JamiiForums Usiku wa manane
Mazungumzo ya Usiku

THAMANI YA MAUMIVU

Mnamo mwaka 1944 Jeshi la Japan lilikuwa limetawanyika karibia eneo kubwa la Asia,lkn wakati huo huo ndio mambo yalibadilika dhidi yao ,Jeshi la Amerika lilifanikiwa kwa kiasi kikubwa kuwadhibiti wajapani,na askari wa Japan walikuwa na machaguzi mawili tu ama wauwawe au wawe mateka

Lakini wakati huo huo aliteuliwa lutenanti Hiroo Onoda,huyu kazi yake au mission yake ilikuwa ni kuhakikisha anapunguza nguvu ya jeshi la marekani kwa gharama yoyote ile,na katu asikubali kujisalimisha

Mnamo mwaka 1945 mwezi wa august wakashushiwa bomu la nyuklia katika mji wa Hiroshima na Nagasaki na hapo Japan ilisalimu amri rasmi

Lakini huko katika uwanja wa vita lutenant Onoda alikuwa katika vita vya msituni nchini philiphine katika kisiwa cha Lubang,akiwa na watu wake kama watatu hivi aliendelea kupambana dhidi ya jeshi la Marekani

Yeye hakujua kama vita imeisha,lkn baadae Japan kwa kushirikiana na Marekani wakasambaza vipeperushi kutoa ujumbe kwamba vita imeisha,lkn pamoja na Lutenant Onoda kuona ujumbe huo,yeye aliamini hizo ni njama za Marekani katika kutaka kumdhoofisha,aliamini bado vita inaendelea

Alikuwa anavamia wanakijiji na kupora na kuwaua yeye na vijana wake,karibia miaka 30 huyu mwamba anapambana tu msituni,pamoja na jitihada kufanywa tena kwa kurusha vipeperushi kwamba vita imeisha lkn bado mwamba aliamini huo ni uongo tu,alichojua yeye ni kufanya misheni yake

Baadae akabakia yeye mwenyewe baada ya wenzie kufa,msako ulifanywa sana na majeshi kumtafuta lkn hakupatikana,kukawa na maneno mengi sana juu ya legend huyu huko Japan,hivyo ikampa hamasa kijana mdogo Suzuki ambaye aliacha shule na mapenzi yake makubwa ilikuwa ni kufanya adventure

Hivyo akaamua this time akamtafute huyo legend,kwakuwa kulikuwa na imani kwamba huenda bado yupo hai,akaenda huko kisiwa cha Lubang akiwa hana mbinu zozote za kijeshi wala dhana za kivita wala silaha

Alichofanya ni kuita kwa sauti kubwa "Onoda emperor anahuzunika kwa kutopatikana kwako' na cha kustaajabisha ndani ya siku nne tu Suzuki alimpata lutenant Hiroo Onoda

Watu hawa wakawa marafiki huko msituni, Onoda baada ya kugundua kuwa ni kweli vita ilishakwisha alishangaa na kuhuzunika sana,lakini alisema wala hajutii kwa yalitokea kwasababu alikuwa anatimiza mission yake

Hiroo Onoda akamuuliza sababu gani iliyomfanya kijana mdogo kama Suzuki kwenda msituni kumtafuta yeye, Suzuki akajibu kuwa alikuwa na mission tatu,ya kwanza ni kumtafuta Onoda,ya pili ni kumtafuta Panda na tatu ni kwenda kumtafuta Snowman/mtu wa barafu huko Himalayas

Kweli huyu dogo aliendelea na adventure yake ambayo huenda baridi kali huko ilikuwa ndio kifo chake

Baada ya Onoda kurudi Japan mwaka 1975 akawa mtu mashuhuri sana,si televisions wala redio stations zote zilikuwa zikimuarika kwa mahojiano ya hapa na pale,na vile vile akachapisha kitabu,pamoja na hayo yote serikali ikampa hela nzuri sana

Lakini Onoda alikuwa na huzuni juu ya maadili ambayo yamebadilika nchini kwake Japan,sasa haikuwa tena ile Japan aliyoipigania na kuwa tayar kufa kwa ajili ya taifa lake,ilikuwa Japan ya kibepari,wanawake wanavaa nusu uchi kama nchi za magharibi

Hili lilimpa huzuni sana hakufurahia tena maisha ya Japana,kwakuwa sio ile Japan ambayo aliipigania,kwake ni afadhali angeendelea kuishi msituni huko Lubang nchini Philiphine kuliko kuona Taifa lake la Japan lilivyobadilika

Mnamo mwaka 1980 akaamua kuhamia kl Brazil na ndiko alikofia huko

Lutenant Hiroo Onoda alijali sana kuhusu Japan ya zamani ambayo alikuwa tayar kufa kwa ajili yake,na hakuwa tayar kuikubali Japan mpya,na huo ndio ukawa mwanzo wa kukosa furaha na kuwa na msongo wa mawazo

Nasi hivyo hivyo huwa kama Lutenant Onoda,huwa tunashindwa kukubali kwamba kuna mambo fulani fulani katika maisha yetu lazima yabadilike,na hatuwezi kuyazuia,tuna option mbili ama tukatae ukweli tuwe na huzuni pamoja na stress au tuuKubali ukweli na kwenda nao sawa na tuwe na furaha

Mlinzi wa zamu!
 
Mazungumzo ya usiku

JITAMBUE WEWE BINAFSI


Tuchukue mfano wa kitunguu,kitunguu kina layer mbali mbali au maganda ambayo yamebebana kutoka juu kwenda chini

Na kadri utakavyo zidi kuyatoa ndio kuna uwezekano mkubwa wa kujikuta unatoa machozi

Jambo la kwanza mtu anatakiwa ajue kuhusu hisia zake,ajifahamu anahisia zipi,kadri anavyozidi kujichunguza atazidi kufahamu je hisia hizi ni za furaha au huzuni

Na baada ya kujua hisia zake,mathalani amejitambua kwamba ana husia za huzuni,basi hatua inayofuata anatakiwa ajiulize je hizi hisia zinasababishwa na nini?

Na hapa ndio kwenye mtihani mkubwa,kwa kutojua nini hasa ni sababu ya kuhisi hivi tunavyo hisi basi inakuwa vigumu kutatua changamoto ambayo iko mbele yetu

Usipopata sababu halisi zinazo sababisha huzuni yako tegemea kutotua tatizo na kuendelea kupata huzuni siku zote

Badala yake utakuwa unajiipoza kwa kujipa furaha ya mda mfupi na baadae tatizo liko pale pale

Mfano unasumbuliwa na tamaa ya kutaka hiki na kile,kila fashion mpya ikiingia unataka uende nayo sawa,kuna simu toleo jipya unataka upate,gari toleo jipya unataka uwe nalo

Matokeo yake ukivikosa unakuwa na huzuni,sasa usipojichunguza kwa makini unawe dhani kwamba tatizo la huzuni yako tatizo la kutokuwa na pesa ya kununua product mpya,matokeo yake hata ukipata pesa na kupata vitu hivyo,utafurahi baada ya mda,ila ikija model mpya utakuwa na huzuni tena

Lkn kumbe lau ungejichunguza kwa makini ungejitambua kwamba tatizo au chanzo cha huzuni yako ni HUTOSHEKI NA ULICHO NACHO

Lau ukijua kumbe shida yangu ni kutotosheka na nilicho nacho ndio chanzo cha huzuni yangu,,,litakuja swali la pili,je nifanye nini ili niepukane na tabia hii

Jibu ambalo ni la kudumu la kuondoa huzuni yangu ni KUJIFUNZA KUTHAMINI NILICHO NACHO PAMOJA NA KURIDHIKA NACHO

Hapo utakuwa na amani pamoja na furaha siku zote

So jichunguze na jitafakari na ujitambue

Mlinzi wa zamu!
 
Back
Top Bottom