Ngonalugali
JF-Expert Member
- Jan 12, 2008
- 659
- 110
Nianze kwa kuwashukuru wana JF kwa kuwa pamoja katika jukwaa hili lisilokuwa na upendeleo kwa jamii.
Baada ya kusoma Biblia nilikutana na Sura moja katika Biblia inayosimulia kisa cha wana Israeli kudai mtawala juu yao. naomba tukisome kisa hiki kwa kuwa kuna mambo yana fanana sana na maamuzi ya Watanzania kumpitisha kikwete kwa kura nyingi huku wakidharau ushauri wa Baba wa Taifa. Kifupi ni kwamba baba wa taifa alifahamu uwezo wa ndugu kikwete ndo maana alimuangusha mwaka 1995. Lakini watanzania hilo hatukulijua, tukachukulia suala la umri kama kigezo, ila hicho hakikuwa kigezo halisi.
Habari hii imeanzia awamu ya nne ambayo sikuihusisha hapa kwa maana imelaumiwa kwa rushwa na kupindisha sheria. Kwa manufaa yako unaweza kusoma aya ya 1 - 3 ili kupata ujumbe sahihi.
Tusome:
Samwel 8:4-22
4.Ndipo wazee wote wa Israeli wakakutana pamoja, wakamwendea Samwel huko Rama; 5 wakamwambia, Angalia, wewe umekuwa mzee, na wanao hawaendi katika njia zako; basi tufanyie mfalme atuamue, mfano wa mataifa yote. 6 Lakini neno hilo likawa baya machoni pa Samweli, Waliposema tupe mfalme atuamue. Naye Samweli akamwomba BWANA. 7 BWANA akamwambia Samweli, Isikilize sauti ya watu hawa katika kila neno watakalokuambia; kwa maana hakukukataa wewe, bali wamenikataa mimi, ili nisiwe mfalme juu yao. 8 Kwa kadiri ya matendo yote waliyonitenda tokea siku ile nilipowatoa katika nchi ya Misri hata leo, kwa kuniacha mimi, na kwa kutumiakia miungu mingine, ndivyo wanavyokutenda wewe. 9 Basi sasa, isikilize sauti yao; walakini uwaonye sana, na kuwaonyesha desturi ya mfalme atakayewamiliki.
10 Naye Samweli akawaambia wale watu waliotaka mfalme maneno yote ya BWANA. 11 Akasema, mfalme atakayewamiliki ninyi atakuwa na desturi hii; atatwaa wana wenu na kuwaweka kwake, kwa magari yake, na kuwapanda farasi wake; nao watapiga mbio mbele ya magari yake. 12 Naye atawaweka kwake kuwa maakidajuu ya elfu, na maakida juu ya hamsini; na wengine atawaweka walime shamba lake, na kuvuna mavuno yake, na kufanyiza zana zake za vita, na vyombo vya magari yake. 13 Na binti zenu atawatwaa kuwa wafanyaji wa marhamu, na wapishi, na waokaji. 14 Atatwaa makonde yenu, na mashamba yenu ya mizabibu, na ya mizeituni, yale yaliyo mazuri sana, ili awape watumishi wake. 15 Naye atawatoza ushuru wa mbegu zenu na wa mizabibu yenu, awape maakida wake, na watumishi wake. 16 Atawatwaa watumishi wenu na wajakazi wenu, na ngombe zenu walio wazuri sana, na punda zenu, naye atawatia katika kazi zake mwenyewe. 17 Atawatoza fungu la kumi la makundi yenu; nanyi mtakuwa watumwa wake. 18 Nanyi mtalia siku ile kwa sababu ya mfalme wenu mliyejichagulia; BWANA asiwajibu siku ile. 19 Walakani hao watu wakakataa kuisikiliza sauti ya Samweli; wakasema, Sivyo hivyo; lakini tunataka kuwa na mfalme juu yetu; 20 ili sisi nasi tufanane na mataifa yote; tena ili mfalme wetu atuamue, tena atoke mbele yetu na kutupigia vita vyetu. 21 Samweli akayasikia maneno yote ya watu akayanena masikioni mwa BWANA, 22 BWANA akamwambia Samweli, Isikilize sauti yao, ukawafanyie mfalme. Kisha Samweli akawaambia watu wa Israeli, Enendeni kila mtu mjini kwake.
Nawakilisha!!!
Baada ya kusoma Biblia nilikutana na Sura moja katika Biblia inayosimulia kisa cha wana Israeli kudai mtawala juu yao. naomba tukisome kisa hiki kwa kuwa kuna mambo yana fanana sana na maamuzi ya Watanzania kumpitisha kikwete kwa kura nyingi huku wakidharau ushauri wa Baba wa Taifa. Kifupi ni kwamba baba wa taifa alifahamu uwezo wa ndugu kikwete ndo maana alimuangusha mwaka 1995. Lakini watanzania hilo hatukulijua, tukachukulia suala la umri kama kigezo, ila hicho hakikuwa kigezo halisi.
Habari hii imeanzia awamu ya nne ambayo sikuihusisha hapa kwa maana imelaumiwa kwa rushwa na kupindisha sheria. Kwa manufaa yako unaweza kusoma aya ya 1 - 3 ili kupata ujumbe sahihi.
Tusome:
Samwel 8:4-22
4.Ndipo wazee wote wa Israeli wakakutana pamoja, wakamwendea Samwel huko Rama; 5 wakamwambia, Angalia, wewe umekuwa mzee, na wanao hawaendi katika njia zako; basi tufanyie mfalme atuamue, mfano wa mataifa yote. 6 Lakini neno hilo likawa baya machoni pa Samweli, Waliposema tupe mfalme atuamue. Naye Samweli akamwomba BWANA. 7 BWANA akamwambia Samweli, Isikilize sauti ya watu hawa katika kila neno watakalokuambia; kwa maana hakukukataa wewe, bali wamenikataa mimi, ili nisiwe mfalme juu yao. 8 Kwa kadiri ya matendo yote waliyonitenda tokea siku ile nilipowatoa katika nchi ya Misri hata leo, kwa kuniacha mimi, na kwa kutumiakia miungu mingine, ndivyo wanavyokutenda wewe. 9 Basi sasa, isikilize sauti yao; walakini uwaonye sana, na kuwaonyesha desturi ya mfalme atakayewamiliki.
10 Naye Samweli akawaambia wale watu waliotaka mfalme maneno yote ya BWANA. 11 Akasema, mfalme atakayewamiliki ninyi atakuwa na desturi hii; atatwaa wana wenu na kuwaweka kwake, kwa magari yake, na kuwapanda farasi wake; nao watapiga mbio mbele ya magari yake. 12 Naye atawaweka kwake kuwa maakidajuu ya elfu, na maakida juu ya hamsini; na wengine atawaweka walime shamba lake, na kuvuna mavuno yake, na kufanyiza zana zake za vita, na vyombo vya magari yake. 13 Na binti zenu atawatwaa kuwa wafanyaji wa marhamu, na wapishi, na waokaji. 14 Atatwaa makonde yenu, na mashamba yenu ya mizabibu, na ya mizeituni, yale yaliyo mazuri sana, ili awape watumishi wake. 15 Naye atawatoza ushuru wa mbegu zenu na wa mizabibu yenu, awape maakida wake, na watumishi wake. 16 Atawatwaa watumishi wenu na wajakazi wenu, na ngombe zenu walio wazuri sana, na punda zenu, naye atawatia katika kazi zake mwenyewe. 17 Atawatoza fungu la kumi la makundi yenu; nanyi mtakuwa watumwa wake. 18 Nanyi mtalia siku ile kwa sababu ya mfalme wenu mliyejichagulia; BWANA asiwajibu siku ile. 19 Walakani hao watu wakakataa kuisikiliza sauti ya Samweli; wakasema, Sivyo hivyo; lakini tunataka kuwa na mfalme juu yetu; 20 ili sisi nasi tufanane na mataifa yote; tena ili mfalme wetu atuamue, tena atoke mbele yetu na kutupigia vita vyetu. 21 Samweli akayasikia maneno yote ya watu akayanena masikioni mwa BWANA, 22 BWANA akamwambia Samweli, Isikilize sauti yao, ukawafanyie mfalme. Kisha Samweli akawaambia watu wa Israeli, Enendeni kila mtu mjini kwake.
Nawakilisha!!!