Wimbo wetu wa Taifa tuufanyie maboresho au tutunge mpya kabisa

Yoda

JF-Expert Member
Jul 22, 2018
37,641
46,290
Wimbo wa taifa unakuwa mzuri sana pale unapoelezea historia ya taifa husika au unatoa sifa za kipekee za nchi au unapokuwa unahamasisha uwajibikaji/ call for action kwa taifa au vyote vitatu kwa pamoja.

Sasa sisi wimbo wetu unahusisha maombi zaidi mwanzo mpaka mwisho, hauna call for action, historia ya nchi yetu, mwito wa uzalendo au uwajibikaji. Nafikiri nyimbo kama Tazama ramani au Tanzania nakupenda kwa moyo wote zinaweza kutufaa sana. Pia nyingine mpya kabisa zinaweza kutungwa na kuchaguliwa mojawapo.

Au hata huu wa sasa ufanyiwe mabadiliko muhuimu, badala ya kusema Mungu wabariki viongozi wake iwe wabariki WATU wake ili uwe jumuishi. Dumisha uhuru na umoja iongozwe iwe dumisha uhuru, HAKI na umoja ili kuleta msisitizo wa kutendeana haki.

Sisi hatutatukwa wa kwanza kufanya mabadiliko kama haya. Uingereza wao hubadilisha "God save the Queen" na sehemu zote zenye he zinakuwa she wanapokuwa na Malkia kama mtawala, wakipata mfalme wanarudi kwenye "God save the King" na he.

Russia, Canada, Ujerumani na nchi nyingi pia wamewahi kubadilisha au kufanya mabadiliko katika nyimbo zao za taifa
 
Hoja zako hazina msingi, wimbo wetu wa taifa uko vizuri sana.

BTW? huwa unasikiliza nyimbo za mataifa mengine?
 
Wimbo wa taifa unakuwa mzuri sana pale unapoelezea historia ya taifa husika au unatoa sifa za kipekee za nchi au unapokuwa unahamasisha uwajibikaji/call for action kwa taifa au vyote vitatu kwa pamoja...
Hivi ule Tazama ramani ni wa nchi gani?
 
Nyimbo za taifa kwa asilimia kubwa zinahusisha maombi kwa Mungu kuliombea taifa, nchi au viongozi wao mfano mzuri ni hapa

Kwa hiyo sisi siyo wa kwanza wimbo kuwa na "maombi"
Kwenye wimbo wa Uingereza kuna maneno ya muhimu sana ya zaidi ya maombi, ya wito wa uzalendo na kuilinda katiba

"May he defend our laws,
And ever give us cause,
To sing with heart and voice"
 
Ubadilishwe tu halafu tuchanganyiwe na vionjo tofauti tofauti mfano 🎵rap, 🎶reggae na 🎼kaswida siyo kila wimbo kwaya tu!🤣🤣🤣

Sauti imetosha au niongeze?🔊🔉
 
Badala ya kusema wabariki viongozi, tuseme wabariki wananchi wa Tanzania, wawe na umoja, uzalendo na uwajibikaji. Tukiweka maneno haya wimbo wetu wa taifa utakuwa bora Sana..
 
Badala ya kusema wabariki viongozi, tuseme wabariki wananchi wa Tanzania, wawe na umoja, uzalendo na uwajibikaji. Tukiweka maneno haya wimbo wetu wa taifa utakuwa bora Sana..
Hakika, ungekuwa bora sana.
 
Samia akiona hoja hii hachelewi kututengenezea uharo kama ule wa africa mashariki. Watawala wa Tanzania hupenda kiki sana
 
Ile sehemu ya "Mungu wabariki viongozi wetu", napendekeza iwe "Mungu wateketeze viongozi wetu mafisadi".

Naomba kuwasilisha.
 
Sikiliza huu wimbo wa macho madogo ndio utajua kwao historia ina maana gani ?

Lyrics of the Chinese National Anthem​

起来!不愿做奴隶的人们!


Stand up! Those who are unwilling to become slaves!


把我们的血肉,筑成我们新的长城!


Take our flesh, and build it to become a new Great Wall!


中华民族到了最危险的时候,


The Chinese people have reached a most dangerous time,


每个人被迫着发出最后的吼声。


Every person is being compelled to send issue a final roar.


起来!起来!起来!


Arise! Arise! Arise!


我们万众一心,


We are millions with one heart,


冒着敌人的炮火,前进


Braving our enemy’s gunfire, march on!


冒着敌人的炮火,前进!


Braving our enemy’s gunfire, march on!


前进!前进!进!


March on! March on! Charge!
 
Sikiliza huu wimbo wa macho madogo ndio utajua kwao historia ina maana gani ?

Lyrics of the Chinese National Anthem​

起来!不愿做奴隶的人们!


Stand up! Those who are unwilling to become slaves!


把我们的血肉,筑成我们新的长城!


Take our flesh, and build it to become a new Great Wall!


中华民族到了最危险的时候,


The Chinese people have reached a most dangerous time,


每个人被迫着发出最后的吼声。


Every person is being compelled to send issue a final roar.


起来!起来!起来!


Arise! Arise! Arise!


我们万众一心,


We are millions with one heart,


冒着敌人的炮火,前进


Braving our enemy’s gunfire, march on!


冒着敌人的炮火,前进!


Braving our enemy’s gunfire, march on!


前进!前进!进!


March on! March on! Charge!
View attachment 2881161
Wimbo wa kishujaa sana, hauna unyonge wowote
 
Wimbo wa kishujaa sana, hauna unyonge wowote
Ubaya ni wimbo wetu unafana na wa S.A, Zambia . Ule Tanzania nakupenda kwa moyo wote wa ufupishe na upitishwe rasmi kuwa wa Taifa.

Hili taifa letu sio la kidini ila kuna baadhi ya mambo yana shangaza kweli ukiwemo huo wimbo wa taifa.

Wimbo mzima umejaa Mungu ibariki, Mungu ibariki hau hamasishi kwa kweli.
 
Ubaya ni wimbo wetu unafana na wa S.A, Zambia . Ule Tanzania nakupenda kwa moyo wote wa ufupishe na upitishwe rasmi kuwa wa Taifa.

Hili taifa letu sio la kidini ila kuna baadhi ya mambo yana shangaza kweli ukiwemo huo wimbo wa taifa.

Wimbo mzima umejaa Mungu ibariki, Mungu ibariki hau hamasishi kwa kweli.
Sahihi, Hizi nyimbo zinafanana katika haya mataifa kwa sababu mtunzi mkuu ni Enoch Sontonga wa Africa Kusini aliyekuwa muhuburi. Inawezekana haya mataifa yalifanya hivyo kuonyesha umoja na mshikamano wa Waafrika(Pan Africanism) enzi zile za harakati za uhuru na vita dhidi ya ubaguzi na bado kukiwa na ndoto za kuwa na Africa moja.
 
Back
Top Bottom