Juu ya OIC na Mahakama ya Kadhi

Juu ya OIC na Mahakama ya Kadhi

Hivi siku rais akiwa Mkristo na mahakama hii ikiwa imeanzishwa atakuwa na udhu wa kumteua kadhi mkuu?Imani hapo inasemaje?
 
Magobe T, kama hatuuigi...tuweke week end Jumatatu na Jumanne, then siku zilizobaki zote tufanye kazi...otherwise ujue TUNAIGA....na sijui umwiga mnyama gani...
 
Mimi napinga hii Mahakama kwa sababu itaingilia uhuru wa mtu kuabudu anavyotaka. Ikiwa hata namna ya kum'define' muislamu inatusumbua sembuse kuwe na chombo kinachowashughulikia wao tu! Kwa nini huyo aliyezaliwa muislamu akatazwe na ahukumiwe kwa kuamua kunywa pombe, kula nguruwe n.k.? Kama anaonekana haendani na miiko ya dini yake kwa nini asitengwe tu? Kuna haja kweli kuwapeleka kifungoni watu wanaokula wakati wa mwezi wa ramadhan kwa mfano? Si wataadhibiwa watakapokutana na muumba wao?Hata kama walizaliwa waislamu? Na je hao watakaoamua kujitoa kwenye uislamu, adhabu yao nao iwe nini?

Mimi kama mkristu, nikiamua kuoa wake wengi wazi wazi, kanisa lina mamlaka ya kunitenga na madhehebu mengine wanakataa hata kunizika. Hii ni adhabu tosha bila kuhitaji baraka za serikali. Nitakuwa mpuuzi kama nitadai serikali iwape uwezo kanisa kunifunga kama nitaoa mwanamke zaidi ya mmoja.

Cha muhimu ni kuwaelimisha wananchi wetu haki zao chini ya sheria. Kama serikali inatambua ndoa ya kiislamu sioni kwa nini serikali hiyo ikatae kutoa shahada ya ndoa kwa mke wa pili hadi wa nne wa muislamu. Hawa wakinyimwa haki akifariki mume wao wanastahili kwenda mahakamani kudai haki yao. Si wanawake waislamu peke yao wanaodhulumiwa na ndugu na jamii punde mume anapofariki. Na mume ( wa dini yeyote) kama kweli anawapenda wake zake kwa nini asiache maandishi ya kugawa mali yake akiwa bado yu hai? Katika nchi yenye mgawanyiko kama wetu katika dini hizi ni muhimu kuwa serikali inajionyesha waziwazi haielemei upande wowote. Kuruhusu mahakama ya Kadhi kama inavyoombwa ni kujiingiza katika masuala ya dini. Kesho na kesho kutwa sitashangaa kama baadhi ya hao hao wanaodai hizi mahakama wakigeuka na kuzikana kwa sababu tu zilianzishwa kwa blessing ya serikali. kama ilivyo Bakwata.
 
hahaha kusilimisha itakuwa ngumu vatican nayo itakuwa haijalala ati.
kama nia ni kushinda uchaguzi Zanzibar inabidi wachambue kwa kina unaweza kupata hela nyingi kutoka uarabuni, na kushinda zanzibar !BARA je?wakristo nao watataka kuwaondoa katika uchaguzi ili waweze kuvunja mkataba wa kujiunga na IOC, then Kitakachofuata ni kuvunjika kwa Amani, TUNAHITAJI HEKIMA ZAIDI KULIKO KUNG'ANG'ANIA NI NANI KAJIUNGA NA NIFAIDA GANI KAPATA,

Serikali ya Tanzania haina dini ........period......... !!
yeyote anayezumgumzia udini ndani ya seriakli ikiwemo IOC hana tofauti na anayedai Zanzibar ni Sovereign State........

Bernard Membe anataka kugombea Urais na anataka cheap popularity toka kwa Waislam kama alivyowahi kufanya Mzee mmoja ambaye Mwalimu alimfutilia mbali pamoja na kusilimu kwake. This is my take ......be careful with politicians.......
 
Serikali ya Tanzania haina dini ........period......... !!
yeyote anayezumgumzia udini ndani ya seriakli ikiwemo IOC hana tofauti na anayedai Zanzibar ni Sovereign State........

Bernard Membe anataka kugombea Urais na anataka cheap popularity toka kwa Waislam kama alivyowahi kufanya Mzee mmoja ambaye Mwalimu alimfutilia mbali pamoja na kusilimu kwake. This is my take ......be careful with politicians.......

IOC haina masharti kwamba ukijiunga basi nchi yako iwe ya kidini

Nchi ambazo zinaona zinapata manufaa kujiunga kwenye hio IOC kwanini zisijiunge?

Ni kama Waislam wanapokua open minded na wanapowapeleka watoto wao kwenye shule za st

Wanawapeleka watoto wao sio kwamba wanataka kuwabadilisha dini bali wanafuata ubora wa shule.

Mimi kama Darwin sijui manufaa ya IOC ila kama kuna wanaojua wanifahamishe.
Na kama IOC ina manufaa kwa watanzania kwanini iwe dhambi Tanzania kujiunga kwenye IOC.
Au mnataka kuniambia kwamba hospitali Agha khan inawasaidia waislam tu?
Au KCMC inawasaidia wakiristo tu.
 
IOC haina masharti kwamba ukijiunga basi nchi yako iwe ya kidini

Nchi ambazo zinaona zinapata manufaa kujiunga kwenye hio IOC kwanini zisijiunge?

Ni kama Waislam wanapokua open minded na wanapowapeleka watoto wao kwenye shule za st

Wanawapeleka watoto wao sio kwamba wanataka kuwabadilisha dini bali wanafuata ubora wa shule.

Mimi kama Darwin sijui manufaa ya IOC ila kama kuna wanaojua wanifahamishe.
Na kama IOC ina manufaa kwa watanzania kwanini iwe dhambi Tanzania kujiunga kwenye IOC.
Au mnataka kuniambia kwamba hospitali Agha khan inawasaidia waislam tu?
Au KCMC inawasaidia wakiristo tu.

Mifano yako inahusu vitu vidogo visivyoweza kulinganishwa na nchi, wala haviwezi kufananishwa au kulinganishwa. Tusiwe biased, wakati tunakataa kufungua ubalozi wa Israel ndo wakati tunaotaka kujiunga na OIC!
 
Sahihisho:

Tafadhali waungwana hii jumuiya inaitwa OIC (English Speakers, na OCI kwa francophone) na sio IOC

Shukran
 
FM usihadae watu, nani aliitaka Bakwata?..Mwalim ndie source ya Bakwata, na hadi leo inalindwa na Serikali...Waislam walikuwa na chombo chao, EAMWS, Nyerere akaivunja, na akapandikiza racism...

Mahakama ya kadhi ..haiamui kesi ulizozitaja hapo juu, uliza uambiwe!!!

Waulize wanasheria wako hapo Mliman au ktk vigenge vyao wakuambie kuwa sheria za Kiislam(Allah revealed laws) zilivyokuwa makini kuliko man made laws... leo akija Mchundo inafaa kesho akija Ben haifai...
 
Kama walivyosema wenyewe kwenye web-site yao, OIC ni chombo kinachowaunganisha waislamu. Kipo kulinda maslahi ya waislamu. Sasa kwa nini tuone ugumu kusema hili? Watu hawapingi kwa sababu kiongozi wake ni muislamu au makao yake makuu yako kwenye nchi ya kiislamu. La hasha. Ni identity yake kama chombo cha waislamu ndiyo inayowatia uoga.

Cha kujiuliza, ni jee, kuna ubaya wa chombo cha kiislamu kutetea maslahi ya waislamu? Na je, kuna ubaya gani kwa nchi yetu yenye waislamu wengi tu, kujiunga na chombo ambacho kitaangalia na kutetea maslahi yake? Je hawa waislamu wetu wangeweza kupata uwakilishi katika chombo hicho kupitia namna nyingine? Ukweli ni kuwa, hamna, hiki chombo kinaunganisha nchi na si vinginevyo. Kama jumuia ya madola. Kama Umoja wa Mataifa. Bakwata na hata EAMWS ingekuwepo isingeweza kujiunga. Zanzibar haiwezi. Mji wa Pangani hauwezi. Ni nchi tuu ndiyo inayoweza.Kama tunawakubali hao waislamu kuwa sehemu ya jamii yetu kwa nini tukatae ku'facilitate' wao kuweza kupata neema? Tukiona kuwepo kwetu huko kuna wadhuru wasio waislamu si tutaweza kujitoa? Ni kama vile Tanzania kujiunga na FIFA wakati si raia wake wote wanaopenda au kucheza mpira! Au shirikisho la Netball wa dunia. Tatizo liko wapi? Kwa vile hakuna chombo kama hicho kwa wakristu, si sababu ya kukataa kujiunga. Kama OIC wana ajenda nyingine zaidi ya kuwasaidia wenye dini wenzao basi iwekwe wazi.

Nakubalkiana nawe moja kwa moja Fundi. Ni busara tu-facilitate matakwa ya wanaotaka kujiunga na OIC. Kwa kufanya hivyo, ndivyo Jamhuri ya Muungano itakuwa inatumia "sovereignity" yake kiuadilifu kukidhi matakwa ya watu wake wote na maslahi yao. Kwani kama kuna ukorofi si inaweza kuchukua hatua kudhibiti ukorofi huo (unaohofiwa). Sasa ya nini kuweka pingamizi au kuhofia ukorofi , amabao pengine hata haupo?
 
hahaha kusilimisha itakuwa ngumu vatican nayo itakuwa haijalala ati.
kama nia ni kushinda uchaguzi Zanzibar inabidi wachambue kwa kina unaweza kupata hela nyingi kutoka uarabuni, na kushinda zanzibar !BARA je?wakristo nao watataka kuwaondoa katika uchaguzi ili waweze kuvunja mkataba wa kujiunga na IOC, then Kitakachofuata ni kuvunjika kwa Amani, TUNAHITAJI HEKIMA ZAIDI KULIKO KUNG'ANG'ANIA NI NANI KAJIUNGA NA NIFAIDA GANI KAPATA,

Tusitumia hekima kwa hili la OIC peke yake. Kama pesa za Waarabu mbona tunachukua nyingi na hilo la kuvunjika kwa Amani hatulitambui? Mwarabu na Uislamu ni wale wale kwenye OIC au kiinchi pekee.
Tuna kasumba kuwa chochote cha Waarabu ni kibaya na kuona cha Papa Bush ndio halali.
Tulishaambiwa kuwa Wao wana Mambo yao ya Ndani na Wao walikwishajiunga huko basi kama Sisi hatutaki na tuwaachie Wao waendelee na kungoja misaada mibaya ya OIC. Kwa Sisi OIC haitufai basi hata Wao pia tuwaamulie?
 
Serikali ya Tanzania haina dini ........period......... !!
yeyote anayezumgumzia udini ndani ya seriakli ikiwemo IOC hana tofauti na anayedai Zanzibar ni Sovereign State........

Bernard Membe anataka kugombea Urais na anataka cheap popularity toka kwa Waislam kama alivyowahi kufanya Mzee mmoja ambaye Mwalimu alimfutilia mbali pamoja na kusilimu kwake. This is my take ......be careful with politicians.......

DU WADINI NYIE Mmmm?
 
Mifano yako inahusu vitu vidogo visivyoweza kulinganishwa na nchi, wala haviwezi kufananishwa au kulinganishwa. Tusiwe biased, wakati tunakataa kufungua ubalozi wa Israel ndo wakati tunaotaka kujiunga na OIC!

Maisha na faida za wananchi zinapatikana kwenye hivyo unavyoviita vitu vidogo. Ama hili la Israel sijui linakujaje hapa na sijui kakwambia nani uongo huo. Kaufanyie kazi tena.
Jee Israel inakuuma kwa dini au umpenzi wa ukatili na ukandamizaji. Iwapo dini basi Mayahudi wana dini yao si hiyo yako.
 
hili ndi lililoibua kizungumkuti wa zanzibar ni nchi au la mwaka 1993. tuachane nalo halitufai. nchi haina dini na tuache kuiga
 
FM usihadae watu, nani aliitaka Bakwata?..Mwalim ndie source ya Bakwata, na hadi leo inalindwa na Serikali...Waislam walikuwa na chombo chao, EAMWS, Nyerere akaivunja, na akapandikiza racism...

Mahakama ya kadhi ..haiamui kesi ulizozitaja hapo juu, uliza uambiwe!!!

Waulize wanasheria wako hapo Mliman au ktk vigenge vyao wakuambie kuwa sheria za Kiislam(Allah revealed laws) zilivyokuwa makini kuliko man made laws... leo akija Mchundo inafaa kesho akija Ben haifai...

Ndipo hapa ninaposhindwa kuwaelewa. Nani aliyewafanya nyie kuwa wasemaji wa waislamu WOTE? Siwezi kuamini kuwa ni waislamu WOTE walioikataa hiyo BAKWATA wakati ingalipo inadunda. Waiteni vibaraka wa serikali lakini msiwany'ang'anye uislamu wao!

Tusiingie kwenye validity ya hizo Sharia. Mimi si muislamu na kwa hiyo sheria inayosema mzinifu apigwe mawe hadi kufa siwezi kui'support' hata siku moja. Sheria inayosema kauli ya mwanamke ni pungufu kwa ya mwanaume siwezi kuikubali hata siku moja. Lakini mimi ni mmisheni. Si ajabu nikipinga.
 
Ngonalugali, jenga hoja ueleweke swala la imani mara zote linanyima uhuru wa kufikiri na kujadili kwa upeo mkubwa. Kwa yule ambae hana imani kama ya kwako inamuwia vigumu kuelewa unamaanisha nini.

Israel ni nchi nyingine na unazungumzia miaka zaidi ya elfu mbili iliyopita kwa akili ya kawaida ya kulinganisha haiwezekani. Waache watanzania wajifunze na kuchukua hatua kwa yanayowatokea leo na kwa mazingira waliyonayo. Hakuna haja ya kuwakatisha tamaa, ustaarabu wa leo vyovyote vile ni bora kuliko miaka hiyo, Imani tulizo letewa ndio zimetufikisha hapa tulipo, kutugandamizia tena huko huko si poa mtu wangu.

Kuna wenzio walinukuu verse hizo hizo kusema muungwana kachaguliwa na Mungu kuwaongoza wa bongo tena ni viongozi wa juu na wamehitimu dini kinoma. waache wabongo waone, wapime na wachukue hatua 2010 kwa discipline wanayoipata wala haitaji verse kutoka kokote.
 
mungu akubariki kwa kuliona hilo.Kusema ukweli sisi wanadamu tukimuacha mungu na kufuata njia zetu huwa yeye anajitoa maana mungu wetu ni wa demokrasia.
 
Comrade Mkandara,

Nimekupata vizuri, labda hukunielewa au hujui msimamo wangu uko wapi katika jambo hili.

Nauliza maswali ya msingi kwa kuwa hoja imekuwa ni lazima Tanzania ijiunge na OIC ili kulinda maslahi ya Waislamu. Sasa OIC ni ushirika wa Nchi za Kiislamu. Swali linakuja, je Tanzania ni nchi ya Kiislamu? majibu yanakuja Msumbiji na Uganda ni Wanachama lakini si kujibu kama Tanzania ni nchi ya Kiislamu au laa.

Ndipo nikauliza kuna shida gani basi kwa Tanzania kujiunga na World Council of Churches?

Swali si kuzuia Waislamu kama jumuiya kujiunga na kunufaika na OIC, suala ni ukingiza Tanzania kama nchi ambayo hakuna majority religion kuwa mwanachama wa Jumuia ya Nchi za Kiislamu!

Ndio maana nilipoleta mfano wa Marekani, Pakistani, Canada na India nilisema kama ni misaada, basi hata yao ina walakini kwa kuwa kuna umasikini.

Sasa umezungumzia jumuiya ya Watanzania Kanada, minnesota kuna jumuiya ya Watanzania Umoja society, kuna wanachama Wakenya, Waganda hata kutoka Rwanda. Hawa wameingia kwa utashi binafsi kwa kuwa jumuiya ni za mtu mmoja mmoja.

Kujiunga OIC ambayo lengo lake kuu ni umoja wa Kidini huku Tanzania si nchi iliyofungamana na dini na mgawanyo wa raia kidini ni sawa, huku ni kujitakia matatizo maana hakuna ridhaa ya wananchi.

Kama alivyosema mtoa haja mmoja mapema, hatuwezi kujifananisha na Msumbiji au Uganda kwa kuwa hatufahamu katiba zao au taratibu walizofuata wao kujinga na OIC.

Ubaya wa huu mjadala ni jinsi ulivyoletwa na kushinikizwa kwetu na Wanasiasa.

Inaelekea wazi kuwa kauli hizi za harakaharaka hazijafikiriwa na ni juhudi za kuhalalisha mambo fulani ya kisiasa kama nilivyosema hapo awali kuwa Kikwete anakuwa compromised na ku-succumb to blackmail ili fukuto la Muungano litulie.

Kama jinsi tatizo hili la kujiunga OIC lilitokea 1993 pamoja na Membe kudai kuwa Zanzibar na Diria walijiingiza kinyemela, bado kwa Tanzania kujiunga OIC kutaleta vurugu na kutokuelewana.

I wish we could sit down and resolve the Muungano issue first as a nation and then let other things like OIC and Kadhi fall in place after reconciliation and new constitution with Union or without union!

REV nakubaliana nawe na hoja zako nyingi kuwa Tanzania si nchi ya kidini lakini sifikiri kuingia jumuiya ya kidini ni kuvunja katiba,

Mtiririko wa matokeo hapa kwetu umenifunza jambo moja. Wengi wetu hukimbilia Katiba kwa lile tusilolipenda na tuko tayari kuikana na kuiponda Katiba hiyo hiyo kwa yale tunayoyajengea hoja. Pengine hapa utakubaliana nami kuwa tabia hii ni double Standard. Tumekuwa wa mbele kudai kubadilishwa Katiba kwa yale nyoyo zetu tunayapenda na kudai kuwa Katiba inataka marekebisho.
Aidha nafikiri msingi wa kuundwa Katiba ni kuuweka utaratibu unaokubalika na wengi. Tunapodai jambo lipigiwe kura tuna maana kupata idadi ya wanaounga mkono au kwa maana nyengine wale wanaoona kuwa jambo husika litawanufaisha.
Sioni sababu ya kudharau Waislamu kwa wingi wao na kudai jambo fulani ambalo litawanufaisha. Rev, unaposema kuwa mgawanyo wakidini ni sawa na hapo hapo ukabeza matakwa ya nusu hiyo kwa madai kuwa halina ridhaa sasa ridhaa ni ipi hapa? Ile ya nusu inayotaka au nusu isiyotaka ? Hivyo kati yetu na dini zetu kama tungekuwa na uhuru wa kuamuwa tunayotaka kidini nani hataki Tanzania iishi kidini yake? Kwa muda wote tumekuwa tukiishi kwa kustahamiliana na kuona kuwa mwenzangu akifaidika basi nami nitafaidika kwa jengine. Tunaishi kwa give and take na tunaishi kwa Amani.
Tatizo la watu wawili linakuja zaidi kwa mmoja kumkatalia mwenziwe asifaidike na kitu ambacho yule mwengine hana faida nacho wala hakina madhara nae.
Pengine Rev ungeonyesha madhara ambayo wataipata sehemu ya pili nafikiri Waislamu nao wangekuwa tayari kutilia maanani uhusiano wa kindugu na kuzuiya kuuvunja kwa kujiunga na OIC. Suala la kusema Katiba nafikiri halina hoja thabiti kwani ni Katiba hiyohiyo tunataka ifanyiwe marekebisho na hata hivyo nafikiri hakuna kipengele kinachokaza Tanzania kujiunga na Jumuiya kama ya OIC.
 
Ni kweli unachosema na hasa mawazo yako ndiyo yenye lengo la kibaguzi. Kinacholetwa hapa ni maoni na kila mtu ana maoni yake. Kwa nini maoni yasiyoendana na yako uone ni ya kibaguzi?

Hoja kwamba hata Nigeria ni mwanachama siyo hoja hata kidogo kwani ungeweza kusema pia kuwa mbona Kenya, Afrika Kusini au DRC siyo wanachama. Kwangu mimi swali ni kwa nini sisi kama Tanzania tunataka kujiunga na OIC. Kitu ambacho naweza kuhoji ni kwamba Tanzania imesaini The Universal Declaration of Human Rights wakati OIC hailitambui kwa vile siyo 'consistent with Sharia Law'.

Ila OIC inatambua The Cairo Declaration of Human Rights in Islam na Article 24 inasema: "All the rights and freedoms stipulated in this Declaration are subject to the Islamic Shari'ah" wakati Article 25 inasema: "The Islamic Shari'ah is the only source of reference for the explanation or clarification of any of the articles of this Declaration."

Swali langu ni kwamba kwetu sisi kuwa wanachama wa OIC ina maana kwamba na sisi pia tunazikubali hizi articles zilizotajwa hapo juu au tutaendelea na zile za Universal Declaration of Human Rights?

Na pili, tunajiunga kwa mambo yapi hasa? Haya yote yangewekwa wazi isije huko mbele tukaanza kuingizwa kwenye mikataba itakayoanza kuleta machafuko nchini.

Tatu, hakutakuwa conflict of interests hasa kwa vitu ambavyo ni 'fundamentals'? Naomba machango wenu.

Kama tatizo lako ni Article fulani ndani ya OIC hilo lisikupe wasiwasi kwani Jumuiya za Kimataifa hazilazimishi wanachama wake kufuata kila kilicho ndani ya Artcle bali kunakuwa na uhuru wa Reservation katika mambo yanayojadiliwa. Kipengele usichokikubali huwa hakikufungi na hizo ni sheria za Kimataifa.
Si ajabu ukaona hata Charter ya UN kuna baadhi ya wanachama hawavitambuwi baadhi ya vifungu.
Serikali nafikiri si mbumbumbu kama tunavyodai kwa yale tusiyoyapenda,
 
Back
Top Bottom