JK awapandisha vyeo majenerali

JK awapandisha vyeo majenerali

Yeye atapandishwa cheo lini kutoka kwenye uluteni kanali wake ambao hata hivyo huwa hapendi kuutumia zaidi ya udaktari wa kuchakachuliwa na kupewa?
kama wala hata hataki kujiita wala kuitwa kwa vyeo vya kijeshi ila watu wanamlaumu kuwa dikteta,sasa akiitwa kwa vyeo vya kijeshi,utasikia,hatutaki utawala wa kijeshi sie! mwanadamu anaisha maneno?
 
Tujaribu kuwa waelewa na wepesi wa kupambanua mambo Jeshini kuna Vyeo na Madaraka pia hata Jeshi la Polisi pia kuna Vyeo na Madaraka kwa mfano Ma RPC karibu wote ni Ma Senior Assisstant Commissioners of Police ingawa wapo wenye nafasi Vyeo chini ya hapo ama juu ya hapo.

Kwa Jeshi la Wanainchi tulikuwa na utaratibu wa kuwa na Luteni Jenerali mmoja tu ambae ndiyo anakuwa ni Afisa Mnadhimu Mkuu wa Jeshi na Meja Jenerali wengi wanakuwa wakuu wa Vitengo sasa inafika wakati una Meja Jenerali Watano na wote wanastahiki kuwapandisha cheo lakini madaraka wanayotakiwa kuyashika iko nafasi moja kimsingi utaangalia vigezo vingi sana mpaka umpate mmoja ambae utmteua na kumpandisha cheo kushika madaraka husika ila hautatenda haki kama wengine wanaostahili kupandishwa cheo hawatapandishwa cheo, nafasi ya kuwalipa stahiki zao kama ipo basi huna haja ya kuwanyima cheo husika ila madaraka yatabaki kwa mtu mmoja ambae umemteuwa kushika madaraka husika.

Hivi sasa watu wamejenga utaratibu usio rasm wakumbeza Mheshimiwa Raisi kila anapofanya uteuzi mara oohooo hakuzingatia sifa za wateuliwa mara aliowateua hawana elimu stahiki mara amewateua waislam watupu mara ameteua marafiki zake tuu hii imejijenga kuwa tabia miongoni mwetu tena ni tabia mbaya ambayo haina mfano.

Mimi namfahamu sana Luteni Jenerali Makakala mpaka famillia yake karibu yote iliyopo Kijiji cha Ndengere na Mbamba Bay ila miaka ya karibuni Luteni Jenerali huyu amejiunga na Dhehebu la KILOKOLE sasa angeweza kuwa Afisa Mnadhimu Mkuu kabla ya Luteni Jenerali Ndomba ambao wote hawa wanatoka Mkoa wa Ruvuma tena hapo mwanzo walikuwa wanatoka Wilaya moja ya Mbinga kabla ya kutenganishwa na kuwa na Wilaya ya Nyasa ambako Makakala ndiko anakotoka.

Hivyo basi Ulokole wa Makakala ndiyo umempunguzia saifa ya ziada kumbuka Jeshini kuna kitengo cha Ujasusi cha Jeshi[Military Intelligence Unit] ambacho kina kazi ya ziada ya kuwachunguza Maofisa wa Jeshi mienendo yao ya kila siku na kuripoti moja kwa moja kwa Mkuu wa Majeshi hivyo tusilaumu kila uteuzi maana vigezo vingine vinavyotumika ni vigumu kuvitambua. Jeshi ni Taasisi nyeti ambayo inafanya mambo yake kwa utaratibu na tamaduni zinazoeleweka.

Jeshi siyo Chama cha siasa vinginevyo tungekuwa hatuishi kwa amani hapa angalia mifano ya Nchi kama Mali kila siku Jeshi ni kupindua tu Serikali halali ni kwa sababu hawana utaratibu tusilaumu hovyo hovyo!
 
Mkuu yeye alishatoka huko jeshini.

Hongereni sana Lt. Gen. Ryoba na Lt. Gen. Makakala. Naona tunazidi kusonga mbele. Huko nyuma jeshini kulikuwa kwa kawaida kuna Four-Star General (CDF) mmoja na Three-Star General mmoja (CoS) lakini sasa naona tuna Four Star General mmoja na three star generals watatu mmoja akiwa ni CoS. Tuendako huenda tukapata general of the army (five-star general) na hivyo four-star generals kuwa wengi pia.

Mkuu inaelekea wewe kama siyo mwanajeshi basi umekaa line za jeshi maana unavijua vyeo vya jeshi balaa. Naomba kama unajua unifafanulie hiki cheo kipo kwenye jeshi la marekani kinaitwa ADMIRAL kinafanana na cheo gani maana mfumo wao wa vyeo unafanana na wetu TPDF

mimi mwenyewe ni kamanda nipo makutu cheo changu ni koplo jenerali
 
Du!kikwete kanichinja tena Maj.General mwakitobile,bora niingie msituni tu.
 
Ndio maana baadhi yetu tunapendekeza kwenye katiba mpya madaraka ya Rais yapunguzwe.

Ilipaswa kuwa na muundo unaotaka wawepo hao maluteni jenerali na sio tu watu wanapandishwa vyeo kwa kuwaangalia, sasa mmoja ameshatoka jeshini (sina hakika kama kitengo cha maafa ni sehemu ya jeshi) halafu anapandishwa cheo!

Zaidi zaidi ni kupata mafao ya uleteni general ukistaafu na ni gharama kwa walipa kodi. Hata hivyo kwa utaratibu wa Jeshi Ndomba ni senior kwa hawa aliwatangulia kupata hiki cheo!

Hujasikia mwanajeshi mkuu wa mkoa anapandishwa cheo?
 
Tujaribu kuwa waelewa na wepesi wa kupambanua mambo Jeshini kuna Vyeo na Madaraka pia hata Jeshi la Polisi pia kuna Vyeo na Madaraka kwa mfano Ma RPC karibu wote ni Ma Senior Assisstant Commissioners of Police ingawa wapo wenye nafasi Vyeo chini ya hapo ama juu ya hapo.......!

Mkuu mbona unazunguka sana mara ooh makalala ni mlokole ooh ni mnyasa, Ngoja nikuambie mkuu vyeo vyote kuanzia lans coplo mpaka kanali ambavyo vinasimamiwa na jeshi lenyewe vina utaratibu wake kisheria katika jeshi vikiangalia nidhamu, muda uliolitumikia jeshi, elimu, utumishi uliotukuka nk.

Ila kuanzia brigadier jen na kuendelea vyeo vinatoka ikulu na kigezo kikubwa ni mchango wako kwa CCM, yaani ukionekana hawawezi kukupa mabomu ya CCM ujilipue kama yale aliyovaa shimbo basi sio hupewi madaraka tu hata cheo utachelewa kupanda. Kama utaitetea CCM kufa na kupona hata ikiwezekana nyeusi kuiita nyeupe mchana mbele ya kadamnasi unaweza kutoka koplo kuwa jenerali.

Nakubaliana na wewe kuwa Ulokole wa makalala umechangia kwa kiasi kikubwa sana kumnyima COS kwa sababu wanajua hataweza kusema uongo kama shimbo, hawataweza kumuhusisha kwenye mchakato wa kuiba kura 2015. watu wa namna hii wanatengwa hadi usalama wa taifa saa hizi
 
Mkuu unaweza kuwa na mafour hata masix-star generals lakini kumshikisha mtu adabu ni mchakato!

Mkuu Lazima Tulinde Mipaka yetu,Mimi kila siku nashangaa sana, mtu anawezaje kulazimisha ziwa lililoko mpakani kuwa lote ni la Malawi!! Ngumu sana kumeza, yaani hata akili za kawaida tu zinakuwezesha kufikirikuwa huu ni ujinga,Ziwa wamelikuta, Mungu ameliweka pale, yaani hawaoni kuwa jirani anayo haki. Yaani wazungu waliotutawala ndio wanatulazimisha mipaka, sisi wenyewe hatuna busara za kuamua.
 
Mkuu kwani wewe ulitaka JK afanyaje?


Muundo wa Jeshi letu kwa sasa unatoa nafasi moja tu ya General aliyekazini ambaye anakuwa Mkuu wa majeshi....

Luteni Generali mmoja tu ambaye anakuwa Mnadhimu mkuu wa Majeshi[chief of staff]

Ukiangalia historia ya majeshi ya ulinzi ...zamani wakatI Wanaanza mkuu wa majeshi alikuwa anakuwa ana cheo cha Brigedia Generali...[Waliohudumu kwa cheo hicho ni Mrisho Sarakikya......na Baadaye Twalipo]

Miaka ya 1978 wakati tunaingia vitani ...mahitaji ya kuwa na devision zaidi yakaongezeka hapo ndipo Twalipo akapandishwa cheo kuwa luteni Generali ...na chini yake wakateuliwa mameja jenerali...kama David Musuguri,Tumainiel Kiwelu ,Chipeta,Walden,Mwita Marwa,Mwakalindile,Mayunga etc...
So muundo wa jeshi upo kama PYRAMID ....
Hii ni mara ya kwanza kwa nchi yetu kuwa na ma Luteni Generali watatu au wanne hapa chini....ngazi ya pili ya utawala na wote wakawa wapo kazini..hata kama mtasema cheo ni kimoja lakini madaraka yapo kwa mmoja.....


Uteuzi wa Heshima

Huko nyuma kuna ambao wamepewa uteuzi wa heshima ...lakini huu hufanyika siku wanapostaafu[siku moja kabla au hata baada ya kustaafu]

Mwalimu Nyerere ....alimpandisha cheo mkuu wa majeshi [enzi hizo ] Luteni generali Twalipo kuwa Generali na Kumteua maj generali msuguri hapo hapo kuwa Mkuu wa Majeshi..

Rais Mwinyi alimteuwa luteni Generali Tumainiel Kiwelu ..kuwa Generali siku alipokuwa anastaafu...kama heshima kwa kutumikia cheo hicho muda mrefu kwa nyakati tofauti..na kumteua Maj Generali Mboma kuwa Mkuu wa Majeshi na Generali siku hiyo hiyo[ kwenye historia Generali Tumainiel Kiwellu ndio pekee mwenye cheo hicho ambaye hakupata kuwa Mkuu wa Majeshi]

Rais Mkapa ...alimpandisha cheo kwa heshima Brigedia Generali Mrisho Sarakikya Kuwa Generali wakati wa maadhimisho ya miaka 45 ya majeshi ..kwa kuwa ndie Mkuu wa majeshi pekee mstaafu ambaye alikuwa hajavaa cheo cha General...[na hii kijeshi ilikuwa inampa unyonge mbele ya wanafunzi wake mwenyewe]...inakumbukwa kuwa Gen Sarakikya kwa shukrani alimwaga machozi ya furaha wakati anavalishwa cheo kipya na mkapa......ikionesha kijeshi ni kweli alikuwa anasononeka.

UTEUZI WA KURUKA

Uteuzi wa kuruka kama aliofanya JK kwa Ndomba kuwaruka ...Riyoba,Makalala na Kisampa ..unakubalika ..,lakini katika tawala zilizopita walichokuwa wanafanya ni kuwapangia kazi nyingine serikali secondment....pamoja na kuwa kiutaratibu hawa bado ni active combat commanders...ie Ubalozi,Ikulu[mshauri wa rais ulinzi au maafa],au Nje ya nchi...]...katika hili tayari alikuwa ameshafanikiwa kuwapangia kazi watu kama Riyoba[ikulu] ,Kisampa [nje]........na kama alitaka kuwapandisha cheo kwa heshima tu...angeweza kusubiri siku wanafikia kustaafu na kuwapandisha...ili kuondoa contradiction kwenye mfumo..


Pamoja na kukubali kuwa waliopanda wana sifa na wanastahili...hapa kikubwa tunachojadili ni mfumo na muuondo na haja ya katiba mpya kuweka hizi ngazi rasmi..jeshini
.
 
Nipo comrade,,, nlikua kwny blog moja ya wakenya nlikua nawaharibia siku asbh na mapema kuhusu mambo yao ya uchaguzi

Mm nawapongeza hawa wakuu.., hawa wote ni vifaa vilivyoiva sana kijeshi.., makakala ndio mkuu kunduchi pale, kile chuo kipya

Hongera zao mkuu ingawa hawa mageneral wote wanakwenda kutumika wapi? Tusiwaache wawe wanazagaa zagaa tu bila kitu cha kufanya...vyeo viwe vinaendana na kazi wanazoenda kufanya ili watumike ipasavyo...
 
Mkuu Phillemon Mikael ufafanuzi mzuri nimekuelewa vyema bila chenga.



Muundo wa Jeshi letu kwa sasa unatoa nafasi moja tu ya General aliyekazini ambaye anakuwa Mkuu wa majeshi....

Luteni Generali mmoja tu ambaye anakuwa Mnadhimu mkuu wa Majeshi[chief of staff]

Ukiangalia historia ya majeshi ya ulinzi ...zamani wakatI Wanaanza mkuu wa majeshi alikuwa anakuwa ana cheo cha Brigedia Generali...[Waliohudumu kwa cheo hicho ni Mrisho Sarakikya......na Baadaye Twalipo]....
 
Luteni Jenerali huyu amejiunga na Dhehebu la KILOKOLE sasa angeweza kuwa Afisa Mnadhimu Mkuu kabla ya Luteni Jenerali Ndomba ambao wote hawa wanatoka Mkoa wa Ruvuma tena hapo mwanzo walikuwa wanatoka Wilaya moja ya Mbinga kabla ya kutenganishwa na kuwa na Wilaya ya Nyasa ambako Makakala ndiko anakotoka. Hivyo basi Ulokole wa Makakala ndiyo umempunguzia saifa ya ziada !

Boss hapa ndo umenifungua macho, Jeshini hakuna dini? je Jeshi linapingana na katiba ya uhuru wa kuabudu..ila nashukuru kwa kuniweka huru na mawazo yangu mgando...
 
Nilipoona uteuzi wa maluteni general nikajua chief of stuff ndomba kapigwa chini kumbe la! waliostahili kupanda na kuwa chief of stuff wakanyimwa na aliyepanda fasta fasta Major Gen Ndomba akaukwaa u Lut. Gen na hatimae kuwa chief of stuff. Sasa naona ameona how unfair it was na hatimae ameamua kuvunja utamaduni wa kuwa na luteni general mmoja. Dawa ni katiba mpya, Mungu ana njia nyingi sana ametupa hili at a very right time. Too much Presd. apointments.
 

Na Mwandishi Wetu, Dar na Rufiji

Posted Jumanne,Decemba4 2012 saa 22:59 PM

Rwegasira alisema wananchi wa Rufiji wametakiwa kujitokeza kwa wingi kumpokea kiongozi huyo atakapoingia wilayani hapa ikiwa ni ziara yake ya kwanza tangu kumalizika kwa Uchaguzi Mwaka 2010.

Hata hivyo, Rwegasira
aliwataka madiwani kuwajulisha wananchi kushiriki kumpokea.



Kwa nini wananchi wasiombwe kujitokeza bali watakiwe kujitokeza? Tunaishi kwa amri amri tuu........kama ziara ya Rais ni jambo zuri watu watakuja tu bila amri
 
Mkuu unazungumza utamaduni lakini sio muundo wa jeshi. Generali ni cheo cha kijeshi na sio madaraka. Mkuu wa jeshi ni madaraka. Hivyo kunaweza kuwepo kwa mageneral watatu.

Na luteni general ni cheo vilevile na sio madaraka ya kuwa chiefu of staff. Kwa Tanzania hata major general anaweza kuwa chief of staff.
Sina uhakika na la Major General kuwa Chief of Staff tatizo langu ni pale kunapokuwa na seniors kwake katika muundo wa vyeo vya kijeshi ukizingatia nidhamu za kijeshi zilivyo maamuzi yake yanaweza kuwa yanatokana na nidhamu ya woga pale itakapobidi kutoa maamuzi ya kuathiri ma-luteni generali!

Muundo uliozoeleka ni wa kuwa Generali mmoja kama CDF na Luteni Generali kama COS hili la maluteni generali kuwa zaidi ya mmoja sijayaona sana lakini nakumbuka Abdallah Twalipo alikuwa Luteni Generali wakati kuna Luteni Generali mwingine nisichojua ni kama alikuwa active au hakuwa active wakati huo maana nafikiri alikuwa ameingia kwenye nafasi za Kisiasa wakati huo!!
 
Nipo comrade,,, nlikua kwny blog moja ya wakenya nlikua nawaharibia siku asbh na mapema kuhusu mambo yao ya uchaguzi

Mm nawapongeza hawa wakuu.., hawa wote ni vifaa vilivyoiva sana kijeshi.., makakala ndio mkuu kunduchi pale, kile chuo kipya
Mkuu karibu tumekupata, samahani ni blog ipi hiyo maana nina jamaa wengi hapa wao wenyewe hawaelewani, kazi kweli kweli!!!!
 
:violin::fish::clock::behindsofa::behindsofa::mvutaji:

........Amiri Jeshi Mkuu amefanya kazi yake..............
 
Mkuu yeye alishatoka huko jeshini.

Hongereni sana Lt. Gen. Ryoba na Lt. Gen. Makakala. Naona tunazidi kusonga mbele. Huko nyuma jeshini kulikuwa kwa kawaida kuna Four-Star General (CDF) mmoja na Three-Star General mmoja (CoS) lakini sasa naona tuna Four Star General mmoja na three star generals watatu mmoja akiwa ni CoS. Tuendako huenda tukapata general of the army (five-star general) na hivyo four-star generals kuwa wengi pia.

Sawa,

Tukishakuwa na hao ni nini na kwa vipi sie wananchi tutanufaika?
 
Back
Top Bottom