Juu ya OIC na Mahakama ya Kadhi

Juu ya OIC na Mahakama ya Kadhi

Uislamu ni Empire kisha ni Dini.

Baada ya kuanguka kwa Ottoman Islamic Empire Uislamu unajitahidhi kwa kila hali kushawishi nchi masikini kama Tanzania kuji aligne upande wake.

Kishawishi kikubwa sana kwa nchi masikini kujiunga ni fedha na nanchi tajiri za OIC hufaidika kwa ruksa ya nchi hizo kuwekeza bila mpaka katika nchi fukara hizo ikiwa ni pamoja na kununua maeneo na kuyafanya ni sehemu ya urithi wao wa asili milele kwa mfama kama ule wa Loliondo na kule kwa Wahadzabe.

Tatizo lenu wengi hamuwaelewi Waarabu.Mnatishika na historia na kupakazia mengi yasyo ya kweli. Hao Mabwana ze3tu Wazungu wanakimbilia kwa hao Waarabu na hizo pesa wanazotupa msingi wake ni kwa Waarabu.
Nchi kama misri,Commoro< Lebanon, Syria na nyengine ni nchi zinzofuata maadili ya Kikristo zaidi kuliko uislamu. Hapa tunadanganyana kuwa kuna nia ya kusambaza uislamu. wangefanya hivyo kwenye nchi zao na baadae kuja Tanzania.
 
Busara za mzee Nyerere zinaanza kukosekana hapa.!! Wananchi watakuwa hawatendewi haki kama serikali yao itajiunga kwenye hiyo islamic organization bila ya kuwashirikisha.Katiba yetu inasema kuwa serikali yetu haina dini bali ni wananchi ndiyo wenye dini ,hivyo basi kabla ya serikali yetu haijajitumbukiza kwenye hizi religion organizations ni bora wananchi wakaelezwa masharti yote ya kujiunga na kuwaachia wafanye maamuzi baada ya hapo.Haya mambo si madogo kama akina Membe wanavyotaka kuyafanya.Maamuzi yanahitaji kuwashirikisha wananchi zaidi na siyo kukurupuka tu kujiunga ati kwa kuwa Msumbiji wamo au Zanzibar wanapush hii issue.Maana tusipokuwa waangalifu katika hili kesho tunaweza aamka tukaaambiwa nchi yetu ipo kwenye jumuiya za kihindu au kimormon countries ati kwa sababu nchi fulani zipo au kuna mikopo mingi!!
Tufuate sheria na tuwape wananchi muda wa kufanya maamuzi kabla ya kukurupuka na kufanya maamuzi ambayo yanaweza kuja kuligharimu Taifa letu gharama kubwa.
Na hili lisiwe tu kwenye jumuiya za kiislam bali hata kwenye jumuiya za dini nyingine kama za Jehova witnesses countries,Kihindu countries,Church of Jesus Christ of Latter-day Saints(Mormons)countries kama zipo au zitakuja baadaye.

Kwa hiyo hata lile suala la mahakama ya kadhi nalo linaingia humo humo kuwa huwezi kuwahukumu wananchi kwa kufuata sheria za dini fulani kwa kuwa utakuwa huwatendei haki wale wananchi ambao haamini sheria za dini hiyo.Wananchi wahukumiwe kwa kufuata sheria za nchi ambazo zimewekwa na kupitishwa na bunge.Sasa kama tunataka kupambana na rushwa au uwizi au ufisadi dawa siyo mahakama ya kadhi bali dawa ni kuongeza resources kwenye mfumo wetu wa mahakama uliopo ili ufanye kazi yake kama inavyotakiwa.
 
...jamani hadi lini mtaambiwa kuwa VATICAN IPO HAPA NA UBALOZI KAMA NCHI KAMILI...mwanachama wa UMOJA WA MATAIFA.....ni nchi yenye wakristo asilimia 99.9 kama saudi ilivyo na waislamu 99%.....nadhani mtakubali kuwa OIC siyo nchi......na mtaacha kuhalalisha pia mambo ya kadhi na TAIFA LA VATICAN.....kadhi inaweza kuanza hata kesho vile vile ..kwa gharama za waumini wake....

baada ya kila wakati ufafanuzi wa vatican kuwa nchi kutolewa ...na watu ..tena wasomi tu kujifanya hawauelewi...nadhani wanahitaji kupuuzwa!!!

...uganda na msumbiji ndio mataifa pekee circular au yenye population kubwa ya wakristo....yaliyoingia OIC...NARUDIA UGANDA ILIIINGIZWA NA DIKTETA IDDI AMIN akiwa na ambition za kuifanya uganda islamic..rep..mozambique walijiunga baada ya vita ya zaidi ya miaka 30 ...wakitaka masilahi kwa yeyote aliyewanyooshea mkono...ikiwemo kujiunga na commonwealth pamoja na kuwa walitawaliwa na ureno......je tuna mazingira ya hizi nchi mbili???>>>>naombeni mje na mfano wa nchi nyingine zaidi ya hizi mbili zenye population ya wakristo kama hapa kwetu zilizo wanachama...ndio tuanzie hapo.....

upande wa muungano wa zanzibar una waislamu asilimia 98%..lakini ikumbukwe kuwa thats make out of 1 million wananchi....when you bring that data to the union...its not convincing percentage as to allow our nation to either align itself with muslim or christian nations or allience or whatsoever..we are happy they way we are!!!

Nakumbuka palishatolewa vigezo vya kuwa nchi. Tafadhali nkumbushe in relation to Vatican.
 
Jamani, hebu naomba tuisome vizuri katiba yetu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwenye Ibara ya 19(2), naomba ninukuu kwa manufaa ya wengi:

Kazi ya kutangaza dini, kufanya Ibada na kueneza dini itakua ni huru na jambo la hiari la mtu binafsi, na shughuli na uendeshaji wa jumuia za dini zitakuwa nje ya shughuli za mamlaka ya nchi.

Kwa uelewa wangu ni kwamba, kulingana na Ibara hiyo, serikali haipaswi kujihusisha kwa namna yoyote na masuala ya nayohusiana na dini kwa namna yoyote ile, hivyo kitendo cha serikali kufikiria kujiunga na OIC kitakua ni kunyume cha sheria tena kitakua ni uvunjaji wa katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Sambamba na hili, kitendo cha Serikali kujihusisha na mjadala wa mahakama ya Kadhi ni ukiukwaji wa Katiba ya Jamhuri wa Muungano wa Tanzania kwani, Katiba iko wazi wazi kabisa kwamba, suala la kueneza dini au uendeshaji wa jumuia za kidini ni swala la mtu binafsi, hivyo serikali kujihusisha na hii mijadala ya Mahakama za Kadhi na OIC ni kunyume cha sheria na ni uvunjaji wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 (soma toleo la mwaka 2005 ukurasa wa 23)

Sheria hiyo ingeapply kwa kukubali uhusiano na Vaticanh.
 
Jamani, hebu naomba tuisome vizuri katiba yetu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwenye Ibara ya 19(2), naomba ninukuu kwa manufaa ya wengi:

Kazi ya kutangaza dini, kufanya Ibada na kueneza dini itakua ni huru na jambo la hiari la mtu binafsi, na shughuli na uendeshaji wa jumuia za dini zitakuwa nje ya shughuli za mamlaka ya nchi.

Kwa uelewa wangu ni kwamba, kulingana na Ibara hiyo, serikali haipaswi kujihusisha kwa namna yoyote na masuala ya nayohusiana na dini kwa namna yoyote ile, hivyo kitendo cha serikali kufikiria kujiunga na OIC kitakua ni kunyume cha sheria tena kitakua ni uvunjaji wa katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Sambamba na hili, kitendo cha Serikali kujihusisha na mjadala wa mahakama ya Kadhi ni ukiukwaji wa Katiba ya Jamhuri wa Muungano wa Tanzania kwani, Katiba iko wazi wazi kabisa kwamba, suala la kueneza dini au uendeshaji wa jumuia za kidini ni swala la mtu binafsi, hivyo serikali kujihusisha na hii mijadala ya Mahakama za Kadhi na OIC ni kunyume cha sheria na ni uvunjaji wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 (soma toleo la mwaka 2005 ukurasa wa 23)



okay good WAAMBIENI HAO OIC ..WAPOKEE UANDACHAMA WA TAASISI..MIMEONA HIYO CATEGORY....WAPOKEE UANACHAMA WA BAKWATA...AU RELEVANT INSTITUTUTION...SO IF MUSLIM WANATAKA KUWA MEMBERS THEY CAN OPT FOR INSTITUTION MEMBERS OF OIC ..FOR THERES THAT PROVITION IN OIC ITSELF...WANAWEZA KUJIUNGA HATA KESHO..

BUT TO JOIN AS A STATE MEMBER .NOOOOO!!!!
 
nakumbuka palishatolewa vigezo vya kuwa nchi. Tafadhali nkumbushe in relation to vatican.

1.vatican ni mwanachama wa umoja wa mataifa...recognised kama nchi kamili...papa ndio mkuu wa nchi na huhudhuria na kuuhutubia un head of state assembly kama rais,mfalme au mkuu wa nchi yeyote...

2.vatican ina jeshi[swiss guard] ,polisi na vyombo vyake....ingawa sio sera yao kuwa na silaha nzito...zaidi ya magari na bastola...

3.vatican inayo ardhi ...mipaka...inayotambulika kimataifa...

4.vatican inayo serikali...na baraza la mawaziri..na bunge lao..conclave...

5.vatican ina wananchi...population 1,000 people....na inatoa pasi za kusafiria....

6.vatican inayo sarafu..benki kuu...posta..na vyombo vingine vya aina hiyo.....

More and more....

Vatican ni nchi yenye emabassies almost duniani kote.....wana ofisi za ubalozi nyingi ..duniani kuliko hata nchi nyingi tu....na mwakilishi wa vatican duniani kote ana hadhi kama balozi yeyote yule....

....would vatican seeze to be the reason ..to trying to push us.....mtu kama haelewi ..ni ameamua kukataa kuelewa......
 
Hii sasa ni kali inakuwaje hakijapita hata kipindi kirefu toka Tanzania visiwani izuiwe kujiunga na OIC na ghafla leo tujiunge au kwa sababu ilikuwa sehemu ya muungano ndiyo maana ilikataliwa? tujiulize yafuatayo 1. utwala uliopita kwa sababu uongozi wa juu ulikuwa wa kikritu ndiyo sababu ya kukataliwa? 2.uongozi wa sasa kuwa wakiislamu ndiyo maana uamuzi umepita bila kupingwa tena bungeni? 3. serikali isiyo na dini ila watu wake inaweza kushiriki mambo ya kidini au jmuia zake? n. ni mengi ya kuuliza ila kwa leo niishie hapo.
 
We're trying to tap as much help as we can. Oil is booming, Saudi's and his buddies gatta a lot of extra cash. I don't see any problem.

Hebu nitajie nchi ambayo imepewa misaada mikubwa na Saudi Arabia. Hawa wanasifika kwa ubahili wao na ukoo wa ufalme kutumia utajiri wao wakiwekeza katika nchi za magharibi na starehe tu.
 
Amani iliyopo katika nchi hii ni kutokana na serikari kutokuwa ya kidini, sasa leo hii nashangaa eti inataka kujiunga na OIC. je ni wapi tunaelekea sasa?? "There is no harm", na je kuna faida gani, karibuni tuchangie

2008-08-23 11:18:35
By Juma Thomas, Dodoma


There is no harm in Tanzania joining the Organisation of Islamic Countries (OIC), the government said yesterday.

Foreign Affairs and International Cooperation minister Bernard Membe made the announcement here when winding up debate on his ministry`s 2007/09 budget estimates.

According to the minister, a meeting between the government and members of the House of Representatives held this year to discuss the issue had resolved that there was nothing wrong for Tanzania to join the OIC.

He said they had come to learn that 21 countries in the world, including Christian countries, had joined the organisation.

``We have already collected enough information about the mater. We are convinced that there is nothing wrong with Tanzania joining the OIC,`` Membe said.

He said the issue was wrongly handled by former minister for foreign affairs Hassan Diria, who applied for Zanzibar membership in the organisation without involving the Union government.

In the early 1990s, Zanzibar attempted to join the OIC, but was refused permission by the Union government on grounds that, being part of the union, it had no mandate to join international organisations.
 
Huku ndiko tunakotaka kwenda

History and goals of OIC

Since the nineteenth century, Muslims had aspired ideas of uniting their community to serve their common political, economic, and social interests. Despite the presence of secularist, nationalist, and socialist ideologies, in modern Muslim states, King Faysal of Saudi Arabia cooperated with other Muslim leaders to form the Organization of Islamic Conference. The formation of the OIC happened in the backdrop of the loss of Muslim holy sites in Jerusalem. The final cause sufficiently compelled leaders of Muslim nations were to meet in Rabat to establish the OIC in May 1971.[1]

According to its charter, the OIC aims to preserve Islamic social and economic values; promote solidarity amongst member states; increase cooperation in social, economic, cultural, scientific, and political areas; uphold international peace and security; and advance education, particularly in the fields of science and technology.[1]

The flag of the OIC has an overall green background (symbolic of Islam). In the center, there is an upward-facing red crescent enveloped in a white disc. On the disc the words "Allahu Akbar" are written in modern Arabic calligraphy.

On August 5, 1990, 45 foreign ministers of the OIC adopted the Cairo Declaration on Human Rights in Islam to serve as a guidance for the member states in the matters of human rights.
 
Upuuuzi mtupu!! tatizo lenu udini unawasumbua (wote waislamu na wakristo) na ndio maana li-serikali lenu la kifisadi lina take hiyo advantage kuwachanganya zaidi....hivi mtu mzima na busara zako unakalia kubisha mambo ya kadhi na OIC?? halafu mkifisadiwa mnalalamika wakati mnapoteza muda kwenye vitu visivyo na maana, vitu vinavyowagawa, vitu vya kufikirika (nani anahukika na hizi dini )!!


assume kwamba kesho waislamu wamepewa mahakama ya kadhi....so what? nini kitakuwa kimebadilika? au jua litachomozea magharibi na kuzama mashariki? haya wamejiunga na OIC....ndio itakuwaje sasa? nini kitaongezeka na nini kitapungua? wanawachezea tu akili kwasababu mnajaa sana ma-emotions.....goodluck!!!!

HOOOOOVYO.

Yaani wewe ndugu yangu ni sawa na wale watanzania wanasema hata asipopiga kura kwani kuna nini, Rais si atakuwa yule yule... na matokeo yale yale na uchumi ule ule una ujinga wako unabaki pale pale....

Hakuna kitu cha kijamii kinachoamuliwa kisikuathiri kwa namna moja au nyingine bila kujali umeshiriki kukiamua au la. Usipende kupuuzia mambo kihivyo
 
PM....Duh ikiwa fikra zako ndizo sawa na Wakristo wengine...nature ya muelekeo wa nchi unapoelekea unafahamika.... Wengine watakuwa mashahidi wa fikra zako!!!,

Uganda imekuwa member wakati wa OIC thru IDD Amin, lkn wamepita viongozi 2 wakristo mbona hawajajitoa hadi leo...Waambie Uganda wajitoe..kwani kujiunga kwao uganga watasilimishwa ..na wataekewa sheria za Kiislam...!!!

Pia kwa logic zako, VITA dhidi ya Amin, haikuwa ya kutaka kuteka Kagera(Kama vyombo vya habari vya mchong, vilivyosema)...ilikuwa ya Chuki za Kikristo za Mchonga dhidi ya Amin...

ikiwa Msumbiji walijunga kwasababu ya Umaskini, Je sasa kwanini wasijitoe?...Je khofu yako eti kuwa OIC member kutaathiri haki za wengine zimeathiriwa vipi?
 
kama ni kutafuta bei rahisi ya mafuta basi mimi ningeishauri serikali ifanye kila iwezalo ,tujiunge na umoja wa ulaya na hatimaye shengeni ,maana tutaiingiza bidhaa nyingi bila ushuru.na tutajipatia kubeba mabox bila viza wala kubugudhiwa.

Haya mawazo ya membe utafikiri alitoka kuota njozi bwana,hakuna kitu cha dezo hapa duniani.mtu akikupa kitu ameshakupigia mahesabu ya mda mrefu.

bernadr membe ni mjinga mmoja hivi anayeota ndoto za urais akidhani kwa vile anatokea lindi kwao na mke wa prez. Na kwa kwa vile inasemekana tangu enzi zile za makundi 1995 alishaona mbali akaamua kuwa upnde ulioko madarakani kwa sasa. Kwa kuwa amewekwa wizara ya mambo ya nje anadhani atakuwa rais wa nchi hii!

Suala la serkali ya ccm, kushindwa kutafuta ufumbuzi wa kweli wa matatizo ya wananchi. Ccm zanzibar imekuwa ikiiptai ccm zanzibar nafasi nyingi sana katika chama, imagine wajumbe wa halmashauri inakaribia nusu zanzibar na nusu kutoka bara. Kuna mikoa na ukawikilishi karibu sawa katika nafasi nyingi za kichama kwa hiyo serkaili ya zanzibar imejisahu na kutaka pia ipate nafasi sawa za uwakilishi katika serikali. Ninadhani ni wakati muafaka tuanze kuangalia proportinality katika uwakilishi. Haiwezekana kwa mfano mbunge wangu ana wakilisha watu laki 3 halafu mbunge wa zanzibar anawakilisha watu elfu moja tu!! Wapi na wapi ujinga gani huu!

Hata leo hii ukitoa mwanya kwa oic , ili kufurahisha watu wachache itafikia mahali pawe na kikomo chake, tumeamuka.

Tunataka referendum ili kujua ni aina gani ya muungano tuaoutaka, binafsi ninataka serikali moja yenye majimbo yake, zanzibar iwe na majimbo mawili, moja la unguja na la pili la pemba!!

Jimbo la ziwa(mara, mwanza, kagera), kati, kaskazini etc.

Hii itarudisha nidhamu ya matumizi ya raslimali zetu.

Watu wengi pia wataeilimishwa, huduma za afya zitaongezeka katika majimbo. Ujinga wa watu wetu kununuliwa na kuandaliwa kunadamana kisanii utaisha. Ninasikia watandama miko yoye kuunga mkono hotubua ya bungeni, sasa kuandfamana kwa nini badala ya kutumia muda huo kujituma kufanya kazi!! Usanii wote huu wa nini??

Kama ni nzuri ni nzuri tu ya nini uandamanishe watu! Usaniii per cel.
 
Acheeeni vitu vya bure, mnataka kutawaliwa mpaka lini?? yeyote anayeunga swala hili ni mvivu wa kila kitu kuanzia hata kufikiria
 
Jamani nadhani tujitasmini kwanza hizo jumuia zingine ambazo niwanachama tunafaidikaje? nachojua kila jumuia inagharama zake kama ada za uanachama na hata gharama za kuhudhuria vikao. Membe atueleze anatumia kiasi gani kugarimia uanachama wetu SADC EAC AU commonwealth UN na sasa tuongeze tena OIC.

Ukweli hizi grants hazitasaidia kuondoa umasikini wetu, tunatakiwa tuweke mipango thabiti ya uchumi. Hizi jumuia tumekuwemo muda mrefu na umasikini uko palepale!

Kwa mawazo yangu ingewezekana hata UN tungejiondoa tu, Mbona Hugo Shavez kajiondoa world bank na IMF. Kuna nchi ambazo sio wanachama wa UN nabado wanapiga hatua tu!
 
Nimeona nchi zilizojiunga na OIC na kwa kweli sipati picha kwa Tanzania kujiunga na Taasisi hii ya Waislam.
 
Tulijitoa COMESA tukaona hakuna maslahi! Sasa tunaona maslahi OIC!! Kweli tunachezea nchi! Nchi haina dira!
 

1.vatican ni mwanachama wa umoja wa mataifa...recognised kama nchi kamili...papa ndio mkuu wa nchi na huhudhuria na kuuhutubia un head of state assembly kama rais,mfalme au mkuu wa nchi yeyote...

2.vatican ina jeshi[swiss guard] ,polisi na vyombo vyake....ingawa sio sera yao kuwa na silaha nzito...zaidi ya magari na bastola...

3.vatican inayo ardhi ...mipaka...inayotambulika kimataifa...

4.vatican inayo serikali...na baraza la mawaziri..na bunge lao..conclave...

5.vatican ina wananchi...population 1,000 people....na inatoa pasi za kusafiria....

6.vatican inayo sarafu..benki kuu...posta..na vyombo vingine vya aina hiyo.....

More and more....

Vatican ni nchi yenye emabassies almost duniani kote.....wana ofisi za ubalozi nyingi ..duniani kuliko hata nchi nyingi tu....na mwakilishi wa vatican duniani kote ana hadhi kama balozi yeyote yule....

....would vatican seeze to be the reason ..to trying to push us.....mtu kama haelewi ..ni ameamua kukataa kuelewa......

Kwa Uongo unaongoza !!!! yaani unajaribu kuungopea umma wa watz...

soma hapa..
http://www.michaelnugent.com/2008/06/14/the-toy-vatican-state-at-the-un/.. tena jamaa kaita TOY STATE!!!

The Vatican is by far the smallest State in the world, being just over a hundred acres in size. It plays at being a real State by issuing its own stamps, but it has no proper citizens (just transient employees of the Catholic Church), few public services (Italy provides it with police and water) and no real economy (though it does have a novelty ATM machine that issues instructions in Latin).

But that does not matter, because the toy Vatican State does not generally interact with other real States. Instead, an entity called the Holy See, which is the central government of the worldwide Catholic Church, masquerades as a State and deals with actual States from its base in the Vatican.

This distinction is very important. It is the openly religious Holy See, and not the theoretically civic Vatican State, that swaps diplomats with actual States, and that has Permanent Observer status at the United Nations and other bodies. But the Holy See does not have any citizens, or any defined territory, and all that it governs is the religious affairs of some citizens of actual civic States.
 
[QUOTEThe Organization of the Islamic Conference (OIC) is the second largest inter-governmental organization after the United Nations which has membership of 57 states spread over four continents. The Organization is the collective voice of the Muslim world and ensuring to safeguard and project the interests of the Muslim world in the spirit of promoting international peace and harmony among various people of the world. The Organization was established upon a decision of the historical summit which took place in Rabat, Kingdom of Morocco on 12th Rajab 1398 Hijra (25 September 1969) as a result of criminal arson of Al-Aqsa Mosque in occupied Jerusalem.[/QUOTE]
Source: http://www.oic-oci.org/oicnew/page_detail.asp?p_id=52

Tatizo la OIC inaiingiza nchi kwenye masuala ya kidini, yaani inataka mwanachama awe ni nchi na malengo yake yanalenga Waislam. Mimi nisingekuwa na tatizo ingekuwa ni kama NGO.

Kumbuka pia kwamba kuna ada ya kulipa kila mwaka. Mojawapo ya organisation zake ni Organisation ya Mawaziri wa mambo ya nje, hii inamshawishi Rais kuteua Waziri kwa misingi ya kidini, kwani si rahisi/busara kumpeleka Mkristo katika mikutano yao.

Hii Serikali ya awamu ya nne itatupeleka pabaya.
 
Back
Top Bottom