Imagine ZITTO anahama CHADEMA

Imagine ZITTO anahama CHADEMA

Status
Not open for further replies.
Zitto is slowly becoming a very polarizing figure!

Very sad tho,siwezi sahau mjadala ule wakati akiingia kwenye kamati ya madini,kuanzia pale i knew he's just another politician.
 
ZITTO TOOOOOOOOOOOOOKA WAACHIE WANACHADEMA CHADEMA YAO

Siku akitoka (kama hiyo siku ipo) tuta/watakaa chini kujiuliza; hivi kutoka kwake kulianzaanza je? Ndipo wanasayansi ya siasa watakapoibuka na nadharia nyingine kuhusu mambo yasababishayo wanasiasa kutoka au kuama vyama nchini Tanzania.
Chanzo hakitakuwa kingine, kuchukua fomu ya ukigoda wa chama bila ridhaa ya mwenye/wenye!
 
Zitto ni kijana mdogo sana kisiasa na anayejitahidi kwa jitihada zake zote awe mkongwe wa Siasa.

Mimi naona ZITTO angalia maslahi ya Taifa kwanza kisha mustakabali wa Chama ulicho kwa manufaa ya makuzi yako kisiasa hadi kuwa mkongwe.

Kisharia una haki ya kikatiba kusuka au kunyoa kutokana na taasisi uliyojiunga nayo.

Kila la Kheir na fikiri kwanza na pata ushauri toka kwa wakongwe.
 
Na Ramadhan Semtawa

SIKU chache baada ya naibu katibu mkuu wa Chadema, Zitto Kabwe kulalamika kuingiliwa kwenye anuani yake ya barua pepe, Jeshi la Polisi limesema kuingilia mawasiliano ya faragha ya mtu ni jinai na kumtaka mwanasiasa huyo atoe taarifa polisi ili waanze kulishughulikia.

Zitto, ambaye yuko Ujerumani ambako anasoma, alikaririwa na vyombo vya habari wiki iliyopita akidai kuwa anaingiliwa mawasiliano katika anuani yake ya barua pepe (e-mail), kitu alichosema ni aghalabu kufanywa hata na Idara ya Usalama wa Taifa.

Zitto, ambaye juzi alituma barua pepe kwenye gazeti hili kulalamikia kitendo hicho huku akitangaza kutembea na barua ya kujiuzulu uongopzi Chadema, alieleza kusikitishwa na kitendo hicho ambacho alidai kinafanywa na chama chake.

Hata hivyo, DCI Manumba alipoulizwa jijini Dar es Salaama jana kuhusu malalamiko ya Zitto, alijibu: "Sisi hutujapata rasmi malalamiko hayo, lakini akileta tutachunguza kwa kuwa si sahihi kuingilia mawasiliano ya mtu."

Kwa mujibu wa DCI Manumba, mawasiliano ya barua pepe na mengine ni faragha hivyo ni makosa kwa mtu yeyote kuingilia mawasiliano ambayo hayamhusu.

"Kwa kawaida ni makosa kuingilia mawasiliano ya mtu siku zote tukipata taarifa kama hizo tunachoweza kufanya ni kuchunguza kuthibitisha kwanza kwani ni suala kitaalamu zaidi," alifafanua DCI Manumba.

DCI aliongeza kwamba, siku zote wamekuwa wakichunguza malalamiko yote yanayofikishwa kwao kama yanahusiana na uingiliaji wa faragha ya mtu ikiwemo mawasiliano yake.

Alifafanua kuwa iwapo mlalamikaji akifikisha malalamiko yake, wao huwa hawasiti kuchunguza bila kuangalia jambo lenyewe lina mlengo gani.

"Ni sawa na mtu akimpiga mkewe sisi tukiletewa taarifa, kwanza tunachunguza halafu tunachukua hatua za kisheria kwa mhusika baada ya kujiridhisha. Kwa hiyo hata yeye (Zitto) akileta tutachunguza," aliongeza.

"Siku zote tunafanyia kazi taarifa zinazotufikia, kama kuna mtu anazo taarifa akileta kwamba mawasiliano yake yameingiliwa tutafanyia kazi tukio hilo ili kujiridhisha."

Malalamiko ya Zitto yalitokana na taarifa iliyotolewa na chama hicho kilichodai kuwa ofisa habari aliyetimuliwa, David Kafulila anatumia anuani ya barua pepe ya Zitto visivyo halali. Kafulila na Zitto ni marafiki wakubwa.

"Sitaki kugombana na mtu mimi. Wala msiniweke kwenye kifungo cha siasa. Ni bora niishi huru kuliko katika mateso ya siasa za kipumbavu kabisa. Nitafanya maamuzi ambayo hayajawahi kufikiriwa," alisema Zitto katika taarifa yake kwa Mwananchi.

Alisisitiza kwamba kamwe hatasukumwa na Chadema na kwamba "wanapaswa waniache nipumzike na kufanya mambo yangu".

"Hakuna mtu ananayeweza kuzungumza kwa niaba yangu hata kama ni rafiki yangu, siasa siyo chaguo langu la pekee katika maisha," alisema.


Katika kuonyesha kuchukizwa na baadhi ya taarifa alizoziita za kizushi zilizoandikwa na gazeti moja la kila siku (si Mwananchi), Zitto, alisema: "Faragha yangu ni faragha yangu, Zitto ni Zitto kama yeye na siyo mali ya Chadema.

Akizungumzia uhusiano wake na Kafulila aliyehamia NCCR-Mageuzi kutoka Chadema, Zitto alisema: "Siku zote msimamo wangu umekuwa kwa wale wanaokandamizwa... na katika hili David (Kafulila) ndiye anayekandamizwa."

Alisisitiza kwamba kamwe hatasukumwa na Chadema katika kufanya mambo yake.

"Hakuna mtu ananayeweza kuzungumza kwa niaba yangu hata kama ni rafiki yangu, siasa siyo chaguo langu la pekee katika maisha yangu."

"Msimwandame Kafulila. Mumwache mtoto wa watu. Mmeshamwita sisimizi inatosha. Msijaribu kunigombanisha na Kafulila. Sitaki... sitaki... sitaki," aling'aka Zitto.
 
Du chadema ni mwisho kumbe ndiyo maana waliwahi free media kusema Kafulila ndiye anatumia password .Hawa watu ni noma.

Ndivyo vivyo walivyowahi kwa kifo cha Wangwe kudai uchunguzi, lile walifanikiwa kidogo na akili zao bado wanaendeleza libeneke lile lile kwa staili ile ile.
 
ndugu polisi pia hawana uwezo wa kuaccess email za chadema kwa sababu ni mali ya chadema kama zitto alitumia yahoo au gmail kisha akafanyiwa hivyo pia polisi hawawezi kudhibitisha hivyo mpaka wapate ripoti toka google au yahoo na pia kampuni hizo hazitambui mtu yeyote ingawa wanaweza kukupa data zote za mtu alivyokuwa anatumia email hiyo na pale alipokuwa alituma nini na vitu kama hivyo
 
ndugu polisi pia hawana uwezo wa kuaccess email za chadema kwa sababu ni mali ya chadema kama zitto alitumia yahoo au gmail kisha akafanyiwa hivyo pia polisi hawawezi kudhibitisha hivyo mpaka wapate ripoti toka google au yahoo na pia kampuni hizo hazitambui mtu yeyote ingawa wanaweza kukupa data zote za mtu alivyokuwa anatumia email hiyo na pale alipokuwa alituma nini na vitu kama hivyo

polisi si wana mkono mrefu??

Kazi rahisi ni polisi kuomba hao gmail ama yahoo kwamba messaage hii na hii imetumwa kwa IP address ipi na wakati gani?
 
Kuna taratibu zake sio unaenda tu ni zitto mwenyewe kupeleka suala hilo katika vyombo husika sio kwa kulazimishwa na awe na ushahidi kwamba imetokea hivyo sio ukute alitegeshewa programu ya kuhifadhi pwd toka siku nyingi au yeye mwenyewe ana share na mke wake halafu leo aje kulalamika
 
Haha haha ha ha
Mwafrika ngoja achoromoke huko aliko
 
Zitto, tafadhali mkuu usiuze nchi kwa vijipesa kidogo vya hao maharamia wanaodeal na silaha haramu. Kumbuka watu hao wanaua watu kwa ajili tu ya pesa na kumake sure wanaendela kuwa madarakani, usidhani na wala usifikirie wanakupenda sana ila wanataka kuangamiza chadema na wapiganaji wote, sasa mvuto wako ukiisha, jua utakuwa njia panda na chochote wanaweza kukufanyia.

Mkuu Zitto, silazimishi ubaki chadema lakini kama unamipango mingine, sio mbaya wewe jiuzulu tu na mapambano yaendelee au toa bayana msimamo wako kuliko kuacha hali iwe tete hivi na kutumaliza wote tunaoipenda nchi yetu.
 
huyu aondoke bana anatuvuruga tu akili hapa...Kwani ZITTO nani?he is just another sisimizi ..nenda mwana kwenda wafuate wenzio wakina kafulila
 
hili li DCI ndio sifuri kabisa..badala ya ku deal na mambo ya maana unaanza kufuatilia mambo ya email za Zitto..mbona husemi ya RICHMOND uchunguze....
 
Kusaliti UMMA ni dhambi kubwa, CHADEMA, you're attention please.
 
hili li DCI ndio sifuri kabisa..badala ya ku deal na mambo ya maana unaanza kufuatilia mambo ya email za Zitto..mbona husemi ya RICHMOND uchunguze....

Nafikiri DCI ni TAKURU naomba kukosolewa.
 
polisi si wana mkono mrefu??

Kazi rahisi ni polisi kuomba hao gmail ama yahoo kwamba messaage hii na hii imetumwa kwa IP address ipi na wakati gani?

Hii ndio tech ya porrrraaand?

Kwenda yahoo au gmail na kuwaomba wakupatie IP? Ha ha ha ha!
 
Mbona sioni wapi Dr. Slaa aliposema Zitto anatumika? Amesema ameletewa nakala ya mawasiliano kati ya Zitto na jamaa bila kusema kilichomo. Sasa hicho kichwa cha habari kimetokana na nini? Au ndiyo zile hesabu zetu za 2+2=22?

Amandla...
 
Nilikuwa najiuliza hapa ni saa ngapi utataja jina la mwafrika.

Okay ... what's the matter (wrong)?

Haha ha ha ha
Hatimaye umeingiza timu rasmi.
kipyenga priiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii
 
Source : Mwananchi kwenye habari ya DCI Manumba .......

......

"Sitaki kugombana na mtu mimi. Wala msiniweke kwenye kifungo cha siasa. Ni bora niishi huru kuliko katika mateso ya siasa za kipumbavu kabisa. Nitafanya maamuzi ambayo hayajawahi kufikiriwa," alisema Zitto katika taarifa yake kwa Mwananchi.

Alisisitiza kwamba kamwe hatasukumwa na Chadema na kwamba "wanapaswa waniache nipumzike na kufanya mambo yangu".

"Hakuna mtu ananayeweza kuzungumza kwa niaba yangu hata kama ni rafiki yangu, siasa siyo chaguo langu la pekee katika maisha," alisema.

Katika kuonyesha kuchukizwa na baadhi ya taarifa alizoziita za kizushi zilizoandikwa na gazeti moja la kila siku (si Mwananchi), Zitto, alisema: "Faragha yangu ni faragha yangu, Zitto ni Zitto kama yeye na siyo mali ya Chadema.

Akizungumzia uhusiano wake na Kafulila aliyehamia NCCR-Mageuzi kutoka Chadema, Zitto alisema: "Siku zote msimamo wangu umekuwa kwa wale wanaokandamizwa... na katika hili David (Kafulila) ndiye anayekandamizwa."

Alisisitiza kwamba kamwe hatasukumwa na Chadema katika kufanya mambo yake.

"Hakuna mtu ananayeweza kuzungumza kwa niaba yangu hata kama ni rafiki yangu, siasa siyo chaguo langu la pekee katika maisha yangu."
"Msimwandame Kafulila. Mumwache mtoto wa watu. Mmeshamwita sisimizi inatosha. Msijaribu kunigombanisha na Kafulila. Sitaki... sitaki... sitaki," aling'aka Zitto.
 
Status
Not open for further replies.

Similar Discussions

Back
Top Bottom