.
  4. . Kutokana na kutoijua DINI yao vyema maelfu ya Waislamu sasa hivi wamejiingiza katika uwekezaji na mitaji haramu. Haya yote yamesababishwa na kukosekana kwa Mahakama ya Kadhi ambayo ingelibainisha kinaugaubaga ni uwekezaji na mitaji ipi ni halali na ipi ni haramu kwa Waislamu.
  5. . Kwa ujumla Mahakama ya Kadhi ambayo inapingwa na Wakatoliki ni chombo cha kuhakikisha kuwa mahusiano kati ya waumini wa dini hizi mbili yanafanywa bora zaidi na hapaachiwi mianya ya vikundi vidogo vidogo ndani ya dini zetu inayoweza kutumika kuvunja umoja na amani wa nchi hii.

Tofauti na baadhi ya watu wanavyoamini Mahakama ya Kadhi haitaingilia :
  • . kesi zinazowahusu wasio Waislamu.
  • . haitahukumu nje ya Sheria za Kiislamu ambazo zinakubalika katika jamii ya kisekula ya leo.
  • . Haitokata watu mikono wala kupiga watu mawe.
  • . Haitashughulika na masuala ya watu wa dini zingine haya yataachiwa mahakama za kisekula.
  • . Badala ya kuorojesha amani na mshikamano kati ya Watanzania itasaidia sana kuhakikisha kuwepo kwa umoja na amani ya kudumu inayojengwa juu ya misingi ya haki na usawa.
  • . Haitotumia fedha za seikali isipokuwa kwa kiwango kile kile ya mizigo ya kesi itakayopunguziwa mahakama za kisekula.
Hitimisho:
Ni hitimishe kwa kusema kwamba, Kuwepo kwa mahakama ya Kadhi hautokuwa ushindi wa upande mmoja, kwamba hawa wameshindwa na wale wameshinda. La, hasha! Ushindi huu ni ushindi kwa wote, Kwa Waislamu, kwa Watu wa dini nyingine, kwa wasiojua wanachokipinga na kwa Watanzania wote kwa ujumla. Kuwepo kwa Mahakama ya Kadhi ni kuwepo kwa figa la tatu kwa Jamhuri ya Muungano ambayo hadi wa leo imekuwa ikisimamia juu ya mafiga mawili- figa na Kanisa Katoliki na ubalozi wa Vatican nchini na lile la Serikali ya Kisekula peke yake na kulisahau figa la tatu-Mahakama ya Kiislamu.

Yeyote atakayeikataa Mahakama ya Kadhi haitakii mema Tanzania na hawatakii mema Watanzania. Mungu Mkubwa na hana mpinzani! Mungu Ibariki Tanzania, na pia Wabariki watu wote wanaokuabudu wewe tu!

Sheikh,

Kwanza karibu jamvini, jisikie uko nyumbani.

La pili ambalo naomba niliongelee baada yakuona ufafanuzi wako ni kuwa kuna mkoroganyo wa kuelewa ni kwa nini kunahitajika kuwa na mahakama ya Kadhi.

Kutokana na maelezo yako ya kina, mahakama hii haitaishia kusimamia masuala ya ndoa na mirathi pekee, bali ni Serikali kamili ambayo itakuwa inashughulikia maslahi ya Waislamu pekee.

Sasa ninachojiuliza kutokana na maelezo yako hasa unaposema dini nyingine zinavyofanya mambo, je ni kwa nini mambo ya kijamii na kiroho yawe chini ya mahakama ya kisheria na si Baraza au Taasisi kuu ya Kiislamu?

Nafahamu kuna mgawanyiko mkubwa sana kuhusu Bakwata na kutofautiana kwa ideology ama kutokana na mapokeo tofauti ya Quran au Ubinadamu na upeo wa kupambanua mambo. Sasa kwa nini basi kusifanyike kwanza upatanishi na kuundwa kwa Taasisi kuu ya Waislamu wa madhehebu yote na kuweka sheria na kanuni za kujiongoza kabla ya kukimbilia kusema tunataka mahakama?

Ikiwa kwenye hii mahakama ya Kadhi ambao watakuwa mahakimu na wenye kuamua mashauri watakuwa ni watu ambao wako kwenye upande mwingine wa Shilingi na kushindwa kutoa haki ya kweli kutokana na mapokeo yao ya imani na ubinadamu, huoni kuwa tatizo la kusema kuwa Bakwata ni batili au si kamilifu litahamia kwenye mahakama ya Kadhi?

Umezungumzia maslahi ya Waislamu kwa mambo ya elimu, yatima na wazee kwa kuyaoanisha kana kwamba ni mabovu kwa waislamu pekee. Je shule na elimu ya Kiislamu unayozungumzia ni ya kufundishia Dini na Imani ya Uislamu au elimu dunia (msingi, Sekondari hata chuo)? Je Yatima na wazee ambao unadai wanatelekezwa na Serikali (au dini kama ulivyoonyesha) ni tatizo la Waislamu pekee au ni la Taifa zima?

Ninachopinga ni kule kutaka shughuli za jamii ambazo zinaweza kufanywa kwa kutumia Jumuia na Taasisi binafsi au za Kidini kugeuzwa na kushurtishwa kuundiwa vyombo maalumu vya kidini ndani ya Serikali.

Nitakupa mfano, Catholic Charities na Lutheran Welfare Services, zimejisajili kama taasisi binafsi kutokana na madhehebu yao. Zimeunda shule za kidini (mafundishi ya dini pekee) na shule za kawaida, zina zahanati na huduma za jamii kusaidia yatima, walemavu, wazee, ombaomba na wengine wengi bila kuhoji dini ya yule anayekuja omba msaada.

Sasa kwa nini Jumuiya ya Waislamu isiwe na vyombo kama hivi ambavyo si vya Kiserikali au kutegemea uendeshaji wake kupitia Serikali?

Hata kwenye suala la ndoa na mirathi, ikiwa mtu hatakubaliana na maamuzi ya mahakama ya Kadhi, kutokana na mapokeo na tafsiri yake ya Quran, je mtu huyu atakuwa na haki kwenda kwenye mahakama ya Serikali kutaka shauri lake litatuliwe?

Sababu ya kuyasema haya ni kutokana na kuingiliana kwa tamaduni zetu asilia na dini zetu tulizozipokea, Ukristo na Uislamu. Na hata katika dini hizi, tunapokea mafundisho kwa tafsiri mbali mbali kiasi kwamba hakuna absolute definition au understanding kutokana na mapokeo yetu kama binadamu ambayo yanajengwa na tabia na mazingira.

Leo hii mfano, Wakristo hatuwezi kusema tunataka mahakama ya Kikristo huku mapekeo yetu na uendeshaji wa jamii zetu za Kikristo zina tofauti, Maprotestanti na Wakatoliki wakiwa na mapokeo tofauti na mifumo tofauti ya ibada na uendeshaji kwa kutumia dini hiyo hiyo moja.

Mfano, kwa Wakatoliki, viongozi wake wa kidini wanakatazwa kuoa. Lakini hakuna mahali popote katika Biblia iliposema kuwa viongozi wa Kanisa ni mwiko kuoa. Sasa kama Padiri akitaka kuoa, shurti aachane na Upadiri, hawezi kuenda mahakama kuu na kusema aendelee kuwa Padiri na hapo hapo awe ameoa.

Same mechanism nahisi itakuwa ndani ya sehemu za Sharia, ambako waumini na hata viongozi wasiokubaliana na maamuzi ya kanuni, je watakimbilia mahakama ya Serikali na dola kupata haki? au itawabidi wakubali kanuni za Taasisi?

Kwa maelezo yako ya kinagaubaga, yaelekea suala la Mahakama ya Kadhi ni zaidi ya suala la kuamaua matatizo ya ndoa na mirathi pekee. Mimi binafsi nimepokea maoni yako sawa na mtu anayetaka kuwa na himaya au serikali yake ndani ya serikali, badala ya kuwa ni suala la mambo ya kiroho.

Sasa nadhani sia ajabu kuna wengi waliopokea suala hili la kutaka kurudishwa kwa mahakama ya Kadhi sawa na nilivyokupokea mimi ambavyo ni tofautu na nilivyolipokea mapema suala la kuwepo mahakama ya kadhi.

Nitakachoshauri ni kwanaza kupatikana kwa upatanishi na kufungamana kwa Jumuiya zote za Kiislamu na kuunda Taasisi moja yenye nguvu na mamlaka ambayo ndani yake basi ndiko Mahakama iundwe. Kinyume cha hayo, mvurugano ndani ya jamii hautapata ufumbuzi hata kama Mahakama ya Kadhi itaanza kazi.

Sisi ni binaadamu na tuna udhaifu wa kimwili na kiroho, kwa mtaji huo, inabidi tuwe na makubaliano ya kweli kwanza kushirikiana na kufanya mambo ambayo ni ya faida na yale yasiyofaa tuyaache. Ikiwa kutakuwa na umoja na kuondokana na tofauti ambazo zimeonekana hivi karibuni hata za kuzidiana akili na kujiuzia mali za misikiti na jumuiya, basi hata mahakama itakapokuja, haitakuwa na sura au mapokeo ambayo ni hasi.
 
The Organization of the Islamic Conference (OIC) is the second largest inter-governmental organization after the United Nations which has membership of 57 states spread over four continents. The Organization is the collective voice of the Muslim world and ensuring to safeguard and project the interests of the Muslim world in the spirit of promoting international peace and harmony among various people of the world. The Organization was established upon a decision of the historical summit which took place in Rabat, Kingdom of Morocco on 12th Rajab 1398 Hijra (25 September 1969) as a result of criminal arson of Al-Aqsa Mosque in occupied Jerusalem.

Kama walivyosema wenyewe kwenye web-site yao, OIC ni chombo kinachowaunganisha waislamu. Kipo kulinda maslahi ya waislamu. Sasa kwa nini tuone ugumu kusema hili? Watu hawapingi kwa sababu kiongozi wake ni muislamu au makao yake makuu yako kwenye nchi ya kiislamu. La hasha. Ni identity yake kama chombo cha waislamu ndiyo inayowatia uoga.

Cha kujiuliza, ni jee, kuna ubaya wa chombo cha kiislamu kutetea maslahi ya waislamu? Na je, kuna ubaya gani kwa nchi yetu yenye waislamu wengi tu, kujiunga na chombo ambacho kitaangalia na kutetea maslahi yake? Je hawa waislamu wetu wangeweza kupata uwakilishi katika chombo hicho kupitia namna nyingine? Ukweli ni kuwa, hamna, hiki chombo kinaunganisha nchi na si vinginevyo. Kama jumuia ya madola. Kama Umoja wa Mataifa. Bakwata na hata EAMWS ingekuwepo isingeweza kujiunga. Zanzibar haiwezi. Mji wa Pangani hauwezi. Ni nchi tuu ndiyo inayoweza.Kama tunawakubali hao waislamu kuwa sehemu ya jamii yetu kwa nini tukatae ku'facilitate' wao kuweza kupata neema? Tukiona kuwepo kwetu huko kuna wadhuru wasio waislamu si tutaweza kujitoa? Ni kama vile Tanzania kujiunga na FIFA wakati si raia wake wote wanaopenda au kucheza mpira! Au shirikisho la Netball wa dunia. Tatizo liko wapi? Kwa vile hakuna chombo kama hicho kwa wakristu, si sababu ya kukataa kujiunga. Kama OIC wana ajenda nyingine zaidi ya kuwasaidia wenye dini wenzao basi iwekwe wazi.
 
Jokakuu,

Tatizo sio mahakama ya kadhi hilo kwanza..
Sisi hapa JF tusitazame kwa ufinyu hiki chombo ila tutazame issue inayopiganiwa kwa kuwatazama Watu na Mazingira waliopo, kisha tujenge mapendekezo yetu kwa kuanisha sababu za kukubali ama kutokubali mahakama ya kadhi..Mahakama ya kadhi haiwezi kutoa suluhu hata kidogo isipokuwa ni kuonyesha nia ya kushughulikia tatizo lililopo..

Kwanza umesema mahakama zetu huwa zinauliza mahusika wanataka sheria gani! Hili ni kosa la kwanza kabisa kwani serikali haiwezi ama haitakiwi kuamua kesi kwa kuuliza mshitaka au mshitakiwa kwa sababu ni ktk mazingira haya hawa watu wawili huwa hawakubaliani na ndio maana wamekwenda ktk sheria. Mahakama haitakiwa kabisa kutokuwa na sheria moja kwa wananchi wake wote..

Pili, kama nilivyosem hapo awali waislaam dini yao inaruhusu wake zaidi ya mmoja ambayo kwa msahafu wa Wakristu ni polygyny.. Hata hivyo kutokana na mazingira tunayoishi Waislaam hawafuati sheria za ndoa hizi kidini zaidi wanatumia mila na desturi za kiafrika wakichanganya na dini kidogo..Wakristu pia pamoja na kwamba wake wengi ni haramu lakini mazingira yetu yanatuonyesha kwamba wao pia wanaoa nje ya sheria ya ndoa za dini.. Hivyo hivyo madhehebu mengine yote utakuta wananchi wa Tanzania wanafuata zaidi mila na desturi hivyo unapopitisha sheria ni muhimu sana ufuate sheria moja ambayo inaweza kutumika kote... kisha basi ndoa za siku hizi ni mchanganyiko waislaam kwa Wakristu na Mapagani, ibada zote za dini hizi imekuwa HIARI ya muumini kufuata ama kutofuata lakini ktk dola ni lazima kuwepo na utaratibu wa kuhakikisha sisi sote hatuendi overboard kwa kutumia mila hizi mbaya zinazodhalilisha wanawake na watoto.

Hivi sasa wanawake wengi wanaolewa ovyo kwa kuahidiwa uongo mtupu, Watoto wengi wanazaliwa nje ya ndoa za kidini na hawana haki ktk sheria za dini zote iwe waislaam ama wakristu.. Hivyo kwa sababu hili ni tatizo sugu inabidi lazima serikali itafute sheria moja kwa ajili ya tatizo hilo.

Navyoelewa mimi waislaam kwa kutaka Mahakama ya Kadhi ni kutokana na kutokuwepo sheria inayowalinda wanawake..kesi nyingi sana zimekuwa zikiamriwa kiholela tena against wanawake na watoto... Kutokana na kuwepo kwa tatizo hilo ndio maana waislaam wame raise hii issue kama vile tulivyoomba uzinduzi wa chombo na sheria inayowahukumu MAFISADI, muswada wa utunzi wa sheria hiyo lazima umeanzishwa na watu ambao wamekereka na mfumo uliopo sasa hivi na hakuna sheria moja dhidi ya Ufisadi...sasa ni ufinyu wa kifikra kama tukianza kuwatazama wale walioleta hoja ya Ufisadi kama wanatoka chama gani... kama ni Dr. Slaa basi issue nzima haina maana kwa sababu ni issue ya Dr.Slaa na Chadema ni matakwa ya Chadema kwa Chadema..tukitoa visingizio kuwa hapa Tanzania sio kila mtu ni Mwana Chadema na fisadi hivyo sheria hiyo haituhusu.

Nachosema mimi ni kwamba hata kwa hawa ndugu zetu wakristu, hutuwezi kuendelea na sheria ya dini inayokataza kuoa mke wa pili hali wafuasi wake wengi wanaoa wake zaidi ya mmoja na watoto wamezaliwa ambao hawatambuliki kulingana na sheria za dini.. Hawa watu hatuwezi kuwaaacha ati kwa sababu wamekiuka maadili ya dini laa hasha ni kitu kinachotokea na kwa kasi ya ajabu sana. naweza kusema Tanzania ya leo hakuna mtu asiyekuwa na mistress, mke zaidi ya mmoja na watoto wengi wamezaliwa nje ya ndoa ama ktk ndoa ya kiislaam ama kiasili.. hawa watu wanatakiwa haki pindi inapofikia ktk maswala ya kuvunjika kwa ndoa ama mirathi.. wanawake wengi na watoto hawa wamekuwa hawana haki mbele ya sheria ya dini ama katiba, hakuna sheria moja inayoweza kuamua kwa maslahi ya hawa waathirika... na inaonyesha kwamba we don't care!

Kwa hiyo ni lazima tutafute njia bora ya ku deal na swala hili.....kuomba mahakama ya kadhi iwe kama ni hamasisho la kuitazama upya sheria zetu na kwa nini waislaam wamejenga hoja hii..hapo itakuwa rahisi kwetu kufahamu tatizo liko wapi na litafutiwe solution.

Mkandara,

Kukiundwa mahakama ya Kadhi, bado hakutakuwa ndio suluhisho la udhaifu wa Sheria za Ndoa na Mirathi kwa jamii ya Tanzania.

Nadhani tatizo kubwa kuhusiana na Ndoa na Mirathi ni lile la mila asili ambalo umelizungumzia mara kadhaa, ya Wajomba na Shangazi, Baba Wakubwa na Wadogo, Mama Wakubwa na Wadogo na kadhalika.

Sheria za Tanzania pamoja na kuwa inawezekana kabisa zipo kumlinda mfiwa na watoto wa mfiwa, bado zina ulegevu kwa kuwa tunaruhusu tamaduni na mila asili zifanye mambo dhidi ya Sheria. Hili si tatizo la Waislamu pekee kama ulivyofafanua, nakubali ni la Taifa zima.

Mfano, inasemekana ndugu zangu wa Kihaya, mke anapofiwa na mume, anarithishwa mdogo wa marehemu. Je hili hufanywa kwa ridhaa ya huyu mke na watoto au ni kulazimishwa kwa kuwa ni jadi? Je Mwanamke huyu ana haki gani mbele ya jadi na sheria za nchi kukataa kurithishwa kwa mtu ambaye si chaguo lake?

Au kwenye mirathi, ndugu wa mume kumnyanyasa mjane na watoto kwa kutumia mila na tamaduni za kikabila na kikoo, je hili ni suala la Uislamu pekee? hapana ni suala la Taifa.

Hivyo basi, ni muhimu taasisi zetu za kidini na jumuiya kukaa chini na kuangalia ni vipi sheria na kanuni kutokana na mapokeo yao ya kidini yanaweza kuunganishwa katika sheria za nchi zitakazotoa haki sawa.

Ninachohofia tena kuhusiana na suala la mahakama ya kadhi ni hili, ikiwa aliyeshindwa kesi hakuridhika na maamuzi, je anaweza kata rufaa kwenye mahakama ya kawaida? Je ikiwa shauri la ndoa, watoto na mirathi linahusisha mume na mke ambao mmoja ni Muislamu na mwingine ni dini ingine je suala hili litatatuliwaje na Mahakama ya Kadhi?
 
Nauliza tena je tuanzishe Pettition ya Tanzania kujiunga na World Council of Churches?
 
Rev. Kishoka,
Mkuu asikudanganye mtu kuwa nchi kama marekani zinatupa misaada bila masharti... Ni lazima tujiunge na kundi fulani kulipa fadhila zao...Ni sawa na mwamake akwambie ati mzee fulani huwa anamopa hela bila kumwomba mchezo!.. comeon mkuu kuna kitu huyo mzee anataka.
OIC ni politics tupu ktk dini hakuna la maana zaidi ya kuwa sawa na SADC ambao wanadai wao waafrika wa kusini while kumejaa vibaraka na pengine nchi ambazo hazipo kusini..Kwa hiyo wanapotumia OIC kama kweli ingekuwa ni swala la dini basi bila shaka wasingekuwa Kenya ama Uganda ila hawa jamaa wanamtafuta binti yetu kama wanavyomtafuta Wamarekani..
Tatizo la mada hii ni kwamba sisi tunamtazama OIC kama muislaam kaleta posa, mama (waislaam) anamkubali kwa sababu ni muislaam mwenzake lakini baba hataki mume huyu kwa sabau ni muislaam. sasa mama anapouliza dini ya Bush baba anasema Bush hakuja kuomba mke kwa misingi ya dini...Kwa hiyo he is out of question..Mke bado haelewi kwa sababu bado haiondowi ukweli kuwa Bush ni mkristu pamoja na kwamba hakutaja dini yake..
To join OIC haikulazimishi uwe muislaam isipokuwa misaada yake inawafuata wale waliojiunga..hawasimamishi sala tano wala kufanyia mikutano yao misikitini...
Mkuu nenda pale Lions club huwezi kuingia ndani kama wewe sio member lakini kua kwako member wa Lions Club haikufanyi wewe kuwa mhindi ama uzungu fulani kiasi kwamba tofauti hizo ukaziweka kulinganisha na viwanja viwanja vinginevyo ambavyo havihitaji membership... kote wanaitaka fedha zako..Swala la Marekani, pakistan na kwingineko mkuu umekuanzisha wewe mwenyewe kwa sababu umechukulia tu kuwa member OIC ni Uislaam...OIC haiko ktk hata kitabu kimoja cha Uislaam...iweje OIC ni Uislaam. Mkuu hapa canada tuna Jumuiya ya watanzania na kuna Wakenya, Waganda, Wazambia nao wamejiunga nasi sasa sijui wao nitasema vipi hali kuna jina la Umoja wa WaTanzania.

Comrade Mkandara,

Nimekupata vizuri, labda hukunielewa au hujui msimamo wangu uko wapi katika jambo hili.

Nauliza maswali ya msingi kwa kuwa hoja imekuwa ni lazima Tanzania ijiunge na OIC ili kulinda maslahi ya Waislamu. Sasa OIC ni ushirika wa Nchi za Kiislamu. Swali linakuja, je Tanzania ni nchi ya Kiislamu? majibu yanakuja Msumbiji na Uganda ni Wanachama lakini si kujibu kama Tanzania ni nchi ya Kiislamu au laa.

Ndipo nikauliza kuna shida gani basi kwa Tanzania kujiunga na World Council of Churches?

Swali si kuzuia Waislamu kama jumuiya kujiunga na kunufaika na OIC, suala ni ukingiza Tanzania kama nchi ambayo hakuna majority religion kuwa mwanachama wa Jumuia ya Nchi za Kiislamu!

Ndio maana nilipoleta mfano wa Marekani, Pakistani, Canada na India nilisema kama ni misaada, basi hata yao ina walakini kwa kuwa kuna umasikini.

Sasa umezungumzia jumuiya ya Watanzania Kanada, minnesota kuna jumuiya ya Watanzania Umoja society, kuna wanachama Wakenya, Waganda hata kutoka Rwanda. Hawa wameingia kwa utashi binafsi kwa kuwa jumuiya ni za mtu mmoja mmoja.

Kujiunga OIC ambayo lengo lake kuu ni umoja wa Kidini huku Tanzania si nchi iliyofungamana na dini na mgawanyo wa raia kidini ni sawa, huku ni kujitakia matatizo maana hakuna ridhaa ya wananchi.

Kama alivyosema mtoa haja mmoja mapema, hatuwezi kujifananisha na Msumbiji au Uganda kwa kuwa hatufahamu katiba zao au taratibu walizofuata wao kujinga na OIC.

Ubaya wa huu mjadala ni jinsi ulivyoletwa na kushinikizwa kwetu na Wanasiasa.

Inaelekea wazi kuwa kauli hizi za harakaharaka hazijafikiriwa na ni juhudi za kuhalalisha mambo fulani ya kisiasa kama nilivyosema hapo awali kuwa Kikwete anakuwa compromised na ku-succumb to blackmail ili fukuto la Muungano litulie.

Kama jinsi tatizo hili la kujiunga OIC lilitokea 1993 pamoja na Membe kudai kuwa Zanzibar na Diria walijiingiza kinyemela, bado kwa Tanzania kujiunga OIC kutaleta vurugu na kutokuelewana.

I wish we could sit down and resolve the Muungano issue first as a nation and then let other things like OIC and Kadhi fall in place after reconciliation and new constitution with Union or without union!
 
Rev. Kishoka,
haswaa mkuu wewe umenipata vizuri...
ndio maana nimeshauri hapa badala ya kutazama swala la mahakama ya kadhi kwa jina lake kama ni mahakama ya waislaam ni muhimu tutazame kwanza nini hasa malengo yake...je, ni waislaam peke yao ndio waathirika?.. jibu hapana kwa hiyo ni lazima lipatiwe ufumbuzi hata kama miaka ile ya 60 walijaribu kutafuta ufumbuzi na ikashindikana na kwa sababu kila mtu alifikiria kwanza dini yake hali hakuna kati yao waliofuata dini hiyo.
hata yale madai ya Awali ya biti Titi kudai mapungufu ktk dini ya kiislaam kuhusiana na wanawake yalikuwa zaidi yametokana na mila zetu kuwadhalilisha wanawake lakini kwa ujinga wake na ufinyu wa kutoangalia mbali aliweka madai yake kwa sababu ya exprerience yake ndani ya Uislaamhivyo alikutana na Upinzani mbaya zaidi. Lakini kama angesema kwa upana zaidi kuwa wanawake nchini walikuwa hawapewi haki zao kisha akajitumia yeye kama mfano ktk ndoa ingekuwa na nguvu zaidi.
Kwa nini mada hii imekuwa na upinzani mkubwa?.. ni kwa sababu ya approach ya waislaam ktk swala zima. badala ya wao kueleza matatizo ya ndoa na mirathi kwa nchi nzima kisha wakatumia mifano ndani ya dini yao ingekuwa na support ya wengi tu hata wale wanaopinga hoja nzima humu... Tatizo ni pale wanapotumia jina la dini kujitenga ili kupewa sheria hali waathirika ni toka waumini wa kila dini..Upinzani umekuwa mkubwa sana na watu wameanza kufikiria mengi nje ya hata makusudio ya wale walioomba mahakama hii ya kadhi...Hili ndilo tatizo la sisi kushindwa kujipanga kabla ya mapambano.

Shukran sana hoja yako kama upo kichwani mwangu.
 
Rev Kishoka,
Mkuu wangu bado unalitazama swala hili kwa rangi zake ndio maana unashindwa kuona mambo madogo madogo. Kwanza umesema tunajiunga kwa sababu ya kulinda maslahi ya waislaam!..Bila shaka kabisa ndio lugha ya biashara inayoweza kuwavuta wateja lakini have you heard OIC ktk migogoro ya Iraq, Iran au nchi nyingine za kiislaam iwe kidini ama kisiasa! au hawa jamaa wanachokifanya biasahara na misaada kama vile IMF.
Tofauti na World council of Churches, OIC ni chombo kinachoendeshwa na wafadhili ambao hawana elimu kubwa ya dini, hakuna Padre mle na kuna wakristu pia wanaofanya kazi kwani madhumuni yake hayahusiani na dini yenyewe isipokuwa maendeleo ya watu kama jamii..

Mkuu mimi wala sina la kusema napofungua Tv kila siku nikisikia vyombo vya kikristu vikishutumu Uislaam kutokana na mambo ya Iraq lakini akili yangu inanambia hawa watu hawajui Uislaam na hawatafahamu hivyo waache waseme weee kuhusu Uislaam lakini nijuavyo mimi adui yake mkubwa ni mwarabu na wanamsindwa hivyo wanajaribu kuongeza wigo la kuonyesha wanapigwa na wengi ama adui wasiyemuona..

Nitakwambia kisa kingine cha kweli kabisa... unajua tena kuishi kwingi huona mengi.
Unajua red cross waarabu waliposdskia kuwa imeanzishwa na wakristu waliipiga marufu kabisa. Hao red coross walijieleza kwa kila lugha na ueleza hata wanachama wake kuwa zipo nchi za kiislaam nyingi tu zinawapokea..Duh! mwarabu hakukubali hadi pale Red cross ile ile ilipobadilisha jina na kuwa Red Crescent na kuweka nembo ya mwezi badala ya msalaba wa ajili ya nchi za kiarabu pekee pamoja na kwamba operation zote zinatoka sehemu moja.

Wayahudi pia wao hutumia nembo ya nyota (Star of David) na waarabu wote wamepinga kuitambua Red Star kama chombo cha Red cross kwa sababu ya alama hiyo na sio kwamba waislaam hawaaamini David na utume wake ama utukufu wake isipokuwa alama hiyo inahusiana na Wayahudi ambao kwa mtazamo wao ni adui ya waarabu..kwa mtazamo mfinyu mwarabu ni uislaam hali wapo waarabu wakristu wanaopinga matumizi ya Red star..
Wakati huo huo hiyo red cross ipo nchi nyingine zote na hakuna matatizo ya kufikiria dini pamoja na kwamba ni chombo cha UN sasa hivi..Siku zote matatizo huyaanza sisi wenyewe tunapoanza ku question kitu na hapo ndipo tunazua maswali mengi kuhusiana na vitu vingine kwa rangi zake.
Hapa mkuu nachojaribu kukuonyesha ni ule ufinyu wa watu kutoangalia mbali kutokana na kiza cha udini ama Ikabila kinachoweza kumeza kabisa malengo ya chombo ambacho ni muhimu sana ktk maendeleo yao. Red cross haifundishi dini wala hailazimishi mtu kuwa myahudi na hata siku moja David hakupigana na waislaam isipokuwa Wapalestina enzi za Goliath ambao hawakuwa waislaam wala waarabu. So why not accept a Red star services simple because anayekifagilia ni myahudi walkati watu wako wanakufa...

Nitaongezea kidogo kuhisiana na wanachama wa jumuiya ya watanzania... tatizo linakuja pale mtu atakapo itazama jumuiya yenu ya Watanzania na kuanza kuihusisha na serikali ya Tanzania hali vyombo hivi havihusiani kabisa ila ni watu toka Tanzania wameamua kuunda chombo cha kuwaunganisha. sasa Kama hao Wakenya watakuwa na mtazamo kama wenu watashindwa kabisa kuona sababu ya kujiunga na chama cha Kitanzania.. OIC haina mahusiano kabisa na dini za kiislaam tena basi unalelewa wazi kuwa sisi kwa madhehebu yetu haziivi kabisa kama vile Wazanzibar na Wabara.
 
Mkuu.

Pongezi kwako kwa hili.
Unajua mawazo ya kibaguzi huwa hayaletwe na mtu ila ni sisi wenyewe.Nyinyi wachangiaji wenzangu hapo juu,mngeweza hata kufanya uchambuzi tu kidogo wa hayo malalamiko yenu alafu ndio mlete hapa.

sasa ona hata Nigeria imo kwenye hii organisation,kama wafatiliaji wa mambo mnakumbuka Nigeria ndio BIAFRA ilipo,hiyo ndio hata ilimfanya Nyerer agombane na Amin lakini agalia hata wao leo wamo kwenye OIC.
tufikiri kwanza kabla ya kuleta UBAGUZI wetu kwa wenzetu

Ni kweli unachosema na hasa mawazo yako ndiyo yenye lengo la kibaguzi. Kinacholetwa hapa ni maoni na kila mtu ana maoni yake. Kwa nini maoni yasiyoendana na yako uone ni ya kibaguzi?

Hoja kwamba hata Nigeria ni mwanachama siyo hoja hata kidogo kwani ungeweza kusema pia kuwa mbona Kenya, Afrika Kusini au DRC siyo wanachama. Kwangu mimi swali ni kwa nini sisi kama Tanzania tunataka kujiunga na OIC. Kitu ambacho naweza kuhoji ni kwamba Tanzania imesaini The Universal Declaration of Human Rights wakati OIC hailitambui kwa vile siyo 'consistent with Sharia Law'.

Ila OIC inatambua The Cairo Declaration of Human Rights in Islam na Article 24 inasema: "All the rights and freedoms stipulated in this Declaration are subject to the Islamic Shari'ah" wakati Article 25 inasema: "The Islamic Shari'ah is the only source of reference for the explanation or clarification of any of the articles of this Declaration."

Swali langu ni kwamba kwetu sisi kuwa wanachama wa OIC ina maana kwamba na sisi pia tunazikubali hizi articles zilizotajwa hapo juu au tutaendelea na zile za Universal Declaration of Human Rights?

Na pili, tunajiunga kwa mambo yapi hasa? Haya yote yangewekwa wazi isije huko mbele tukaanza kuingizwa kwenye mikataba itakayoanza kuleta machafuko nchini.

Tatu, hakutakuwa conflict of interests hasa kwa vitu ambavyo ni 'fundamentals'? Naomba machango wenu.
 
The World Council of Churches (WCC) is the broadest and most inclusive among the many organized expressions of the modern ecumenical movement, a movement whose goal is Christian unity.

The WCC brings together 349 churches, denominations and church fellowships in more than 110 countries and territories throughout the world, representing over 560 million Christians and including most of the world's Orthodox churches, scores of denominations from such historic traditions of the Protestant Reformation as Anglican, Baptist, Lutheran, Methodist and Reformed, as well as many united and independent churches. While the bulk of the WCC's founding churches were European and North American, today most are in Africa, Asia, the Caribbean, Latin America, the Middle East and the Pacific.

Ref:http://www.oikoumene.org/en/who-are-we.html

Tanzania kama nchi haiwezi kujiunga na World Council of Churches. Kama jina lake linavyosema, shirikisho hili ni kwa makanisa tu.Tanzania inawakilishwa katika jumuia hii kupitia makanisa yake ya Anglikana, Kilutheri na Moravian ambayo ni wanachama. WCC haifanani na OIC ambayo inalenga kuwaunganisha waislamu kupitia nchi wanazoishi. Askofu Dr. Owdenburg Moses Mdegella wa Kanisa la kiinjili la kilutheri Tanzania ni member wa Central Committee ya WCC.


Kwa wale wanaosema kuwa kila mtu anaweza kuajiriwa OIC bila kuangalia dini, angalia tangazo la kazi lililo live:

VACANCY ANNOUNCEMENT

DEADLINE FOR APPLICATIONS: 1 SEPTEMBER 2008

JOB TITLE: Professional Officer (Deputy Head of Mission of the OIC Permanent Observer Mission to the United Nations, New York).

ORGANIZATIONAL UNIT: OIC Permanent Observer Mission, New York.

DUTY STATION: OIC Permanent Observer Mission, New York.

CATEGORY/GRADE: Professional P/3 or P/4.

REMUNERATION: Depending on professional background and experience, a competitive compensation and benefits package is offered.

JOB DESCRIPTION:

* Under the supervision of the Permanent Observer Mission,
* Perform all the necessary functions as the Deputy Head of Mission,
* Assist the Head of Mission, under his supervision, in administering the Office and the staff.
* Maintain up-to-date knowledge of events on International developments in general, and the agenda and activities of the United Nations system in particular,
* Monitor and gather comprehensive information from all available sources including academic works, media and internet, on the developments with regard to the assigned area of responsibility
* Play an interactive role, under the supervision of the Head of Mission, vis-a-vis the OIC Ambassadorial Group and its experts in New York by sharing views, insights and information as to the performance of the OIC as well as ctions and initiatives to be taken by the OIC.
* Assist in preparation of various documents such as research documents, reports of the Mission as well as of the General Secretariat, mission reports, memoranda, talking points, press releases, diplomatic notes and letters, etc. which may be required by the headquarters or Head of the Mission.
* Develop action-oriented partnerships with international institutions and universities, think-tanks, NGOs and media organs based in the United States in order to highlight and support the new vision and activities of the OIC,

COMPETENCIES:
Ability to successfully represent the OIC in every manner Dedication, efficiency, professional and personal integrity, sense of responsibility, ability to integrate in international, multi-linguistic and multicultural environment. Demonstrated ability to complete in-depth studies and research conclusions, sound analytical skills, good planning and organizational skills, strong reporting and drafting ability, proven ability to write in a clear and concise manner and to communicate orally in an articulate manner, ability to interact and function within a team spirit by establishing and maintaining effective working relationship and cooperation with colleagues, ability to conduct and develop social relations, good computer skills, demonstrated interest in issues related to the international affairs in general and the Islamic world, Islamic Culture and United Nations system in particular, strong desire and commitment to pursue a professional career at the OIC and personal and professional commitment to the missions and visions of the organization and to serve the causes of the Muslim World.

WORK EXPERIENCE:
At least 7 years of progressively responsible experience in international relations, gained preferably within the foreign services of the member states or at intergovernmental organizations. The candidates who are presently working at the OIC Member States' Permanent Missions in the UN New York, and the UN staff members based in New York who are citizens of OIC Member States will have absolute preference and advantage over other candidates.

EDUCATION:
University degree in political science, international relations and diplomacy, peace studies, developmental studies, international economics, international law or related fields. (Master's or doctorate degree is preferred).

LANGUAGES:
Professional fluency and proficiency (reading, writing and speaking) in English, and a fair knowledge of French and/or Arabic.

GENERAL REQUIREMENTS:

* To be a Muslim national of one of the OlC member states. If married the spouse must be Muslim.
* To be below 35 years old.
* To be free of diseases and infirmities (to be attested by certified examination by an accredited hospital)
* To have completed compulsory military service, where applicable.
* To be either nominated by his/her state or his/her state should transmit a no-objection letter to the OIC General Secretariat regarding the particular appointment.

The applications, accompanied by detailed CVs in English language, should be addressed before the deadline to the following e-mails: cabinet@oic-oci.org, gokcen@oic-oci.org

ref:http://www.oic-oci.org/oicnew/page_detail.asp?p_id=48

Hata kama nchi yako ni mwanachama ili kupata kazi ya maana katika OIC ni lazima uwe muislamu. Na kama umeoa, mke wako lazima awe muislamu. Kama ni mkristu au dini nyingine hautapata nafasi ya uongozi.

Kusema tena kuwa kinaongozwa na watu wasio wakali katika masuala ya dini si kweli! Katibu Mkuu wa sasa hivi ni Professor Ekmeleddin Ihsanoglu kutoka Turkey ambaye awali alikuwa akiongoza the Research Centre for Islamic History, Culture and Arts huko Istanbul.

OIC haijifichi kuwa ni shirika la kidini. Ni kujidanganya kusema vinginevyo. Ukiangalia hata kamati zake zimeundwa kulinda maslahi ya waislamu.

Kwangu mimi hili si tatizo. Tatizo ni kukataa kulizungumzia hata kama limeingizwa kisanii.
 
Sheria hiyo ingeapply kwa kukubali uhusiano na Vaticanh.

A slave of allah in action!

Umeshaambiwa kuwa Vatican ni nchi baba..na wala mafungamano yake na Tanzania ni ya ki-nchi sio deen ..
 
Kwangu mimi hili si tatizo. Tatizo ni kukataa kulizungumzia hata kama limeingizwa kisanii.[/SIZE][/FONT]

Tatizo ni serikali kujitia msemaji ktk hili wakti Ibara ya 19(2), imeshajieleza dhahir shahir.

Kwani kazi ya BAKWATA ni nini?
 
World Council of Churches na mashirika mengine hayako kwenye vitabu vya kikristu lakini bado ni mashirika ya kidini. OIC ni ya kiislamu na sio ni uislamu kwa vile kimeundwa na kinalenga waislamu! Si lazima kiwe katika Quran. Kama ambavyo BAKWATA na hata EAMWS ambavyo havikuwahi kutajwa katika vitabu vitakatifu vya kiislamu. Pamoja na hili yote haya ni mashirika ya kidini. Kwani hata hayo madhehebu tunayoyafuata yametajwa katika vitabu vitakatifu?
 
Rev. Kishoka,
Mkuu asikudanganye mtu kuwa nchi kama marekani zinatupa misaada bila masharti... Ni lazima tujiunge na kundi fulani kulipa fadhila zao...Ni sawa na mwamake akwambie ati mzee fulani huwa anamopa hela bila kumwomba mchezo!.. comeon mkuu kuna kitu huyo mzee anataka.
OIC ni politics tupu ktk dini hakuna la maana zaidi ya kuwa sawa na SADC ambao wanadai wao waafrika wa kusini while kumejaa vibaraka na pengine nchi ambazo hazipo kusini..Kwa hiyo wanapotumia OIC kama kweli ingekuwa ni swala la dini basi bila shaka wasingekuwa Kenya ama Uganda ila hawa jamaa wanamtafuta binti yetu kama wanavyomtafuta Wamarekani..
Tatizo la mada hii ni kwamba sisi tunamtazama OIC kama muislaam kaleta posa, mama (waislaam) anamkubali kwa sababu ni muislaam mwenzake lakini baba hataki mume huyu kwa sabau ni muislaam. sasa mama anapouliza dini ya Bush baba anasema Bush hakuja kuomba mke kwa misingi ya dini...Kwa hiyo he is out of question..Mke bado haelewi kwa sababu bado haiondowi ukweli kuwa Bush ni mkristu pamoja na kwamba hakutaja dini yake..
To join OIC haikulazimishi uwe muislaam isipokuwa misaada yake inawafuata wale waliojiunga..hawasimamishi sala tano wala kufanyia mikutano yao misikitini...
Mkuu nenda pale Lions club huwezi kuingia ndani kama wewe sio member lakini kua kwako member wa Lions Club haikufanyi wewe kuwa mhindi ama uzungu fulani kiasi kwamba tofauti hizo ukaziweka kulinganisha na viwanja viwanja vinginevyo ambavyo havihitaji membership... kote wanaitaka fedha zako..Swala la Marekani, pakistan na kwingineko mkuu umekuanzisha wewe mwenyewe kwa sababu umechukulia tu kuwa member OIC ni Uislaam...OIC haiko ktk hata kitabu kimoja cha Uislaam...iweje OIC ni Uislaam. Mkuu hapa canada tuna Jumuiya ya watanzania na kuna Wakenya, Waganda, Wazambia nao wamejiunga nasi sasa sijui wao nitasema vipi hali kuna jina la Umoja wa WaTanzania.

Aisee na wewe unapiga siasa sasa! Hivi tunahitaji msaada gani ambao hatuna na wakati serikali imetwambia haitaki kutegemea misaada? Basi kilichosemwa bungeni ni uongo kama bado tunatafuta misaada. Ndiyo maana mimi niko 'reserved' kwa hili.

Nijuacho mimi hata kama OIC itatupa misaada itatafunwa na wachache tu! Hivi kuna hela ambazo zinazidi zitokazo kwenye dhahabu, tanzanite, almasi, gasi...mbuga za wanyama tulizonazo, samaki wa baharini na ziwani, nk? Mbona hazionekani?

Binafsi, sioni sababu ya maana ya kujiunga na OIC. Nimechoka kudanganywa na wanasiasa na wapiga debe!
 
Rev Kishoka,
Mkuu wangu bado unalitazama swala hili kwa rangi zake ndio maana unashindwa kuona mambo madogo madogo. Kwanza umesema tunajiunga kwa sababu ya kulinda maslahi ya waislaam!..Bila shaka kabisa ndio lugha ya biashara inayoweza kuwavuta wateja lakini have you heard OIC ktk migogoro ya Iraq, Iran au nchi nyingine za kiislaam iwe kidini ama kisiasa! au hawa jamaa wanachokifanya biasahara na misaada kama vile IMF.
Tofauti na World council of Churches, OIC ni chombo kinachoendeshwa na wafadhili ambao hawana elimu kubwa ya dini, hakuna Padre mle na kuna wakristu pia wanaofanya kazi kwani madhumuni yake hayahusiani na dini yenyewe isipokuwa maendeleo ya watu kama jamii..

Kama hoja ni ufadhili, hivi hawawezi kutupatia hiyo misaada mpaka tuwe 'kwenye himaya yao'? . Au tukishaingia kwenye uanachama ndio uhitaji wetu utakuwa loud & clear zaidi?

I'm very suspicious here...
 
Hivi tunahitaji msaada gani ambao hatuna na wakati serikali imetwambia haitaki kutegemea misaada? Basi kilichosemwa bungeni ni uongo kama bado tunatafuta misaada.

Nashukuru umeliona hili, maana ukikusanya pamoja, kauli, mienendo,mipango na maazimio ya serikali yetu havileti maana.
 
World Council of Churches na mashirika mengine hayako kwenye vitabu vya kikristu lakini bado ni mashirika ya kidini. OIC ni ya kiislamu na sio ni uislamu kwa vile kimeundwa na kinalenga waislamu! Si lazima kiwe katika Quran. Kama ambavyo BAKWATA na hata EAMWS ambavyo havikuwahi kutajwa katika vitabu vitakatifu vya kiislamu. Pamoja na hili yote haya ni mashirika ya kidini. Kwani hata hayo madhehebu tunayoyafuata yametajwa katika vitabu vitakatifu?

Je, unaweza kutwambia nchi yoyote ambayo imejiunga na World Council of Churches? Si huwa ni madhehebu husika ndiyo yanayojiunga (mfano Wakatoloki, Waluteri, Waangalikani, nk)? Usichanganye vitu hapa!
 
Je, unaweza kutwambia nchi yoyote ambayo imejiunga na World Council of Churches? Si huwa ni madhehebu husika ndiyo yanayojiunga (mfano Wakatoloki, Waluteri, Waangalikani, nk)? Usichanganye vitu hapa!

Soma kwanza na uelewe. Kabla ya hilo uliliona niliisha sema yafuatayo:

Tanzania kama nchi haiwezi kujiunga na World Council of Churches. Kama jina lake linavyosema, shirikisho hili ni kwa makanisa tu.Tanzania inawakilishwa katika jumuia hii kupitia makanisa yake ya Anglikana, Kilutheri na Moravian ambayo ni wanachama. WCC haifanani na OIC ambayo inalenga kuwaunganisha waislamu kupitia nchi wanazoishi. Askofu Dr. Owdenburg Moses Mdegella wa Kanisa la kiinjili la kilutheri Tanzania ni member wa Central Committee ya WCC.

Wakatoliki si wanachama wa World Council of Churches na wala hawajawahi kuomba kuwa wanachama.
 
Fundi Mchundo,
lakini hao mashahidi wa Jehova mbona wamerudi?..sasa jiulize wameweza vipi!..

If we go by comparisons we may not reach any sensible solution. There's what is called 'positive discrimination'. It is hardly possible to do everything exactly in the same way.

For instance, if Christians rest on Saturday or Sunday, them Muslims should rest on Friday. If there's Vatican Ambassador in Tanzania, then there must be one for Muslims in the Vatican.

In my opinion, let us do what we consider important for us and not because others do it. Usiige kunya kwa tembo...!
 
Du mzee naona unajazba. Usiwe na wasi wasi wakitusilimisha tutawapigia kelele mpaka watusilimuwe.

hahaha kusilimisha itakuwa ngumu vatican nayo itakuwa haijalala ati.
kama nia ni kushinda uchaguzi Zanzibar inabidi wachambue kwa kina unaweza kupata hela nyingi kutoka uarabuni, na kushinda zanzibar !BARA je?wakristo nao watataka kuwaondoa katika uchaguzi ili waweze kuvunja mkataba wa kujiunga na IOC, then Kitakachofuata ni kuvunjika kwa Amani, TUNAHITAJI HEKIMA ZAIDI KULIKO KUNG'ANG'ANIA NI NANI KAJIUNGA NA NIFAIDA GANI KAPATA,
 
Uislam ni mfumo wa maisha unaojitegemea....

Wakristo hawajakatazwa...na kama wanahitaji nao waombe...
 
Back
Top Bottom