JamiiForums Usiku wa manane
Kalamu ya bey [zamani mazungumzo ya usiku]

IF YOU DO ME I DO YOU

Duniani pote ipo hivyo kile utachomfanyia mwenzako ndicho atachokufanyia pia.

Lakini bahati mbaya Sana huwa tunapenda kuwafanyia watu ubaya huku tukitarajia wao watufanyie vizuri kitu ambacho hata asili inakataa kabisa.

Formular ni moja tu, ukinifanyia jema nitakufanyia pia,ukinipenda nitakupenda pia,ukini dharau nitakudharau pia na listi inaendelea.

Uungwana ni kuwafanyia watu kile ambacho tungependa kufanyiwa Sisi pia, Kwa kufanya hivyo tutajihakikishia furaha na Amani siku zote.

Utakuta mtu anataka mke awe romantic kwake wakati yeye hajawa romantic Kwa mke wake! Je unarajia kupata nini sasa?

Na wanawake hivyo hivyo unataka Mme wake awe romantic kwako wakati wewe hujawa romantic Kwa Mume wako,je unarajia nini?

Always remember if u do me I do you

Unataka kuishi vizuri na majirani zako basi show love kwao na watashow love kwako pia, unataka kazini kwako kuwe sehemu nzuri ya kuishi wajali co workers wako nao watakujali pia.

Unaona mambo ni rahisi Sana lakini sijui kwanini tunapenda kuyafanya yawe magumu?

Ebu tuanze Leo kuifanya dunia iwe sehemu nzuri ya kuishi na kumbuka mabadiliko siku zote yanaanza na wewe.

Mlinzi wa zamu!
 
Kalamu ya Bey

KUFELI NDIO MWANZO WA MAFANIKIO

Kufeli ni sehemu ya mchakato wa maisha,ukiona mtu amefanikiwa sana basi ujue alifeli sana

Bahati mbaya tu,huwa hatupewi taarifa za kufeli za walio fanikiwa,lau tungejua upande wa shilingi tungejifunza mengi sana

Ukiona mtu hajafanikiwa kama level uliyofikia wewe basi tambua hakujaribu na kufeli sana,kwani maedeleo yanapatikana kwenye kufeli sana

Lau tukiambiwa huu mtandao wa Jamiiforums umepitia changamoto gani,basi huenda tukawapa big up sana hawa waanzilishi akiwemo founder mwenyewe Melo

Naamini nao walifeli sana mpaka kufanikiwa kuisimamisha hii App mpaka nasi tunatamba nayo,kwahiyo siri ya mafanikio ipo kwenye kufeli zaidi

Kwahiyo usiogope kufeli,haijalishi ni mara ngapi unafeli,kwa kila kosa unalokutana nalo linakupa nafasi ya kujifunza zaidi

Inasemekana yalifanyika makosa 1000 mpaka balbu hii tulinayo inaonekana kama tunavyoiona

Bwana Henry Ford aliwahimiza mafundi wake wapambane karibia mwaka mmoja mpaka wakafanikiwa gari ya silinda sita,kila mafundi wake walipo mwambia mheshimiwa haiwezekani,aliwaambia keep working,na matokeo yake walifanikiwa

Kwahiyo usihuzunike kufeli zaidi bali endelea na mchakato mpaka kielweke

Mlinzi wa zamu!
 
Kwa jinsi,, Kwa jinsi kwa nini,, Kwa jinsi,, ninii,, Kwa jinsi,, jinsi gani enhee,,, Kwa jinsi Mungu,,, Mungu nanii,, Mungu,,, nanii,, Mungu,,, Ni mama yako,,, Hapana,,, Ni baba yako,,, Hapana,,, Ni ndugu yako,,, Hapana,,, Ni beste yako,,, Hapana,,, Ni jirani yako,,, Hapana Pastor,,, Ni naniiiii,,, Kwa jinsi Mungu alivyoupenda,,, Ngoja alifanya ninii,,,, Alivyoupenda,,, Aliukataa,,, Hapana,,, Aliutusi,,, Hapana,,, Aliuachilia,,,, Hapana ,,, Aliupaka matee,,, Hapana,,, Aliufanya niniii,, Aliupenda,,, Aliupenda ninii,,, Kwa jinsi Mungu alivyoupenda ulimwengu,,,Aliupenda ninii,,, Ulimwengu,,, Umbwa yako,,, Hapana,,, Ni ng'ombe yako,,, Hapana Mchungaji,,, Ni bibi yako,,, Hapana Pastor,,, Ni mama yako,,, Hapana Padri,, Ni nyanya yako,,, Hapana ,,,, Ni naniiiiii?
 
Swala la kupata usingizi linazidi kua changamoto kadri siku zinavyosonga

Kuna dawa/tiba/suluhisho la hili tatizo wakuu?
20250516_225237.jpg
 
Back
Top Bottom