Mastory ya bey
Kuna jamaa mmoja wakiwa mbele ya umati wa watu kwenye kikao kidogo,alimsimamisha dada mmoja kisha akamwambia nataka katika watu uwaangalie je wanafikiria nini kuhusu wewe?
Dada akampoint mtu wa kwanza akasema huyu ana ananitathimini jinsi nilivyovaa,alipoulizwa yule mtu,je huyu yupo sahihi ndio ulivyokuwa unawaza akasema hapana
Dada akampoint mkaka mmoja ambaye alikuwa anamuangalia kwa makini sana,akaulizwa je unadhani huyu anawaza nini kuhusu wewe,yule Dada akasema huyu kaka ananijaji muonekano wangu,alipoulizwa yule je ni kweli ulikuwa unajaji muonekano wa huyu dada akasema,akajibu hapana nipo najiwazia mambo yangu mwenyewe
Huu ndio mfano halisi wa maisha yetu ya kila siku,wakati mwingine huwa tunahofia watu wengine huwa wanawaza nini kuhusu sisi au je wanatuonaje kwa yale tunayoyafanya,lakini kiukweli huwa hawana hata time na sisi kabisa,wao wako busy na mambo yao,ila sisi ndio huwa tunajishtukia tu
Wakati mwingine tunashindwa kufanya mambo yenye tija kwetu binafsi kwa kuhofia watu watatuonaje au watatufikiriaje
Mtu msomi anashindwa kujichanganya na kufanya kazi ambazo zinaweza kumuingizia walau kipato hata kidogo huku akisubiria dili kubwa,anaacha kufanya kwa kuhofia eti watu watamuonaje na usomi wake halafu afanye kazi za watu wa chini
My people hakuna anaye hangaishwa na mambo yako,no body cares ishi maisha yako na fanya mambo yako kikubwa havunji haki za wengine
Habari za jioni wadau wa Mastory ya Bey hope mko gud! Leo nimewasilimia kizaramo,maana wazaramo wakikutana wanapiga mastory kwanza halafu baadae ndio wanasalimiana nami nimepiga mastory halafu nimewasalimia,unajua nini maisha ni rahisi sana usikariri
Bey