Ref:http://www.oikoumene.org/en/who-are-we.html
Tanzania kama nchi haiwezi kujiunga na World Council of Churches. Kama jina lake linavyosema, shirikisho hili ni kwa makanisa tu.Tanzania inawakilishwa katika jumuia hii kupitia makanisa yake ya Anglikana, Kilutheri na Moravian ambayo ni wanachama. WCC haifanani na OIC ambayo inalenga kuwaunganisha waislamu kupitia nchi wanazoishi. Askofu Dr. Owdenburg Moses Mdegella wa Kanisa la kiinjili la kilutheri Tanzania ni member wa Central Committee ya WCC.
Kwa wale wanaosema kuwa kila mtu anaweza kuajiriwa OIC bila kuangalia dini, angalia tangazo la kazi lililo live:
ref:http://www.oic-oci.org/oicnew/page_detail.asp?p_id=48
Hata kama nchi yako ni mwanachama ili kupata kazi ya maana katika OIC ni lazima uwe muislamu. Na kama umeoa, mke wako lazima awe muislamu. Kama ni mkristu au dini nyingine hautapata nafasi ya uongozi.
Kusema tena kuwa kinaongozwa na watu wasio wakali katika masuala ya dini si kweli! Katibu Mkuu wa sasa hivi ni Professor Ekmeleddin Ihsanoglu kutoka Turkey ambaye awali alikuwa akiongoza the Research Centre for Islamic History, Culture and Arts huko Istanbul.
OIC haijifichi kuwa ni shirika la kidini. Ni kujidanganya kusema vinginevyo. Ukiangalia hata kamati zake zimeundwa kulinda maslahi ya waislamu.
Kwangu mimi hili si tatizo. Tatizo ni kukataa kulizungumzia hata kama limeingizwa kisanii.
So what?
Wao wako wazi na jina lao linaonyesha hivyo. Tatizo letu Watanzania kuwa hili ni jumuiya ya Kiislamu au kuwa ni Jumuiya ya Kidini? Kama tatizo ni jumuiya ya Kiislamu basi na Tanzania ina Waislamu hivyo inawahusu Waislamu wa Tanzania na kama tatizo OIC ni jumuiya ya kidini basi tatizo liko wapi mbona Wananchi wa Tanzania wana dini hivyo wanahaki kujiunga na jumiya za kidini kama tunavyojiunga na jumuiya nyengine kwa magurupu yetu ndani ya jamii.
HILI SUALA LA UPANDE MMOJA FAIDA YAKE LAZIMA IKUBALIKE NA UPANDE MWENGINE HALITOTUPELEKA MBALI TUTAVUTANA BURE.