Je, kulikuwa na ulazima gani Tanzania kuchukua wimbo wa Afrika Kusini na kuufanya wimbo wa Taifa? Kwanini tusingetunga wa kwetu?

Huenda ni uvivu tulionao ndio unasababisha umasikini wetu na tumebaki kutafuta visingizio visivyo na idadi.

Swala nyeti kama wimbo wa taifa, ambao ndio kitambulisho chetu, iweje tuukwapue wimbo wa Afrika Kusini na kuufanya wetu?

Je kwanini hatukuufanya wimbo wa Tazama ramani utaona nchi nzuri, uwe wimbo wa taifa letu?

Nadhani sasa ni wakati wa kurudi kwenye asili yetu, tutunge wimbo wetu wenyewe au tuufanye wimbo wa TAZAMA RAMANI uwe ndio wimbo wa taifa.
The vice versa is true. Ni SA ndio walikopi toka TZ.
 
Upo mwingine pia wa kizalendo, sikumbuki 'title' yake.

AHAAAA: Tanzania, Tanzania, Nakupenda kwa moyo wote---

Watunzi wa nyimbo hizi wanastahili tuzo na heshima ndani ya nchi yetu.

Anayejuwa watunzi na historia ya nyimbo hizi, tafadhali simulia.
Pia kuna mwingine tulikuwa tunaimba shule ya msingi, huu ni wa kuisifia zaidi unaimbwa hivi;

"Tanzania Tanzania, nchi yenye mali nyingi... Watu wengi wa ulayaaaa wanaililia sana, niliona ndege wengi...chini wametia fora...walinipendeza mlio kama mtoto wa nyumbani...Ngooorongoro ile ngoorongoro ile ngoorongoro ileee ngoorongoro ileee.."

Sijui ndo hivi
 
Pia kuna mwingine tulikuwa tunaimba shule ya msingi, huu ni wa kuisifia zaidi unaimbwa hivi;

"Tanzania Tanzania, nchi yenye mali nyingi... Watu wengi wa ulayaaaa wanaililia sana, niliona ndege wengi...chini wametia fora...walinipendeza mlio kama mtoto wa nyumbani...Ngooorongoro ile ngoorongoro ile ngoorongoro ileee ngoorongoro ileee.."

Sijui ndo hivi
Uzalendo namba moja unaanza kwa kuwa na wimbo wa taifa uliotungwa na sisi wenyewe, sio wimbo mtumba
 
Huenda ni uvivu tulionao ndio unasababisha umasikini wetu na tumebaki kutafuta visingizio visivyo na idadi.

Swala nyeti kama wimbo wa taifa, ambao ndio kitambulisho chetu, iweje tuukwapue wimbo wa Afrika Kusini na kuufanya wetu?

Je kwanini hatukuufanya wimbo wa Tazama ramani utaona nchi nzuri, uwe wimbo wa taifa letu?

Nadhani sasa ni wakati wa kurudi kwenye asili yetu, tutunge wimbo wetu wenyewe au tuufanye wimbo wa TAZAMA RAMANI uwe ndio wimbo wa taifa.
Tazama ramani ni bonge la wimbo! Na una sifa zote za kuwa wimbo wa Taifa la Tanganyika! Sema tu unatakiwa pia kufanyiwa maboresho kwenye mashairi yake! Kusiwepo mstari wowote ule wa kutaja majina ya viongozi! Sijui Nyerere, sijui Karume!!

Tena kama huyo Karume ndiyo hatakiwi kabisa kutajwa! Maana tayari Zanzibar wana wimbo wao wa Taifa.

Kiukweli hui wimbo wa sasa hauna mvuto! Eti Mungu ibariki Afrika! For what!! Wimbo wa Taifa uiongelee Tanzania tu na watu wake.
 
Huenda ni uvivu tulionao ndio unasababisha umasikini wetu na tumebaki kutafuta visingizio visivyo na idadi.

Swala nyeti kama wimbo wa taifa, ambao ndio kitambulisho chetu, iweje tuukwapue wimbo wa Afrika Kusini na kuufanya wetu?

Je kwanini hatukuufanya wimbo wa Tazama ramani utaona nchi nzuri, uwe wimbo wa taifa letu?

Nadhani sasa ni wakati wa kurudi kwenye asili yetu, tutunge wimbo wetu wenyewe au tuufanye wimbo wa TAZAMA RAMANI uwe ndio wimbo wa taifa.
Kwani TANZANIA na South Afrika, ipi Hasa ilianza kupata Uhuru???

Tuanzie hapo .
 
Tazama ramani ni bonge la wimbo! Na una sifa zote za kuwa wimbo wa Taifa la Tanganyika! Sema tu unatakiwa pia kufanyiwa maboresho kwenye mashairi yake! Kusiwepo mstari wowote ule wa kutaja majina ya viongozi! Sijui Nyerere, sijui Karume!!

Tena kama huyo Karume ndiyo hatakiwi kabisa kutajwa! Maana tayari Zanzibar wana wimbo wao wa Taifa.

Kiukweli hui wimbo wa sasa hauna mvuto! Eti Mungu ibariki Afrika! For what!! Wimbo wa Taifa uiongelee Tanzania tu na watu wake.
Well said brother
 
Bro, South Africa imepata uhuru mwaka 1994 kutoka kwa kaburu. Sisi Tanganyika tumepata uhuru 1961 na muungano 1964. Sasa sijui hapo unahitaji taarifa gani zaidi kujua nani kamuiga nani?!
 
Huenda ni uvivu tulionao ndio unasababisha umasikini wetu na tumebaki kutafuta visingizio visivyo na idadi.

Swala nyeti kama wimbo wa taifa, ambao ndio kitambulisho chetu, iweje tuukwapue wimbo wa Afrika Kusini na kuufanya wetu?

Je kwanini hatukuufanya wimbo wa Tazama ramani utaona nchi nzuri, uwe wimbo wa taifa letu?

Nadhani sasa ni wakati wa kurudi kwenye asili yetu, tutunge wimbo wetu wenyewe au tuufanye wimbo wa TAZAMA RAMANI uwe ndio wimbo wa taifa.
Kuna watu mnaweweseka sana na kipande kinachosema "Mungu ibariki Afrika kwa sababu ya ufinyu wa elimu ya kiroho. Kimaandiko unapowaombea wengine kwanza halafu wewe ukajiombea mwisho kwa Mungu wewe ndio unabarikiwa zaidi. Wengi hawafanikiwi kwa kuweka ubinafsi mbele halafu wengine baadae.

"Ungameni dhambi zenu ninyi kwa ninyi, na kuombeana, mpate kuponywa". Yakobo 5:16
 
Bro, South Africa imepata uhuru mwaka 1994 kutoka kwa kaburu. Sisi Tanganyika tumepata uhuru 1961 na muungano 1964. Sasa sijui hapo unahitaji taarifa gani zaidi kujua nani kamuiga nani?!
Bro,
Maneno katika wimbo huo yalitungwa na mtunzi Enoch Sentonga huyu ni Raia wa Afrika Kusini.

Wimbo huo aliutunga mwaka 1897 ukiwa na maneno "Nkosi sikelel i'Afrika wenye tafsiri yake "Mungu Ibariki Afrika katika lugha ya Kiswahili.

Wimbo huo ni wimbo maarufu Afrika ukitumiwa katika harakati za ukombozi kwa baadhi ya nchi za Afrika. Sontonga alizaliwa 1873 na alifari tarehe 18-04-1915 huko nchini Afrika kusini.
 
Hakika
Tazama ramani mrefu kinoma, ni kheri tuache hivyo hivyo maana hizo kamati sijui wanakway wa kutunga, kuhariri na kupata wimbo wa taifa watakula pesa zaidi ya pesa ya sensa. Mkuu Bujibuji Simba Nyamaume waambie waache tu hasara ni kubwa kuliko faida.
 
Kuna watu mnaweweseka sana na kipande kinachosema "Mungu ibariki Afrika kwa sababu ya ufinyu wa elimu ya kiroho. Kimaandiko unapowaombea wengine kwanza halafu wewe ukajiombea mwisho kwa Mungu wewe ndio unabarikiwa zaidi. Wengi hawafanikiwi kwa kuweka ubinafsi mbele halafu wengine baadae.

"Ungameni dhambi zenu ninyi kwa ninyi, na kuombeana, mpate kuponywa". Yakobo 5:16
Unaendeshwa na roho za mapepo wachafu wewe. Kwa hiyo tuutumie wimbo mtumba, huoni huo ni umasikini kabisa wa fikra?
 
Alishiriki nani kutoka Tanzania kuutunga wimbo huo?
Tulishiriki Idea ya wimbo wao wakatunga mashairi na kuimba.

Uhuru wa S.Afrika tumehusika pakubwa.

By the way waasisi Nia Yao Hasa wimbo Ule uje kuwa wimbo wa Africa nzima maana tulidhamiria kuanzisha Dola moja ya Afrika.
 
Back
Top Bottom