Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,476
- 39,995
Kwa mara nyingine tena hoja ya Bunge kupitisha sheria ya kurudisha ofisi ya Kadhi Mkuu linajitokeza tena huku waislamu wakitaka Bunge litunge sheria ya kutambua uwepo wake na wakristu wakipiga kelele kuwa kufanya hivyo ni kuvunja Katiba. Hoja yangu leo ni kuwa, Waislamu hawahitaji kibali cha serikali kuanzisha ofisi ya Kadhi Mkuu kushughulikia mambo yao yanayoendana na sheria za Kiislamu.
Waislamu wakae wao wenyewe wapitishe uwepo wa ofisi hiyo na kuendelea na shughuli zao. Ilimradi tu, maamuzi ya ofisi yao hiyo hayaingilii uhuru wa Mtanzania mwingine au utendaji kazi wa sheria zetu za makosa ya uhalifu na jinai. Pia waelewe ya kwamba uwepo wa ofisi ya Kadhi Mkuu ni subject ya Katiba ya Muungano na Mtanzania yeyote kimbilio lake la mwisho ni mahakama ya Kiraia. Zaidi ya yote, watakapoanzisha ofisi hiyo, wajue kuwa isiwalazimishe waislamu wote kutatua matatizo yao kupitia ofisi hiyo isipokuwa wale ambao kwa hiari yao wanataka kufanya hivyo.
Kanisa Katoliki kwa mfano linayo mahakama yake na sheria zinazoliongoza kanisa hilo (Canon Law) na mahakama yake hiyo ina ngazi za rufaa hadi Vaticano. Hata hivyo Mkatoliki ana haki ya kutumia sheria hizo kuhusu masuala mbalimbali ya kanisa lake, lakini anapofanya kosa la jinai, sheria za kiraia (civil law) zinakuwa na mamlaka. Hivyo basi, waislamu wasisubiri Bunge kupitisha ofisi ya Kadhi Mkuu bali waianzishe wao wenyewe huku wakiweka bayana kabisa kuwa ofisi hiyo haitahusika na makosa ya jinai au kupingana na Katiba ya nchi. Then, hakutakuwa na haja ya kugongana!!!
Waislamu wakae wao wenyewe wapitishe uwepo wa ofisi hiyo na kuendelea na shughuli zao. Ilimradi tu, maamuzi ya ofisi yao hiyo hayaingilii uhuru wa Mtanzania mwingine au utendaji kazi wa sheria zetu za makosa ya uhalifu na jinai. Pia waelewe ya kwamba uwepo wa ofisi ya Kadhi Mkuu ni subject ya Katiba ya Muungano na Mtanzania yeyote kimbilio lake la mwisho ni mahakama ya Kiraia. Zaidi ya yote, watakapoanzisha ofisi hiyo, wajue kuwa isiwalazimishe waislamu wote kutatua matatizo yao kupitia ofisi hiyo isipokuwa wale ambao kwa hiari yao wanataka kufanya hivyo.
Kanisa Katoliki kwa mfano linayo mahakama yake na sheria zinazoliongoza kanisa hilo (Canon Law) na mahakama yake hiyo ina ngazi za rufaa hadi Vaticano. Hata hivyo Mkatoliki ana haki ya kutumia sheria hizo kuhusu masuala mbalimbali ya kanisa lake, lakini anapofanya kosa la jinai, sheria za kiraia (civil law) zinakuwa na mamlaka. Hivyo basi, waislamu wasisubiri Bunge kupitisha ofisi ya Kadhi Mkuu bali waianzishe wao wenyewe huku wakiweka bayana kabisa kuwa ofisi hiyo haitahusika na makosa ya jinai au kupingana na Katiba ya nchi. Then, hakutakuwa na haja ya kugongana!!!