Ndugu yangu Mkamap,
Jana kwenye post yangu nilidiriki kunukuu kwa urefu kabisa Katiba yetu inasemaje kuhusu swala hili la dini. Kulingana na Katiba yetu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, serikali haina dini, wala haijihusishi na masuala yoyote kuhusu dini, kwani Katiba inasema, mambo yote yanayohusu dini ni masuala ya mtu binafsi na hivyo serikali haitaingilia masuala hayo, hivyo basi suala la Serikali kujaribu kujiunga OIC au kujiingiza kwenye mchakato wa uanzishwaji wa Mahakama ya Kadhi ni kinyume na ukiukwaji wa Katiba. Kwa kifupi nanukuu tena Ibara (kifungu) ya 19 cha Katiba ya Jamhuri wa Mungano wa Tanzania:
19(1)- Kila mtu anastahili kuwa uhuru wa mawazo, imani na uchaguzi katika mambo ya dini, pamoja na uhuru wa mtu kubadilisha dini au imani yake.
19(2)- Kazi ya kutangaza dini, kufanya Ibada na kueneza dini itakua ni huru na jambo la hiari la mtu binafsi, na shughuli na uendeshaji wa jumuia za dini zitakuwa nje ya shughuli za mamlaka ya Nchi.
19(3)- Hifadhi ya haki zilizotajwa katika ibara hii itakua chini ya taratibu zilizowekwa na sheria ambazo ni muhimu katika jamii ya kidemokrasia kwa ajili ya usalama wa jamii, amani katika jamii maadili ya jamii na umoja wa kitaifa.
19(4)- Kila palipotajwa neno "dini" katika ibara hii ifahamike kwamba maana yake ni pamoja na madhehebu ya dini, na maneno mengineyo yanayofanana ua kuambatana na neno hilo nayo yatatafsiriwa kwa maana hiyo.
Hivyo basi, naomba kusisitiza kauli yangu kwamba, Katiba yetu ipo wazi kabisa kwamba serikali haina dini wala haijihusihi kwa namna yoyote na masuala ya dini, Kama ni kujiunga na OIC basi BAKWATA inaweza ikajiunga kama institution na sio Serikali ya Jamhuri wa Muungano wa Tanzania kujiunga kama Nchi.