JamiiForums Usiku wa manane
MAZUNGUMZO YA USIKU


HISIA ZINAPEWA UZITO SANA

Hili ni tatizo kubwa,tujue kwamba hisia zipo kwa ajili ya kutupa mrejesho wa mambo na kutufanya tujisikie vizuri kwa kipindi fulani,kwa maana hauta jisikia vizur mda wote

Hisia huwa hazidumu ndio maana unaweza kujisikia vizur sasa hivi lkn baada ya mda fulani ile furaha au hisia za furaha uliyokuwa nayo inapotea,na unaweza ukawa na hisia za huzuni sasa hivi na baaada ya masaa kadhaa hiyo huzuni ikapotea

Na hisia ni kama kiashiria cha kutuambia kitu fulani kiko sawa na kitu hakiko sawa,ambacho hakiko sawa ukitafutie ufumbuzi na ambacho kiko sawa endelea kukiboresha zaidi

Mfano katika mahusiano ,hisia mbaya huwa ni ishara inayo kwambia kwamba haya mahusiano sio mazuri,ndio maana kila mara unapata hisia ambazo hazikupi furaha,maana yake unapewa ujumbe ebu tatua hili tatizo ambalo linakufanya ujisikie huzuni au vibaya katika mahusiano yako

Na hisia nzuri katika mahusiano zinakupa ishara kwamba huu uhusiano ni wa kuupigania kwasababu unakufanya ujisikie vizur,kwahiyo kama ulikuwa unauchukulia poa basi ebu jitahidi kuuboresha zaidi

Kama vile ambavyo unapata maumivu baada ya kidole chako kugusa moto,hayo maumivu yanakwambia next time uwe muangalifu zaidi,na hisia za huzuni zinakwambia just try to fix something chap

Kwahiyo kwakuwa hisia ni zenye kubadilika badilka basi usifanye maamuzi tu kwa kutumia hisia peke yake utafeli amigo,bali fanya maamuzi kwa kutumia akili pia,na kwa kufanya hivyo utafanya maamuzi sahihi siku zote

Anayehitaji kufanya maamuzi kwa hisia tu ni mtoto wa miaka mitatu au mbwa,unajua kwanini kwasababu hawana cha kufanya zaidi ya kushit katika kochi au kitanda

Kwahiyo jua kwamba hisia hubadilika,na haimaanishi kitu kinachokufanya uhisi vibaya sasa hivi ni kibaya,bali unaweza hisi vibaya lkn kitu hicho kikawa kizuri,na unaweza kuwa na hisia fulani juu ya kitu fulani kuwa ni kizuri lkn ukweli wa mambo kitu hicho sio kizuri

Ndio maana inasisitiwa fanya maamuzi kupitia hisia pamoja na reason

Mlinzi wa Zamu!
Safi😎🤏🏿
 
Mazungumzo ya Usiku

JE UPO TAYAR KUPAMBANA NA HALI IPI?

Watu wengi ukiwauliza je unataka mambo gani katika maisha? Watakwambia natak kuwa na kazi nzuri,nyumba nzur,mke mzuri na great sex,na gar nzuri

Lakini

Hakuna hata mmoja ambaye atakwambia nataka kupambana na changamoto fulani katika maisha,kitu ambacho hakikwepeki

Je unataka kuwa na sex body? Upo tayar kutumia mda mwingi gym ili uwe na sex body?

Unataka kuwa na mwanamke mrembo,je upo tayar kupambana na stress zinazotokana na mahusiano hayo?

Unataka kufanya biashara,je upo tayar kupoteza mda mwingi na kujitoa mhanga kwa biashara ambayo hata huna uwakika kama utatoboa?

Unataka kazi nzuri yenye malipo mazuri,je upo tayar kumvumilia boss ambaye anaweza kuyafanya masaa ya kazi mchana kutwa kuwa kama hell?

Je upo tayar kupambana na changamoto?

Watu wengi tunapenda matokeo lkn sio process/mchakato,ndio maana ni rahisi mtu kukwambia nataka kuwa na maisha mazuri,nataka kuwa na makazi mazuri na mambo kama hayo

Lakini je,tumejipanga kwa ajili ya mchakato wa kuyafikia hayo tunayo yataka,kuwa tayar kwa mchakato maana yake upo tayar kupambana na changamoto yoyote utakayo kutana nayo mbele yako na utadili nayo bila kujilaumu hata kama utakutana na magumu kiasi gani

Ndio maana swali la msingi la kujiuliza kwa kila mtu je,nipo tayar kupambana na changamoto la hili jambo ninalotaka kufanya?

Mathalani unataka kuoa,je upo tayar kupambana na changamoto za maisha ya ndoa? Wale ambao hawakujiuliza hili swali ndio huwa wa kwanza kuona ndoa chungu ndani ya miezi michache tu tangu wafunge ndoa

Lakini kama ulijiuliza na ulikuwa tayar kupambana na changamoto za ndoa,naamini kabisa mpake leo ndoa yako bado ipo imara,kwasababu haijalishi ni changamoto kiasi gani unakutana nazo lkn kwa kuwa ulikuwa tayar kupambana nazo bado unaendelea kudili nazo kwakuwa matatizo ni sehemu ya maisha ya kila siku

Tusijidanganye katika hii dunia hakuna siku ambayo matatizo yatakwisha,ila matatizo yataendelea kuwepo kwahiyo kikupwa ni kuwa tayar kupambana nayo

Wakati mwingine hatufikii malengo yetu kwakuwa huwa tunapenda matokeo zaidi kuliko mchakato wa kuyafikia hayo malengo,nakumbuka miaka ya nyuma lau ungeniuliza ungetaka ukubwani kufanya kazi gani ningekujibu nataka kuwa "mtangazaji wa redio" ni sio siri nilikuwa navutiwa sana watangazaji kama marehemu Julias Nyei Sanga maarufu Anko J redio Tanzania enzi hizo,nyie jen z hamuwezi kumjua huyu,jen x tunamjua

Nilikuwa pia navutiwa sana na mtangazaji Taji Liundi,mpaka leo naamini kabisa kama ningekuwa mtangazaji basi ningekuwa mtangazaji bora sana,lkn niliamini matokeo ya kuwa mtangazaji bora ila sikuwa tayar kufuata mchakato,ndio maana ndoto yangu ilififia kwa kutoenda hata kusomea uandishi wa habari,lkn nilidhani ningekuwa mtangazaji tu from no where

Hii ni kwasababu sikuwa tayar kupambana na changamoto ya kusomea uandishi wa habari,kwahiyo kwa kila unachotaka kufanya jiulize je,upo tayar kupambana na changamoto iliyopo mbele yako?

Unataka kufanya biashara,je upo tayar kupoteza mtaji na kusimama tena na kuanza upya? Je upo tayar kutake risk?
Upo tayar kutumia mda wako mwingi kupambania biashara yako?

Always be ready to choose your own struggle

Mlinzi wa Zamu!
 
Mazungumzo ya Usiku

WEWE SIO MTU SPECIAL

Hivi umeshawi kukutana na watu ambao wanajifanya wana mambo mengi sana hapa mjini,kuna ambaye yeye hujifanya anajuana na watu mashuhuri hapa town,nimemkumbuka bro wangu mmoja tulioa nyumba moja,huyu bwana ukikaa nae anaweza kujifanya kapiga simu anaogea na mtoto wa mzee wa Msoga,mara sijui anaongea na mfanyabiashara gani mkubwa,yani ili mradi aonekane mtu wa maana hapa town

Watu kama hawa wapo wengi sana na hufanya hivyo ili waonekane ni watu wa maana sana,na watafanya lolote lile ili hadhi yao ibakie pale pale hata kama wanajidanganya wenyewe

Kibaya zaidi wapo radhi kuficha madhaifu yao ili mradi tu wawe juu siku zote au waonekane watu wa maana,ikitokea wamefanikisha jambo fulani hata kwa kusaidiwa na wengine watajisifu sana,na wakifanya makosa basi lawama zote zitapelekwa kwa watu wengine kwamba ndio wamsababisha hayo

Msomaji wangu ngoja nikwambie ukweli,thamani ya mtu inapatikana pale anapo jifanyia tathimini yeye mwenyewe na kugundua madhaifu yake na kisha akayafanyia kazi na kujirekebisha na kuwa mtu bora zaidi

Thamani yako haiji kwa kujipa vyeo feki,au kujipa hadhi usiyokuwa nayo,sana sana unazidi kujishushia heshima,huyo bro wangu yani sometime anatega simu inapiga alarm kama mlio wa simu halafu kisha anajifanya anaongea na papaa gani sijui,yani haishiwi drama,na wallah kama hujamjua mbona unaingia king,na madem anawatafuna sana tu hadi marafiki wa mkewe kawatembezea sana,lkn je mwisho wa siku ana fanikisha nini katika maisha?

Sisi tunao mjua ingawa mwenyewe hajui kama tunamjua tunaishia kumradharau,yani yeye kukupiga sound kwamba atakukutanisha na Abdul ni jambo dogo tu dah wacha nicheke mie hahaha!

Mlinzi wa zamu!
 
Back
Top Bottom