ERTUGRUL BEY
JF-Expert Member
- Aug 6, 2020
- 11,597
- 21,642
Mazungumzo ya Usiku
THAMANI YA MAUMIVU
Mnamo mwaka 1944 Jeshi la Japan lilikuwa limetawanyika karibia eneo kubwa la Asia,lkn wakati huo huo ndio mambo yalibadilika dhidi yao ,Jeshi la Amerika lilifanikiwa kwa kiasi kikubwa kuwadhibiti wajapani,na askari wa Japan walikuwa na machaguzi mawili tu ama wauwawe au wawe mateka
Lakini wakati huo huo aliteuliwa lutenanti Hiroo Onoda,huyu kazi yake au mission yake ilikuwa ni kuhakikisha anapunguza nguvu ya jeshi la marekani kwa gharama yoyote ile,na katu asikubali kujisalimisha
Mnamo mwaka 1945 mwezi wa august wakashushiwa bomu la nyuklia katika mji wa Hiroshima na Nagasaki na hapo Japan ilisalimu amri rasmi
Lakini huko katika uwanja wa vita lutenant Onoda alikuwa katika vita vya msituni nchini philiphine katika kisiwa cha Lubang,akiwa na watu wake kama watatu hivi aliendelea kupambana dhidi ya jeshi la Marekani
Yeye hakujua kama vita imeisha,lkn baadae Japan kwa kushirikiana na Marekani wakasambaza vipeperushi kutoa ujumbe kwamba vita imeisha,lkn pamoja na Lutenant Onoda kuona ujumbe huo,yeye aliamini hizo ni njama za Marekani katika kutaka kumdhoofisha,aliamini bado vita inaendelea
Alikuwa anavamia wanakijiji na kupora na kuwaua yeye na vijana wake,karibia miaka 30 huyu mwamba anapambana tu msituni,pamoja na jitihada kufanywa tena kwa kurusha vipeperushi kwamba vita imeisha lkn bado mwamba aliamini huo ni uongo tu,alichojua yeye ni kufanya misheni yake
Baadae akabakia yeye mwenyewe baada ya wenzie kufa,msako ulifanywa sana na majeshi kumtafuta lkn hakupatikana,kukawa na maneno mengi sana juu ya legend huyu huko Japan,hivyo ikampa hamasa kijana mdogo Suzuki ambaye aliacha shule na mapenzi yake makubwa ilikuwa ni kufanya adventure
Hivyo akaamua this time akamtafute huyo legend,kwakuwa kulikuwa na imani kwamba huenda bado yupo hai,akaenda huko kisiwa cha Lubang akiwa hana mbinu zozote za kijeshi wala dhana za kivita wala silaha
Alichofanya ni kuita kwa sauti kubwa "Onoda emperor anahuzunika kwa kutopatikana kwako' na cha kustaajabisha ndani ya siku nne tu Suzuki alimpata lutenant Hiroo Onoda
Watu hawa wakawa marafiki huko msituni, Onoda baada ya kugundua kuwa ni kweli vita ilishakwisha alishangaa na kuhuzunika sana,lakini alisema wala hajutii kwa yalitokea kwasababu alikuwa anatimiza mission yake
Hiroo Onoda akamuuliza sababu gani iliyomfanya kijana mdogo kama Suzuki kwenda msituni kumtafuta yeye, Suzuki akajibu kuwa alikuwa na mission tatu,ya kwanza ni kumtafuta Onoda,ya pili ni kumtafuta Panda na tatu ni kwenda kumtafuta Snowman/mtu wa barafu huko Himalayas
Kweli huyu dogo aliendelea na adventure yake ambayo huenda baridi kali huko ilikuwa ndio kifo chake
Baada ya Onoda kurudi Japan mwaka 1975 akawa mtu mashuhuri sana,si televisions wala redio stations zote zilikuwa zikimuarika kwa mahojiano ya hapa na pale,na vile vile akachapisha kitabu,pamoja na hayo yote serikali ikampa hela nzuri sana
Lakini Onoda alikuwa na huzuni juu ya maadili ambayo yamebadilika nchini kwake Japan,sasa haikuwa tena ile Japan aliyoipigania na kuwa tayar kufa kwa ajili ya taifa lake,ilikuwa Japan ya kibepari,wanawake wanavaa nusu uchi kama nchi za magharibi
Hili lilimpa huzuni sana hakufurahia tena maisha ya Japana,kwakuwa sio ile Japan ambayo aliipigania,kwake ni afadhali angeendelea kuishi msituni huko Lubang nchini Philiphine kuliko kuona Taifa lake la Japan lilivyobadilika
Mnamo mwaka 1980 akaamua kuhamia kl Brazil na ndiko alikofia huko
Lutenant Hiroo Onoda alijali sana kuhusu Japan ya zamani ambayo alikuwa tayar kufa kwa ajili yake,na hakuwa tayar kuikubali Japan mpya,na huo ndio ukawa mwanzo wa kukosa furaha na kuwa na msongo wa mawazo
Nasi hivyo hivyo huwa kama Lutenant Onoda,huwa tunashindwa kukubali kwamba kuna mambo fulani fulani katika maisha yetu lazima yabadilike,na hatuwezi kuyazuia,tuna option mbili ama tukatae ukweli tuwe na huzuni pamoja na stress au tuuKubali ukweli na kwenda nao sawa na tuwe na furaha
Mlinzi wa zamu!
THAMANI YA MAUMIVU
Mnamo mwaka 1944 Jeshi la Japan lilikuwa limetawanyika karibia eneo kubwa la Asia,lkn wakati huo huo ndio mambo yalibadilika dhidi yao ,Jeshi la Amerika lilifanikiwa kwa kiasi kikubwa kuwadhibiti wajapani,na askari wa Japan walikuwa na machaguzi mawili tu ama wauwawe au wawe mateka
Lakini wakati huo huo aliteuliwa lutenanti Hiroo Onoda,huyu kazi yake au mission yake ilikuwa ni kuhakikisha anapunguza nguvu ya jeshi la marekani kwa gharama yoyote ile,na katu asikubali kujisalimisha
Mnamo mwaka 1945 mwezi wa august wakashushiwa bomu la nyuklia katika mji wa Hiroshima na Nagasaki na hapo Japan ilisalimu amri rasmi
Lakini huko katika uwanja wa vita lutenant Onoda alikuwa katika vita vya msituni nchini philiphine katika kisiwa cha Lubang,akiwa na watu wake kama watatu hivi aliendelea kupambana dhidi ya jeshi la Marekani
Yeye hakujua kama vita imeisha,lkn baadae Japan kwa kushirikiana na Marekani wakasambaza vipeperushi kutoa ujumbe kwamba vita imeisha,lkn pamoja na Lutenant Onoda kuona ujumbe huo,yeye aliamini hizo ni njama za Marekani katika kutaka kumdhoofisha,aliamini bado vita inaendelea
Alikuwa anavamia wanakijiji na kupora na kuwaua yeye na vijana wake,karibia miaka 30 huyu mwamba anapambana tu msituni,pamoja na jitihada kufanywa tena kwa kurusha vipeperushi kwamba vita imeisha lkn bado mwamba aliamini huo ni uongo tu,alichojua yeye ni kufanya misheni yake
Baadae akabakia yeye mwenyewe baada ya wenzie kufa,msako ulifanywa sana na majeshi kumtafuta lkn hakupatikana,kukawa na maneno mengi sana juu ya legend huyu huko Japan,hivyo ikampa hamasa kijana mdogo Suzuki ambaye aliacha shule na mapenzi yake makubwa ilikuwa ni kufanya adventure
Hivyo akaamua this time akamtafute huyo legend,kwakuwa kulikuwa na imani kwamba huenda bado yupo hai,akaenda huko kisiwa cha Lubang akiwa hana mbinu zozote za kijeshi wala dhana za kivita wala silaha
Alichofanya ni kuita kwa sauti kubwa "Onoda emperor anahuzunika kwa kutopatikana kwako' na cha kustaajabisha ndani ya siku nne tu Suzuki alimpata lutenant Hiroo Onoda
Watu hawa wakawa marafiki huko msituni, Onoda baada ya kugundua kuwa ni kweli vita ilishakwisha alishangaa na kuhuzunika sana,lakini alisema wala hajutii kwa yalitokea kwasababu alikuwa anatimiza mission yake
Hiroo Onoda akamuuliza sababu gani iliyomfanya kijana mdogo kama Suzuki kwenda msituni kumtafuta yeye, Suzuki akajibu kuwa alikuwa na mission tatu,ya kwanza ni kumtafuta Onoda,ya pili ni kumtafuta Panda na tatu ni kwenda kumtafuta Snowman/mtu wa barafu huko Himalayas
Kweli huyu dogo aliendelea na adventure yake ambayo huenda baridi kali huko ilikuwa ndio kifo chake
Baada ya Onoda kurudi Japan mwaka 1975 akawa mtu mashuhuri sana,si televisions wala redio stations zote zilikuwa zikimuarika kwa mahojiano ya hapa na pale,na vile vile akachapisha kitabu,pamoja na hayo yote serikali ikampa hela nzuri sana
Lakini Onoda alikuwa na huzuni juu ya maadili ambayo yamebadilika nchini kwake Japan,sasa haikuwa tena ile Japan aliyoipigania na kuwa tayar kufa kwa ajili ya taifa lake,ilikuwa Japan ya kibepari,wanawake wanavaa nusu uchi kama nchi za magharibi
Hili lilimpa huzuni sana hakufurahia tena maisha ya Japana,kwakuwa sio ile Japan ambayo aliipigania,kwake ni afadhali angeendelea kuishi msituni huko Lubang nchini Philiphine kuliko kuona Taifa lake la Japan lilivyobadilika
Mnamo mwaka 1980 akaamua kuhamia kl Brazil na ndiko alikofia huko
Lutenant Hiroo Onoda alijali sana kuhusu Japan ya zamani ambayo alikuwa tayar kufa kwa ajili yake,na hakuwa tayar kuikubali Japan mpya,na huo ndio ukawa mwanzo wa kukosa furaha na kuwa na msongo wa mawazo
Nasi hivyo hivyo huwa kama Lutenant Onoda,huwa tunashindwa kukubali kwamba kuna mambo fulani fulani katika maisha yetu lazima yabadilike,na hatuwezi kuyazuia,tuna option mbili ama tukatae ukweli tuwe na huzuni pamoja na stress au tuuKubali ukweli na kwenda nao sawa na tuwe na furaha
Mlinzi wa zamu!