JamiiForums Usiku wa manane
Kiwango cha msamiati sijui,hili tunaweza kuwauliza maguru wa lugha hii,ila msingi mama wa lugha moja kutoafautiana na lugha nyingine ni SARUFI,sababu katika fani au somo la sarufi ndio huwa tunapa maneno na maumbile yake.

Kiswahili kitakuwa ni kibantu kwa sababu niliyokupa na hakiwezi kuwa mseto na ligha nyingine sababu kila lugha ina sarufi yake,Kiswahili hakiwezi kuwa kiarabu sababu sarufi ya kiarabu ni tofauti kabisa na sarufi ya Kiswahili,kwa minajili hii ndio maana tunaishia katika kukopa maneno kwa maana zake au matamshi yake lakini hatukopi sarufi.
Naelewa Zurri. Nilikuwa nakuchemsha tu. Lugha kukopa maneno kutoka lugha nyingine ni jambo la kawaida na kusema kweli haliepukiki kwa sababu hakuna lugha inayojitosheleza. Kiingereza pengine ndiyo lugha iliyokopa maneno mengi zaidi hasa ya kitaaluma lakini kukopa huku hakukuibadilisha lugha hiyo...na Kiswahili ni Kibantu kwa asilimia 100 kabisa...Upo vizuri sana !!!
 
pumzika salama
Nitakuwa mchoyo wa fadhila kama sitarudisha shukrani zangu za dhati kwenu na kuwapa kongole za kutosha,kwa ushirikiano wenu mpaka muda huu.

Hakuna marefu yasiyo na ncha. Hapa nina usingizi balaa,nikiendelea kuandika sana nisije kuandika "bbade i love you". Hatari sana usingizi.
 
Fanya tuje tunywe hata Maji. ...
Ni heartbreak tu hakuna maji ni hewa
Screenshot_20190202-020639.jpeg
 
Naelewa Zurri. Nilikuwa nakuchemsha tu. Lugha kukopa maneno kutoka lugha nyingine ni jambo la kawaida na kusema kweli haliepukiki kwa sababu hakuna lugha inayojitosheleza. Kiingereza pengine ndiyo lugha iliyokopa maneno mengi zaidi hasa ya kitaaluma lakini kukopa huku hakukuibadilisha lugha hiyo...na Kiswahili ni Kibantu kwa asilimia 100 kabisa...Upo vizuri sana !!!

Tunaendelea kujifunza. Ila kaka mkubwa umeiva,ulishusha nondo za ukweli sana nikajifunza kitu pale mwanzo ulipotoa sababu za kwanini ilipigiwa chapuo sana lahaja ya Kiunguja dhidi ya nyingine,sijawahi kuzisoma hizo sababu hapo kabla,ila itanibidi niende kuchimba zaidi ili niendelee kufaidika tena na tena.
 
Tunaendelea kujifunza. Ila kaka mkubwa umeiva,ulishusha nondo za ukweli sana nikajifunza kitu pale mwanzo ulipotoa sababu za kwanini ilipigiwa chapuo sana lahaja ya Kiunguja dhidi ya nyingine,sijawahi kuzisoma hizo sababu hapo kabla,ila itanibidi niende kuchimba zaidi ili niendelee kufaidika tena na tena.
Kuna huo mzozo ndiyo na ndiyo ilikuwa hoja kuu ya Sheikh Nabhany na kundi lake la wanajungu kuu. Hawa wanadai kwamba karibu kila neno la mkopo katika Kiswahili limekopwa kizembe tu kutokana hasa na uteuzi na usanifishaji tata wa Kiunguja; uteuzi wenye malengo ya kibeberu. Kundi hili limekwenda mbali zaidi hadi kupendekeza maneno mbadala kwa kila msamiati wa mkopo. Wanasema kuwa kuna utajiri mkubwa sana wa kimsamiati katika lahaja kongwe za Kiswahili; lahaja ambazo zilipuuzwa na badala yake lahaja changa tu na iliyonajisiwa na Kiarabu (Kiunguja) kuteuliwa. Kundi hili ndilo limetupatia maneno kama runinga (mbadala wa televisheni), nywila na mengineyo mengi ambayo hayajashika kasi katika matumizi ya kawaida. Kama vile jungu kuu lisivyokosa ukoko, wanajungu kuu wanaamini kuwa Kiswahili kinajitosheleza kabisa kimsamiati na wanapambana kufa na kupona kubadilisha athari za Kiarabu na Kiingereza katika Kiswahili Sanifu.

Wanapendekeza kuwa tukitaka kukopa neno kwanza tuangalia ndani ya lahaja za Kiswahili kwenyewe (kwenye jungu kuu). Tukikosa huko ndo twende kwenye lugha nyingine za Kibantu. Tukikosa humo tuangalie katika lugha zingine za Kiafrika ambazo siyo za Kibantu. Na tukikosa huko ndo tuhamie kwenye utohoaji wa moja kwa moja (radio = redio, helicopter = helikopita...). Ni kwa kufanya hivi tu ndiyo tutaweza kuzishinda juhudi za makusudi za mabeberu (zilizoasisiwa katika usanifishaji wa Kiunguja) na kuwa na lugha safi yenye hadhi halisi ya Kiafrika na siyo hii iliyojazwa msamiati wa Kiarabu.

Japo siyo taaluma yangu lakini napenda sana mambo haya ya kitamaduni, Uafrika wetu na ukombozi wa kifikra.
 
Kuna huo mzozo ndiyo na ndiyo ilikuwa hoja kuu ya Sheikh Nabhany na kundi lake la wanajungu kuu. Hawa wanadai kwamba karibu kila neno la mkopo katika Kiswahili limekopwa kizembe tu kutokana hasa na uteuzi na usanifishaji tata wa Kiunguja; uteuzi wenye malengo ya kibeberu. Kundi hili limekwenda mbali zaidi hadi kupendekeza maneno mbadala kwa kila msamiati wa mkopo. Wanasema kuwa kuna utajiri mkubwa sana wa kimsamiati katika lahaja kongwe za Kiswahili; lahaja ambazo zilipuuzwa na badala yake lahaja changa tu na iliyonajisiwa na Kiarabu (Kiunguja) kuteuliwa. Kundi hili ndilo limetupatia maneno kama runinga (mbadala wa televisheni), nywila na mengineyo mengi ambayo hayajashika kasi katika matumizi ya kawaida. Kama vile jungu kuu lisivyokosa ukoko, wanajungu kuu wanaamini kuwa Kiswahili kinajitosheleza kabisa kimsamiati na wanapambana kufa na kupona kubadilisha athari za Kiarabu na Kiingereza katika Kiswahili Sanifu.

Wanapendekeza kuwa tukitaka kukopa neno kwanza tuangalia ndani ya lahaja za Kiswahili kwenyewe. Tukikosa twende kwenye lugha nyingine za Kibantu. Tukikosa humo tuangalie katika lugha zingine za Kiafrika. Na tukikosa huko ndo tuhamie kwenye utohoaji wa moja kwa moja (radio = redio, helicopter = helikopita...)

Japo siyo taaluma yangu lakini napenda sana mambo haya ya kitamaduni, Uafrika wetu na ukombozi wa kifikra.
Duh hata sijaelewa kitu.. Lahaja ni nini chief?
 
Back
Top Bottom