JK awapandisha vyeo majenerali

JK awapandisha vyeo majenerali

mi nakubaliana nawe kuwa kwa ndomba hakukosea. jamani jeshi sio chama cha siasa kinachohitajika utendaji. mimi nilitegemea tutamsifia jk alifanya vizuri bila kuangalia seniority na kuzingatia utendaji zaidi. i wish all of them

Tena Watanzania. watambue jeshi letu linafanya kazi nzuri ktk medani za kimataifa ndio maana tumepata nafasi huko nje na zinahitaji watu ma rank hiyo rais aliyowatunuku hao makamanda.

Muache mazoea ya kumsema rais.pia mwanzo hatukuwa na chuo cha NDC sasa tunacho ambacho kitapunguza gharama za kupeleka makamanda wetu kusoma nje ya nchi na kustadi hapa nchin.hongera mh rais wangu.
 
akili zako ndio zinakutuma ivyo kwa taarifa yako hadi wamerekani,wachina wapo pale wanapiga buku. so kama ingekuwa kama shule za kata wasingeleta watu wao tena nchi inalipwa madola
 
Phillemon Mikael kaka mahitajio yameongezeka usilalame tu.sasa kama tumepata nafasi kufanya kazi nje ya nchi na wanahitaji watu ma rank hizo tusiende kisa tuna Lt gen mmoja.
 
Last edited by a moderator:
wewe usiwe mjinga kuzungumza vitu usivyovijua. makakala anastaafu mwakani na cheo alichopata ataendelea kuwa mkuu wa NDC .chuo kinahitaji kuongozwa .a. mtu wa
cheo alichopewa.pia kisamba ni anaongoza majeshi ya kulinda amani kutoka nchi mbali mbali huko Darfuu-sudan (kenya,ngeria,misri,bangaradesh,india,ghana,gabon,burundi,rwanda nk) pia huyo mwingine anakwenda kuongoza majeshi ya kulinda amani huko kongo.so muache kumbeza rais anapofanya kazi yake.

So una maana Luteni General Sylvester Chacha Riyoba.....anaenda kuongoza TanzBatt Goma?.....from state house disaster coordinator ..in PM office?

Naweza kukubaliana na Hoja ya NDC...kwakuwa naona NDC college za kenya na south pia zinaongozwa na watu wa rank kubwa hasa kutokana na fact kuwa wanachuo wengine wanapewa u meja general kwenye baadhi ya nchi kabla ya kuwa na NDC kulingana na mahitaji....na kuwalazimu kwenda Mafunzo hayo ya juu....
Mkuu wa Chuo cha Maafisa TMA...Arusha...anakuwaga na cheo cha Brigedia General au Meja General...

Kuhusu issue zinazofanana na ya Luteni General W Kisampa....ambaye ni kamanda wa UN darfur .....kuna contradiction inayotokana na baadhi ya nchi ie Rwanda ,Uganda etc,,,,ambapo makamanda wao hupandishwa vyeo bila kufuata milolongo na protocols Kama za kwetu ( ambazo ni nzuri na sio vibaya Wananchi kuhoji zikienda toffauti )....hii inasabanisha kamanda wetu kupata wakati mgumu pale kamanda wa chini yake huko UN kwenye nchi nilizotaja anapopandishwa cheo na Rais wake...
Tanzania tunajivunia kuwa hakuna njia za mkato kupanda cheo ...na wengi wa wanaopanda hata Askari wa chini ...ambao ndio wenye taarifa nyingi waawakubali......mfano Mkuu wa Majeshi wa Uganda wenzake aliotrain nao Cadet watanzania ndio kwanza wamevaa u Kanali......kwa hiyo pasipo kuhoji uwezo wa wenzetu kimedani....Ukweli ni kuwa wao wanaopanda Haraka Sana vyeo ...spendi kutumia neno holela kwakuwa wao wana vigezo pia ...wakati sisi tunafuata utamaduni wa Majeshi ya UK...commonwealth ...na ule ulioboreshwa na Mwalimu Nyerere wakati wa kuunda upya Jeshi
 
So una maana Luteni General Sylvester Chacha Riyoba.....anaenda kuongoza TanzBatt Goma?.....from state house disaster coordinator ..in PM office?

Naweza kukubaliana na Hoja ya NDC...kwakuwa naona NDC college za kenya na south pia zinaongozwa na watu wa rank kubwa hasa kutokana na fact kuwa wanachuo wengine wanapewa u meja general kwenye baadhi ya nchi kabla ya kuwa na NDC kulingana na mahitaji....na kuwalazimu kwenda Mafunzo hayo ya juu....
Mkuu wa Chuo cha Maafisa TMA...Arusha...anakuwaga na cheo cha Brigedia General au Meja General...

Kuhusu issue zinazofanana na ya Luteni General W Kisampa....ambaye ni kamanda wa UN darfur .....kuna contradiction inayotokana na baadhi ya nchi ie Rwanda ,Uganda etc,,,,ambapo makamanda wao hupandishwa vyeo bila kufuata milolongo na protocols Kama za kwetu ( ambazo ni nzuri na sio vibaya Wananchi kuhoji zikienda toffauti )....hii inasabanisha kamanda wetu kupata wakati mgumu pale kamanda wa chini yake huko UN kwenye nchi nilizotaja anapopandishwa cheo na Rais wake...
Tanzania tunajivunia kuwa hakuna njia za mkato kupanda cheo ...na wengi wa wanaopanda hata Askari wa chini ...ambao ndio wenye taarifa nyingi waawakubali......mfano Mkuu wa Majeshi wa Uganda wenzake aliotrain nao Cadet watanzania ndio kwanza wamevaa u Kanali......kwa hiyo pasipo kuhoji uwezo wa wenzetu kimedani....Ukweli ni kuwa wao wanaopanda Haraka Sana vyeo ...spendi kutumia neno holela kwakuwa wao wana vigezo pia ...wakati sisi tunafuata utamaduni wa Majeshi ya UK...commonwealth ...na ule ulioboreshwa na Mwalimu Nyerere wakati wa kuunda upya Jeshi

kaka huyo uliyemtaja hapo juu nasikia anakwenda kuongoza majeshi uko Lebanon au kongo na huyn mwingine atabaki uko darfu.mpeni sifa raisi wetu
 
Inaamana huyu Muheshimiwa Amiri jeshi mkuu amejitungia tuu vyeo vya kijeshi hapo katikati ndio maana mambo ya namna ya kutoa vyeo kwenye idara nyeti za serikali ziwekwe kwenye katiba ona sasa tuna Raisi anaitia najisi katiba anafanya mambo kinyume kabisa vyuo vikuu anafanya afanyavyo, usalama wataifa mabest tu wake, mahakama yeye anavurunda ,mawaziri ndio usisema ,jeshi la polisi mama wewe wakuu wa mikoa na wilaya vimwana kwa kwenda mbele , tunakazi kabisa nadhani kuna umuhimu wa mambo haya kuwekwa vizuri
Nadhani kikubwa hapa ni ile nafasi ya Shimbo(COS).

Imetafutiwa mtu aliyekua junior(Ndomba), na ndiyo maana unaona kuna mkanganyiko hapa.

Sidhani kama tatizo ni kuwa rais kajitungia vyeo,bali ni cheo cha afisa mnadhimu mkuu wa jeshi(baada ya Luteni general Shimbo kustaafu),ikabidi wafanye fanye mambo ili apatikane wanayemtaka.

Ndivyo nilivyoelewa.Inabidi tuchungze shughuli za huyo afisa mnadhimu mkuu ili tuone kama zinahusiana vipi na well being ya chama cha mapinduzi,maana Shimbo aliingilia hata uchaguzi uliopita,na kuna ile issue ya mapesa(trillions), ya SA.
 
Kwani nafasi za JWTZ zitatoka lini?????????????
Wadau nisaidieni kwani napenda kuitumikia nchi yangu kutitia JWTZ
 
Kaka Phillemon Mikael, kwa sasa mahitajio yameongezeka kaka jeshi limepanuka na kuwa la kisasa hawa wote wanahitajika ktk majukumu ya kitaifa ndio maana wamepanda ata katiba mpya ikiwekwa na kuamuliwe kuwa na LT GEN WATANO lakini wigo wa kazi na mahitajio ya rank watu wasipewe kisa katiba inakataa.wewe unajua nchi inaingiza kiasi gani cha Dola kwa hawa wakuu kufanya kazi nje ya nchi uko.
 
Last edited by a moderator:
Hemed Maronda IN ADDITION Gen. Charles Lawrence Makakala is a brilliant general, very smart upstairs. He has written the Strategic and Tactical TPDF Manuals and many other publications for the army. He has always excelled in Military Colleges starting from Odessa Military Engineering College in Ukraine (Formerly USSR) to NDC in India. He has very strong recommendations from ALL those institutions. Ulokole wake si tatizo but there is strong opinion that ulokole was just a ploy to deny him one of the top jobs, which as it looks those efforts were successful.
 
Last edited by a moderator:


Kwa mujibu ya taarifa iliyotolewa na Kurugenzi ya Habari na Uhusiano ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), inaeleza kuwa maofisa wakuu waliopandishwa cheo ni
Meja Jenerali, Sylvester Chacha Ryoba ambaye ni Mkurugenzi wa Kitengo cha Maafa ofisi ya Waziri Mkuu kuwa Luteni Jenerali.

Mwingine ni Meja Jenerali,
Charles Lawrance Makakala ambaye ni Mkuu wa Chuo cha Taifa cha Ulinzi.
Mfumo Kristo hadi huku??!
 
Wajuzi na wachambuzi wa mgawanyo wa vyeo jeshini anisaidie kuelewa zaidi,kwa nini hao wawili wamepandishwa kuwa Lt Gen (Mkuu wa Chuo na Mkuu wa kitengo cha Maafa) na si wale wakuu wa divisheni za jeshi kwa maana Jeshi la Anga,Majini na Nchi Kavu? Nilitegemea hao wa 3 ndio wangekuwa Lt Gen katika utendaji ingewasaidia sana,

Careful, usichanganye kati ya command(kamandi) na division..., command zipo tatu nazo ni navy, air defence na land...,
 
Nadhani kikubwa hapa ni ile nafasi ya Shimbo(COS).

Imetafutiwa mtu aliyekua junior(Robya), na ndiyo maana unaona kuna mkanganyiko hapa.

Sidhani kama tatizo ni kuwa rais kajitungia vyeo,bali ni cheo cha afisa mnadhimu mkuu wa jeshi(baada ya Luteni general Shimbo kustaafu),ikabidi wafanye fanye mambo ili apatikane wanayemtaka.

Ndivyo nilivyoelewa.Inabidi tuchungze shughuli za huyo afisa mnadhimu mkuu ili tuone kama zinahusiana vipi na well being ya chama cha mapinduzi,maana Shimbo aliingilia hata uchaguzi uliopita,na kuna ile issue ya mapesa(trillions), ya SA.

Chief of staff ni ndomba, ndiye amemrithi shimbo, makakala mkuu wa chuo cha NDC, ryoba anafanya ujasusi wake chini ya kivuli cha disaster coordination
 
Rais kikwete Huu mfumo wa Jeshi anautoa wapi?

JWTZ at any given time inakuwa na Active General mmoja tu ambaye ni Mkuu wa Majeshi.......

..........na active Lt Gen mmoja tu ambaye ni Chief of Staff.............

As of hawa wawili...Sylvester Riyoba na Charles Makalala.....ambao kabla ndio waliokuwa na seniority na wakapendekezwa mmoja wao awe chief of staff...Lakini badala yake Kikwete ammpandisha cheo Junior wao....Sylvester Ndomba kuwa chief of staff...

Kinachoonekana haPa kikwete...ameamua Kuvunja utaratibu wa kimuundo wa Jeshi kuipeleka kuwa na ma luteni generali watatu Kazini badala ya mmoja........ni mbinu tu ya Rais kuwapooza hawa senior general kwa kitendo chake cha kuwaruka wakati na kumuwekA junior kuwa chief of staff......

Pamoja na kuwa hawa wanastahili kupanda .....upandishaji Huu ni holela kwa kuwa umevuruga mfumo wa Jeshi .........hii inatokea wakati Jeshi bado watu wanashangaa muundo wake wa kuwa na mameja jenerali wawili ...wanamama kwenye kitengo cha utuumishi ambacho Mara zote kimekuwa kikiongozwa na brigedia generali au maj generali....na msaidizi kanali au brigedia .....kitendo cha kuweka maj generals wawili kitengo Kimoja ni matumizi mabaya ya rasilimali watu....

Umeniwahi mkuu!huu ni mzigo baadae tutakuja ujutia,Zamani ilikuwa Rank kubwa sana mtu anaweza kupandishwa na kwa watu wachache ni Brigadier General lakini tumekuwa na utitiri wa vyeo vya juu pasipo sababu za msingi
 
Jwtz linajumuisha wanzibari pia? Seems Makame's and Faki's are extremely rare in the top echelons.
 
Chief of staff ni ndomba, ndiye amemrithi shimbo, makakala mkuu wa chuo cha NDC, ryoba anafanya ujasusi wake chini ya kivuli cha disaster coordination
Thanks mkuu,ngoja nifanye marekebisho niweke Ndomba badala ya Robya.
 
Mfumo Kristo hadi huku??!

Kahuna MIFUMO yoyote ISIPOKUWA ni KUTOSHEKA kwa WAISLAMU wachache... MAWAZO yenu yamepitwa na WAKATI



Major-General-Said-Shaaban-Omar.jpg


Major General Said Shaaban Omar
 
Back
Top Bottom