Mastory ya bey
Mambo zenu,hope mpo gud wasomaji wangu nami nipo vizuri kwa uzito wa tano
Mastory yangu ya leo tutaangalia ni sababu zipi ambazo zinafanya kuwe na umuhimu wa kusahau machungu yaliyo pita
Mosi, hutupa amani ya ndani kwasababu machungu yaliyopita hutupa huzuni,hasira na hata kujikuta tunachukia maisha kwa ujumla wake,kwahiyo kuna umuhimu mkubwa sana tusahau au tupambane kuachana na machugu ya zamani
Pili, hutuwezesha kuishi kwa furaha ,unajua kumbukumbu mbaya za matukio ya zamani hutufanya tushindwe kuishi maisha yetu to the fullest,yani ingawa ni matukio ya zamani lkn huyafanya maisha yetu yasiwe na mvuto wala thamani,hutufanya tuwe wanyonge muda wote,lakini pale tutakapo azimia kusonga mbele na kusahau yalipita na kuyasamehe tunapata furaha
Hunufaisha afya ya akili na mwili pili,kumbukumbu mbaya za zamani hutupa msongo wa mawazo na hii hupelekea hata afya zetu kudhoofu,kwahiyo tunapo amua kupambana na kuachana na machungu ya zamani tunaimarisha afya zetu na kiwiliwili pia
Ni ishara ya kukua kiroho na kiakili pia,mtu anajua kwamba majaribu ni sehemu ya maisha,na maisha siku zote hayakupi unachotaka kwahiyo unakubaliana na fate au majaliwa yako. Vile unajifunza kwamba kwa jaribu ambalo unakutana nalo ni somo na elimu tosha inakuwezesha kufika mahala fulani katika maisha
Kwa kumalizia wasomaji wangu kila mtu hupitia changamoto mbali mbali katika maisha,tunachotofautiana ni namna gani tunazikabili na kuenda nazo sawa ili zisitunyime fursa ya kusonga mbele na kufurahia maisha yetu,kingine msomaji wangu ebu tujiulize kuna faida gani ya kuruhusu kuumizwa na mambo ambayo hatuwezi kuyabadilisha kwa maana yalishatokea tayari?
Anza kuwaza na kufikiria tofauti
Bey