JK awapandisha vyeo majenerali

JK awapandisha vyeo majenerali

Na mimi leo Mmasai wangu wa home nampandisha cheo kuwa ten star General........ila mshahara uko palepale
 
Mmmh napita naogopa kuburuzwa,mambo ya Jeshi hayajdiliwi public!! meremeta!
 
Kwa uelewa wangu mdogo wa mambo ya Jeshi, alichofanya JK ni siasa ambazo hazieleweki na huko mbele zinaweza kutufungua macho au kutucost kama taifa. Suala la kuwa na vyeo gani jeshini si hoja ya rais mmoja tu kusema jeshi langu litakuwa na ma5 star general 3, 9 au 20. Kuna vigezo vya kijeshi ambavyo vinakubalika kimataifa. Na kigezo moja wapi na ukubwa na ubora wa jeshi. Kwa hadhi ya jeshi letu lilivyo kwa sasa tunasifa ya kuwa na 4star general mmoja, 3star mmoja na 2stars ambao ni major generals kama walivyosasa. Sasa unavyowapandisha hawa 2 na kuwa na 3 utajikuta unakuwa na 4 wawili na kutaka kuwa na 5mmoja wakati jeshi letu halina hadhi hiyo. Kwa Africa nzima nchi 2 tu ndoo zina 5star mmoja nazo ni Misri na Afrika kusini. Ukubwa na ubora wa majeshi ya nchi hizo pamoja na bajeti zao ni far from Tanzania. Twendeni mbele sio kwema. Siasa jeshini hazifai kuwa kubwa kwa kiasi hiki.
 
Phillemon Mikael: Kweli JF ni darasa tosha, maelezo yako hayo yamenifungua hata mimi macho ambaye niliishia tu JKT.

Mimi ninafikiri mambo kama haya inabidi sasa yaandikwe waziwazi kwenye katiba mpya, badala ya kutegemea BUSARA za RAIS kwani mara nyingine busara zinaweza zisiwe busara.

Sasa Ndomba ambaye alikuwa Junior amekuwa Lut. General na COS na hawa akina Makalala na Kisampa walikuwa Senior kwa Ndomba nao wamekuwa Lut. Generals lakini mwenzao ni COS. Je wakikutana nani anapaswa kumpigia mwenzake SALUTE? Watu wengi wanaweza kuona ni swali la kijinga, lakini kwa wale mliopitia JESHINIkidogo you know what SALUTE means to men and women in uniform.
Mkuu Lt Gen Ndomba ni senior kwa wote maana yeye aliwatangulia kuukwaa Uluteni Gen, wata salute kwake!!!

 
Tujaribu kuwa waelewa na wepesi wa kupambanua mambo Jeshini kuna Vyeo na Madaraka pia hata Jeshi la Polisi pia kuna Vyeo na Madaraka kwa mfano Ma RPC karibu wote ni Ma Senior Assisstant Commissioners of Police ingawa wapo wenye nafasi Vyeo chini ya hapo ama juu ya hapo.

Kwa Jeshi la Wanainchi tulikuwa na utaratibu wa kuwa na Luteni Jenerali mmoja tu ambae ndiyo anakuwa ni Afisa Mnadhimu Mkuu wa Jeshi na Meja Jenerali wengi wanakuwa wakuu wa Vitengo sasa inafika wakati una Meja Jenerali Watano na wote wanastahiki kuwapandisha cheo lakini madaraka wanayotakiwa kuyashika iko nafasi moja kimsingi utaangalia vigezo vingi sana mpaka umpate mmoja ambae utmteua na kumpandisha cheo kushika madaraka husika ila hautatenda haki kama wengine wanaostahili kupandishwa cheo hawatapandishwa cheo, nafasi ya kuwalipa stahiki zao kama ipo basi huna haja ya kuwanyima cheo husika ila madaraka yatabaki kwa mtu mmoja ambae umemteuwa kushika madaraka husika.

Hivi sasa watu wamejenga utaratibu usio rasm wakumbeza Mheshimiwa Raisi kila anapofanya uteuzi mara oohooo hakuzingatia sifa za wateuliwa mara aliowateua hawana elimu stahiki mara amewateua waislam watupu mara ameteua marafiki zake tuu hii imejijenga kuwa tabia miongoni mwetu tena ni tabia mbaya ambayo haina mfano.

Mimi namfahamu sana Luteni Jenerali Makakala mpaka famillia yake karibu yote iliyopo Kijiji cha Ndengere na Mbamba Bay ila miaka ya karibuni Luteni Jenerali huyu amejiunga na Dhehebu la KILOKOLE sasa angeweza kuwa Afisa Mnadhimu Mkuu kabla ya Luteni Jenerali Ndomba ambao wote hawa wanatoka Mkoa wa Ruvuma tena hapo mwanzo walikuwa wanatoka Wilaya moja ya Mbinga kabla ya kutenganishwa na kuwa na Wilaya ya Nyasa ambako Makakala ndiko anakotoka.

Hivyo basi Ulokole wa Makakala ndiyo umempunguzia saifa ya ziada kumbuka Jeshini kuna kitengo cha Ujasusi cha Jeshi[Military Intelligence Unit] ambacho kina kazi ya ziada ya kuwachunguza Maofisa wa Jeshi mienendo yao ya kila siku na kuripoti moja kwa moja kwa Mkuu wa Majeshi hivyo tusilaumu kila uteuzi maana vigezo vingine vinavyotumika ni vigumu kuvitambua. Jeshi ni Taasisi nyeti ambayo inafanya mambo yake kwa utaratibu na tamaduni zinazoeleweka.

Jeshi siyo Chama cha siasa vinginevyo tungekuwa hatuishi kwa amani hapa angalia mifano ya Nchi kama Mali kila siku Jeshi ni kupindua tu Serikali halali ni kwa sababu hawana utaratibu tusilaumu hovyo hovyo!
mkuu haya majamaa yametumwa kazi moja tu humu. ni kumtukana na kumlaumu tu JK. siku hizi wala huwa siyafikirii tena na hata ukiyaeleza hayataelewa. yanatembea utadhani yana vichwa sehemu ya juu ya miili yao kumbe ni vifuu vya nazi.
 
Mkuu inamaana kama kuna watu 20 wenye sifa ya kuwa Rais tuwe na Marais 20 na mmoja mwenye mamlaka? Nadhani tunachobishana sio nani kapewa nini, ni kuwe na mfumo unaohitaji kuongozwa na mtu wa cheo fulani halafu ndio anatafutwa, sio kuundia watu kazi.

Pili umesema kuna mtu kanyimwa cheo kwa sababu ya ulokole, kwa mtazamo wangu huo ni ubaguzi, kama mtu hafai kuwa mwanajeshi basi toka cheo cha luteni usu asingepewewa na systems ilipaswa kumtoa mapema, sasa amefika hadi jenerali wa nyota 2 bado mna mashaka naye tena kwa imani yake? (kama ni kweli).

Ninaimani sikueleweka sana kwako vyeo Jeshini vipo vingi ila inapofika kwenye madaraka ni lazima mmoja wenu awe ndiye Mkuu,kwa mfano wapo wakuu wengi wa vitengo ndani ya jeshi wana vyeo vinavyofanana na wasaidizi wao ila ipo tofauti kidogo ya "Seniority" Tukichukua mfano halisi wa hawa MaLuteni Jenerali watatu Ndomba , Ryoba na Makakala wote walikuwa MaMeja Jenerali lakini ambao walikuwa Senior ni Makakala pamoja na Ryoba.

Meja Jenerali Ndomba alikuwa Junior kwa wenzake sasa baada ya Luteni Jenerali Abdulrahman Shimbo kustaafu kwa mujibu wa sheria Mheshimiwa Raisi akaamua sasa kumteua Meja Jenerali Ndomba ambae alikuwa Mkuu wa JKT kuwa Afisa Mnadhimu Mkuu wa Jeshi wakati huohuo akampandisha Cheo kuwa Luteni Jenerali ili aendane na madaraka sasa aliyokuwa nayo na Mheshimiwa Rais alipowapandisha Cheo Luteni Jenerali Makakala na Riyoba wao bado wanabaki na nafasi zao walizokuwa nazo na Mnadhimu wao sasa ni Luteni Jenerali Ndomba ambae ni Senior kwao ingawa mwanzo alikuwa Junior kwao. Madaraka na Cheo katika Jeshi ni vitu viwili tofauti tusivichanganye.
 
Inaamana huyu Muheshimiwa Amiri jeshi mkuu amejitungia tuu vyeo vya kijeshi hapo katikati ndio maana mambo ya namna ya kutoa vyeo kwenye idara nyeti za serikali ziwekwe kwenye katiba ona sasa tuna Raisi anaitia najisi katiba anafanya mambo kinyume kabisa vyuo vikuu anafanya afanyavyo, usalama wataifa mabest tu wake, mahakama yeye anavurunda ,mawaziri ndio usisema ,jeshi la polisi mama wewe wakuu wa mikoa na wilaya vimwana kwa kwenda mbele , tunakazi kabisa nadhani kuna umuhimu wa mambo haya kuwekwa vizuri
 
sielewi kitu hapo kwenye majina ya hayo mavyeo..but i can guess the more mavyeo unapata jeshini the more guns you own

Umenifurahisha sana mkuu, hapa kwangu haya ma vyeo ni giza totoro, inanikumbusha enzi za sekondari kwenye mtihani wa hesabu ( mathematics) unaona wenzako wanaomba four figure ila wewe kwa kuangalia swali la kwanza hadi la mwisho huoni pahala pa kutumia four figure.
 
JKT nini na JWTZ nini??:confused2:

Viongozi wengi walio JKT ndio sasa hivi Wanalishikila JWTZ na WENGI wa JWTZ hawafurahii UAMUZI huo
Mfano MKUU WA MAJESHI ni wa JKT - ALisha kuwa MKUU wa KIKOSI MAKUYUNI ARUSHA
Afisa Utawala NDOMBA -- JKT Wanadai kuwa hawana MAFUNZO kama walio JWTZ waliyonayo; MASELULE walipokuwa JKT walikuwa wanahepa MAFUNZO MENGI TU na kulikuwa hakuna MSISITISO kwao
 
JKT nini na JWTZ nini??:confused2:


Dah mi mwenyewe nimeshindwa kumuelewa mkuu nngu007 alikua ana maana gani. Au MOI(Muhimbili Orthopedic Institute) na MNH(Muhimbili National Hospital) zina tofauti?? Ipi bora?
 
Last edited by a moderator:
Dah mi mwenyewe nimeshindwa kumuelewa mkuu nngu007 alikua ana maana gani. Au MOI(Muhimbili Orthopedic Institute) na MNH(Muhimbili National Hospital) zina tofauti?? Ipi bora?

Kama Ulikwenda JKT unajua MAAFANDE wengi na Wakuu wa VIKOSI walikuwa Wanahepa Sana KOZI za UONGOZI MONDULI na UKIONGEA na yoyote wa JWTZ atakuambia wa JKT ni VILAZA walikuwa wanahepa KOZI kibao
 
Hemed Maronda, ngwendu, gobore, Phillemon Mikael,

..JK akiendelea namna hii itafika mahali tutalazimika kuwa na FIELD MARSHAL ktk jeshi letu.

..sote tunapaswa kuelewa kwamba CHEO/RANK ndiyo inayompa final say mhusika yeyote yule jeshini.

..waliofanya uamuzi kwamba CDF na COS wawe na vyeo vya Jenerali, na Luteni Jenerali, na no other active soldier should have those ranks walikuwa na busara zao.

..je, leo hii ikitokea kwamba Lt.Gen.Ndoma ana-retire au kwa namna moja au nyingine hawezi kuendelea na wadhifa huo, what is going to be the rank of the COS will replaces him??

..Je, JK atalazimika kumteua Makakala au Ryoba kuwa COS kutegemea nani ndiyo senior Lt.Gen?? Je, the incoming COS itabidi awe na cheo cha Jenerali ili aweze kutoa amri kwa Makakala na Ryoba? Au, Makakala na Ryoba wastaafishwe toka jeshini hata kama hawajafikia umri wa kustaafu?

..kwa kweli uamuzi huu wa JK umeniacha na maswali mengi sana.
 
Last edited by a moderator:
Mkuu nngu007 unavyouliza hivyo kuna watu ambao hawana elimu yoyote kuhusu jeshi hivyo utaona wanaanza kukukosoa, bila kujua kuwa JKT ni moja ya components za JWTZ....we subiri tu muda si mrefu utaona.[QUOTE=nngu007;5160318]Finally, Hakuna WA JKT... WOTE ni JWTZ!!![/QUOTE]
 
..Huyu kazoea kudanganywa, yaani hata akiambiwa kesho anatakiwa kwenda kufungua mashindano ya mbuzi kule Lindi, yaliodhaminiwa na Sultan wa Omani atakwenda mbio na hatauliza akikuta sio mbuzi bali ni simbrisi !!!

Kaka Huu ni mwendelezo wa uteuzi za kijikosha.....hawa wawili ndio walikuwa maj generals senior kuliko wote....active Jeshini .....kiutaratibu mmoja wao lazima alikuwa awe chief of staff...na likely ilikuwa awe Makalala...kwa kuwa mbinu ya kawaida ya kumuhamishia senior Riyoba ikulu ...ofisi ya PM...pia ni option pale ambapo unataka kumkwepesha kuwa CoS kwa wakati husika.
kitendo cha Ndomba kurushwa...na kuwaruka hawa...kilileta minongono...miongoni mwa majenerali na senior commenders........naona Mkuu anajikosha at the expense ya kuvuruga utamaduni...ni udhaifu Huu
 
Mkuu nngu007 unavyouliza hivyo kuna watu ambao hawana elimu yoyote kuhusu jeshi hivyo utaona wanaanza kukukosoa, bila kujua kuwa JKT ni moja ya components za JWTZ....we subiri tu muda si mrefu utaona.
Finally, Hakuna WA JKT... WOTE ni JWTZ!!!
Sisi wengine ni waajiriwa wa majeshi hato JkT mwajiri wake ni wizara ya ulinzi na jeshi lakujenga taifa katika idara ya mafunzo ya kijeshi na uzalishaji mali ambapo walioajiliwa wana status moja na wa JW kwa maana MT,MTM,P!JW ni idara ya ulinzi wanchi na mipaka yake na wenyewe ni status yao ni MT,MTM,P,JKU wote wapo katika wizara mama wizara ya ulinzi!Sasa unaposema JKT tofauti na JW si kweli course unazosema ni zile za senior leader course wanaenda Iringa,Makongo sitakutajia Kj kwasababu===IMEZUILIWA====!Hivyo wote ni waajiriwa jeshi la ulinzi la tanzania ni idara ndizo zina watenganisha!!Kwa hayo machache ndugu nngu007 utakuwa umenisoma hata Thanda
 
Last edited by a moderator:
Sisi wengine ni waajiriwa wa majeshi hato JkT mwajiri wake ni wizara ya ulinzi na jeshi lakujenga taifa katika idara ya mafunzo ya kijeshi na uzalishaji mali ambapo walioajiliwa wana status moja na wa JW kwa maana MT,MTM,P!JW ni idara ya ulinzi wanchi na mipaka yake na wenyewe ni status yao ni MT,MTM,P,JKU wote wapo katika wizara mama wizara ya ulinzi!Sasa unaposema JKT tofauti na JW si kweli course unazosema ni zile za senior leader course wanaenda Iringa,Makongo sitakutajia Kj kwasababu===IMEZUILIWA====!Hivyo wote ni waajiriwa jeshi la ulinzi la tanzania ni idara ndizo zina watenganisha!!Kwa hayo machache ndugu nngu007 utakuwa umenisoma hata Thanda

Mwajiri wa MAGEREZA na MGAMBO ni WIZARA ya ULINZI lakini Woote wanapewa MAFUNZO tofauti; Nakumbuka kuwa MAOFISA wa JKT MFANO MAJOR kozi anazokwenda sio sawa na kozi anazokwenda MAJOR JWTZ pamoja na kuwa MWAJIRI ni MMOJA...
 
Nafikiri Mkuu tuko pamoja labda kama tofauti hapo ni hilo neno "components"....ila tuko pamoja.

Sisi wengine ni waajiriwa wa majeshi hato JkT mwajiri wake ni wizara ya ulinzi na jeshi lakujenga taifa katika idara ya mafunzo ya kijeshi na uzalishaji mali ambapo walioajiliwa wana status moja na wa JW kwa maana MT,MTM,P!JW ni idara ya ulinzi wanchi na mipaka yake na wenyewe ni status yao ni MT,MTM,P,JKU wote wapo katika wizara mama wizara ya ulinzi!Sasa unaposema JKT tofauti na JW si kweli course unazosema ni zile za senior leader course wanaenda Iringa,Makongo sitakutajia Kj kwasababu===IMEZUILIWA====!Hivyo wote ni waajiriwa jeshi la ulinzi la tanzania ni idara ndizo zina watenganisha!!Kwa hayo machache ndugu nngu007 utakuwa umenisoma hata Thanda
 
Mwajiri wa MAGEREZA na MGAMBO ni WIZARA ya ULINZI lakini Woote wanapewa MAFUNZO tofauti; Nakumbuka kuwa MAOFISA wa JKT MFANO MAJOR kozi anazokwenda sio sawa na kozi anazokwenda MAJOR JWTZ pamoja na kuwa MWAJIRI ni MMOJA...
Mkuu wewe unaishi nchi gani nisije nikawa na bishana na mtu anaishi algeria asiyejua nini mahudhi!!Hivi kweli unathubutu kusema,Mwajiri wa MAGEREZA na MGAMBO ni WIZARA ya ULINZI,??Nakusaidia Mgambo hawana wizara wapo wizara ya ulinzi kama jeshi la akiba kwakuwa hawalipwi mshahara hivyo si waajiriwa wawizara ya ulinzi ila wakati wa operation mambo yao ushughulikiwa na wizara ya ulinzi!1Magereza wao wameajiriwa na wizara ya mambo ndani ya nchi pamoja na Polisi,Immigration mpaka hapo utakuwa uko na mimi!!Swali????
 
Mwajiri wa MAGEREZA na MGAMBO ni WIZARA ya ULINZI lakini Woote wanapewa MAFUNZO tofauti; Nakumbuka kuwa MAOFISA wa JKT MFANO MAJOR kozi anazokwenda sio sawa na kozi anazokwenda MAJOR JWTZ pamoja na kuwa MWAJIRI ni MMOJA...

Inaonekana kabisa uelewa wako wa haya masuala ni mdogo sana, maa umeshindwa kutofautisha hata mwajiri wa MAGEREZA na MGAMBO.

Jeshi la Magereza, Polisi, Uhamiaji na Zimamoto yako chini ya Wizara ya Mambo ya ndani, hivyo askari wa majeshi hayo mwajiri wao ni Wizara ya Mambo ya ndani kupitia hizo idara. JWTZ, JKT na MGAMBO wana simamiwa na wizara ya Ulinzi. Mafunzo na vyuo wanavyoenda makamanda wa JWTZ, JKT na MGAMBO ni sawa na kwa Standard ili ile. JKT ni sehemu ya JWTZ, hali kadharika MGAMBO.
 
Mpaka sasa jk hajateua wajumbe wa cc. Unajua ni kwa nini aliahirisha mpaka mwakani kinyume na katiba ya chama chake?
.
 
Back
Top Bottom