JamiiForums Usiku wa manane
Wephukulu nomaa
tapatalk_1535982239908.jpeg
 
Hii ni kutokana na sarufi ya Kiswahili. Kwa maana Kiswahili kina msamiati mwingi wa kiarabu. Lakini Kiswahili ni kibantu.

Wewe unakubali kama Kiswahili si kibantu ? Na kama si kibantu,Kiswahili ni nini ?

Lugha inapaswa kuwa na msamiati kiasi gani wa kigeni ndiyo inakoma kuwa lugha asilia?

Yaweza kuwa ni Kibantu. Yaweza kuwa ni lugha mseto (Kibantu na Kiarabu)...sijui
 
Lugha inapaswa kuwa na msamiati kiasi gani wa kigeni ndiyo inakoma kuwa lugha asilia?

Yaweza kuwa ni Kibantu. Yaweza kuwa ni lugha mseto (Kibantu na Kiarabu)...sijui

Kiwango cha msamiati sijui,hili tunaweza kuwauliza maguru wa lugha hii,ila msingi mama wa lugha moja kutoafautiana na lugha nyingine ni SARUFI,sababu katika fani au somo la sarufi ndio huwa tunapa maneno na maumbile yake.

Kiswahili kitakuwa ni kibantu kwa sababu niliyokupa na hakiwezi kuwa mseto na ligha nyingine sababu kila lugha ina sarufi yake,Kiswahili hakiwezi kuwa kiarabu sababu sarufi ya kiarabu ni tofauti kabisa na sarufi ya Kiswahili,kwa minajili hii ndio maana tunaishia katika kukopa maneno kwa maana zake au matamshi yake lakini hatukopi sarufi.
 
Back
Top Bottom