Kubwajinga
JF-Expert Member
- Jan 23, 2008
- 2,193
- 299
Na Mwandishi wetu
7th December 2009
Asema zipo njama kuhamisha ajenda ya ufisadi
Adai kunasa mawasiliano ya Zitto na mwingine
Ajigamba Chadema hakina mgogoro, kipo imara
Katibu Mkuu wa Chadema, Dk. Wilbrod Slaa (kushoto) na Zitto Kabwe.
Mkuu wa Chadema, Dk. Wilbrod Slaa, amesema kuna vita kali sasa ya baadhi ya watu kufanya njama za kuhamisha ajenda ya vita dhidi ya ufisadi na kuzungumzia masuala ya mbunge wao, Kabwe Zitto.
Nadhani sasa Watanzania wanatakiwa wakaelewa naona sasa kuna vita kali ya kuiondoa ajenda ya vita dhidi ya ufisadi, na sasa wanataka kutuelekeza kumjadili mtu, Zitto.
Na mimi nasema hatuhitaji kujadili watu isipokuwa chama, alisema Dk. Slaa wakati akizungumza na Nipashe jijini Dar es Salaam jana na kuongeza: Chadema hakina mgogoro na kipo imara na hiyo ilithibitika wakati na baada ya Mkutano Mkuu wa chama hicho uliofanyika Septemba, mwaka huu.
Akizungumzia kuhusu madai ya Zitto kutembea na barua ya kujiuzulu Chadema, Dk. Slaa alisema ofisi yake haijapata barua, maelezo yoyote au ushauri kutoka kwa Zitto unaoelezea suala hilo.
Hatuwezi kuendelea na mambo haya ya kuhamisha ajenda ya vita dhidi ya ufisadi na kuanza sasa kujadili suala la mtu binafsi, kama ambavyo sasa inaanza kujitokeza, alisema.
Alisema Chadema ni taasisi itaendelea kuwepo hata kama yeye ama Mbowe (Mwenyekiti wa taifa wa chama hicho) au Zitto wataondoka katika chama hicho.
Alisisitiza kuwa chama hicho kitaendelea kupiga vita ufisadi kwa nguvu zote licha ya baadhi ya watu kuanza kudhoofisha ajenda hiyo.
Akifafanua kuhusu suala la Zitto, Dk. Slaa alisema siku moja saa 1:00 jioni kabla ya Mkutano Mkuu wa Chadema uliopita, alipata nafasi ya kuzungumza na mama ya Zitto, ambaye ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya chama hicho, Shida Salum, aliyemhakikishia kwamba Zitto hahusiki na mambo hayo.
Siku moja kabla ya Kamati Kuu, niliongea na mama yake Zitto na akanihakikishia kwamba hahusiki na mambo haya yanayojitokeza ya kukichafua chama, alisema.
Alisema alielezwa na mama huyo kuwa wapo watu wanaomtumia Zitto kwa maslahi wanayoyajua wenyewe na kwamba mtu mmoja (jina linahifadhiwa) anayo password ya anuani ya barua pepe ya Zitto ambayo anaitumia kuandika taarifa mbalimbali alizoeleza zinaonyesha kama vile zinatoka kwa Zitto.
Lakini alisema baada ya mazungumzo na mama huyo, kesho yake gazeti moja lilikuwa na habari ya Zitto kukanusha kwamba hahusiki na suala la David Kafulila isipokuwa watu wametumia jina lake.
Dk. Slaa aliongeza baada ya mazungumzo hayo, asubuhi yake alipata taarifa za barua pepe kutoka kwa Mtanzania mwema zinazoonyesha mawasiliano kati ya Zitto na mtu mmoja (jina linahifadhiwa).
Bila kueleza kwa undani taarifa mbalimbali zilizokuwemo katika barua hizo pepe, alisema kwa kifupi kwamba zilikuwa zikionyesha mawasiliano ya kichama kati ya mkazi mmoja wa jijini Dar es Salaam na Zitto ambaye kwa sasa yupo masomoni nchini Ujerumani.
Alisema baada ya kuzisoma aliwasiliana na mkazi huyo wa Dar es Salaam akitamka athibitishe iwapo mawasiliano hayo ya barua pepe yalikuwa ya kwake au la.
Alisema alifanya hivyo kwa kumtumia ujumbe na baada ya muda mkazi huyo alimpigia Dk. Slaa, na akathibitisha kwamba anazitambua barua hizo na mawasiliano hayo yalikuwa ni ya kwake.
Lakini baadaye katika mazungumzo yao ya simu, mkazi huyo wa jijini alimweleza Dk. Slaa kwamba ameingilia mawasiliano yao binafsi, jambo ambalo alilipinga.
Nilimweleza mkazi huyo kwamba sijaingilia mawasiliano binafsi, kwa kuwa taarifa zilizokuwa zikizungumzwa katika barua hizo zilikuwa zikikihusu Chadema na kwa maana hiyo hazikuwa binafsi, alisema.
Alisema baadaye mkazi huyo alimjibu Dk. Slaa kwamba anafanya kazi katika kampuni kubwa na kwamba Dk. Slaa hataiweza na afadhali aache.
Aliongeza baada ya gazeti moja kuchapisha habari za Zitto jana, alimtumia Zitto ujumbe wa barua pepe akitaka maelezo kuhusu habari hizo zilizodai kuwa anatembea na barua ya kujiuzulu Chadema.
Dk. Slaa alisema tangu alivyomtumia ujumbe huo jana asubuhi, hajapata majibu yoyote hadi alipowasiliana na Nipashe saa 11:00 jana jioni.
CHANZO: NIPASHE 12/07/2009
7th December 2009
Katibu Mkuu wa Chadema, Dk. Wilbrod Slaa (kushoto) na Zitto Kabwe.
Mkuu wa Chadema, Dk. Wilbrod Slaa, amesema kuna vita kali sasa ya baadhi ya watu kufanya njama za kuhamisha ajenda ya vita dhidi ya ufisadi na kuzungumzia masuala ya mbunge wao, Kabwe Zitto.
Nadhani sasa Watanzania wanatakiwa wakaelewa naona sasa kuna vita kali ya kuiondoa ajenda ya vita dhidi ya ufisadi, na sasa wanataka kutuelekeza kumjadili mtu, Zitto.
Na mimi nasema hatuhitaji kujadili watu isipokuwa chama, alisema Dk. Slaa wakati akizungumza na Nipashe jijini Dar es Salaam jana na kuongeza: Chadema hakina mgogoro na kipo imara na hiyo ilithibitika wakati na baada ya Mkutano Mkuu wa chama hicho uliofanyika Septemba, mwaka huu.
Akizungumzia kuhusu madai ya Zitto kutembea na barua ya kujiuzulu Chadema, Dk. Slaa alisema ofisi yake haijapata barua, maelezo yoyote au ushauri kutoka kwa Zitto unaoelezea suala hilo.
Hatuwezi kuendelea na mambo haya ya kuhamisha ajenda ya vita dhidi ya ufisadi na kuanza sasa kujadili suala la mtu binafsi, kama ambavyo sasa inaanza kujitokeza, alisema.
Alisema Chadema ni taasisi itaendelea kuwepo hata kama yeye ama Mbowe (Mwenyekiti wa taifa wa chama hicho) au Zitto wataondoka katika chama hicho.
Alisisitiza kuwa chama hicho kitaendelea kupiga vita ufisadi kwa nguvu zote licha ya baadhi ya watu kuanza kudhoofisha ajenda hiyo.
Akifafanua kuhusu suala la Zitto, Dk. Slaa alisema siku moja saa 1:00 jioni kabla ya Mkutano Mkuu wa Chadema uliopita, alipata nafasi ya kuzungumza na mama ya Zitto, ambaye ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya chama hicho, Shida Salum, aliyemhakikishia kwamba Zitto hahusiki na mambo hayo.
Siku moja kabla ya Kamati Kuu, niliongea na mama yake Zitto na akanihakikishia kwamba hahusiki na mambo haya yanayojitokeza ya kukichafua chama, alisema.
Alisema alielezwa na mama huyo kuwa wapo watu wanaomtumia Zitto kwa maslahi wanayoyajua wenyewe na kwamba mtu mmoja (jina linahifadhiwa) anayo password ya anuani ya barua pepe ya Zitto ambayo anaitumia kuandika taarifa mbalimbali alizoeleza zinaonyesha kama vile zinatoka kwa Zitto.
Lakini alisema baada ya mazungumzo na mama huyo, kesho yake gazeti moja lilikuwa na habari ya Zitto kukanusha kwamba hahusiki na suala la David Kafulila isipokuwa watu wametumia jina lake.
Dk. Slaa aliongeza baada ya mazungumzo hayo, asubuhi yake alipata taarifa za barua pepe kutoka kwa Mtanzania mwema zinazoonyesha mawasiliano kati ya Zitto na mtu mmoja (jina linahifadhiwa).
Bila kueleza kwa undani taarifa mbalimbali zilizokuwemo katika barua hizo pepe, alisema kwa kifupi kwamba zilikuwa zikionyesha mawasiliano ya kichama kati ya mkazi mmoja wa jijini Dar es Salaam na Zitto ambaye kwa sasa yupo masomoni nchini Ujerumani.
Alisema baada ya kuzisoma aliwasiliana na mkazi huyo wa Dar es Salaam akitamka athibitishe iwapo mawasiliano hayo ya barua pepe yalikuwa ya kwake au la.
Alisema alifanya hivyo kwa kumtumia ujumbe na baada ya muda mkazi huyo alimpigia Dk. Slaa, na akathibitisha kwamba anazitambua barua hizo na mawasiliano hayo yalikuwa ni ya kwake.
Lakini baadaye katika mazungumzo yao ya simu, mkazi huyo wa jijini alimweleza Dk. Slaa kwamba ameingilia mawasiliano yao binafsi, jambo ambalo alilipinga.
Nilimweleza mkazi huyo kwamba sijaingilia mawasiliano binafsi, kwa kuwa taarifa zilizokuwa zikizungumzwa katika barua hizo zilikuwa zikikihusu Chadema na kwa maana hiyo hazikuwa binafsi, alisema.
Alisema baadaye mkazi huyo alimjibu Dk. Slaa kwamba anafanya kazi katika kampuni kubwa na kwamba Dk. Slaa hataiweza na afadhali aache.
Aliongeza baada ya gazeti moja kuchapisha habari za Zitto jana, alimtumia Zitto ujumbe wa barua pepe akitaka maelezo kuhusu habari hizo zilizodai kuwa anatembea na barua ya kujiuzulu Chadema.
Dk. Slaa alisema tangu alivyomtumia ujumbe huo jana asubuhi, hajapata majibu yoyote hadi alipowasiliana na Nipashe saa 11:00 jana jioni.
CHANZO: NIPASHE 12/07/2009