JamiiForums Usiku wa manane

Mastory ya bey​


Ni majira ya usiku hope mpo gud kama kawa kama dawa,karibuni kijiweni ambapo mastory ndio mahala pake

Leo ningependa tuzungumzie ishu nzima ya kuwa na Dhana juu ya jambo fulani au mtu fulani,haya ni maradhi ya namna jinsi tunavyowaza na kufikiri

Tumejikuta tu automatic huwa dhana zetu huwa negative zaidi kuliko kuwa positive,ni mara chache sana itokee umdhanie mtu Dhana njema,ila mara nyingi huwa tunaangukia katika mtazamo hasi zaidi

Hii inatokana na makuzi yetu na namna tulivyoona wengine jinsi wanavyodhani nasi bila kujua tunaangukia upande ule ule

Mfano anaweza onekana mtu amevaa vizur tu wala hana baya na mtu,lakini watu utawasikia wanasema "anajifanya ana hela sana siku hizi au anajionyesha tu tumuone siku hizi yupo vizur"

Au mtu anaamua ajiongelee zake broken English basi waja hawakawii kuwa na dhana mbaya hawakawii kusema "huyu nae anajifanya kasoma au anataka tujue kuwa kaenda shule"

Hii na mifano mingine mingi ni udhibitisho tosha kwamba hakika watu wengi tumejikuta tumejaa dhana mbaya juu ya watu wengine

Sasa msomaji wangu wa Mastory ya Bey,tupo hapa kujifunza kuwaza na kufikiri tofauti,tuvunje minyonyoro na makufuli yote ambayo yamefunga fikra zetu na maono yetu juu ya kuwa na dhana mbaya

Ni wakati sasa wa kuanza kuwaza na kufikiria tofauti, tuwachukulie watu kama walivyo, tuache kuwa na dhana juu ya watu just tuwaangalie na kuwaacha kama walivyo, kwa vyovyote watakavyo fanya au kubehave is nothing to do with us at all,let's give them a break

Na tupende sana kuwadhania watu dhana nzuri,katika Uislamu inasemwa katika maandiko hakika baadhi ya dhana ni dhambi,wakati mwingine tunajichumia madhambi kwa kuwadhania watu vibaya

Next time if you feel like you wanna judge people just chill and tell urself isn't worth it

Jifunze kuwaza na kufikiria tofauti
 

Leo katika historia​


Hapa ni baadhi ya matukio ya kihistoria yaliyotokea tarehe 14 Oktoba:


---

🇹🇿 Katika Tanzania

14 Oktoba 1999 — Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, Baba wa Taifa wa Tanzania, alifariki dunia kutokana na leukemia huko London, Uingereza.

Siku hii pia huchukuliwa nchini Tanzania kama Siku ya Mwalimu Nyerere, ambapo wananchi hukumbuka na kuheshimu urithi wake wa viongozi, elimu, na ujenzi wa taifa.



---

🌍 Kimataifa / Ulimwenguni

1066 — Vita vya Hastings: Walowezi wa Norman wakiongozwa na William the Conqueror waliwashinda Waingereza na kuanza udhibiti wa England.

1947 — Chuck Yeager alikuwa mwanadamu wa kwanza kuruka kwa kasi kubwa kuliko sauti (breaking the sound barrier) akiwa na ndege ya Bell X-1 juu ya Muroc Dry Lake, Marekani.

1964 — Martin Luther King Jr. alipata Tuzo ya Amani ya Nobel kwa juhudi zake za kuhimiza haki sawa na kusimamiza ubaguzi wa rangi.

1964 — Billy Mills, mwanafunzi wa Marekani, alishinda dhahabu katika mbio za 10,000m katika Michezo ya Olimpiki huko Tokyo — ushindi mkubwa kutokana na matabaka ya ushindani.
 

Ujumbe wa Leo​

🌞 Ujumbe wa Leo 🌞

Maisha ni safari yenye milima na mabonde. Usikate tamaa unapokutana na changamoto, maana mara nyingi ndizo zinazoandaa njia ya mafanikio. Kumbuka — hata giza nene zaidi halidumu milele; alfajiri huja tu baada ya usiku mrefu. ✨
 

Quotes of the day​


Here are some positive quotes to brighten your day 🌞✨

1. “Keep your face always toward the sunshine—and shadows will fall behind you.” — Walt Whitman


2. “Believe you can and you're halfway there.” — Theodore Roosevelt


3. “Start where you are. Use what you have. Do what you can.” — Arthur Ashe


4. “Happiness is not by chance, but by choice.” — Jim Rohn


5. “The only way to do great work is to love what you do.” — Steve Jobs


6. “Every day may not be good, but there’s something good in every day.” — Alice Morse Earle


7. “You are never too old to set another goal or to dream a new dream.” — C.S. Lewis


8. “Your attitude determines your direction.” — Unknown


9. “Don’t let what you cannot do interfere with what you can do.” — John Wooden


10. “Be the reason someone smiles today.” — Roy T. Bennett
 

Mastory ya bey​

Poleni kwa pilika pilika za kutwa nzima ya leo,kumekuchwa huku tulio angaziwa jua mchana tunaelekea kulala na walio funikwa na usiku wanaelekea kuamka ndio nidhamu ya ulimwengu hiyo.

Tumeshawahi kusikia neno wasi wasi wa mapenzi au huenda sisi wenyewe ndio ambao wahusika ambao ni wahanga wakubwa wa jambo hili

Kwanza ebu tujue kwanini huwa tuna wasi wasi wa mapenzi,kwa mtazamo wangu kuna mambo mawili

Mosi huenda watu ambao tunao sio hadhi yetu hivyo tunajua muda wowote watatukimbia au watakuwa na wapenzi wengine au hatuwapi kile wanachostahili hivyo tunahofia wakikutana na watakao wapa wanachostahili ndio tutawakosa mazima

Sasa solution ili kuondokana na wasi wasi wa mapenzi ni kuwa na mtu wa size yako,kihadhi,kimuonekano,kiuchumi na kadhalika,huyo mtaenda sawa

Pili, ukiwa na mweza hakikisha hajisikii mpweke,upweke sio mtu kuwa single bali upweke hasa ni mtu kuwa na mume au mke kisha akawa mpweke,hakuna mapenzi,hakuna furaha,hakuna mazunguzo na vicheko na kadhalika

Ukijitathimini na kujikagua vizuri utafanya maamuzi ambayo yatakuwezesha kuepukana na mawazo na fikra za wasi wasi wa mapenzi

Jambo lingine huenda umeyafanya yote hayo lakini mchawi jinsi unavvyowaza na kufikiria,yani umejiweka kuwaza katika mtizamo hasi tu muda wote,huenda kutokana na unayoyasikia vijiweni au kuwa na watu ambao siku zote mitazamo yao ni kuwaza negative tu

Kupitia Mastory ya Bey tunajifunza kuwaza na kufikiria tofauti

Anza sasa kuwaza na kufikiria tofauti

Bey
 
Back
Top Bottom