ERTUGRUL BEY
JF-Expert Member
- Aug 6, 2020
- 11,597
- 21,640
Mastory ya bey
Ni majira ya usiku hope mpo gud kama kawa kama dawa,karibuni kijiweni ambapo mastory ndio mahala pake
Leo ningependa tuzungumzie ishu nzima ya kuwa na Dhana juu ya jambo fulani au mtu fulani,haya ni maradhi ya namna jinsi tunavyowaza na kufikiri
Tumejikuta tu automatic huwa dhana zetu huwa negative zaidi kuliko kuwa positive,ni mara chache sana itokee umdhanie mtu Dhana njema,ila mara nyingi huwa tunaangukia katika mtazamo hasi zaidi
Hii inatokana na makuzi yetu na namna tulivyoona wengine jinsi wanavyodhani nasi bila kujua tunaangukia upande ule ule
Mfano anaweza onekana mtu amevaa vizur tu wala hana baya na mtu,lakini watu utawasikia wanasema "anajifanya ana hela sana siku hizi au anajionyesha tu tumuone siku hizi yupo vizur"
Au mtu anaamua ajiongelee zake broken English basi waja hawakawii kuwa na dhana mbaya hawakawii kusema "huyu nae anajifanya kasoma au anataka tujue kuwa kaenda shule"
Hii na mifano mingine mingi ni udhibitisho tosha kwamba hakika watu wengi tumejikuta tumejaa dhana mbaya juu ya watu wengine
Sasa msomaji wangu wa Mastory ya Bey,tupo hapa kujifunza kuwaza na kufikiri tofauti,tuvunje minyonyoro na makufuli yote ambayo yamefunga fikra zetu na maono yetu juu ya kuwa na dhana mbaya
Ni wakati sasa wa kuanza kuwaza na kufikiria tofauti, tuwachukulie watu kama walivyo, tuache kuwa na dhana juu ya watu just tuwaangalie na kuwaacha kama walivyo, kwa vyovyote watakavyo fanya au kubehave is nothing to do with us at all,let's give them a break
Na tupende sana kuwadhania watu dhana nzuri,katika Uislamu inasemwa katika maandiko hakika baadhi ya dhana ni dhambi,wakati mwingine tunajichumia madhambi kwa kuwadhania watu vibaya
Next time if you feel like you wanna judge people just chill and tell urself isn't worth it
Jifunze kuwaza na kufikiria tofauti