JamiiForums Usiku wa manane
Lakini wakazi wa Tanga wanadai wao wanaongea Kiswahili safi..
Kule Zanzibar nako wanadai wao ndio mabingwa wa Kiswahili...
Sisi uku wa Tanganyika wanatuona Kiswahili chetu hakipo kwenye mstari ulionyokaa..

Ila lahaja iliyoteuliwa Kiswahili fasaha kiwe humo ni lahaja ya Kiunguja.
 
Guu guu ng'wanawane
mguu.jpeg
 
Ila lahaja iliyoteuliwa Kiswahili fasaha kiwe humo ni lahaja ya Kiunguja.
Unazijua sababu zilizopelekea ikateuliwa? Na mzozo mkali uliofuatia?

Ipo hoja kwamba lahaja ya Kiunguja iliteuliwa na Waingereza ili kukiharibu Kiswahili kwa makusudi na kukiondolea ubantu wake hasa katika msamiati. Lahaja hii ndiyo ilikuwa imeathirika zaidi na maingiliano na Kiarabu kuliko lahaja zingine zote (Unguja yalikuwa makao makuu ya himaya ya Mwarabu). Kama lahaja za huko Lamu zingeteuliwa Kiswahili leo kingekuwa na sura tofauti sana kuliko hiki Kiunguja kilichosheheni maneno ya Kiarabu mpaka kupelekea wengine kuhoji kama Kiswahili kweli ni lugha ya Kibantu.
 
Unazijua sababu zilizopelekea ikateuliwa? Na mzozo mkali uliofuatia?

Ipo hoja kwamba lahaja ya Kiunguja iliteuliwa na Waingereza ili kukiharibu Kiswahili kwa makusudi na kukiondolea ubantu wake hasa katika msamiati. Lahaja hii ndiyo ilikuwa imeathirika zaidi na maingiliano na Kiarabu kuliko lahaja zingine zote (Unguja yalikuwa makao makuu ya himaya ya Mwarabu). Kama lahaja za huko Lamu zingeteuliwa Kiswahili leo kingekuwa na sura tofauti sana kuliko hiki Kiunguja kilichosheheni maneno ya Kiarabu mpaka kupelekea wengine kuhoji kama Kiswahili kweli ni lugha ya Kibantu.


Swadaktaa umesema kweli. Ila Kiswahili ni kibantu tu na hakiwezi kuwa kinyume na kibantu.
 
Back
Top Bottom