JamiiForums Usiku wa manane
Mazungumzo ya usiku

Muendelezo wa mazungumzo ya jana.....


c/ Tabia ya kuwa Sahihi mda wote

Ubongo wetu sio mashine ambayo ipo sahihi,huwa inafanya makosa,ni mara ngapi tunafanya maamuzi kwa kutumia hisia,tunatabia ya kuwajaji watu,tunakuwa na dhana juu ya mambo mbali mbali tofauti na ukweli halisi

Ukweli ni kwamba watu ambao wanapenda kuwa sahihi kwa kila kitu huwa wanajikosesha nafasi ya kujifunza mambo mapya,wanashindwa kuyaona mambo katika mtazamo mwingine tofauti na wanao uamini wao,watu hao vile vile wanashindwa kujifunza kutokana na makosa yao

Ni vizur zaidi kujifanya hujui na mjinga ili ujifunze mambo mengi zaidi.



d/ Kuwa positive muda wote

Kuna watu ambao wanaangalia thamani ya maisha yao kwa kuwa positive mda wote,akikosa kazi anasema walau amepata mda wa kuexplore,mume wake akicheat na dada yake anasema it's okay walau amemjua mumewe ni mtu wa aina gani

Ila kuna wakati maisha yanazingua sana na kitu bora cha kufanya ni kukubaliana na ukweli tu

Kujaribu kuzikwepa negative emotions ni sawa na kuzidi kuleta matatizo zaidi

Wakati mwingine kuwa positive ni njia ya kukwepa ukweli wa mambo na sio suluhisho la kudumu la kutatua matatizo yako


Kuna nyakati watu wanatuuzi,mambo hayaendi sawa na dili zina buma,kwahiyo kuukubali ukweli na kuwa na negative emotions ni kitu cha kawaida kabisa na ndio ubinadamu wetu

Kukataa negative emotions ni kuleta matatizo na hatutopata suluhisho la kudumu

Siri moja nzuri ya negative emotions ni kuiexpress katika namna nzur inayokubalika na jamii na katika namna inayoendana na thamani yako

Kwa mfano value ya Etugrul bey ni kutopenda ugomvi,kwahiyo nitasolve jambo kwa mazungumzo zaidi,na wewe unajua value yako msomaji wangu

Kwa mfano ninapokuwa na hasira naielezea kwa mhusika lkn sichukui hatua ya kurusha ngumi,hasira kama hasira sio tatizo kwakuwa ndio asili tuliyo umbwa nayo,ila kibaya ni kuielekeza hasira katika ugomvi na uharibifu

Kitu cha msingi ni kuwa na maono mazuri ya thamani yetu na furaha itakuja kama matokeo ya kuwa na good value

Mlinzi wa zamu!
 
Huwa nawakubali sana ninapoona walinzi wanao sign in mida ya night kali!


Hii inaonyesha lindo halibaki bila ulinzi
 
Mazungumzo ya usiku

MARA ZOTE HUWA TUNAFANYA MAAMUZI


Leo hii ukilazimishwa kufanya mazoezi na mzazi wako,hakika utaona ni maumivu makubwa na utajihisi unaonewa ingawa ni kwa faida yako mwenyewe

Lakini

Ukiamua kwa hiari yako kufanya hayo mazoezi utajituma na utafurahia kwa kuwa umechagua mwenyewe kufanya hivyo

Kwahiyo siku zote huwa ni watu wenye kufanya maamuzi ya kutafsiri mambo hata kama yametokea nje ya uwezo wetu au maamuzi yetu,mfano ule mfano wa mazoezi,pamoja na kwamba umelazimishwa kufanya na mzazi wako,lkn una maamuzi ya kuyatafsiri kwa namna mbili

Ama utafsir kwamba ni jambo zuri la kiafya ambalo mzazi wako anataka uwe na afya nzuri au utafsiri kwamba ni adhabu kwako

Ebu twende katika mfano wa maisha halisi:

Anaitwa William James,ametoka katika familia bora yenye kujiweza kiuchumi,lkn pamoja na hayo,huyu mwamba alizaliwa akiwa na changamoto nyingi za kiafya

Alikuwa na tatizo la macho ambalo lilimpa upofu wa mda,akawa na matatizo ya kusikia,alikuwa na changomoto ya uti wa mgongo kiasi kwamba wakati mwingine alishindwa kukaa au kutembea kwa siku kadhaa


Alishindwa kuendelea katika masomo,alishindwa kufanya jambo lolote,alionekana lazy katika familia,kibaya zaidi mdogo wake Henry James alikuwa mwandishi wa riwaya alifanya vizur sana katika kazi yake

Mdogo wake Alice James nae alikuwa mwandishi,alifanya vizur na kuishi kwa kutegemea kazi yake

Baba yake na William kwakuwa ana connections na maguru,basi akamfanyia mpango akajiunge na shule ya masomo ya utatibu pale Havard,na akaambiwa kwamba akifeli this time atajijua yeye mwenyewe

Baada ya miaka kadhaa pale Chuoni,alishindwa na kurudi mtaani,akiwa hana hili wala lile,na alikata tamaa na kutaka kujiua kwakuwa alijiona amefeli maisha

Siku moja usiku akiwa anasoma lectures za profesa mmoja,akakutana na somo ambalo linasema lolote linalo mtokea mwanadamu ni kutokana na maamuzi yake

Rejea mfano kule nyuma nilisema ni kwa namna gani tunafanya maamuzi ya kutafsiri matukio kwa yale yanayo tutokea ndio itatufanya tuwajibike kwa namna moja au nyingine

Basi akaamua afanye majaribio ya somo lile,akadhamiria kwamba ataishi kwa mwaka mmoja akiamini kwamba yote yalitokea katika maisha yake lilikuwa ni kosa lake,na baada ya huo mwaka mmoja kama hali haitabadilika basi atakatisha maisha yake

Mwisho wa siku William James alijulikana kama Baba wa Filosofi nchini Marekani,alipewa heshima kama msomi,mwanasaikolojia,mwanafilosa

Alienda kutoa lecture Havard University,na Vyuo mbalimbali Marekani pamoja na Ulaya

Tambua kwamba siku zote huwa tunafanya maamuzi,hata kwa yale mambo ambayo yapo nje ya uwezo ila bado tunafanya maamuzi

Ni kwa kiasi gani utatafsiri yale yanayo kutokea na kuchukua maamuzi ambayo yatakuathiri au laa iko juu yako

Mfano umeachwa na mpenzi wako,una mambo mawili ama uchague kulialia na kupata msongo wa mawazo na kushindwa kufanya majukumu yako ya kila siku

Au

Utafsiri kwamba huyo hakuwa mtu wako wa kudumu alipita kwako akupe uzoefu fulani kisha utakutana na mwenza wa maisha yako

Hapo utaona kwamba always huwa tunafanya maamuzi

Mlinzi wa zamu!
 
Back
Top Bottom