JamiiForums Usiku wa manane

JamiiForums Usiku wa manane

Mwenyekiti Rayns kwa ruhusa yako,naomba niwasilishe hoja binafsi

Naomba serikali iimarishe muonekano wa treni ya abiria ya wakazi wa dar,ile treni ni ya mjini lkn muonekano wake hauridhishi kabisa

Kuna haja ya mamlaka husika kulifanyia kazi swala hili walau ikarabatiwe ili iendane na hadhi ya mjini

Naamini kabisa ikikarabatiwa itaongeza mvuto kwa abiria wengi watapenda kutumia usafiri huo

Nawasilisha hoja

Mlizi wa zamu!
Hoja yako imepokelewa kwa mikono miwili 💯🤝🤝🤝

Punde utapikea ujumbe wa majibu ya hoja yako 😅💯
 
2246

Mazungumzo ya Usiku

Kalamu yangu inawamulika maafisa usafirishaji / boda boda,hivi mkiwa juu ya boda boda zenu huwa mnawaza nini?

Kwanini huwa mnaharaka sana kiasi kwamba hamchukui tahadhari mnapo kuwa barabarani,na kibaya zaidi hamfanyi uzembe huo mkiwa wenyewe,isipokuwa mnapo kuwa na abiria wenu


Siku tatu nyuma bado kidogo tushuhudie ajali ya boda na abiria wake watatu,hawa huenda mababa wa familia,kama kawaida kwa haraka zao pale flyover ya njia panda kuelekea veta

Tupo kwenye tata tunatokea karume tunaelekea nyerere road,boda anatoka maeneo ya veta,si akapita mbele ya tata ambayo tayar imekata kona kuelekea nyerere road,yani kama sio break imara za tata wale wangekuwa mochwari now

Kama nyie mmechoka na maisha basi mtambue abiria wenu bado wanapenda kuishi

Mlinzi wa Zamu!
 
Back
Top Bottom